Get premium membership and access questions with answers, video lessons as well as revision papers.

Taja sababu zinazochangia katika kubadilika kwa Fasihi Simulizi

      

Taja sababu zinazochangia katika kubadilika kwa Fasihi Simulizi

  

Answers


KELVIN
a)Kuwasilishwa vibaya.
b)Fanani kusahau na kubadilisha yaliyomo na mtiririko.
c)Kubadilisha ili kukidhi mahitaji ya hadhira k.m. umri na uelewa wao- kutumia lugha nyepesi kwa watoto na pevu kwa watu wazima.
d)Mabadiliko ya mandhari/mazingira-vitu vilivyo katika mazingira halisi kukosekana katika mazingira ya usimulizi na msimulizi kutumia vitu katika mazingira yake vinavyokaribiana navyo.
e)Kutoeleweka na hivyo kuhifadhiwa vibaya.
f)Mabadiliko ya wakati k.m kitendawili cha wakati wa mkoloni kutumia mzungu na cha wakati wa mwarabu kutumia mwarabu na maana ni ile ile-Mzungu/mwarabu amesimama kwa mguu mmoja-mwavuli.
g)Mabadiliko ya falsafa ya vizazi na maingiliano katika jamii kusababisha kurithisha tu yale ambayo ni muhimu na kuacha mengine.
h)Kila fanani huwa na mtindo wake wa kuwasilisha/kisanii.

kalvinspartan answered the question on October 20, 2017 at 16:33


Next: Kuna umuhimu gani kufunza fasihi simulizi katika chuo za upili?
Previous: Taja na ueleze aina za wahusika katika Fasihi Simulizi.

View More Kiswahili Questions and Answers | Return to Questions Index


Learn High School English on YouTube

Related Questions