
a) Ubinafsi- Kuna ubinafsi na ulafi katika jamii ya kisasa kama ilivyo katika hadithi.Jitu linamaliza chakula chote kwenye Mkahawa Mshenzi bila kuwajali wateja wengine.
b) Unyakuzi- Wakubwa wanataka kunyakua ardhi ya watu wadogo kama ilivyo katika jamii ya leo ambapo viongozi hunyakua ardhi ya watu maskini.
c) Dhuluma- Wananchi hukandamizwa kwa kubomolewa vibanda/makazi yao hata bila ilani na kuachwa wakihangaika jinsi ambavyo inafanyikia Wanamadongoporomoka.
d) Ufisadi- Wakubwa wanataka kuwahonga na vijisenti vidogo ili wahame makazi yao jinsi viongozi katika jamii ya leo huwahonga wananchi maskini na kunyakua mali yao.
e) Sheria zenye vikwazo- Katika jamii ya leo,sheria huwapendelea matajiri na viongozi kwani wao huweka vikwazo makusudi ili kuwazuia maskini na wasio na nguvu kutetea haki zao.Hali ni hiyo hiyo katika hadithi ya Tumbo Lisiloshiba.
f) Kutengwa- Wananchi hawahusishwi Na viongozi kikamilifu katika mipango ya maendeleo ya maeneo yao.Wanamadongoporomoka hawahusishwi katika mipango ya maendeleo.
g) Mazingira chafu- Hali katika mtaa wa Madongoporomoka ni mbaya,viongozi hawasafishi mtaa wao,kama ilivyo katika mitaa duni nyingi katika jamii ya leo.
h) Wanasheria wasio waadilifu- Jinsi inavyokuwa vigumu kupata wanasheria waadilifu katika jamii ya leo, ndivyo ilivyokuwa adimu kuwapata wanasheria waaminifu kama haki yenyewe katika jamii ya hadithi ya Tumbo Lisiloshiba.
i) Msongamano mijini- Jiji lilikuwa limejaa limejaa kila mahali;mall,majumba ya muziki,maduka makuu,shule, vyuo,hospitali,mahakama,majumba ya ofisi,n.k. Jinsi ilivyo katika miji mikuu mingi leo.
j) Matumizi mabaya ya vyombo vya dola- Askari wa baraza la mji na jeshi la polisi walitumiwa kuwafurusha wanamadongoporomoka badala ya kuwahakikishia usalama wao,Vyombo vya dola vinatumiwa vibaya na viongozi wa sasa.
k) Maendeleo- Kuna maendeleo yaliyopiga kasi katika jamii ya sasa kama ilivyo katika jamii ya hadithini.Jiji limejaa majumba ya mikahawa,malls,deparmental stores,casinos,n.k.
l) Ushirikiano- Kuna ushirikiano na umoja wa wananchi wanaonyanyaswa katika jamii ya sasa jinsi Mzee Mago alivyowakusanya wanamadongoporomoka ili kutetea haki zao.
Kavungya answered the question on May 6, 2019 at 06:53
-
Alfa Chokocho : Tulipokutana tena
“ Mamangu siku ile aliniamsha mapema.”
i) Eleza muktadha wa dondoo hili.
ii) Tathmini umuhimu wa usimulizi wa mzungumzaji katika kuendeleza dhamira...
(Solved)
Alfa Chokocho : Tulipokutana tena
“ Mamangu siku ile aliniamsha mapema.”
i) Eleza muktadha wa dondoo hili.
ii) Tathmini umuhimu wa usimulizi wa mzungumzaji katika kuendeleza dhamira ya hadithi hii.
iii) Onyesha jinsi mashaka linavyomwafiki mhusika mwenyewe katika hadithi ya “Ndoto ya Mashaka”
Date posted:
May 6, 2019
.
Answers (1)
-
Kwa kurejelea hadithi zozote tano katika diwani ya, ‘Tumbo lisiloshiba na hadithi nyingine.’ Jadili maudhui ya nafasi ya wazazi katika malezi.
(Solved)
Kwa kurejelea hadithi zozote tano katika diwani ya, ‘Tumbo lisiloshiba na hadithi nyingine.’ Jadili maudhui ya nafasi ya wazazi katika malezi.
Date posted:
May 6, 2019
.
Answers (1)
-
Jadili maudhui ya elimu katika Diwani ya Tumbo lisiloshima ukizingatia hadithi zifuatazo:
a) Mapenzi ya kifaurongo
b) Shagake dada ana ndevu.
c) Mamake Bakari .
d) Mwalimu mstaafu.
e) Mtihani...
(Solved)
Jadili maudhui ya elimu katika Diwani ya Tumbo lisiloshima ukizingatia hadithi zifuatazo:
a) Mapenzi ya kifaurongo
b) Shagake dada ana ndevu.
c) Mamake Bakari .
d) Mwalimu mstaafu.
e) Mtihani wa maisha.
Date posted:
May 6, 2019
.
Answers (1)
-
“Hebu sikiza jo! Pana hasara gani nzi kufia kidondani?”
a) Eleza muktadha wa dondoo hili.
b) Taja na utoe mifano ya mbinu nne za lugha zilizotumika katika...
(Solved)
“Hebu sikiza jo! Pana hasara gani nzi kufia kidondani?”
a) Eleza muktadha wa dondoo hili.
b) Taja na utoe mifano ya mbinu nne za lugha zilizotumika katika dondoo
c) Onyesha ukweli wa kauli “ nzi kufia kidondani” unavyodhihirishwa na wahusika katika hadithi.
Date posted:
May 6, 2019
.
Answers (1)
-
“ Wahusika katika hadithi shibe inatumaliza wanatumia uhuru wao vibaya.” Onyesha ukweli wa kauli hii kwa kutoa mifano.
(Solved)
“ Wahusika katika hadithi shibe inatumaliza wanatumia uhuru wao vibaya.” Onyesha ukweli wa kauli hii kwa kutoa mifano.
Date posted:
May 6, 2019
.
Answers (1)
-
“ Mwandishi wa haditi ya Tumbo lisiloshiba ametumia mbinu ya Jazanda kwa ufanisi mkubwa.” Thibitisha
(Solved)
“ Mwandishi wa haditi ya Tumbo lisiloshiba ametumia mbinu ya Jazanda kwa ufanisi mkubwa.” Thibitisha
Date posted:
May 6, 2019
.
Answers (1)
-
Jadili mashaka ya Mashaka katika hadithi ya “Ndoto ya Mashaka”
(Solved)
Jadili mashaka ya Mashaka katika hadithi ya “Ndoto ya Mashaka”
Date posted:
May 6, 2019
.
Answers (1)
-
Bara la Afrika limekumbwa na umaskini mkubwa. Fafanua dhana ukirejelea hadithi ya Tumbo lisiloshiba na Mapenzi ya Kifaurongo
(Solved)
Bara la Afrika limekumbwa na umaskini mkubwa. Fafanua dhana ukirejelea hadithi ya Tumbo lisiloshiba na Mapenzi ya Kifaurongo
Date posted:
May 6, 2019
.
Answers (1)
-
Onyesha jinsi maudhui ya utabaka na mapenzi ,yanavyojitokeza katika hadithi ya mapenzi ya kifaurongo.
(Solved)
Onyesha jinsi maudhui ya utabaka na mapenzi ,yanavyojitokeza katika hadithi ya mapenzi ya kifaurongo.
Date posted:
May 6, 2019
.
Answers (1)