Get premium membership and access questions with answers, video lessons as well as revision papers.

Eleza matumizi tofauti ya alama ya mkato au kipumuo

      

Eleza matumizi tofauti ya alama ya mkato au kipumuo.

  

Answers


kelvin
a) pumziko fupi katika senyensi
? Tulipofika sokoni, tulinunua mboga.
b) kuorodhesha
? Alinunua mboga, samaki, nyanya na viazi.
c) kuonyesha mwanzo au mwisho wa usemi halisi
? “Njoo kesho,”mama akamwambia.
d) kuandika anwani
? Shule ya upili Gatwe, S.L.P 160, Kerugoya.
e) baada ya kutaja jina la mtu anayepewa habari
? Daktari, ningependa kukuona.
f) kutenganisha sentensi zenye masharti
? Usipofanya kazi, usile.
g) kuandika tarehe
? Alizaliwa mwezi wa Julai, tarehe 18, 1999.
h) kuandika tarakimu zinazozidi elfu
? 1,000, 13,000, n.k.

kevowmuchiri answered the question on August 10, 2018 at 09:16


Next: Eleza njia tatu ambazo alama za dukuduku hutumika
Previous: Ritifaa au kibainishi hutumika vipi

View More Kiswahili Questions and Answers | Return to Questions Index


Learn High School English on YouTube

Related Questions