Get premium membership and access questions with answers, video lessons as well as revision papers.

Ni sifa zipi zinazotambulisha chemshabongo.

      

Ni sifa zipi zinazotambulisha chemshabongo.

  

Answers


KELVIN
i.Hutumia lugha ya kimafumbo.
ii.Hutumia ufananisho wa kijazanda.
iii.Huhitaji mtu kuwaza ili kupata jibu.
iv.Hujengwa na vitu vinavyotokana na mazingira.
v.Hazina muundo maalum kama methali, nahau na vitendawili
vi.Hupima uwezo wa msikilizaji wa kutambua jambo lililofichwa.

AMA

a) Ni semi zinazofumba jambo.
b) Huhitaji mtu kuwaza ili aweze kubuni fumbo lenyewe.
c) Shughuli, maumbile au vitu vilivyo katika mazingira ya jamii kama vile mifugo, njia za usafiri na nyenzo za biashara vinaweza kufumbiwa.
d) Baadhi ya mafumbo hufananisha kitu kilichotajwa katika fumbo na mazingira halisi.
e) Baadhi ya mafumbo huwa marefu na mengine huwa mafupi.
f) Mafumbo huhitaji mantiki ili kuyatmbua. Mfano nina chui mbuzi na majani ya kuliwa na mbuzi je nitafanya aje ili nivuke ngambo ile
kalvinspartan answered the question on October 24, 2017 at 14:26


Next: Linganisha vitendawili na methali
Previous: Eleza maana ya vitanza ndimi huku ukitoa umuhimu wake

View More Kiswahili Questions and Answers | Return to Questions Index


Learn High School English on YouTube

Related Questions