Get premium membership and access questions with answers, video lessons as well as revision papers.

Ichambue jalada ya tamthilia ya Kigogo

      

Ichambue jalada ya tamthilia ya Kigogo

  

Answers


ESTHER
Jalada ni ile sehemu ngumu ya kitabu. Kupitia jalada, tunaweza kudokeza ya kutarajiwa katika kazi ya fasihi.
Jalada la tamthilia hii lina anwani ya tamthilia: Kigogo. Kigogo ni mtu mwenye mamlaka au madaraka ya kiutawala au kiongozi. Mwandishi wake ni Pauline Kea
Anwani ya kitabu imeandikwa kwa rangi ya majano.
Kuna mchoro wa bara la Afrika lililoinama. Mchoro huu umekolezwa rangi nyeusi; ishara ya kiza.
Nyuma ya mchoro huu kuna picha ya jua linalochomoza.
Chini ya mchoro huu upande wa kushoto, kuna mzee mkongwe aliyebeba fimbo. Vile vile amekolezwa weusi. Anaonekana kuzama katika mawazo.
Rangi ya kijani kibichi imetamalaki katika jalada
Nyuma ya jalada kuna muhtasari wa tamthilia yenyewe.
Afrika kuwa katika kiza inaashiria madhila chungu nzima barani baada ya uhuru.
Mzee mkongwe anayeonekana mwenye mawazo anaashiria viongozi wa awali waliopigania uhuru na ambao tayari wameiaga dunia. Ila, hata katika pumziko lao, hawana amani kwani waliochukua hatamu baada yao kufariki wameiua ndoto ya uhuru kamili wa mwafrika
Rangi ya kijani kibichi inaashiria ardhi. Masuala ya ardhi barani Afrika ni masuala sugu yanayoleta migogoro mingi
Rangi ya majano na jua linalochomoza linaashiria mwamko mpya au mabadiliko. Kuna tumaini kama wasemavyo wahenga, siku njema huonekana asubuhi

ESTHER STEVE answered the question on April 28, 2018 at 15:20


Next: Name two examples of space crafts
Previous: Jadili maudhui ya utabaka katika tamthilia ya Kigogo

View More Kiswahili Questions and Answers | Return to Questions Index


Learn High School English on YouTube

Related Questions