Get premium membership and access questions with answers, video lessons as well as revision papers.

Sahihisha bila kubadilisha maana: (i) Usikuje hapa kwetu kwani sitakuwamo (ii) Basi la shule imeharibika moshi nyingi inatokea dirishani na maji inatiririka ovyo

      

Sahihisha bila kubadilisha maana:
(i) Usikuje hapa kwetu kwani sitakuwamo
(ii) Basi la shule imeharibika moshi nyingi inatokea dirishani na maji
inatiririka ovyo

  

Answers


Kavungya
i) Usije hapa kwani sitakuwapo
Usije huku kwetu kwani sitakuwapo
Usije humu mwetu kwani sitakuwapo
ii) Basi la shule limeharibika, moshi mwingi unatokea dirisani na maji
yanatirika ovyo
Kavungya answered the question on June 27, 2019 at 07:49


Next: Andika katika kauli ya kutendesha (i) Nataka upike chakula hiki vizuri (ii) Toa ushuru wa forodhani
Previous: Bila kubadilisha maana, andika sentensi zifuatazo ukitumia kirejeleo cha ngeli kifaacho (i) Nyumbu alishinda farasi kukimbia (ii) Milango yote yajifunga ovyo, nenda uakafunge (iii) Hamisi amekata nyasi vizuri...

View More Kiswahili Questions and Answers | Return to Questions Index


Learn High School English on YouTube

Related Questions


  • Andika katika kauli ya kutendesha (i) Nataka upike chakula hiki vizuri (ii) Toa ushuru wa forodhani(Solved)

    Andika katika kauli ya kutendesha
    (i) Nataka upike chakula hiki vizuri
    (ii) Toa ushuru wa forodhani

    Date posted: June 27, 2019.  Answers (1)

  • Badilisha katika udogo kasha uukanushe udogo huo (i) Guu lake limepona baada ya kuumwa na jibwa la jijini (ii) Nyumba yenyewe ilijengwa bondeni karibu na mto(Solved)

    Badilisha katika udogo kasha uukanushe udogo huo
    (i) Guu lake limepona baada ya kuumwa na jibwa la jijini
    (ii) Nyumba yenyewe ilijengwa bondeni karibu na mto

    Date posted: June 27, 2019.  Answers (1)

  • Andika katika msemo wa taarifa Mzazi: Kesho nataka ufike nyumbani mapema, unasikia? Mtoto: Nitajaribu, lakini mwalimu alisema tutafanya mtihani jioni(Solved)

    Andika katika msemo wa taarifa
    Mzazi: Kesho nataka ufike nyumbani mapema, unasikia?
    Mtoto: Nitajaribu, lakini mwalimu alisema tutafanya mtihani jioni

    Date posted: June 27, 2019.  Answers (1)

  • Soma habari ifuatayo kisha ujibu maswali Vijana wengi wake kwa waume, walikuwa ndio tu wakamilishe shughuli ya kusajiliwa chuoni. Walikuwa bado nadhari zao zimetekwa na ugeni, hawajapata starehe...(Solved)

    Soma habari ifuatayo kisha ujibu maswali
    Vijana wengi wake kwa waume, walikuwa ndio tu wakamilishe shughuli ya
    kusajiliwa chuoni. Walikuwa bado nadhari zao zimetekwa na ugeni, hawajapata
    starehe akilini mwao wala kujisikia wamekaribia kama kwao nyumbani. Kwa hakika
    mazingira yale mapya yalikuwa yanawapa kiwewe kidogo au tuseme hata woga kiasi.
    Kusema kweli, kwa wakati ule walikuwa hawajui ni maisha ya namna gani
    yanayowasubiri mahali pale. Hawakuweza kukadiria kwa uyakinifu wowowtw iwapo
    makaazi yao pale ya miaka mine mizama kuanzia wakati ule, yangekuwa ya utulivu
    na raha au pengine yangeondokea kuwa ya roho juu juu na matatizo chungu mzima.

    Wamsubiri mkuu wa Chuo aingie wamsikize atakalosema, kisha ndipo waweze
    kubashiri vyema mkondo wa maisha yao utakavyokuwa. Lakini jinsi walivyosubiri
    Mkuu wa chuo aingie ukumbini ndivyo wayo wayo lao lilivyozidi kuwacheza shere.
    Waliwaza: Ugeni jamani kweli ni taabu. Mawazo mengi yaliwapitia bongoni mwao.
    Wakawa kinywa ukumbi mzima, kama kwamba wamekuja mazishini badala ya kuja
    kusoma. Waliwaza na kuwazua. Waliona au pengine walidhani kuwa hapa kila kitu
    ni tofauti.

    Wanafunzi hawa waliona tofauti nyingi kati ya mambo pale chuoni na yale
    waliyokuwa wameyazoea. Kwa mfano, mwalimu mkuu hapa hakuitwa ‘ headmaster’
    kama kule katika shule za msingi na vile shule za upili aliitwa ‘ vice – chancellor’
    Nyumba za kulala hazikuitwa ‘dormitory’ au ‘mabweni’, kama walivyozoea, bali
    ziliitwa ‘ halls’ kwa sababu sio kumbi za aina yoyote ile, bali ni nyumba hasa, zenye
    vyumba vya kulala, kama walivyozoea kita walipokiwa shule zao za upili huko, bali
    hapa wenyewe wenyeji waliita kwa majina mengine kabisa! Mara University, mara
    zutafindaki, mara Ndaki kwa ufupi, mara Jamahiri ya na kadhalika na kadhalika!
    Waliwaza: kweli mahali hapa wenyewe wenyeji waliita kwa majina mengine kabisa!
    Mara kumzubaisha mtu hadi kufikia kiwango cha kuonekana kama zuzu! Hata hivyo
    hawakuvunjika moyo, bali walipiga moyo konde wakanena kimoyomoyo: Potelea
    mbali! Ukiyavulia nguo, yaoge! Walikuwa wamo katika hali ya kurandaranda katika
    ulimwengu wa mawazo pale katika ulimwengu wao mpya, ulimwengu mwingine
    kabisa usioafanana hata chembe na ule waliouzoea, mkuu wa chuo alipoingia.

    Kuingia mkuu wa chuo wote walisimama kwa pamoja na kwa mijiko, wamekauka
    kama askari katika gwaride. Kuona hivyo, mkuu wa chuo akwaashiria wakae tu, bila
    kujisumbua. Kicheko kikawatoka bila kukosa adabu na heshima, kasha wakakaa kwa
    makini ndio mwanzo wakajisikia wamepoa.

    Kuona kuwa sasa wametulia na wamestarehe. Mkuu wa chuo akaanza kwa
    kuwaamkua kisha akawajulisha kwa wakuu wote wa vitivo mbali mbali na idara
    mbali mbali waliokuwa wamekaa pale jukwani alipo yeye upande huu na huu.

    Kufikia hapo, alaka ikawa imeungwa baina ya wenyeji na wageni wao. Kila mtu
    akaona mambo yamesibu tena; huo bila shaka ni mwanzo mwema, na kama
    ilivyosemwa na wenye busara, siku njema huonekana asubuhi. Hii, Kwa wote ndiyo
    asubuhi tu, bali ni asubuhi njema, si haba.

    (a) Ukirejelea aya ya kwanza na ya pili, eleza wasiwasi wanafunzi waliokuwa nao
    wakati wakisubiri (maneno 45- 55)
    (b) Ni mambo gani mageni wanafunzi hawakuyazoea yanayoelezwa katika kifungu
    (maneno 25 – 30)
    (c) Bila kubadilisha maana, fupisha aya tatu za mwisho kwa kutumia maneno yako
    mwenyewe. Tumia maneno 40 -45

    Date posted: June 27, 2019.  Answers (1)

  • UFAHAMU Soma habari ifuatayo kisha ujibu maswali Binadamu kwa wakati huu amemaka kwa sababu amechafua mazingira yake pasipo tahadhari. Mathalani insiya amejaza gesi za sumu zitokazo viwandani na...(Solved)

    UFAHAMU
    Soma habari ifuatayo kisha ujibu maswali
    Binadamu kwa wakati huu amemaka kwa sababu amechafua mazingira yake pasipo
    tahadhari. Mathalani insiya amejaza gesi za sumu zitokazo viwandani na hata kuchafua
    mito kutokana na maji machafu kutoka viwanda hivyo. Takataka zinazotupwa ovyo
    ovyo zinarundikana kila mahali. Isitoshe miti inakatwa vivyo hivyo bila simile. Matokeo
    ya haya yote ni kwa mfano tunapata mvua ya asidi ambayo huhasiri mimea. Aidha nao
    ukanda wa ozoni unaotukinga dhidi ya miali hatari kutoka kwa jua umeharibiwa tayari na
    hivyo kuongeza joto duniani. Sehemu nyingi zimeanza kugeuka na kuwa jangwa huku
    sehemu zingine zikifurika kwa maji ya mito na mvua. Maji haya yameanza kumeza
    visiwa vingi vilivyo baharini. Kutokana na madhara haya, binadamu sasa anatapatapa ili
    kutafuta makao kwingine kwenye salama. Ndiposa siku hizi nadhari za binadamu
    zimeelekezwa katika mawanda mengine nje kabisa ya kisayari hiki kidogo kiitwacho
    dunia.

    Kwa miaka mingi sasa binadamu amekuwa akitafakari uwekano wa kuishi katika sayari
    nyingine. Hii ndiyo sababu mwaka wa 1969 waamerika walimkanyagisha binadamu wa
    kwanza kabisa mwezini. Lengo lilikuwa ni kutalii na kuchunguza uwekano wa binadamu
    kuishi huko ili wale watakaoweza wahamie huko, hata mimea. Mwezini ni vumbi tupu
    lisiloota chochote. Kipatikanacho kwa wingi sana ni madini tu ambayo hayawezi kufaidi
    binadamu kwa lolote.

    Sayari nyingine alizozitalii binadamu ni Zuhura, Mirihi, Mushtara na tuseme karibu zote
    zinazolizunguka jua. Kilichogunduliwa ni kuwa upo uwezekano wa sayari kama Zuhura
    na pengine Mirihi kuwa na mvua, lakini nyingi mno isiyoweza kuruhusus mimea kukua.
    Sit u, zuhuria inasemekna kuwa joto sana wakati wa mchana ilhali Mirihi ni baridi sana
    siku zote; baridi kiasi cha kuuwa binadamu na wanyama hawawezi kuishi huko.
    Mushtara yasemekana kuwa joto ajabu, ambapo hizo sayari nyingine zina joto sana au
    zina baridi sana. Habari hii imemfunga binadamu katika jela ya kijisayari chake kiki
    hiki kiitwacho dunia anachokichafua uchao.

    Je, binadamu amekata tama? Hata kidogo! Ndio mwanzo anajaribu sana kuzikata pingu
    alizofunzwa na maumbile. Vipi? Amejaribu kuchunguza uwezekano wa kuihama ardhi
    na kuishi baharini, kwa sababu bahari inazidi ardhi mara tatu kwa ukubwa. Na ni vipi
    binadamu anadhani anaweza kuishi baharini mahali ambapo hakuumbwa aishi humo
    kama samaki?
    Jawabu ni kuwa angefanya hivyo kwa kutumia maarifa yake.

    Binadamu anaamini kabisa kuwa ana uwezo wa kujenga miji mikubwa mikubwa humo
    humo baharini… mikubwa zaidi yah ii tuliyo nayo ardhini. Anaamini ya kuwa anaweza kuitawala bahari kiasi alichitawala ardhi, na hivyo basi kufanya bahari impe
    makao na kumlisha bila ya kuyabadilisha maumbile yake. Na iwapo hili halitawezekana
    basi, ikiwajibika, abadilishe maumbile yake kwa kujiunda mashavu kwa mfano, ili avute
    pumzi ndani ya maji

    Njia ya pili ya kuepukana na pingu za maumbile ni kuishi angani. Hii ina maana ya
    kujenga miji iliyoelea angani, kama madungu vile. Na kwa vile anga haina kikomo,
    binadamu atakuwa amejipatia visayari vyake visivyo idadi ingani!

    Njia ya tatu ni kubadilisha umbo lake ili asihasirike na joto wala baridi. Binadamu wa
    kisasa anaamini kuwa inawezekana kumuunda upya mtu katika maabara badala ya katika
    mamba.
    Mtu huyu wa maabra, aitwaye ‘cyborg’ kwa lugha ya Kiingereza, anaweza kuwa na
    chuma ndani badala ya mifupa, na mwili wa kawaida wa udongo na maji nje.

    Kiunde huyu atakuwa hadhuriki ovyo ovyo kama binadamu wa sasa aliyeumbwa kwa
    chumvi, maji na protini. Au bora zaidi, binadamu mpya wa maabarani aundwe kwa
    zebaki. Binadamu huyu wa zebaki hafi wala hakatikikatiki. Na iwapo atakatika vipande
    vipande, basi kama zebaki hivyo vitaundika tena upya na kumrudishia umbo la awali
    kamili.

    Njia nyingine ya kuepukana na uangamizi ni kutumia viunde vyake vya electroniki kama
    vile tarakilishi yaani kompyuta, na mitambo mingine kama iyo. Binadamu anaamini
    kwamba uwezo wa vyombo hivi utakapokamilishwa, basi vitamsaidia kwa lolote lile.

    (a) Inasemekana kwamba binadamu anakichafua hiki kisayari chake kila uchao.
    Kwa kutumia mifano mitatu, eleza vile binadamu amechafua mazingira yake.
    (b) Kwa nini ongezeko la joto limeleta jangwa duniani wa wakati huo huo likaleta
    mafuriko?
    (c) Eleza sababu mbili zinazomfanya binadamu kuhangaika na kutafuta makao
    kwingine
    (d) Ni mambo gani yanayomfunga binadamu katika ardhi. Taja mawili
    (e) Unadhani ni kwa nini madini mengi yaliyoko mwezini hayaletwi duniani.
    Taja na ufafanue sababu mbili
    (f) Kulingana na aya mbili za mwisho, eleza jambo ambalo binadamu anajaribu
    kukwepa
    (g) Eleza maana ya maneno yafuatayo kama yalivyotumika katika kifungu
    (i) Mashavu
    (ii) Madungu
    (iii) Asihasirike
    (iv) Kiunde

    Date posted: June 27, 2019.  Answers (1)

  • Mtu akicheza mchezo mahali Fulani tunaweza kusema alichezea hapo Ukifuata mfano huu, tumia vitenzi vilivyoko katika mabao kukamilisha (i) Ali hapo (la) (ii) Ali hapo (fa) (iii) Ali hapo...(Solved)

    Mtu akicheza mchezo mahali Fulani tunaweza kusema alichezea hapo
    Ukifuata mfano huu, tumia vitenzi vilivyoko katika mabao kukamilisha
    (i) Ali hapo (la)
    (ii) Ali hapo (fa)
    (iii) Ali hapo (oa)

    Date posted: June 27, 2019.  Answers (1)

  • Eleza matumizi ya ‘Po’ katika sentensi hii Nilipofika nilimwona pale alipokuwa amesimama(Solved)

    Eleza matumizi ya ‘Po’ katika sentensi hii
    Nilipofika nilimwona pale alipokuwa amesimama

    Date posted: June 27, 2019.  Answers (1)

  • Andika katika msemo wa taarifa “Nitakuwa nikija hapa kila siku kukuona”, Kamau alimwambia shangazi yake(Solved)

    Andika katika msemo wa taarifa
    “Nitakuwa nikija hapa kila siku kukuona”, Kamau alimwambia shangazi
    yake

    Date posted: June 27, 2019.  Answers (1)

  • Andika katika msemo halisi Mvulana alimwambia baba yake kuwa alitaka kwenda sokoni(Solved)

    Andika katika msemo halisi
    Mvulana alimwambia baba yake kuwa alitaka kwenda sokoni

    Date posted: June 27, 2019.  Answers (1)

  • Kutokana na vitenzi tunaweza kuunda majina na pia kutokana na majina tunaweza kuunda vitenzi. Mfano Jina ...(Solved)

    Kutokana na vitenzi tunaweza kuunda majina na pia kutokana na majina
    tunaweza kuunda vitenzi. Mfano
    Jina Kitendo
    Mwuzaji Uza
    Mauzo Uza
    Wimbo Imba

    Sasa kamilisha:
    Jina Kitenzi
    (i) Mnanda
    (ii) Kikomo
    (iii) Ruhusa
    (iv) ashiki
    (v) husudu

    Date posted: June 27, 2019.  Answers (1)

  • Tunasema: Mtoto huyu mzuri anapendeza Ukitumia majina yafuatayo kamilisha sentensi ukifuata mfano ulio hapo juu (i) Ngome (ii) Mitume (iii) Heshima (iv) Ng’ombe (v) Vilema(Solved)

    Tunasema: Mtoto huyu mzuri anapendeza
    Ukitumia majina yafuatayo kamilisha sentensi ukifuata mfano ulio hapo juu
    (i) Ngome
    (ii) Mitume
    (iii) Heshima
    (iv) Ng’ombe
    (v) Vilema

    Date posted: June 27, 2019.  Answers (1)

  • Eleza kazi ifanywayo na (i) Mhariri (ii) Jasusi(Solved)

    Eleza kazi ifanywayo na
    (i) Mhariri
    (ii) Jasusi

    Date posted: June 27, 2019.  Answers (1)

  • Akifisha kifungu kifuatacho Bwana mwenyekiti wetu wa leo wazazi wote na hata wanafunzi leo ni siku muhimu je mngependa niwafahamishe msaada tuliopokea kutoka kwa wizara ya elimu(Solved)

    Akifisha kifungu kifuatacho
    Bwana mwenyekiti wetu wa leo wazazi wote na hata wanafunzi leo ni siku
    muhimu je mngependa niwafahamishe msaada tuliopokea kutoka kwa wizara ya
    elimu

    Date posted: June 27, 2019.  Answers (1)

  • Fafanua maana za misemo ifuatayo kwa kuitungia sentensi (i) Kula uyundo (ii) Kula uhondo(Solved)

    Fafanua maana za misemo ifuatayo kwa kuitungia sentensi
    (i) Kula uyundo
    (ii) Kula uhondo

    Date posted: June 27, 2019.  Answers (1)

  • Andika sentensi zifuatazo ukitumia kinyume cha neno lililoandikwa kwa herufi za Mlazo (i) Usijaribu kupaaza sauti unapoimba (ii) Huyu ni mtu mwenye busara (iii) Binadamu hawezi kumuumbua mwenzake(Solved)

    Andika sentensi zifuatazo ukitumia kinyume cha neno lililoandikwa kwa herufi za
    Mlazo
    (i) Usijaribu kupaaza sauti unapoimba
    (ii) Huyu ni mtu mwenye busara
    (iii) Binadamu hawezi kumuumbua mwenzake

    Date posted: June 27, 2019.  Answers (1)

  • Eleza maana ya sentensi hizi (i) Mikono yao imeshikana (ii) Mikono yao imeshikamana(Solved)

    Eleza maana ya sentensi hizi
    (i) Mikono yao imeshikana
    (ii) Mikono yao imeshikamana

    Date posted: June 27, 2019.  Answers (1)

  • Sahihisha makosa yaliyomo katika sentensi mbili zifuatazo (i) Bei za vitu zimepanda juu sana siku hizi (ii) Weka mizigo kwa gari(Solved)

    Sahihisha makosa yaliyomo katika sentensi mbili zifuatazo
    (i) Bei za vitu zimepanda juu sana siku hizi
    (ii) Weka mizigo kwa gari

    Date posted: June 27, 2019.  Answers (1)

  • Soma habari ifuatayo kisha ujibu maswali Mababu walituachia msemo maarufu kuwa “ Kuzaa sio kazi. Kazi kubwa ni kulea.” Busara iliyomo katika methali hii inatupambazukia peupe pindi...(Solved)

    Soma habari ifuatayo kisha ujibu maswali
    Mababu walituachia msemo maarufu kuwa “ Kuzaa sio kazi. Kazi kubwa ni kulea.”
    Busara iliyomo katika methali hii inatupambazukia peupe pindi tukianza kuchunguza
    maisha ya vijana wa siku hizi katika jamii zote, hasa zile za Afrika. Kwa upande
    mmoja, maisha ya vijana hawa yanaonyesha cheche ya matumaini kwa maisha ya siku
    za usoni kwa sifa zao za mori na kupenda kujaribu na kushika mambo upesi kama
    sumaku. Lakini kwa upande wa pili, tunashuhudia upotevu wa kimawazo na hulka
    ambayo ndiyo kipingamizi cha kuendelea kwao kama raia wa kutegemewa.

    Kuwanyeshea vijana lawama na kashifa za kila aina hakufai wala hakufui dafu katika
    juhudi za kuwaongoza na kuwalea. Kwa hili hatuna budi kusadiki, “mtoto umleavyo
    ndivyo akuavyo.” Basi hivyo badala ya kuwashambulia vijana wenyewe. Tutafanya
    hivyo kwa imani kuwa “mwiba uchomeako ndiko utokeako.” Kiini cha matatizo ya
    vijana wa leo ni namna ya mwongozo na vielezo wanavyopokea kutoka kwa wazazi,
    waalimu, viongozi wa kijamii wakiwemo pia wale wa medhehebu tofauti na hasa kutokana na vyombo tofauti vya habari: vitabu majarida, filamu, magazeti na
    kadhalika.

    Jamii ina haki gani kuwashtumu vijana iwapo mzazi, tangu utotoni mwao
    amewahubiria maji na huku mwenyewe anakunywa mvinyo? Kama fasihi na
    maandishi mengine wanayoyabugia vijana yamejazwa amali, picha, jazanda na taswira
    zinazohimidi ugeni na kutweza Uafrika, tutashangazwa na nini pale vijana
    watakapoanza kupania zile zile amali za ugenini? Iwapo jamii na mazingira
    wanamokulia vijana yanatukuza kitu kuliko utu. Hatupaswi kupepesa macho na
    kukonyeza tunapowaona vijana wakihalifu sheria zote kwa tamaa ya kujinufaisha binafsi.

    Ni hoja isiyopingika kuwa kulea sio tu kulisha na kuvisha au kumpeleka mtoto
    shuleni sharti itambulike wazi wazi kuwa sehemu kubwa ya elimu na mwongozo
    unaoathiri mienendo ya jijana na watoto haitokani na yale waambiwayo bali hasa yote
    wanaoyashuhudia kwa macho na hisia zao.

    (a) Katika aya ya kwanza, maisha ya vijana wa kisasa yameelezwaje?
    (b) Kwa nini vijana hawapaswi kulaumiwa kulingana na mwandishi
    Maneno 30 – 35
    (c) Eleza sifa za malezi bora
    (Maneno 20 – 25)

    Date posted: June 27, 2019.  Answers (1)

  • Soma makala yafuatayo Kisha Ujibu Maswali Zamani sana na hata hivi karibu watu wengi kote duniani walikuwa wakiamini kuwa kuna ardhi na mbingu tu basi. Imani hii...(Solved)

    Soma makala yafuatayo Kisha Ujibu Maswali
    Zamani sana na hata hivi karibu watu wengi kote duniani walikuwa wakiamini kuwa
    kuna ardhi na mbingu tu basi. Imani hii ilijikita katika mantiki inayosema kwamba
    ardhi au dunia ipo katikati ya maumbile yote na isitoshe, ni tambarare.

    Juu ya ardhi ni mbingu ambayo imejaa vimulimuli vidogovidogo sana viitwavyo nyota.
    Baina ya vimulimuli vipo viwili vikubwa viitwavyo mwezi na jua. Hivi viwili japo ni
    vikubwa kuliko vingine, bado ni vidogo kuliko ardhi.

    Hii ndiyo imani iliyoutawala ulimwengu kwa miaka na miaka, na ikawa imekita mizizi.
    Lakini jinsi wanajimu walivyozidi kuelimika, waligundua kwamba ukweli wa mambo
    umejitenga kando kabisa na imani hii

    Ukweli ni kwamba zima tulionalo la rangi ya samawati nusumviringo juu ya paa zetu za
    vichwa ni kubwa sana tena. Na si kubwa tu bali lazidi kupanuka. Katika bwaka hili
    lipanukalo kila uchao mna galaksi nyingi ajabu zisizokadirika. Ndani ya kila galaksi
    mna nyota mamilioni na mamilioni, malaki na kanui. Imejulikana kuwa nyota hizo japo
    huonekana kama vimulimuli vidogo sana usiku usiku ni kubwa ajabu. Kadiria
    mwenyewe! Jua letu ni nyota kubwa sana. Ukubwa wake umezidi wa dunia mara
    nyingi sana, zaidi ya elfu moja! Basi fikiria juu ya ukubwa wote huo. Imegunduliwa ya
    kwamba jua ni nyota ndogo sana ikilinganishwa na zingine zilizo katika galaksi yetu tu,
    licha ya galaksi nyinginezo zilizoko katika bwaka.

    Na haya sio maajabu peke yake. Wataalam wamevumbua mengi ya kushangaza zaidi.
    Mathalan, imekuja kufahamika kuwa jua letu ambalo ni nyota, lina sayari tisa
    zinazolizunguka. Baadhi ya sayari hizi ni Arthi yetu. Zaibaki, Zuhura, Mirihi, na mshitara
    baina ya tisa jumla. Baadhi ya sayari hizi zina visayari vidogo vinavyozizunguka.
    Visayari hivi ndivyo viitwavyo miezi. Ardhi yetu ina mwezi miwili ilhali Mshitara ina
    kumi na miwili! Sayari hizi zote na visayari vyao, au vitoto ukipenda, havitoi mwanga.
    Nuru ya mwezi na nuru ya hizo sayari zinazolizunguka jua letu inatokana na jua
    lenyewe. Kwa hakika ni mmeremeto tu unaotufikia sisi kupitia sayari hizi kutoka kwa
    nyota hii yetu iitwayo JUA.

    Kama wasemavyo washahili ya Mungu ni mengi. Taswira tuliyo nayo katika maelezo
    haya yaonyesha jinsi ambavyo mwanadamu licha ya kuwa na akili nyingi, bado
    hajawahi kuigusia siri kamili ya mungu. Lakini kwa ufupi twaweza kusema hivi. Ikiwa
    katika bwaka lote kuna galaksi nyingi, bila shaka kwa vile jua ni nyota basi zimo sayari
    nyingi ajabu zinazozunguka kila nyota au jua kama zipasavyo kuitwa. Kwa vile katika
    mfumo- jua imo sayari moja yenye viumbe vyenye uhai, binadamu wakiwemo, basi
    bila shaka katika mifumo- jua mingine katika galaksi yetu zipo sayari zinazofanana na ardhi hii yetu, ambazo sina viumbe vilivyo hai- penginepo watu pia! Wanona maajabu?
    Na katika magalaksi mengine je? Mambo pengine ni yayo hayo! Kwa hivyo huenda
    ikawa peke yetu katika bwaka hili; labda tuna viumbe wenzetu ambao hatutakutana nao
    katika uhai wetu kwa sababu uwezo wetu wa kimaumbile, na vile kisayansi ni hatifu.
    Lakini, kwa vile mwenye kupanga maajabu hayo yote, yaani Mwenyezi Mungu ni
    huyo mmoja basi huenda sote tukakutana Ahera.
    Mungu ni mkubwa

    (a) Kulingana na habari hii, taja mambo manne ambayo ni imani potovu
    (b) Kwa kusema “ ukweli wa mambo umejitenga kando” Mwandishi anamaanisha
    nini?
    (c) Taja sifa zozote nne za maumbile ya anga zinazopatikana katika habari hii
    (d) Taja vitu viwili vipatikanavyo katika galaksi
    (e) Taja sayari mbili ambazo ni kubwa kuliko ardhi
    (f) Ni ithibati gani iliyotolewa kuonyesha kuwa nyota sio vijataa vidogo?
    (g) Bainisha nuru aina mbili tuzionazo angani
    (h) (i) Ni neno gani lenye maana sawa na “anga” ama “upeo” katika habari hii?
    (ii) Andika neno moja ambalo lina maana sawa na paa kama lilivyotumiwa
    katika taarifa
    (i) Mwandishi anaposema kuwa katika magalaksi mengine “mambo pengine ni yayo
    hayo” anamaanisha nii?

    Date posted: June 27, 2019.  Answers (1)

  • Akifisha kifungu kifuatacho “Baba Wafua, ona Barua iliyotoka kwa mwanao. Hata hati haisomeki” “lo” baba watoto akamaka. Hii barua kweli imetoka kwa mwanangu Wafua. “Waniuliza mimi?” Mama akamjibu...(Solved)

    Akifisha kifungu kifuatacho
    “Baba Wafua, ona Barua iliyotoka kwa mwanao. Hata hati haisomeki” “lo” baba
    watoto akamaka. Hii barua kweli imetoka kwa mwanangu Wafua. “Waniuliza
    mimi?” Mama akamjibu “Tazama maandishi na anwani basi. Shule ya Msingi ya
    Barungani S.L.P 128 Vuga.”

    Date posted: June 27, 2019.  Answers (1)