Get premium membership and access questions with answers, video lessons as well as revision papers.

Maigizo huwa na madhumuni yepi katika jamii

      

Maigizo huwa na madhumuni yepi katika jamii

  

Answers


KELVIN
? Huburudisha watazamaji na waigizaji wenyewe. Burudani hii mara nyingine hupumbaza.
? Huhifadhi na kuendeleza utamaduni wa jamii kama vile upashaji tohara, matambiko, majigambo, ngoma, miviga na michezo ya watoto hudumishwa kupitia maigizo.
? Ni kitambulisho cha jamii; kila jamii ina Sanaa ya maigizo ya jamii husika. Miviga na sherehe za arusi na mazishi hutofautiana kutoka jamii moja hadi nyingine.
? Hukuza umoja na ushirikiano wa watu wanapojumuika kushiriki katika maigizo. Hao hujitambulisha kama jamii moja.
? Ni nyenzo za kupitisha maarifa na amali za jamii kupitia michezo ya jukwaani.
? Husawiri mtazamo wa jamii kuhusu masuala mbalimbali kama vile woga, wizi na usaliti.
? Hukuza ubunifu madhalan watoto wanaposhiriki michezo ya watoto, hujifunza kubuni michezo wakiwa wachanga na pia Sanaa ya uigizaji.
? Hukuza kipawa cha uongozi katika michezo, huweza kujifunza stadi za uongozi
? Ni njia ya kuimarisha urafiki. Kwa vile mizaha na utani katika malumbano hukuza urafiki na uhusiano bora
? Huongoza jamii kupambana na na mazingira wanamojipata. Kutegemea imani ya wanajamii,matambiko yanaweza kuondoa matatizo katika jamii kama vile njaa, ugonjwa na ukame kwa kuomba Mungu
? Maigizo huelimisha kupitia maudhui na hulka za waigizaji na kushauri nafsi zao, kuiga au kukashifu hulka hizo.

kalvinspartan answered the question on July 24, 2018 at 11:23


Next: Taja sifa zozote tano za maigizo
Previous: Jadili maana ya malumbano ya utani

View More Kiswahili Questions and Answers | Return to Questions Index


Learn High School English on YouTube

Related Questions