Get premium membership and access questions with answers, video lessons as well as revision papers.

Bara la Afrika limekumbwa na umaskini mkubwa. Fafanua dhana ukirejelea hadithi ya Tumbo lisiloshiba na Mapenzi ya Kifaurongo

      

Bara la Afrika limekumbwa na umaskini mkubwa. Fafanua dhana ukirejelea hadithi ya Tumbo lisiloshiba na Mapenzi ya Kifaurongo

  

Answers


Kavungya
TUMBO LISILOSHIBA
• Eneo la Madongoporomoka ndiko wanamoishi watu wepesi wasio na mashiko
• Watu wa Madongoporomoka walikuwa maskini
• Katika eneo la Madongoporomoka kulikuwa na mkahawa mshenzi wa Mzee Mago
• Bi Suruti alishangaa kwa kuuliza kuhusu wanachojali matajiri kuhusu maskini kama wao
• Huko Madongoporomoka kuna mashonde ya vinyesi, vibwagizo wa choo, uchafu unaonekenya, vibanda uchwara na majichafu
• Tunaambiwa kuwa watu wengi waliokuwa wamelala waliamka na kutoka nje ya vibanda vyao haraka

MAPENZI YA KIFAURONGO
• Dennis Machora alisema kuwa umaskini uhostakimu kwao haukuwa na mfano
• Dennis Machora alisema kuwa wazazi wake hawakuwa na mali ya kuwarithisha
• Dennis Machora hana chakula, inabidi apike uji usiokuwa na sukari
• Dennis Machora alikuwa na kijiredio na ametandika kitandani shuka zilizozeeka na kuchanikachanika
• Penina alimwangalia msimulizi kwa huzuni yamkini alitelewa na hali yake duni
• Dennis Machora alimwambia Penina kuwa hawawezi kuwa na usuhuba kwa kuwa Dennis anatoka kutoka familia ya umaskini naye Penina anatoka kwenye familia yenye nafasi
• Kwa kuwa Penina alimshinda Dennis Machora kiuchumi angejidunisha na Penina angemwona kama kupe
• Penina alimwita Dennis Machora kama mkata
• Penina alimwambia Dennis kuwa Mungu angempa mpenzi mwingine aupakati ufukara wake aliouzoea
• Mwanafunzi aliyekuwa na pesa angelipa kujinasibisha na mwenzake maskini
Kavungya answered the question on May 6, 2019 at 05:31


Next: “..Wanafunzi wa chuo kikuu si kama watoto vikembe wa shule ya chekechea…..” a) Weka dondoo hili katika muktadha wake. b) Taja na ufafanue tamathali ya usemi uliyotumiwa...
Previous: “Rasta twambie bwana!” a) Weka dondo katika muktadha b) Taja mbinu zilizotumiwa na mwandishi katika dondoo hili c) Ni kwa vipi mzungumziwa anamchukulia mwalimu mkuu kama hambe? d) Je,...

View More Kiswahili Fasihi Questions and Answers | Return to Questions Index


Learn High School English on YouTube

Related Questions