Get premium membership and access questions with answers, video lessons as well as revision papers.

Mayai waziri wa maradhi na hadithi nyingine. Adui ya mwanamke ni mwanamke. Eleza kauli hii ukirejelea hadithi ya ngome ya nafsi na uteuzi wa moyoni

      

Mayai waziri wa maradhi na hadithi nyingine.

Adui ya mwanamke ni mwanamke. Eleza kauli hii ukirejelea hadithi ya ngome ya nafsi na uteuzi wa moyoni

  

Answers


Davis
Mwanamke anaendeleza mateso/dhuluma dhidi ya mwanamke mwenzake kwa
njia zifuatazo:
(i). Kazi-Mtoto wa kike anafanyishwa kazi nyingi za nyumbani na kutarajiwa
asome kwa wakati huo huo bila utetezi wowote kutoka kwa wanawake
(ii). Ndoa-Wanawake hawakuwa wakisomeshwa sana na hata wangeliozwa
mara tu pangetokea mume wa kuwashika mkono.
(iii) Zena anamweleza mamake kuhusu makuruhu aliyotendewa na mumewe
badala yake analaumiwa kwa kutotimiza wajibu wake hakutoa, suluhisho
mwafaka
(iv) Dhuluma ndoani zinapozidi hadi kufikia kipigo, Zena anashindwa
kumweleza mamake na hivyo kuendelea kuteseka hadi mwisho anashindwa
kuhimili.
(v) Wazazi wa Ali akiweko mamake Ali hawakufanya lolote kuzuia madhara
yaliyompata Zena ndani va ndoa. Ali alikuwa kama mfalme kwa mamave.
(vi) Zena anapomshauri mamake kuhusu swala la kujiingiza siasani, mamake
anamkashiu
(vii) .Wakati wa kampeni za kisiasa baadhi ya wanawake walichangia katika
kumsengenya na kupaka jina lake tope/ walimwita Malaya


Githiari answered the question on April 19, 2019 at 09:50


Next: Mayai waziri wa maradhi na hadithi nyingine 2. “Karibu ndugu yangu waumini ni kukirimiana tunashukuru, alhamdulilahi sifa zote ni zake Maulana a)Eleza muktadha wa dondoo hili b)...
Previous: How did the 1914 Sarajevo incident contribute to the rise of the first World war?

View More Kiswahili Questions and Answers | Return to Questions Index


Learn High School English on YouTube

Related Questions