Get premium membership and access questions with answers, video lessons as well as revision papers.

Kuna umuhimu gani kufunza fasihi simulizi katika chuo za upili?

      

Kuna umuhimu gani kufunza fasihi simulizi katika chuo za upili?

  

Answers


KELVIN
a)Kuburudisha-kustarehesha, kufurahisha, kuchangamsha, kutuliza, kusisimua na kupumbaza akili na kiwiliwili - nyimbo, hadithi, vitendawili
b)Kufunza maadili kwa wanajamii kwa kuwahimiza kuiga sifa chanya na kukataa sifa hasi za wahusika.
c)Kukuza uwezo wa kufikiri/kudadisi k.m vitendawili na chemshabongo.
d)Kufariji k.m mbolezi na methali k.m. ‘Baada ya dhiki faraja’.
e)Vipengele vya fasihi simulizi k.v mashairi, nyimbo, nahau, hutumiwa katika uandishi wa fasihi andishi.
f)Kuhifadhi historia ya jamii k.m. mighani, visaviini, mapisi, tarihi n.k.
g)Kukejeli tabia zinazokiuka matarajio ya jamii k.v soga, methali, n.k.
h)Kuendeleza tamaduni za jamii kwani husawiri imani na desturi za jamii. k.v kitendawili ‘Nyumbani mwetu mna papai lililoiva lakini siwezi kulichuma.’ - Mtu hawezi kumwoa dadake.
i)Kuunganisha watu pamoja kwa kuwajumuisha pamoja wakati wa ngoma, kuimba, utambaji, n.k.
j)Kukuza lugha k.v. misimu inapokita kimatumizi na kujumuishwa katika lugha sanifu.
k)Kukuza uwezo wa kutumia lugha kadiri mtu anapoendelea kuwasilisha k.v. hotuba, vitanza ndimi husaidia kuboresha matamshi na kutofautisha maana za maneno.

kalvinspartan answered the question on October 20, 2017 at 16:32


Next: Eleza tofauti kati ya hadhira ya fasihi andishi na fasihi simulizi.
Previous: Taja sababu zinazochangia katika kubadilika kwa Fasihi Simulizi

View More Kiswahili Questions and Answers | Return to Questions Index


Learn High School English on YouTube

Related Questions