Trusted since 2008
Study resources on Kenyaplex

Get ready-made curriculum aligned revision materials

Exam papers, notes, holiday assignments and topical questions – all aligned to the Kenyan curriculum.

Soma makala yafuatayo kisha ujibu maswali Wahenga walisema “mtoto umleavyo ndivyo akuavyo.” Hii ina maana ya kuwa ukiogopa kutumia ufito kumchapa mtoto wako, ukamdekeza atadeka na hatimaye...

Soma makala yafuatayo kisha ujibu maswali
Wahenga walisema “mtoto umleavyo ndivyo akuavyo.” Hii ina maana ya kuwa ukiogopa
kutumia ufito kumchapa mtoto wako, ukamdekeza atadeka na hatimaye ataharibika.
Methali hii ina picha yake ambyo ni, “Ukicha mwana kulia, utalia wewe.”

Hizi ni methali zilizojaa busara kubwa. Mathalini wewe ni mzazi au mtu yeyote mzima
aliyetunikiwa madaraka juu ya watoto. Lakini kila wanapokiuka uadilifu au mmoja wao
anapokosea wewe unambembeleza tu, basi huwa unaizorotesha tabia yake. Mwisho,
mtoto huyo anaweza kuishia kuwa mtundu.

Hata hivyo, ni sharti tujue ya kwamba tuko katika njia panda hapa. Kwa upande mmoja,
zamani ilichukuliwa kwamba watoto na hata wanawake watu wazima hawana akili. Kwa
ajili hiyo, iwapo mwanaume mtu mzima ana jambo la kuwaeleza, njia pekee ya
kuliingiza katika “ akili” yao “ hafifu” ni kuwatwanga ili kulikongomeza jambo hili.
Ukweli ni kwamba akili ya mtoto si hafifu hata. Unaweza kusema ni kama mmea, ambao
usiporutubishwa kimakusudi, ukapaliliwa vyema na kustawishwa stahiki yake, basi
hudhoofu” na mwishowe kufifia.

Kwa upande mwingine, mtazamo wa kisasa ni tofauti kabisa, imethibitishwa ya kwamba
wanawake ni sawa kabisa katika maumbile yao wakilinganishwa na wanaume. Kwa jinsi
hiyo, kweli wapo wanawake amabo hawana mwelekeo timamu kuhusu maisha. Lakini ni
kweli pia kuwa wapo wanaume watu wazima mamilioni ambao hawana akili.
Kadhalika, si kweli kuwa watoto wote, kwa sababu ya umri wao tu, basi hawana akili.
Ama kwa kusema kweli binadamu yeyote kuwaliwa na akili zake timamu isipokuwa wale
ambao kwa bahati mbaya maumbile yamewapa akili pungufu. Hili litokeapo basi
tunalikubali tu. Hatuwezi kumlaumu mtu kama huyo au muumba wake. Kwa hakika huu
ndio msingi wa methali. “Akili ni nywele, kila mtu ana zake.” Vinginevyo, mtazamo wa
kizamani ni taasubi kogwe tu za kiume zilizopitwa na wakati.

Aidha, kwa sababu watu wote huzaliwa na akili timamu, tena hawawi watu wazimu
kabla ya kuwa watoto kwanza, mtu mzima yeyote ana hali gani ya kuwadhulumu
watoto na kujipambaniza na lawama za uongo dhidi ya vijana hao kwa madai kuwa
hawana akili? Na je, ikiwa hawana akili, basi ndipo waonewe? Wanyanyaswe? Hili si
jambo la busara. Kurudi mtoto kwa visa vya maonevu ni kumrudisha nyuma kiumbe huyo.
Kurudi kufaako ni kwa kupeleka mbele, sio kwa kurudisha nyuma. Kurudi kuelekezako
mbele ni kwa uongozi mwafaka, uongozi ambao lengo lake ni kummulikia mtoto kurunzi
ilimradi kumwongoza mtoto.

Mtoto ana haki ya kuhudumiwa kwa njia yoyote ifaayo ili akue na akili yake ikomae
kikamilifu. Inafaa asomeshwe, apewe malezi bora ili naye aje alee wengine kistahiki.

(a) “Mapenzi yasiyo kipimo yanaweza kuwa hatari kwa mtoto.” Eleza kikamilifu
huku ukirejelea habari uliyosoma
(b) Fafanua njia panda inayorejelewa na mtunzi
(c) Mtoto analinganishwa na mmea katika taarifa hi, kwamba “usiporutubishwa
kimakusudi, ukapaliliwa vyema na kustawishwa stahiki yake basi hudhofu.”
Tahtmini kulinganishwa huku, huku ukirejelea taarifa
(d) “Akili ni nywele, kila mtu ana zake.” Eleza maana ya ndani ya methali hii
kulingana na taarifa
(e) Onyesha kwamba unaelewa maana ya:
“Kurudi mtoto kwa visa vya maonevu ni kumrudisha nyuma kiumbe huyo”
(f) Eleza maana ya:
(i) Kulikongomeza
(ii) Kujipambaniza

Answers


Kavungya
a) Kutomchapa/kubembeleza/kumdekeza motto anapokosea/anakiuka uadilifu
unamharibu/unamzorotesha tabia zake/Unamfanya mtundu
Akitumia Methali
Sehemu mbili maki 3. akishughulika nusu ya jumla ya
b) Mtazamo wa zamani ambapo ulichukuliwa kuwa watoto na hata wanawake
hawana akili lakini ukweli ni kwamba watu wana akili sawa/wote wan akili
sawa/wote wanafanana/wanaume na wanawake. Ni utata unaoletwa na misimamo
miwili tofauti usasa na ukale. Lazima agusie usasa na ukale
c) Kama ambavyo mmea hudhoofa usipotuuzwa ndivyo ambavyo motto huzorota
kitabia asipopewa malezi mazuri atazorota kitabia. Upande moja ni
Mtoto asipopewa malezi mazuri atazorota kitambia Akisema ni kweli
au ni sawa/ ni hivyo ni
d) Wanaume kuwadharau watoto na wanawake kwamba wana akili pungufu ni
makosa
Akinusisha wanawake, watoto na taarifa
Si lazima ataje wanaume.
Binadamu yoyote huzaliwa na akili zake; hivyo basi si haki kudharualiana kwa
misingi ya kiakili
Binadamu yoyote huzaliwa na akili zake
f) i) Kushindilia/ kulifanya lieleweke
kulishukumiza/kulilazimisha
ii) Kujiaminisha /kujidai/kujiepusha
Kujifanya/kujigangaza/ kukwepa/ kujiberegeza/ kujibambanya/ kujitia/
kujipambaniza.
Kavungya answered the question on June 27, 2019 at 13:03

Answer Attachments

Exams With Marking Schemes

Related Questions