Get premium membership and access questions with answers, video lessons as well as revision papers.

Eleza sifa za nahau

      

Eleza sifa za nahau.

  

Answers


KELVIN
a) Nahau huundwa kwa lugha ya mkato iliyo na ujumbe mzito wa mafumbo k.m kidudu mtu-mfitini.
b) Nahau mbili au zaidi zinaweza kuwa na maana moja k.m jamvi la wageni/bao la mkahawani –kahaba.
c) Nahau moja inaweza kuwa na maana zaidi ya moja k.m kushika mguu-kuomba radhi /kutoa shukrani kupiga mbio.
d) Maneno katika nahau hupoteza sifa zake za kawaida na kuchukua maana nyingine iliyo tofauti kabisa .k.m kula chumvi –kuwa mzee.
e) Nahau huundwa kwa maneno mawili au zaidi kupaka mafuta kwa mgongo wa chupa-danganya.
f) Bega kwa bega pamoja.
g) Nahau huweza kuundwa kwa mitindo mbalimbali au kwa maneno ya kategoria mbambali k.m
i. Kitenzi na nomino –piga chuku, andika meza
ii. Kitenzi na kitezi-kufa kupona,pata shika
iii. Kitenzi na kielezi –jikaza kisabuni, kufa kikondoo
iv. Noino na nomino-askari kanzu, domo kaya
v. Nomino na kitenzi-mguu haumshiki, damu kumkauka.
vi. Nomino na vivumishi –nyoat njema, ndege mbaya
kalvinspartan answered the question on October 24, 2017 at 14:34


Next: Tambua miundo tano inayotumika katika nahau huku ukitolea mifano miwili kwa kila muundo
Previous: Taja sifa tano za misimu

View More Kiswahili Questions and Answers | Return to Questions Index


Learn High School English on YouTube

Related Questions