Get premium membership and access questions with answers, video lessons as well as revision papers.

“..Wanafunzi wa chuo kikuu si kama watoto vikembe wa shule ya chekechea…..” a) Weka dondoo hili katika muktadha wake. b) Taja na ufafanue tamathali ya usemi uliyotumiwa...

      

“..Wanafunzi wa chuo kikuu si kama watoto vikembe wa shule ya chekechea…..”
a) Weka dondoo hili katika muktadha wake.
b) Taja na ufafanue tamathali ya usemi uliyotumiwa katika dondoo hili
c) Hadithi hii inadhihirisha utegemezi wa binadamu. Fafanua.

  

Answers


Kavungya
a) Weka dondoo hili katika muktadha wake.
Msemaji ni Dkt Mabonga
Msemewa - Wanafunzi wa somo la fasihi
Mahali – Ukumbi wa mhadhara
Sababu – Dkt Mabonga anasuta wanafunzi kwa kuwa vitegemezi baada ya mwanafunzi kutaka kueleza namna fasihi inaelekeza

b) Taja na ufafanue tamathali ya usemi uliyotumiwa katika dondoo hili
Tashbihi- Si kama watoto wakembe

c) Hadithi hii inadhihirisha utegemezi wa binadamu. Fafanua
Dennis Machora na wanafunzi wenzake wanangojea Dkt Mabonga amjibu mwanafunzi ili nao wapate kujua
• Dkt Mabonga alisema kuwa binadamu wanapiga ubwete na kugeuka kupe
• Dkt Mabonga alisema kuwa binadamu hatafuti chakula
• Wanafunzi wengine wanaonelea waache masomo waende kusimamia biashara za wazazi wao
• Msichana mmoja alisema kwamba mchumba wake ni katibu katika wizara ya habari, mawasiliano na teknolojia, kwa hivyo karibuni watafunga ndoa aondokewe na adha ya masomo
• Penina alikuwa anatumiwa Sh. 5000/-= kila wiki na wazazi kwa matumishi
• Aidha Dennis Machora alikuwa anategemea makupo wa shule kujihikimu. Pesa hizo zinapoisha anahangaika
• Dennis Machora aliona kuwa Penina angekuja kulalamika kuwa Dennis Machora amekuwa kupe.
• Penina alisema kuwa hangeweza kuolewa na mwanamume asiye na kazi yenye mshahara mkubwa.
• Dennis Machora na msimulizi waishi katika mtaa wa New Zealand na kodi ilikuwa inalipwa na wazazi wake Penina
Kavungya answered the question on May 6, 2019 at 05:28


Next: Onyesha jinsi maudhui ya utabaka na mapenzi ,yanavyojitokeza katika hadithi ya mapenzi ya kifaurongo.
Previous: Bara la Afrika limekumbwa na umaskini mkubwa. Fafanua dhana ukirejelea hadithi ya Tumbo lisiloshiba na Mapenzi ya Kifaurongo

View More Kiswahili Fasihi Questions and Answers | Return to Questions Index


Learn High School English on YouTube

Related Questions