Get premium membership and access questions with answers, video lessons as well as revision papers.

Huku ukitolea mifano, eleza aina tofauti za nomino

      

Huku ukitolea mifano, eleza aina tofauti za nomino

  

Answers


KELVIN
? Neno linalotaja kiumbe, kitu, hali, mahali, tendo, dhana, n.k.
Aina
? Nomino za Pekee
? Ambazo hutaja kitu kwa kutumia jina lake/ambazo hutambulisha upekee wa kitu hicho.
? Mwanzoni huandikwa kwa herufi kubwa.
? majina ya watu k.m. Kamau
? mahali k.m. Mombasa
? siku k.m. Alhamisi
? miezi k.m. Disemba
? miaka k.m. 1930
? milima k.m. Kilimanjaro
? Mito k.m. Tana
? maziwa k.m. Victoria
? bahari k.m. Hindi
? Mabara k.m. Africa

? Nomono za Kawaida/Jumla
? Majina ya jumla ya viumbe/vitu vinavyoonyesha umbile la jinsi moja k.m. mtu, gari, kalamu, n.k.
? Nomino za Jamii
? Majina ya makundi ya viumbe au vitu k.m. bunge, jamii, halaiki, bunda n.k.
? Nomino za Wingi
? Majina ya vitu vitokeavyo kwa wingi japo kimsingi hazina umoja au wingi k.m. maji, mate, maziwa, mahubiri, marashi, mchanga, ngeu, poda, unga, n.k.
? Nomino za Dhahania
? Majina ya viumbe au mambo ya kudhani/yasiyoweza kugusika k.m. k.m ujinga, werevu, malaika, shetani, amani, imani, roho, wazo, dhana, n.k.
? Nomino za Vitenzi Jina
? Vitenzi vyenye kiambishi awali ku ambavyo huweza pia kutumika kama nomino k.m. Kucheza kwake kunaudhi.

kalvinspartan answered the question on August 5, 2018 at 13:18


Next: Viyeyusho au nusu irabu ni sauti gani?
Previous: Eleza maana ya sentensi katika kiswahili huku ukitoa sifa zake

View More Kiswahili Questions and Answers | Return to Questions Index


Learn High School English on YouTube

Related Questions