Get premium membership and access questions with answers, video lessons as well as revision papers.

Jadili usemi halisi wa sentensi

      

Jadili usemi halisi wa sentensi.

  

Answers


kelvin
? Maneno halisi kama yanavyotamkwa na msemaji.
a) Huandikwa bila kugeuza chochote.
b) Huanzia kwa herufi kubwa.
c) Hunukuliwa kwa alama za usemi ambazo huandikwa zikiwa mbili mbili na moja moja katika dondoo ndogo k.m. “Mwambie ‘ugua pole’ ukimuona,” baba aliniambia.
d) Koma hutumiwa mwanzoni au mwishoni mwake.
e) Msemaji mpya anapoanza kusema, unapaswa kufungua aya mpya k.m.
Alimuuliza, “Huendi kwa nini?”
“Sikupewa ruhusa,” alijibu Zahara.
f) Baada ya (?) na (!) na (.) maneno huanzia kwa herufi kubwa k.m. Lo! Unatoka wapi saa hii? Aliniuliza.

kevowmuchiri answered the question on August 10, 2018 at 09:59


Next: Kinyota kina matumizi yapi?
Previous: Eleza usemi wa taarifa katika sentensi za kiswahili

View More Kiswahili Questions and Answers | Return to Questions Index


Learn High School English on YouTube

Related Questions