Get premium membership and access questions with answers, video lessons as well as revision papers.

Tumia viunganishi vingine badala ya vile vilivyotumiwa katika sentensi hizi: (i) Anayetafuta hachoki hata akichoka keshapata (ii) Ngonjeeni hadi washiriki wote wafike

      

Tumia viunganishi vingine badala ya vile vilivyotumiwa katika sentensi hizi:
(i) Anayetafuta hachoki hata akichoka keshapata
(ii) Ngonjeeni hadi washiriki wote wafike

  

Answers


Kavungya
i) Na
ii) Mpaka au hata
Kavungya answered the question on June 27, 2019 at 08:19


Next: Taja madini mawili ambayo yametukuzwa zaidi, moja kwa thamani yake ya kifedha na nyingine kwa kutengeneza vyuma vigumu kuliko madini mengine
Previous: Watu wafuatao wanafanya kazi gani (i) Mhasibu (ii) Mhazili

View More Kiswahili Questions and Answers | Return to Questions Index


Learn High School English on YouTube

Related Questions


  • Taja madini mawili ambayo yametukuzwa zaidi, moja kwa thamani yake ya kifedha na nyingine kwa kutengeneza vyuma vigumu kuliko madini mengine(Solved)

    Taja madini mawili ambayo yametukuzwa zaidi, moja kwa thamani yake ya
    kifedha na nyingine kwa kutengeneza vyuma vigumu kuliko madini mengine

    Date posted: June 27, 2019.  Answers (1)

  • Onyesha kielezi, kivumishi, kitenzi na jina katika sentensi: Watu wane walipeperushwa juu kwa juu na upepo mkali(Solved)

    Onyesha kielezi, kivumishi, kitenzi na jina katika sentensi:
    Watu wane walipeperushwa juu kwa juu na upepo mkali

    Date posted: June 27, 2019.  Answers (1)

  • Akifisha kifungu hiki: Nilopomwendea aliniangalia kisha akaniambia siamini kuwa ni wewe uliyeandika insha hii.(Solved)

    Akifisha kifungu hiki:
    Nilopomwendea aliniangalia kisha akaniambia siamini kuwa ni wewe uliyeandika
    insha hii.

    Date posted: June 27, 2019.  Answers (1)

  • Soma makala haya kisha ujibu maswali yanayofuata Lugha ya Kiswahili ni lugha iliyoendelea sana. Leo hii lugha hii inasema na watu wote nchini Tanzania, Rwanda na Burundi,...(Solved)

    Soma makala haya kisha ujibu maswali yanayofuata
    Lugha ya Kiswahili ni lugha iliyoendelea sana. Leo hii lugha hii inasema na watu wote
    nchini Tanzania, Rwanda na Burundi, inasemwa na watu wote nchini Kenya. Nchini
    Uganda, Zaire, Malawi, msumbiji, Zambia, Somalia, Bukini (Madagascar) na Ngazija
    (Comoro), inasemwa na asilimia kubwa za wananchi wa huko. Aidha lugha hii ina
    wasemaji si haba katika kisiwa cha Sokta na nchini Oman.

    Fauka ya maendeleo haya, Kiswahili kinatumika kwa minajili ya matangazo ya habari
    katika idhaa nyingi za mashirika ya habari ulimwenguni. Nchi zenye idhara za Kiswahili
    ni kama vile hizi zetu za Afrika ya Mashariki na kati, Afrika ya kusini, Nigeria, Ghana,
    Uingereza, ( shirika la B.B.C) Marekani ( shirika la V.O.A), Ujerumani ( shirika la
    Radio Deutch Welle, Cologue), Urusi ( Radio Moscow), China, India na kadhalika.

    Maendeleo mengine yanapatikana katika upande wa elimu, Marekani peke yake, kuna
    vyuo zaidi ya mia moja vinavyofundisha Kiswahili kama lugha muhimu ya kigeni. Huko
    Uingereza vyuo kama London, Carmbridge na Oxford vinafundisha lugha hii. Nci
    nyingine ambazo zina vyuo vinavyofunza lugha ya Kiswahili ni kama vile Japan, Korea,
    Ghana, Nigeria na kadhalika

    Kweli Kiswahili kimeendelea jamani. Lakini je, kilianza vipi? Na ilikuwaje kikaweza
    kupiga hatua hizi zote?
    Kiswahili kilianza kuzungumzwa na kabila dogo la watu waliokuwa wakiitwa wangozi.
    Watu hawa walikuwa wakiishi mahali palipoitwa shumgwaya. Shungata ni nchi ya
    zamani iliyokuwa eneo lililoko katika nchi katika nchi mbili jirani ambazo siku hizi ni
    Kenya na Somalia. Kabila hili la wangozi iliishi irani na makabila mengine kama vile
    wajikenda, wapokomo, Wamalakote ( au Waelwana) na Wangazija ( kabla hawajahamia
    visiwa vya Ngazija) Lugha ya wangozi siku hizo, ambayo ndiyo mzazi wa Kiswahili
    cha leo, ilijulikana kwa jina kingozi. Kama ilivyosemwa hapo awali, kingozi kilisemwa
    na watu wachache sana.

    Je lugha hii ilikuwaje mpaka ikapata maendeleo haya makubwa tunayoyashuhudia siku
    hizi? Ama kwa hakika, Kiswahili ni lugha iliyobahatika tu. Inaweza kusemwa kwamba
    lugha hii ilipendelewa na mazingira na historia.

    Jambo la kwanza, wageni waliotoka mashariki ya kati kifukia hizi janibu zetu Afrika ya
    mashariki walikaribishwa vizuri na hawa wangozi. Wakaingilia wageni na wenyeji
    kindakindaki, kidini, kitawala, kibiashara na kitamaduni kwa jumla. Punde si punde
    wangozi, ambao baadaye walijulikana kama waswahili na wageni hawa, wakaelimika
    katika dini (ya kiisilamu), biashara na mambo ya utawala aina mpya. Lugha yao nayo
    ikapanuka pale ilipochukua msamiati ya kigeni hususan wa Kiarabu na Kiajemi na
    kuufanya uwe wake, ili kueleza kwa rahisi zaidi mambo haya mageni katika taaluma za
    dini, biashara, siasa na hata sayansi kama vile unajimu. Wakati huo, lugha ya Wangozi
    sasa ikaitwa Kiswahili wala sio kiangozi. Tatizo hapa ni kuwa kwa vile Kiswahili
    kilichukua msamiati mwingi wa kigeni ili kuelezea taaluma hizi mpya, baadaye kimekujashukiwa kwamba ni lugha ya kigeni ilhali ni lugha ya Kiafrika asilia, na kitovu
    chake ni nchi mpya za kiafrika ziitwazo Kenya na Somalia hii leo.

    (a) Thibitisha kuwa Kiswahili kimekuwa lugha ya kimaitaifa ( maneno 35 – 40)
    (b) Eleza kwa ufupi asili ya Kiswahili hadi kuja kwa wageni ( maneno 20 – 25)
    (c) Ukitumia maneno yako mwenyewe, eleza ujumbe uliomo katika aya ya mwisho

    Date posted: June 27, 2019.  Answers (1)

  • Soma makala yafuatayo kisha ujibu maswali yanayofuata Kuna sayansi mpya inayoitwa “cloning” kwa lugha ya Kiingereza. Pengine kwa sasa tuite “kutumbisha.” Sayansi hii tayari imeleta mapinduzi makubkwa...(Solved)

    Soma makala yafuatayo kisha ujibu maswali yanayofuata
    Kuna sayansi mpya inayoitwa “cloning” kwa lugha ya Kiingereza. Pengine kwa sasa tuite
    “kutumbisha.” Sayansi hii tayari imeleta mapinduzi makubkwa katika uzalishaji mimea
    na uvunani. Imesemekana ya kwamba, ghairi ya wivu na kijicho baina ya jamii
    mbalimbali ulimwenguni, aina hii ya sayanzi ina uwezo na kuangamiza kabisa janga la
    njaa katika sayari hii yetu. Kivipi? Rahisi kabisa. Ni kwamba mbegu moja tu ya aina
    yoyote ya mmea, baada ya kuneemeshwa vyumba vyake vidogo ambavyo ndivyo hasa
    msingi wa uhai vinaweza kunyunyiziwa dawa maalum ili vitawanyike mara hata
    mamilioni na kuwa mimea kamili…. Mamilioni!

    Sayansi hii tarari inatumiwa kukuza viazi na vyakula vingine. Hii ina maana ya kwamba
    mashamba makubwa si muhimu siku hizi, yaani vyakula vingi kabisa vinaweza kukuzwa
    mahali padogo sana. Kwa hivyo hivi karibuni tu, kutakuwa hakuna haja ya kupigania
    mashamba.

    Vyema. Hebu sasa tuangalie zilizokwishapigishwa hii sayansi ya “kutumbisha” na mahali
    binadamu alipofika kimaendeleo kwa sababu ya hatua hizo. Jambo la kwanza sayansi hii
    tayari imeshatumiwa kuzalishia wanyama wengi, wengi sana wadogo wadogo kwa lengo
    la kuendeleza mbele utafiti. Kufikia sasa, wanyama hawa waliotengenezwa na binadamu
    katika maabara yake bado wanahifadhiwa mumo humo walimotengenezwa. Hii ni hatua
    kubwa na binadamu anastakili pongezi kwa jinsi anayotumia akili yake kuvumbua ibura
    hizi zote.

    Hata hivyo imesemwa kwamba kuchamba kwingi ni kuondoa mavi. Binadamu kama
    ijulikanavyo, anajaribu sana jujitakasa kwa kujitenga mbali sana na asili yake ya unyama
    ili aufikie ubinadamu mkamilifu. Hapana ubaya hapo. Lakini tukirudi nyuma tunakuta ya
    kwamba binadamu sasa aneingia tama kubwa sana kuliko wakati wowote ule. Tamaa hii
    imeletwa na ujuzi wake katika sayansi hii ya “kutumbisha.” Sasa binadamu ana jua
    vizuri sana kwamba kwa vile ana ujuzi wa kutengeza panya na hata kondoo katika
    maabara basi hata ujuzi wa kutengeneza binadamu pia anao! Na hapo ndipo tatizo lilipo.
    Swali hi hili: Je, ujuzi huu utatufikisha wapi? Na kikomo chake kitakuwaje?

    Binadamu sasa ujuzi wake unamtia wasiwasi. Wataalam wa sayansi hii wamejiuliza mara
    nyingi nini kitakachotokea ujuzi huu utakapomilikiwa na mwenda wazimu mweledi.”
    Watu kadha wa kadha, miongoni mwao wakiwa wanasiasa wamejiuliza mara
    zisizohesabika swali hili: kama Hitler angekuwa na ujuzi huu, angekuwa na lazima gani
    ya kuwaulia mbali wayahudi milioni sita wasiokuwa na hitia isipokuwa na nywele
    nyeusi na hawakuwa weupe sana kama wazungu? Hitler aliamini ya kwamba “mtu
    mzuri” ni mwenye pua ya upanga (kama mzungu), macho ya buluu nywele rangi ya dhahabu na mwenye kimo cha futi sita au zaidi kidogo. Hivyo lengo lake lilikuwa ni
    kubuni taifa la watu wazuri pekee ambao mwisho watautawala ulimwengu na kuenea
    duniani kote. Katika mpango wake, watu weusi wote wangefaa kuangamizwa tu ili watoe
    nafasi kwa watu aliowaona yeye kuwa bora.

    Sasa baada ya sayansi hili ya “kutumbisha” kuvumbuliwa, wataalam wametishika sana.
    Wamewaza jinsi ambavyo Hitler angeweza kufanya kama angekuwa mjuzi wa taaluma
    hiyo.

    Kitisho hiki kimezidi kuwatwanga wataalam na wasiokuwa wataalam hivi majuzi tu
    ilipogunduliwa maiti ya msichana wa miaka kumi na mine huko milima ya Andes,
    Amerika ya kusini. Msichana huyo alikuwa ametolewa kafara miaka karne tano zilizo
    pita lakini hakuoza kwa sababu ya baridi kali ya barafu milimani.

    Kwa sababu ya dukuduku la uvumbuzi ambalo haliishi dhana za kiajabu ubongo wa
    binadamu, wataalamu wa “kuchezea” maumbile walipomwona msichana huyo maiti,
    upesi upesi wakampima. Walipofanya hivyo wakagundua ya kwamba mayai yake ni
    timamu kabisa wala hayajaharibiwa na mpito wa karne. Papo hapo wengine wakajiwa na
    wazo la kuyatoa mayai hayo na kuyahifadhi kwenye mabara. Tamaa ikazidi zaidi ya
    zaidi. Baadhi ya wataalamu wakajiwa na wazo la “kuyaneemesha” mayai hayo na mbegu
    za uzazui za wanaume. Kwa lengo gani? Kuunda watoto amabo mama yao alikufa
    zamani za kale ili waonekane watakuwa watu wa aina gani!

    Sasa fikiria mwenyewe! Watoto hawa wa maabara wakiwa weledi zaidi ya binadamu
    yeyote yeyote wa kisasa lakini watiifu kama mbwa na paka itakuwaje? Hakuna
    atakayefikiria “kutumbisha” ili tuwe na vijitumwa vyetu vipenzi majumbani mwetu
    vinavyofanana nasi badala ya paka na mbwa wasiovishwa nguo?

    (a) Andika kichwa kifaacho kwa nakala hii
    (b) Kutumia sayansi ya “kutumbisha” kunaweza kumsaidia binadamu kuangamiza
    mabaa gani mawili yanayomkabili sasa?
    (c) Unadhani ni kwa nini wanyama waliozalishwa kwa kutumia sayansi hii bado
    wamo maabarani?
    (d) Fafanua methali “kuchamba kwingi nikuondoka na mavi” kulingana na muktadha
    wa habari hii
    (e) Kuna ubaya gani kutumbisha watu?
    (f) Mwandishi anaonekana kutishwa sana na uwezekano wa sayansi ya kutumbisha
    kuishia mikononi mwa “wendawazimu weledi” kwani kuna hatari gani?
    (g) Eleza kwa ukamilifu matatizo yanayoweza kuukumba ulimwengu iwapo mayai ya
    msichana wa Andes yatatumbishwa

    Date posted: June 27, 2019.  Answers (1)

  • Bila kunyambua, andika maneno mawili ambayo yanatokana na shina moja na neno: imani(Solved)

    Bila kunyambua, andika maneno mawili ambayo yanatokana na shina
    moja na neno: imani

    Date posted: June 27, 2019.  Answers (1)

  • Tunga sentensi ya neno moja ambayo ina visehemu vifuatavyo vya sarufi - Kiima - Wakati - Kirejeleo - Kiswahili kitendwa - Kitenzi(Solved)

    Tunga sentensi ya neno moja ambayo ina visehemu vifuatavyo vya
    sarufi
    - Kiima
    - Wakati
    - Kirejeleo
    - Kiswahili kitendwa
    - Kitenzi

    Date posted: June 27, 2019.  Answers (1)

  • Mahali palipohamwa panaitwa?(Solved)

    Mahali palipohamwa panaitwa?

    Date posted: June 27, 2019.  Answers (1)

  • Eleza maana mbili mbili zinazotokana na sentensi zifuatazo (i) Mtoto alitimua mbio, kuona nyoka (ii) Juma alifagia chakula (iii) Sisikii vizuri(Solved)

    Eleza maana mbili mbili zinazotokana na sentensi zifuatazo
    (i) Mtoto alitimua mbio, kuona nyoka
    (ii) Juma alifagia chakula
    (iii) Sisikii vizuri

    Date posted: June 27, 2019.  Answers (1)

  • Andika methali nyingine ambayo maana yake ni kinyume cha Riziki kama ajali huitambui ijapo(Solved)

    Andika methali nyingine ambayo maana yake ni kinyume cha
    Riziki kama ajali huitambui ijapo

    Date posted: June 27, 2019.  Answers (1)

  • Eleza maana ya misemo ifuatayo kwa kuitungia sentensi moja moja Kuramba kisogo Kuzunguka mbuyu(Solved)

    Eleza maana ya misemo ifuatayo kwa kuitungia sentensi moja moja
    Kuramba kisogo
    Kuzunguka mbuyu

    Date posted: June 27, 2019.  Answers (1)

  • Bila kubadilisha maana, andika sentensi zifuatazo ukitumia kirejeleo cha ngeli kifaacho (i) Nyumbu alishinda farasi kukimbia (ii) Milango yote yajifunga ovyo, nenda uakafunge (iii) Hamisi amekata nyasi vizuri...(Solved)

    Bila kubadilisha maana, andika sentensi zifuatazo ukitumia kirejeleo cha ngeli
    kifaacho
    (i) Nyumbu alishinda farasi kukimbia
    (ii) Milango yote yajifunga ovyo, nenda uakafunge
    (iii) Hamisi amekata nyasi vizuri
    (iv) Jiwe lile liliangukia matunda

    Date posted: June 27, 2019.  Answers (1)

  • Sahihisha bila kubadilisha maana: (i) Usikuje hapa kwetu kwani sitakuwamo (ii) Basi la shule imeharibika moshi nyingi inatokea dirishani na maji inatiririka ovyo(Solved)

    Sahihisha bila kubadilisha maana:
    (i) Usikuje hapa kwetu kwani sitakuwamo
    (ii) Basi la shule imeharibika moshi nyingi inatokea dirishani na maji
    inatiririka ovyo

    Date posted: June 27, 2019.  Answers (1)

  • Andika katika kauli ya kutendesha (i) Nataka upike chakula hiki vizuri (ii) Toa ushuru wa forodhani(Solved)

    Andika katika kauli ya kutendesha
    (i) Nataka upike chakula hiki vizuri
    (ii) Toa ushuru wa forodhani

    Date posted: June 27, 2019.  Answers (1)

  • Badilisha katika udogo kasha uukanushe udogo huo (i) Guu lake limepona baada ya kuumwa na jibwa la jijini (ii) Nyumba yenyewe ilijengwa bondeni karibu na mto(Solved)

    Badilisha katika udogo kasha uukanushe udogo huo
    (i) Guu lake limepona baada ya kuumwa na jibwa la jijini
    (ii) Nyumba yenyewe ilijengwa bondeni karibu na mto

    Date posted: June 27, 2019.  Answers (1)

  • Andika katika msemo wa taarifa Mzazi: Kesho nataka ufike nyumbani mapema, unasikia? Mtoto: Nitajaribu, lakini mwalimu alisema tutafanya mtihani jioni(Solved)

    Andika katika msemo wa taarifa
    Mzazi: Kesho nataka ufike nyumbani mapema, unasikia?
    Mtoto: Nitajaribu, lakini mwalimu alisema tutafanya mtihani jioni

    Date posted: June 27, 2019.  Answers (1)

  • Soma habari ifuatayo kisha ujibu maswali Vijana wengi wake kwa waume, walikuwa ndio tu wakamilishe shughuli ya kusajiliwa chuoni. Walikuwa bado nadhari zao zimetekwa na ugeni, hawajapata starehe...(Solved)

    Soma habari ifuatayo kisha ujibu maswali
    Vijana wengi wake kwa waume, walikuwa ndio tu wakamilishe shughuli ya
    kusajiliwa chuoni. Walikuwa bado nadhari zao zimetekwa na ugeni, hawajapata
    starehe akilini mwao wala kujisikia wamekaribia kama kwao nyumbani. Kwa hakika
    mazingira yale mapya yalikuwa yanawapa kiwewe kidogo au tuseme hata woga kiasi.
    Kusema kweli, kwa wakati ule walikuwa hawajui ni maisha ya namna gani
    yanayowasubiri mahali pale. Hawakuweza kukadiria kwa uyakinifu wowowtw iwapo
    makaazi yao pale ya miaka mine mizama kuanzia wakati ule, yangekuwa ya utulivu
    na raha au pengine yangeondokea kuwa ya roho juu juu na matatizo chungu mzima.

    Wamsubiri mkuu wa Chuo aingie wamsikize atakalosema, kisha ndipo waweze
    kubashiri vyema mkondo wa maisha yao utakavyokuwa. Lakini jinsi walivyosubiri
    Mkuu wa chuo aingie ukumbini ndivyo wayo wayo lao lilivyozidi kuwacheza shere.
    Waliwaza: Ugeni jamani kweli ni taabu. Mawazo mengi yaliwapitia bongoni mwao.
    Wakawa kinywa ukumbi mzima, kama kwamba wamekuja mazishini badala ya kuja
    kusoma. Waliwaza na kuwazua. Waliona au pengine walidhani kuwa hapa kila kitu
    ni tofauti.

    Wanafunzi hawa waliona tofauti nyingi kati ya mambo pale chuoni na yale
    waliyokuwa wameyazoea. Kwa mfano, mwalimu mkuu hapa hakuitwa ‘ headmaster’
    kama kule katika shule za msingi na vile shule za upili aliitwa ‘ vice – chancellor’
    Nyumba za kulala hazikuitwa ‘dormitory’ au ‘mabweni’, kama walivyozoea, bali
    ziliitwa ‘ halls’ kwa sababu sio kumbi za aina yoyote ile, bali ni nyumba hasa, zenye
    vyumba vya kulala, kama walivyozoea kita walipokiwa shule zao za upili huko, bali
    hapa wenyewe wenyeji waliita kwa majina mengine kabisa! Mara University, mara
    zutafindaki, mara Ndaki kwa ufupi, mara Jamahiri ya na kadhalika na kadhalika!
    Waliwaza: kweli mahali hapa wenyewe wenyeji waliita kwa majina mengine kabisa!
    Mara kumzubaisha mtu hadi kufikia kiwango cha kuonekana kama zuzu! Hata hivyo
    hawakuvunjika moyo, bali walipiga moyo konde wakanena kimoyomoyo: Potelea
    mbali! Ukiyavulia nguo, yaoge! Walikuwa wamo katika hali ya kurandaranda katika
    ulimwengu wa mawazo pale katika ulimwengu wao mpya, ulimwengu mwingine
    kabisa usioafanana hata chembe na ule waliouzoea, mkuu wa chuo alipoingia.

    Kuingia mkuu wa chuo wote walisimama kwa pamoja na kwa mijiko, wamekauka
    kama askari katika gwaride. Kuona hivyo, mkuu wa chuo akwaashiria wakae tu, bila
    kujisumbua. Kicheko kikawatoka bila kukosa adabu na heshima, kasha wakakaa kwa
    makini ndio mwanzo wakajisikia wamepoa.

    Kuona kuwa sasa wametulia na wamestarehe. Mkuu wa chuo akaanza kwa
    kuwaamkua kisha akawajulisha kwa wakuu wote wa vitivo mbali mbali na idara
    mbali mbali waliokuwa wamekaa pale jukwani alipo yeye upande huu na huu.

    Kufikia hapo, alaka ikawa imeungwa baina ya wenyeji na wageni wao. Kila mtu
    akaona mambo yamesibu tena; huo bila shaka ni mwanzo mwema, na kama
    ilivyosemwa na wenye busara, siku njema huonekana asubuhi. Hii, Kwa wote ndiyo
    asubuhi tu, bali ni asubuhi njema, si haba.

    (a) Ukirejelea aya ya kwanza na ya pili, eleza wasiwasi wanafunzi waliokuwa nao
    wakati wakisubiri (maneno 45- 55)
    (b) Ni mambo gani mageni wanafunzi hawakuyazoea yanayoelezwa katika kifungu
    (maneno 25 – 30)
    (c) Bila kubadilisha maana, fupisha aya tatu za mwisho kwa kutumia maneno yako
    mwenyewe. Tumia maneno 40 -45

    Date posted: June 27, 2019.  Answers (1)

  • UFAHAMU Soma habari ifuatayo kisha ujibu maswali Binadamu kwa wakati huu amemaka kwa sababu amechafua mazingira yake pasipo tahadhari. Mathalani insiya amejaza gesi za sumu zitokazo viwandani na...(Solved)

    UFAHAMU
    Soma habari ifuatayo kisha ujibu maswali
    Binadamu kwa wakati huu amemaka kwa sababu amechafua mazingira yake pasipo
    tahadhari. Mathalani insiya amejaza gesi za sumu zitokazo viwandani na hata kuchafua
    mito kutokana na maji machafu kutoka viwanda hivyo. Takataka zinazotupwa ovyo
    ovyo zinarundikana kila mahali. Isitoshe miti inakatwa vivyo hivyo bila simile. Matokeo
    ya haya yote ni kwa mfano tunapata mvua ya asidi ambayo huhasiri mimea. Aidha nao
    ukanda wa ozoni unaotukinga dhidi ya miali hatari kutoka kwa jua umeharibiwa tayari na
    hivyo kuongeza joto duniani. Sehemu nyingi zimeanza kugeuka na kuwa jangwa huku
    sehemu zingine zikifurika kwa maji ya mito na mvua. Maji haya yameanza kumeza
    visiwa vingi vilivyo baharini. Kutokana na madhara haya, binadamu sasa anatapatapa ili
    kutafuta makao kwingine kwenye salama. Ndiposa siku hizi nadhari za binadamu
    zimeelekezwa katika mawanda mengine nje kabisa ya kisayari hiki kidogo kiitwacho
    dunia.

    Kwa miaka mingi sasa binadamu amekuwa akitafakari uwekano wa kuishi katika sayari
    nyingine. Hii ndiyo sababu mwaka wa 1969 waamerika walimkanyagisha binadamu wa
    kwanza kabisa mwezini. Lengo lilikuwa ni kutalii na kuchunguza uwekano wa binadamu
    kuishi huko ili wale watakaoweza wahamie huko, hata mimea. Mwezini ni vumbi tupu
    lisiloota chochote. Kipatikanacho kwa wingi sana ni madini tu ambayo hayawezi kufaidi
    binadamu kwa lolote.

    Sayari nyingine alizozitalii binadamu ni Zuhura, Mirihi, Mushtara na tuseme karibu zote
    zinazolizunguka jua. Kilichogunduliwa ni kuwa upo uwezekano wa sayari kama Zuhura
    na pengine Mirihi kuwa na mvua, lakini nyingi mno isiyoweza kuruhusus mimea kukua.
    Sit u, zuhuria inasemekna kuwa joto sana wakati wa mchana ilhali Mirihi ni baridi sana
    siku zote; baridi kiasi cha kuuwa binadamu na wanyama hawawezi kuishi huko.
    Mushtara yasemekana kuwa joto ajabu, ambapo hizo sayari nyingine zina joto sana au
    zina baridi sana. Habari hii imemfunga binadamu katika jela ya kijisayari chake kiki
    hiki kiitwacho dunia anachokichafua uchao.

    Je, binadamu amekata tama? Hata kidogo! Ndio mwanzo anajaribu sana kuzikata pingu
    alizofunzwa na maumbile. Vipi? Amejaribu kuchunguza uwezekano wa kuihama ardhi
    na kuishi baharini, kwa sababu bahari inazidi ardhi mara tatu kwa ukubwa. Na ni vipi
    binadamu anadhani anaweza kuishi baharini mahali ambapo hakuumbwa aishi humo
    kama samaki?
    Jawabu ni kuwa angefanya hivyo kwa kutumia maarifa yake.

    Binadamu anaamini kabisa kuwa ana uwezo wa kujenga miji mikubwa mikubwa humo
    humo baharini… mikubwa zaidi yah ii tuliyo nayo ardhini. Anaamini ya kuwa anaweza kuitawala bahari kiasi alichitawala ardhi, na hivyo basi kufanya bahari impe
    makao na kumlisha bila ya kuyabadilisha maumbile yake. Na iwapo hili halitawezekana
    basi, ikiwajibika, abadilishe maumbile yake kwa kujiunda mashavu kwa mfano, ili avute
    pumzi ndani ya maji

    Njia ya pili ya kuepukana na pingu za maumbile ni kuishi angani. Hii ina maana ya
    kujenga miji iliyoelea angani, kama madungu vile. Na kwa vile anga haina kikomo,
    binadamu atakuwa amejipatia visayari vyake visivyo idadi ingani!

    Njia ya tatu ni kubadilisha umbo lake ili asihasirike na joto wala baridi. Binadamu wa
    kisasa anaamini kuwa inawezekana kumuunda upya mtu katika maabara badala ya katika
    mamba.
    Mtu huyu wa maabra, aitwaye ‘cyborg’ kwa lugha ya Kiingereza, anaweza kuwa na
    chuma ndani badala ya mifupa, na mwili wa kawaida wa udongo na maji nje.

    Kiunde huyu atakuwa hadhuriki ovyo ovyo kama binadamu wa sasa aliyeumbwa kwa
    chumvi, maji na protini. Au bora zaidi, binadamu mpya wa maabarani aundwe kwa
    zebaki. Binadamu huyu wa zebaki hafi wala hakatikikatiki. Na iwapo atakatika vipande
    vipande, basi kama zebaki hivyo vitaundika tena upya na kumrudishia umbo la awali
    kamili.

    Njia nyingine ya kuepukana na uangamizi ni kutumia viunde vyake vya electroniki kama
    vile tarakilishi yaani kompyuta, na mitambo mingine kama iyo. Binadamu anaamini
    kwamba uwezo wa vyombo hivi utakapokamilishwa, basi vitamsaidia kwa lolote lile.

    (a) Inasemekana kwamba binadamu anakichafua hiki kisayari chake kila uchao.
    Kwa kutumia mifano mitatu, eleza vile binadamu amechafua mazingira yake.
    (b) Kwa nini ongezeko la joto limeleta jangwa duniani wa wakati huo huo likaleta
    mafuriko?
    (c) Eleza sababu mbili zinazomfanya binadamu kuhangaika na kutafuta makao
    kwingine
    (d) Ni mambo gani yanayomfunga binadamu katika ardhi. Taja mawili
    (e) Unadhani ni kwa nini madini mengi yaliyoko mwezini hayaletwi duniani.
    Taja na ufafanue sababu mbili
    (f) Kulingana na aya mbili za mwisho, eleza jambo ambalo binadamu anajaribu
    kukwepa
    (g) Eleza maana ya maneno yafuatayo kama yalivyotumika katika kifungu
    (i) Mashavu
    (ii) Madungu
    (iii) Asihasirike
    (iv) Kiunde

    Date posted: June 27, 2019.  Answers (1)

  • Mtu akicheza mchezo mahali Fulani tunaweza kusema alichezea hapo Ukifuata mfano huu, tumia vitenzi vilivyoko katika mabao kukamilisha (i) Ali hapo (la) (ii) Ali hapo (fa) (iii) Ali hapo...(Solved)

    Mtu akicheza mchezo mahali Fulani tunaweza kusema alichezea hapo
    Ukifuata mfano huu, tumia vitenzi vilivyoko katika mabao kukamilisha
    (i) Ali hapo (la)
    (ii) Ali hapo (fa)
    (iii) Ali hapo (oa)

    Date posted: June 27, 2019.  Answers (1)

  • Eleza matumizi ya ‘Po’ katika sentensi hii Nilipofika nilimwona pale alipokuwa amesimama(Solved)

    Eleza matumizi ya ‘Po’ katika sentensi hii
    Nilipofika nilimwona pale alipokuwa amesimama

    Date posted: June 27, 2019.  Answers (1)