Get premium membership and access questions with answers, video lessons as well as revision papers.

Eleza uhusiano uliopo baina ya mafumbo na chemsha bongo

      

Eleza uhusiano uliopo baina ya mafumbo na chemsha bongo.

  

Answers


KELVIN
Mafumbo ni kauli zenye maana iliyojificha, mafumbo hutumia lugha fiche au ya kiistiari pamoja na tamathali nyingine za usemi. Humtaka anayeambiwa kudadisi mazingira yake na kufikiria ili kupata maana, mafumbo huchemsha bongo za wale wanaoshiriki katika kuyafumbua ingawa vitendawili ni aina za fumbo tunadai kwamba mafumbo kwa kawaida ni semi ndefu kuliko vitendawili.
Kuna mafumbo yaitwayo chemshabongo, chemshabongo ni maswali ambayo humtaka mtu kutumia akili na ujuzi kuyajibu. Maswali mengi ya aina hii ni ya kimapokeo, mengine hubuniwa na msemaji ili kukidhi mahitaji ya hadhira mahususi. Baadhi ya chemshabongo kwa hakika ni hesabu tu nyingine hutolewa kwa mraba unahitaji kujazwa.
kalvinspartan answered the question on August 5, 2018 at 12:35


Next: Vitanza ndimi huwa na dhima gani katika jamii
Previous: Eleza dhima ya mafumbo

View More Kiswahili Questions and Answers | Return to Questions Index


Learn High School English on YouTube

Related Questions