Get premium membership and access questions with answers, video lessons as well as revision papers.

Jadili mashaka ya Mashaka katika hadithi ya “Ndoto ya Mashaka”

      

Jadili mashaka ya Mashaka katika hadithi ya “Ndoto ya Mashaka”

  

Answers


Kavungya
• Mhusika Mashaka aliopata mikasa mingi maishani mwake tnagu alipozaliwa. Kwanza mama yake Ma Mtumwa alifariki alipomkopoa tu, kutokana na kifafa cha uzazi.
• Babake yake naye upweke ulimshinda akafariki na wakazikwa pamoja.
• Mashaka hakuwahi kuwaona hata kwa sura, hivyo hawakumbuki.
• Biti Kidebe ndiye aliyemlea kwa shida na makuzi yalikuwa ya taabu – makuzi ya tikitimaji au tango kuponea umande.
• Biti Kidebe alikuwa haishi kulalamikia miguu yake iliyomuuma. Hivyo, licha yay eye kumlea Mashaka, naye Mashaka akamlea huyu bibi. Alitafuta kila aina ya vijikazi alivyoviweza tangu akiwa motto.
• Biti Kidebe aliwahi kumsomesha kwa shida hadi darasa la nane.
o Alipomaliza shule tu Biti Kidebe akafariki na kumwach mpweke.
• Siku moja akiwa anapiga gumzo na rafiki yake Waridi mlango ulifunguliwa ghafla wakafungishwa ndoa ya mkeka.
• Mashka anapata mke akiwa hana chochote.
• Waliowavamia chumbani mwake ni Mzee Rubeya baba yake Waridi, Sheikh Mwinyumvua, kaka yake Waridi Mansuri na rafiki yake Idi.
• Ndoa hii ilimita Rubeya aibu kwa kuwa binti yake ameolewa na fukara. Mzee Rubeya na familia yake wakaamua kurudi kwao Yemeni.
• Mashaka na Waridi waliishi katika mtaa wa watu wa hali ya chini (fukara) uitwao Tandale.
• Mandhari ya chumba chao kimoja yalikuwa kando ya choo kilichofurika vibaya wakati wa mvua na kueneza kinyesi kila mahali.
• Kulikuwa na uvundo uliotisha kwenye nyumba yao daima.
• Chumba chao kilivuja wakati wa mvua. Wakati huu wanapata tabu sana.
• Mashaka na Waridi walipata watoto saba. Hivyo ilikuwa shida watu tisa kuishi kwenye chumba kimoja.
• Mashaka alikuwa na kazi duni yenye mshahara wa mkia wa mbuzi – alikuwa mlinzi wa usiku katika kampuni za Zuia Wizi Security (ZWS)
• Watoto wake wavulana walilala jikoni kwa jirani Chakupewa.
• Watoto wake wakike walilala chini ya sakafu kwenye mkeka; Mashaka na Waridi walikuwa na vitu vichache sana maana hawakumudu kununua vyombo.
• Nafasi ilikuwa duni kabisa. Ilibidi mkewe apikie nje ya chumba chao isipokuwa, nyakati za mvua ambapo jiko huwekwa juu ya kinu kuzuia maji yanayotiririka.
• Dhiki nyumbani mwa Mashaka ndiyo ilikuwa nguo na harufu yao. Walikuwa na dhiki kubwa sana.
• Siku moja Mashaka aliporudi kutoka kazini alikuta Waridi ametoroka na watoto wote. Toka wakati huo hakuwaona tena. Akabaki mnhyonge na mpweke zaidi.
• Utengano huo ulimfanya ajutie ufukara wake na kuuona kuwa ni udhia mkubwa maishani.
• Mashaka mengi yalijikita akilini mwake kuhusu ukuta na pengo kubwa lililopo katika jamii kati ya walio nacho na wasio nacho.
• Kutokana na shida yake alikuwa na mawazo mazito na maswali yasiyo na majibu – kwa nini jumuiya za kimatiafa zinafumbia macho suala la ufukara?
• Ni ufukara uliomtenginsha yeye na Waridi, yeye na watoto wake na kumwacha katika lindi la maumivu.
• Mashaka alijipa moyo kuwa subira huenda ikamletea heri. Hata hivyo, aliendelea kusubiri akitarajia kuwa mambo yatabadilika. Lakini mambo hayakubzadilika.
• Wakati mwingine aliota ndoto kuwa pengo kati ya maskini na matajiri limepungua, na Waridi mkewe amemrudia Na wote wanaishi kwa furaha. Taabu zake zimepungua mno.
• Kumbe hayo yote ni ndoto. Akalazimika kuamka na kupanbana na ulimwengu wake wa mashaka ya umaskini.
Kavungya answered the question on May 6, 2019 at 05:40


Next: “Rasta twambie bwana!” a) Weka dondo katika muktadha b) Taja mbinu zilizotumiwa na mwandishi katika dondoo hili c) Ni kwa vipi mzungumziwa anamchukulia mwalimu mkuu kama hambe? d) Je,...
Previous: Read the poem below and answer the questions below. Advise to my son

View More Kiswahili Fasihi Questions and Answers | Return to Questions Index


Learn High School English on YouTube

Related Questions