Get premium membership and access questions with answers, video lessons as well as revision papers.

Tambua na ueleze aina tofauti za vielezi

      

Tambua na ueleze aina tofauti za vielezi.

  

Answers


KELVIN
a) Vielezi vya Namna/Jinsi
? Ambavyo hueleza vile jambo lilifanyika.
Aina
? Vielezi namna mfanano
? Vinavyoeleza vile jambo lilifanyika kwa kufananisha na nomino au vivumishi.
? Huchukua viambishi KI na VI.
? Anakula kifisi.
? Tulifanya kazi vizuri.
? Vielezi namna viigizi
? Maneno ambayo kiasili ni vielezi k.m. sana, haraka, ghafla, mno, kabisa, pole, barabara n.k.
? Mwenda pole hajikwai.
? Vielezi namna hali
? Hueleza hali ya tendo.
? Alilelewa kwa shida.
? Alilewa chakari
? Vielezi namna vikariri
? Huelezea vile jambo lilifanyika kwa kurudiwarudiwa
? Alinijibu kimzahamzaha.
? Tembea polepole.
? Yeye hufanya kazi yake hivi hivi/ovyo ovyo
? Mbwa alibweka bwe! Bwe! Bwe!
? Vielezi namna ala
? Walimpiga Stephano mawe/kwa mawe.
? Vielezi Namna Viigizi
? Hueleza vile kitendo kilitendeka kwa kutumia tanakali.
? Mbuni alianguka majini chubwi!
b) Vielezi vya Idadi/Kiasi
? Maneno ambayo hutaja kitendo kimetendeka mara ngapi.
Aina
? Vielezi vya idadi halisi
? Tulivamiwa mara moja.
? Vielezi vya idadi ya jumla
? Alitoroka mara kadha/nyingi/chache.
c) Vielezi vya mahali
? Hutaja mahali kitendo kilitendekea.
Aina
? Vielezi vya mahali vya maneno kamili
? Ndege ilipofika Nairobi, ilitua chini.
? Vielezi vya mahali vya aina ya viambishi
? Ni viambishi po, ko, mo na ni.
? Alipolala palikuwa na siafu.
? Wanacheza uwanjani.
d) Vielezi vya wakati
? Hutaja kitendo kililifanyika wakati gani.
Aina
? Vielezi vya wakati vya maneno kamili
? Rais atawasili kesho/mwaka ujao.
? Kielezi cha wakati cha kiambishi (po ya wakati)
? Nililala nilipofika nyumbani

kalvinspartan answered the question on August 10, 2018 at 08:29


Next: Jadili vielezi
Previous: Jadili viunganishi

View More Kiswahili Questions and Answers | Return to Questions Index


Learn High School English on YouTube

Related Questions