Soma shairi lifuatalo kisha ujibu maswali.
Kilio cha Lugha
Ni wimbo najiimbia, nijiliwaze
Sina wa kusaidia, nasongwa sina nafasi
Kiwa kwetu naumia, kwengine si mahususi
Lugha ya...
(Solved)
Soma shairi lifuatalo kisha ujibu maswali.
Kilio cha Lugha
Ni wimbo najiimbia, nijiliwaze
Sina wa kusaidia, nasongwa sina nafasi
Kiwa kwetu naumia, kwengine si mahususi
Lugha ya mtu mweusi, Kiswahili chalilia
Wataalamu ni nani, mulipo mwaninyanyasa
Hamna nami imani, wala kupanga siasa,
Mwasema sayansini, siku ningalitosa,
Mwanambia nikotosa, kuiva sijafika.
Ela muelewe sana, Maamuma na Imamu,
Mulipokuwa vijana, kwenu nilikuwa timamu,
Sasa mumesoma sana, mwaniona ni haramu,
Mujue kuwa dawamu, utumwa mwauridhia.
Mzaliwapo mwalia, 'maa', maneno ya kwanza,
Lugha munayokulia, ya mama zetu ya kwanza,
Wa lugha muwedoria, muweze na kuikuza,
Sio kujipendekeza, uzungu kuigiza.
Majira ya ukoloni, ukombozi kusambaza,
Lugha mulithamini, Kiswahili kufukiza,
Hata kule risavuni, kizungu hanikuwaza,
Sasa mbona mwanibeza, mbali mwanitupilia?
Sayansi sio asili, msamiatiwe sinao,
Sayansi yataka mbali, msamiati ni wa hao
Nitakuwa Kiswahili, kiomba majina yao
Lugha kujikuza kwao, huomba linalofaa.
Enyi viongozi wetu ipangeni nadharia,
Kujenga siasa yetu, tuzidi kuwa huria
Lugha hata 'mbusha watu, tuche kuriaria,
Sifa ni kwa chake mtu, cha mwenzi hutoringia.
Utajiri wangu hasa, nikiwatajia wote,
Msamiati huwa, ni wa Afrika yote,
Na methali za kuasa, nahau na ngeli zote,
Na nisemwapo popote, ujumbe hukamilika.
Afrika ndipo petu, pa wabantu halisi,
Baba na mama ni Bantu, shina la wangu ukwasi,
Warabu na wengi wetu, sio wangu Adinasi
Kwao 'meomba kiasi, ili kujizidisha.
Mfumo mpya hongera, wa elimu humu Kenya,
Lugha takuwa imara, ukabila tutafinya,
Kiswahili ni ibara, kila mtu kiimanya,
Methali imetuonya, mtumwa si mwasilia
Tamati lugha yalia, yabaguliwa bayana,
Kukua imeridhia, msamiati kufana,
Wengine wataijulia, kwa marefu na mapana,
Lugha yenu ya maana, mwaipuuza yalia.
(a) Shairi hili ni la aina gani? Toa sababu.
(b) Kwa kutoa hoja ime, eleza kwa nini shairi hili likaitwa kilio cha lugha.
(c) Andika ubeti wa tatu kwa lugha ya nathari.
(d) Eleza toni ya shairi hili.
(e) Tambua uhuru wa kishairi uliotumiwa kwa kurejelea mifano milatu.
F)Bainisha nafsineni katika shairi.
G)Eleza maana ya maneno yafuatayo kwa mujibu wa shairi.
(i) nasongwa
(ii) kuriaria
(iii) adinasi
Date posted:
February 6, 2018
.
Answers (1)
Jadili dhima ya fasihi katika jamii
(Solved)
Jadili dhima ya fasihi katika jamii
Date posted:
February 6, 2018
.
Answers (1)
Je, miviga ina upungufu gani?
(Solved)
Je, miviga ina upungufu gani
Date posted:
January 17, 2018
.
Answers (1)
Andika katika usemi wa taarifa
“Karibu Bakari, tafadhali kaa”, Maimuna alisema. “Asante, je, habari za nyumbani?” Bakari aliuliza
(Solved)
Andika katika usemi wa taarifa
“Karibu Bakari, tafadhali kaa”, Maimuna alisema. “Asante, je, habari za nyumbani?” Bakari aliuliza
Date posted:
January 17, 2018
.
Answers (1)
Unda nomino kutokana na kivumishi:refu
(Solved)
Unda nomino kutokana na kivumishi:refu
Date posted:
January 16, 2018
.
Answers (1)
Sahihisha
Ndegwa alipeana kalamu yake kwa mwanafunzi.
(Solved)
Sahihisha
Ndegwa alipeana kalamu yake kwa mwanafunzi.
Date posted:
January 16, 2018
.
Answers (1)
Taja tofauti iliyopo kati ya sauti /f/ na /v/
(Solved)
Taja tofauti iliyopo kati ya sauti /f/ na /v/
Date posted:
January 16, 2018
.
Answers (1)
Sababu za kubadilisha msimbo na athari zake
(Solved)
Sababu za kubadilisha msimbo na athari zake.
Date posted:
January 13, 2018
.
Answers (1)
Taja aina mbili za mofimu na kwa kila toa mfano
(Solved)
Taja aina mbili za mofimu na kwa kila toa mfano
Date posted:
December 29, 2017
.
Answers (1)