Get premium membership and access questions with answers, video lessons as well as revision papers.

Soma Makala yafuatayo kisha ujibu maswali Nchi nyingi za ulimwengu unaoendelea, au ule uliokuwa ukiitwa ulimwengu wa ta zimegawika sehemu mbili mbili. Sehemu hizi zinazidi kutoshabihiana kila...

      

Soma Makala yafuatayo kisha ujibu maswali
Nchi nyingi za ulimwengu unaoendelea, au ule uliokuwa ukiitwa ulimwengu wa ta
zimegawika sehemu mbili mbili. Sehemu hizi zinazidi kutoshabihiana kila uchao
zinatengana kiasi cha kukaribia kupigwa mfano wa masafa ya ardhi na mbingu. Seher
zenyewe ni mijini na mashabani. Sehemu hizi, hasa ukizitia katika mizani ya hali na jia
za watu za maisha, zimetofautiana mno. Kiasi cha tofauti hizi ni kikubwa hadi
kuonekana kama kwamba hazina uhusiano kamwe, mithili ya nchi mbili tofauti.

Hebu sasa tuzingatie yale yana yozifanya sehemu hizi kukosa kufanana. Hapa
tutawajibika kuzizingatia tofauti zilizo bayana baina ya watu wa shamba na wa mijini,
hasa kufungamana na jinsi wanavyoyaendesha maisha yao.

Jambo lililo wazi ni kwamba watu wa mashambani hawajapiga hatua ya maana kuhusu
jinsi wanavyuotakikana kuishi katika karne ya ishirini. Watu hawa bado wanaishi kama
walivyoishi mababu zao. Hawahisi halahala ya jambo lolote. Mategemeo yao ni shamba;
usubiriwe msimu mzuri wa mvua, watu walime, Mungu akineemeshe kilimo, wavune
mavuno mema, Chakula kikiwa tayari, wale, walale, siku nyingine warudie mkondo uo
huo wa kuendesha maisha yao.

Watu hawa maisha yao yamepangika mikondo mitatu tu: kuzaliwa, kuoa au kuolewa, na
kufa. Zaidi ya mikondo hii, maisha ya viumbe hawa hayana mabadiliko makubwa.
Mabadiliko haypendelewi sana huko mashambani. Huko, wanaume ni mabwana,
wanawake ni mfano wa vijakazi na watoto hawana tofauti kubea na watwana. Mwanume
akikohoa, mkewe akimbilie kulikokoholewa, na watoto watetemeke. Wanawake wa
shamba na watoto hawana haki hata ya kunena, wala hawajui haki ni nini.

Kwa upande mwingine, mijini kuna viwanda, kuna majumba, kuna magari na kuna
vyombo vingi sana vya maendeleo ya kisiku izi. Watu wa mijini ni watu wa ulimwengu
kote, wala si watu wa mji mmoja tu. Watu wa mji wowote ulimwenguni huweza
kuwasiliana na wenzao wa miji mingine kokote kule ulimwenguni kwa njia ya runinga.
Pia, kwa watu wa mjini, kuona kiumbe kidogo kabisa kisichoweza kuonekana kwa
macho si ibura hata. Kiumbe cha namna hiyo huonekana kupitia mangala. Na kwa wale
walioondokea kuwa wanajimu wa kisasa, kuziona sayari na thurea zilizoko mbali sana
nasi kupitia ningala ni jabo la kawaida sana.

Watu wa mjini huwa na mabadiliko mengi sana katika maisha yao, wala sio mikondo
aina tatu tu. Kwa mfano, wanawake wa mijini hawakubali tena kuonewa na wanaume.
Wanajua vyema sana maslahi yao na wameiweka menke yao mbele; yaani mahali pao
katika jamii, wakiwa wao ni wanawake. Kupigania haki sawa na wanaume bila kulegeza
kamba. Huku kupambana kimaisha kama wapambanavyo wanaume na kufanikiwa kufanya kazi za kusikika kam vile uwakili, udaktari, uhandisi, urubani na nyinginezo
zilizokuwa zikifanywa na wanaume tu. Wanawake wengine hata ni maprofesa! Kweli
watu wa mijini wameendelea.

a) Toa maelezo kuhusu tofauti zinazosemekana ni bayana baina ya maisha ya watu
wa shamba nay ale ya watu wa mijini.
b) Rejelea “Mungu” katika aya ya tatu na neon “viumbe” katika aya ya nne.
Bainisha uhusiano uliopo baina ya manen haya mawili, hasa ukizingatia jinsi
yavyotumiwa katika habari. Je matumizi haya yankupa hisia gani?
c) Unadhani mwandishi ana maana gani anaposema ya kwamba huko mashambani
“wanawake ni mfano wa vijakazi, na watoto hawana tofauti kubwa na watwana?”
d) Orodhesha vifaa vyovyote vitano vilivyotajwa katika taarifa hii, kisha ueleze
umuhimu wa kila kimoja wapo.
e) “Watu wa mijini ni watu wa ulimwengu kote” Hapa mwandishi anamaanisha
nini?
f) (i) Ni nini maana ya neon menke?
(ii) Mwandishi anamaliza taarifa yake kwa kusema “Kweli watu wa mijini
wameendelea.” Kwa muhtasari, ni tabia gani za wanamiji zilizomfanya
kukiri hivyo.

  

Answers


Kavungya
fig427620191251.png
(b) Uhusiano
Mungu ndiye mwenye uwezo mkubwa/ ndiye aliyeviumba viumbe
Viumbe ni wategemezi/ hafifu/ hawana uwezo/ wanyonge
Hisia
- Viumbe humtegemea Mungu kiasi kuwa bila yeye wataangamia
- Hisia ya huruma
(c) Wanawake na watoto hawana haki/ ni watumwa
(d) Tarakilishi - Kuwasiliana
Mangala Kuona viumbe vidogo
Nangala kuona sayari ya thurea zilizoko mbali
Runinga kusikiliza na kuona
Simu Kuwasiliana
Ghala Usafirishaji
Viwanda Uandaji wa bidhaa
Majumba makaazi/ Biashara
(e) Waweza kuwasiliana ulimwengu kote kwa kutumia teknologia ya kisasa (vifaa
vilivyo tajwa katika (d)
Kuona nakusikia kote ulimwenguni
(f) (i) Mahali/ nafasi/ hadhi/ wajibu/ jukumu zao katika jamii
(ii) Wameendelea kielimu/ sayansi/ teknolia/ kimawasiliano. Kiufundi
Kavungya answered the question on June 27, 2019 at 09:54


Next: Kiambishi- U-hutambulisha majina yote ya ngeli ya U (umoja). Hata hivyo baadhi majina hay huchukua viambishi tofauti tofauti katika wingi. Orodhesha majina ma kama hayo, kisha uonyeshe...
Previous: Soma makala yafuatayo kisha ujibu maswali. Raha ni kitu gani? Je, ni kitu kizuri au kibaya? Mbona kila mutu hipigania na kama ionekanavyo, kila aionjaye hatimaye humwunguza?...

View More Kiswahili Questions and Answers | Return to Questions Index


Learn High School English on YouTube

Related Questions


  • Kiambishi- U-hutambulisha majina yote ya ngeli ya U (umoja). Hata hivyo baadhi majina hay huchukua viambishi tofauti tofauti katika wingi. Orodhesha majina ma kama hayo, kisha uonyeshe...(Solved)

    Kiambishi- U-hutambulisha majina yote ya ngeli ya U (umoja). Hata
    hivyo baadhi majina hay huchukua viambishi tofauti tofauti katika wingi.
    Orodhesha majina ma kama hayo, kisha uonyeshe viambilshi hivyo tofauti
    vya ngeli (Katika umoja na Wingi)

    Date posted: June 27, 2019.  Answers (1)

  • Eleza maana mbili za sentensi: Jua nisemalo ni muhimu kwetu.(Solved)

    Eleza maana mbili za sentensi:
    Jua nisemalo ni muhimu kwetu.

    Date posted: June 27, 2019.  Answers (1)

  • Akifisha: Sijaona kitabu kizuri kama hiki utaniazima siku ngapi bashiri alimuliza sijaona.(Solved)

    Akifisha:
    Sijaona kitabu kizuri kama hiki utaniazima siku ngapi bashiri alimuliza
    sijaona.

    Date posted: June 27, 2019.  Answers (1)

  • Ondoa- amba-bila kubadilisha maana. (i) Kuimba ambako kulisifika siku nyingi sasa kunatia shaka (ii) Mibuni ambayo hupandwa wakati wa mvua hustawi(Solved)

    Ondoa- amba-bila kubadilisha maana.
    (i) Kuimba ambako kulisifika siku nyingi sasa kunatia shaka
    (ii) Mibuni ambayo hupandwa wakati wa mvua hustawi

    Date posted: June 27, 2019.  Answers (1)

  • Nyambua vitenzi vifuatavyo ili kupata majina (nomino) mawili mawili tofauti: (i) Kumbuka ii)Cheka(Solved)

    Nyambua vitenzi vifuatavyo ili kupata majina (nomino) mawili mawili
    tofauti:
    (i) Kumbuka
    ii)Cheka

    Date posted: June 27, 2019.  Answers (1)

  • Andika kwa umoja Tumewaondoleeni matatizo yenu, yafaa mtushukuru.(Solved)

    Andika kwa umoja
    Tumewaondoleeni matatizo yenu, yafaa mtushukuru.

    Date posted: June 27, 2019.  Answers (1)

  • Jaza kiambishi kifaacho: Ume__________ ona kalamu nyekundu ziliz_______potea?(Solved)

    Jaza kiambishi kifaacho:
    Ume__________ ona kalamu nyekundu ziliz_______potea?

    Date posted: June 27, 2019.  Answers (1)

  • Soma makala yafuatayo kisha ujibu maswali Siku hiyo nilipitia mahali hapo kama nilivyokuwa nikimuona siku hizi zote, mwaka nenda mwaka rudi. Nilisimama huku nikishangaa kwa mara nyingine tena. Nilikuwa...(Solved)

    Soma makala yafuatayo kisha ujibu maswali
    Siku hiyo nilipitia mahali hapo kama nilivyokuwa nikimuona siku hizi zote,
    mwaka nenda mwaka rudi. Nilisimama huku nikishangaa kwa mara nyingine
    tena.

    Nilikuwa najitayarisha kujiendea na hamsini zangu mtu huyo alipojipinda kwa
    mbali sana. Kwa hakika nilidhani macho yangu yananihadaa. Nikafikicha macho
    yangu nikitumia nishati yote iliyomo mwilini mwangu ili niyatoe matongo
    ambayo nilituhumu kwamba ni akili yangu tu iliyokuwa imeniadaa, nikaamua
    kuendelea na safari yangu kwenda kujitafutia riziki.

    Hatua ya kwanza na ya pili, moyo haukunipa. Sauti katika kilindi cha moyo
    wangu ikanisihi na kunitafadhalisha nitazame nyuma. Kutupa jicho nyuma,
    nikamnasa mtu huyo akeguka! Nikashtuka sana! Jambo la kwanza nildhani macho
    yangu yameingiwa na kitu kilichoyafanya kuona mambo yasiyokuwepo. Pili,
    nilidhani iwapo niliyoyaona yana msingi wowote, basi huenda ama nina wazimu,
    au yule mtu ni mzuka, hasa kwa vile ilionekana ni mimi tu nimuonaye.
    Nilikikuwa niko katika hali ya kufanya uamuzi kuhusu dhana zangu hizi aina aina
    mtu huyo alipojigeuzageuza, kisha akafunua macho! Moyo ulinienda mbio.
    Nilitaka kutifua vumbi ili wazimu usinizidie, lakini sikupata nafasi. Mtu yule
    alijizoazoa na kuketi kitako. Kisha akatokwa na maneno katika lugha iliyofanana
    sana na Kiswahili. Niliyaelewa aliyokuwa akisema.

    Ajabu ya maajabu, mtu huyo alidai ya kwamba tangu alipolala kivulini hapo
    tangu jana baada ya chakula cha mchana, hakuota ndoto hata moja bali usingizi
    wake ulikuwa mithili ya gogo! Sasa nilikuwa na hakika kwamba ikiwa mimi sina
    wazimu, basi kiumbe yule aliyevaa ngozi iliyochakaa sana katika mpito wa miaka
    hakika ana wazimu. Nilitaka kuhakikisha, hivyo nilimkumbusha kwamba
    amelala mahali hapo kwa muda wa miaka mingi sana.

    Kusikia hayo alianza kunikagua. Akasema nimevaa kizungu. Akanitajia tofauti
    nyingi baina ya vijana aliowazoea na mimi. Mwisho wa yote akauliza kama siku
    hiyo si tarehe kumi na nane mwezi wa pili mwaka wa 1897. Nikadhani anafanya
    mzaha kwa hivyo nikacheka.
    Nilipoona kicheko changu kinamuudhi, nikamwambia siku hiyo ni tarehe kumu
    na nane mwezi wa pili mwaka wa 1997. Nilipoona ameshangaa kwa dhati,
    nikagundua ukweli.
    Alikuwa amelala kwa karne nzima!.

    a) Eleza hoja nne muhimu zinazojitokeza katika aya tatu za mwanzo.
    (Maneno 75-85)
    b) Kwa maneno yako mwenyewe, fupisha aya mbili za mwisho bila
    kubadilisha maana. (Tumia maneno 40-50)

    Date posted: June 27, 2019.  Answers (1)

  • Soma makala yafuatayo kisha ujibu maswali Mwanamke wa kisasa anazaliwa na kukulia katika mazingira yaliyobadilika mno. Matazamio yake maishani ni tofauti na yale ya wanawake walioishi mapote...(Solved)

    Soma makala yafuatayo kisha ujibu maswali
    Mwanamke wa kisasa anazaliwa na kukulia katika mazingira yaliyobadilika mno.
    Matazamio yake maishani ni tofauti na yale ya wanawake walioishi mapote mawili
    yaliyopita; wanawake makamu ya nyanyake na mamaake-kuu.

    Yeye hatarajii kuzaliwa, kukua, kuolewa, kuwa mke wa bwana, kumzalia watoto, na
    daima dawamu kuwa ‘mwendani wa jikoni’ akawapikia watoto na bwanake chakula; na
    akitoka jikoni aelekee shambani kulima, kichakani kuchanja kuni, mtoni kufua nguo na
    kuteka maji ya kutumia nyumbani. Mwanamke wa kisasa huandamana na mwanamume.
    Akanyangapo mume naye papo huutia wayo wake.

    Mwanamke wa kisasa huenda shule na kujifunza yote yafunzwayo huko. Hushindana na
    wanawake kwa wanaume na kuibuka mshindi si mara haba. Huibuka mshindi katika
    masomo ya lugha, historia, jiografia, hesabu, sayansi na mengineyo, sawa na
    mwanamume.

    Mwanamke wa kisasa hutaka kufanya kazi za kibega, akazifanya. Akataka kuwa
    mwalimu, akawa. Akataka kuwa daktari, akafanikiwa. Almuradi, siku hizi mwanamke
    hufanya kazi yoyote ile afanyayo mwanamume. Kuna wanawake marubani wa ndege,
    masonara, waashi, wahandishi, madereva wa magari, mawakili, mahakimu, mawaziri
    wakuu na hata marais wa nchi. Hakuna kazi isiyofanywa na mwanamke siku hizi.

    Mwanamke wa kisasa hateswi akafyata ulimi. Anapohiniwa yeye hupigania haki yake
    kwa dhati na hamasa. Katu hakubali ‘mahali pake’ katika jamii alipotengewa na
    wanaume wenye mawazo ya kihafidhina yaliyopitwa na wakati.

    Siku hizi mwanamke huolewa tu wakati amepata kazi ya kumwezesha kujikimu maishani
    au pale anapokuwa na hakika kwamba biashara yake, iwapo ni mfanyi biashara, imepiga
    hatua ya kutomrudisha ukutani.

    Mwanamke wa kisasa haamuliwi katika jambo lolote, bali hufanya maamuzi yake
    mwenyewe. Kwa upande mwingine, mwanamume wa ‘kisasa’, ambaye bado amefungwa
    pingu na taasubi za kiume, hapendezwi na mwanamke huyu. Huuma kidole akatamani ya
    kale, lakini wapi! Analazimika kumkubali mwanamke huyu kama mshirika sawa
    maishani, na kuishi naye, apende asipende. Shingo upande analazimika kukubali kwamba
    mabadiliko haya sio mithili ya kiwingu kipitacho, bali ni ya aushi.

    a) Msemo ‘mwendani wa vijungu jiko’ unadhihirisha hali gani ya
    mwanamke katika jamii?
    b) Jamii imemfanya mwanamke kuwa hayawani wa mizigo. Fafanua
    c) Eleza maana ya ‘akanyagapo mume papo huutia wayo wake.’
    d) Zungumzia maswala ya ndoa na elimu huku ukilinganisha mwanamke wa
    kiasili na wa kisasa.
    e) Mwanamume wa kisasa anamwonaje mwanamke wa kisasa?
    f) Taja mifano minne ya ‘mawazo ya kihafidhina.
    g) Eleza maana ya:
    (i) Akafyata ulimu……………………………………………
    (ii) Ukatani…………………………………………………….
    (iii) Taasubi za kiume………………………………………….
    (iv) Aushi…………………….………………………………..

    Date posted: June 27, 2019.  Answers (1)

  • Andika upya sentensi ifuatayo ukitumia kirejeshi ( kihusiano) cha ngeli cha mwisho Mwanafunzi anayefanikiwa maishani ni yule anayesoma kwa bidii na pia anayetii wakuu wake(Solved)

    Andika upya sentensi ifuatayo ukitumia kirejeshi ( kihusiano) cha ngeli cha mwisho
    Mwanafunzi anayefanikiwa maishani ni yule anayesoma kwa bidii na pia
    anayetii wakuu wake

    Date posted: June 27, 2019.  Answers (1)

  • Tumia semi hizi katika sentensi kuonyesha maana: (i) Kuchokoachokoa maneno (ii) Kumeza shubiri(Solved)

    Tumia semi hizi katika sentensi kuonyesha maana:
    (i) Kuchokoachokoa maneno
    (ii) Kumeza shubiri

    Date posted: June 27, 2019.  Answers (1)

  • Tunatumia viashiria vya kuthibitisha kwa mfano kitabu kiki hiki. Sasa kamilisha Ni mbwa …………………….. aliyekula chakula cha mtoto(Solved)

    Tunatumia viashiria vya kuthibitisha kwa mfano kitabu kiki hiki. Sasa kamilisha
    Ni mbwa …………………….. aliyekula chakula cha mtoto

    Date posted: June 27, 2019.  Answers (1)

  • Eleza tofauti mbili muhimu za kimaumbile kati ya wanyama (i) Kifaru (ii) Nyati(Solved)

    Eleza tofauti mbili muhimu za kimaumbile kati ya wanyama
    (i) Kifaru
    (ii) Nyati

    Date posted: June 27, 2019.  Answers (1)

  • Tumia kiulizio – pi – kukamilisha (i) Ni mitume ………………………. Aliowataja? (ii) Ni kiziwi ………………………. . Aliyemwona akipita?(Solved)

    Tumia kiulizio – pi – kukamilisha
    (i) Ni mitume ………………………. Aliowataja?
    (ii) Ni kiziwi ………………………. . Aliyemwona akipita?

    Date posted: June 27, 2019.  Answers (1)

  • Watu wafuatao wanafanya kazi gani (i) Mhasibu (ii) Mhazili(Solved)

    Watu wafuatao wanafanya kazi gani
    (i) Mhasibu
    (ii) Mhazili

    Date posted: June 27, 2019.  Answers (1)

  • Tumia viunganishi vingine badala ya vile vilivyotumiwa katika sentensi hizi: (i) Anayetafuta hachoki hata akichoka keshapata (ii) Ngonjeeni hadi washiriki wote wafike(Solved)

    Tumia viunganishi vingine badala ya vile vilivyotumiwa katika sentensi hizi:
    (i) Anayetafuta hachoki hata akichoka keshapata
    (ii) Ngonjeeni hadi washiriki wote wafike

    Date posted: June 27, 2019.  Answers (1)

  • Taja madini mawili ambayo yametukuzwa zaidi, moja kwa thamani yake ya kifedha na nyingine kwa kutengeneza vyuma vigumu kuliko madini mengine(Solved)

    Taja madini mawili ambayo yametukuzwa zaidi, moja kwa thamani yake ya
    kifedha na nyingine kwa kutengeneza vyuma vigumu kuliko madini mengine

    Date posted: June 27, 2019.  Answers (1)

  • Onyesha kielezi, kivumishi, kitenzi na jina katika sentensi: Watu wane walipeperushwa juu kwa juu na upepo mkali(Solved)

    Onyesha kielezi, kivumishi, kitenzi na jina katika sentensi:
    Watu wane walipeperushwa juu kwa juu na upepo mkali

    Date posted: June 27, 2019.  Answers (1)

  • Akifisha kifungu hiki: Nilopomwendea aliniangalia kisha akaniambia siamini kuwa ni wewe uliyeandika insha hii.(Solved)

    Akifisha kifungu hiki:
    Nilopomwendea aliniangalia kisha akaniambia siamini kuwa ni wewe uliyeandika
    insha hii.

    Date posted: June 27, 2019.  Answers (1)

  • Soma makala haya kisha ujibu maswali yanayofuata Lugha ya Kiswahili ni lugha iliyoendelea sana. Leo hii lugha hii inasema na watu wote nchini Tanzania, Rwanda na Burundi,...(Solved)

    Soma makala haya kisha ujibu maswali yanayofuata
    Lugha ya Kiswahili ni lugha iliyoendelea sana. Leo hii lugha hii inasema na watu wote
    nchini Tanzania, Rwanda na Burundi, inasemwa na watu wote nchini Kenya. Nchini
    Uganda, Zaire, Malawi, msumbiji, Zambia, Somalia, Bukini (Madagascar) na Ngazija
    (Comoro), inasemwa na asilimia kubwa za wananchi wa huko. Aidha lugha hii ina
    wasemaji si haba katika kisiwa cha Sokta na nchini Oman.

    Fauka ya maendeleo haya, Kiswahili kinatumika kwa minajili ya matangazo ya habari
    katika idhaa nyingi za mashirika ya habari ulimwenguni. Nchi zenye idhara za Kiswahili
    ni kama vile hizi zetu za Afrika ya Mashariki na kati, Afrika ya kusini, Nigeria, Ghana,
    Uingereza, ( shirika la B.B.C) Marekani ( shirika la V.O.A), Ujerumani ( shirika la
    Radio Deutch Welle, Cologue), Urusi ( Radio Moscow), China, India na kadhalika.

    Maendeleo mengine yanapatikana katika upande wa elimu, Marekani peke yake, kuna
    vyuo zaidi ya mia moja vinavyofundisha Kiswahili kama lugha muhimu ya kigeni. Huko
    Uingereza vyuo kama London, Carmbridge na Oxford vinafundisha lugha hii. Nci
    nyingine ambazo zina vyuo vinavyofunza lugha ya Kiswahili ni kama vile Japan, Korea,
    Ghana, Nigeria na kadhalika

    Kweli Kiswahili kimeendelea jamani. Lakini je, kilianza vipi? Na ilikuwaje kikaweza
    kupiga hatua hizi zote?
    Kiswahili kilianza kuzungumzwa na kabila dogo la watu waliokuwa wakiitwa wangozi.
    Watu hawa walikuwa wakiishi mahali palipoitwa shumgwaya. Shungata ni nchi ya
    zamani iliyokuwa eneo lililoko katika nchi katika nchi mbili jirani ambazo siku hizi ni
    Kenya na Somalia. Kabila hili la wangozi iliishi irani na makabila mengine kama vile
    wajikenda, wapokomo, Wamalakote ( au Waelwana) na Wangazija ( kabla hawajahamia
    visiwa vya Ngazija) Lugha ya wangozi siku hizo, ambayo ndiyo mzazi wa Kiswahili
    cha leo, ilijulikana kwa jina kingozi. Kama ilivyosemwa hapo awali, kingozi kilisemwa
    na watu wachache sana.

    Je lugha hii ilikuwaje mpaka ikapata maendeleo haya makubwa tunayoyashuhudia siku
    hizi? Ama kwa hakika, Kiswahili ni lugha iliyobahatika tu. Inaweza kusemwa kwamba
    lugha hii ilipendelewa na mazingira na historia.

    Jambo la kwanza, wageni waliotoka mashariki ya kati kifukia hizi janibu zetu Afrika ya
    mashariki walikaribishwa vizuri na hawa wangozi. Wakaingilia wageni na wenyeji
    kindakindaki, kidini, kitawala, kibiashara na kitamaduni kwa jumla. Punde si punde
    wangozi, ambao baadaye walijulikana kama waswahili na wageni hawa, wakaelimika
    katika dini (ya kiisilamu), biashara na mambo ya utawala aina mpya. Lugha yao nayo
    ikapanuka pale ilipochukua msamiati ya kigeni hususan wa Kiarabu na Kiajemi na
    kuufanya uwe wake, ili kueleza kwa rahisi zaidi mambo haya mageni katika taaluma za
    dini, biashara, siasa na hata sayansi kama vile unajimu. Wakati huo, lugha ya Wangozi
    sasa ikaitwa Kiswahili wala sio kiangozi. Tatizo hapa ni kuwa kwa vile Kiswahili
    kilichukua msamiati mwingi wa kigeni ili kuelezea taaluma hizi mpya, baadaye kimekujashukiwa kwamba ni lugha ya kigeni ilhali ni lugha ya Kiafrika asilia, na kitovu
    chake ni nchi mpya za kiafrika ziitwazo Kenya na Somalia hii leo.

    (a) Thibitisha kuwa Kiswahili kimekuwa lugha ya kimaitaifa ( maneno 35 – 40)
    (b) Eleza kwa ufupi asili ya Kiswahili hadi kuja kwa wageni ( maneno 20 – 25)
    (c) Ukitumia maneno yako mwenyewe, eleza ujumbe uliomo katika aya ya mwisho

    Date posted: June 27, 2019.  Answers (1)