Get premium membership and access questions with answers, video lessons as well as revision papers.

Kwa kudhidirisha katika sentensi onyesha jinsi aina tofauti za maneno huingiliana

      

Kwa kudhidirisha katika sentensi onyesha jinsi aina tofauti za maneno huingiliana.

  

Answers


KELVIN
? Hali ya maneno kuwa na matumizi tofauti mifano:

? W kuwa V
? Huyu analia.
? Mtoto huyu analia.
? V kuwa W
? Vikombe vizuri vitavunjika.
? Vizuri vitaliwa.
? V kuwa N
? Mti mrefu haupandiki.
? Mrefu alikufa jana jioni.
? V kuwa E
? Viatu vibaya vitachomwa.
? Uliifanya kazi vibaya.
? Mtu mjinga ni huyu.
? Anaongea kijinga.
? N kuwa V
? Tajiri alimdharau Razaro.
? Mtu tajiri huheshimiwa.
? N kuwa E
? Nairobi ni mji mkuu.
? Amewasili Nairobi.
? Kitoto kinalia.
? Unaongea kitoto.
? Haraka haina baraka.
? Fanya haraka tuondoke hapa.
? Sindano ya babu imepotea
? Alidungwa sindano/kwa sindano na daktari.
? E kuwa N
? Niliwasili jana.
? Jana yangu haikuwa nzuri.
? T kuwa N
? Nataka kulala sasa.
? Kulala kwake kunaudhi.
? N kuwa U
? Ila yake imemwathiri sana.
? Watu wote ila yeye walikwenda.
? Kichwa changu kina walakini.
? Nimekula walakini sijashiba.
? E kuwa I
? Mwenda pole hajikwai.
? Pole! Usijali utapona.
? Amepaka rangi sawasawa.
? Sawasawa! Siku moja tutakutana.
? H kuwa E
? Paka amepanda juu ya mti.
? Ameingia katika choo.
? T kuwa E
? Mtoto akilia atatapika.
? Aliingia akilia.
? N kuwa I
? Gege anacheza ala yake ya muziki.
? Ala! Waniwekea uchafu katika chakula?



kalvinspartan answered the question on August 10, 2018 at 08:36


Next: Eleza maana ya vihisishi huku ukieleza aina tofauti
Previous: Eleza maana mofimu

View More Kiswahili Questions and Answers | Return to Questions Index


Learn High School English on YouTube

Related Questions