Get premium membership and access questions with answers, video lessons as well as revision papers.

Linganisha bahari za shairi A na B

      

SHAIRI A: HOFU YA BIN-ADAMU

Hofu za wanyonge, ni nguvu za matajiri,

Ambazo zinawaponda, wanapotaka usawa.


Hofu ya watawala, ni kupoteza uhuru,

Wa kutawala kwa mbavu, pamoja na utukutu.



Hofu za mwanamke ,mwanamke wa sasa,

Ni kutumiwa ja rungu, daima kuwekwa nyuma.


Hofu za mmcha-mungu, ni maisha ya baadaye,

Maana hana hakika, ndio aogopa kifo.


Hofu za wasomi, ni kwamba wako baidi,

Na wale wateteao, ambao ni sawa nao.




SHAIRI B: AMANI

Uhuru pia Amani
Usifikirie ni zawadi
Ambayo inapeanwa
Pasipo mikwaruzano



Kama wataka hakiyo
Shariti uwe tayari Kupokeza roho yako
Pamoja na ya mwingine



Uhuru ja ini la fani
Ambalo kulifikia
Sharti uwe jasiri
Jasiri aso kifani


Linganisha bahari za shairi A na B

  

Answers


Maurice
Shairi A

(i) Tathnia(uwili)

(ii)Kikwamba-neno ‘’hofu’’ huanza kila mshororo wa kwanza.

(iii) Masivina-vina vyote kutofautiana.

(iv) Mandhuma-ukwapi unatoa wazo,utao unatoa jibu.



SHAIRI B:

(i) Utenzi-kipande kimoja.

(ii)Tarbia-mishororo mine.
maurice.mutuku answered the question on August 3, 2019 at 11:37


Next: Jadili ufaafu wa anwani: Tumbo lisiloshiba kwenye hadithi hii
Previous: Andika ubeti wa pili wa shairi B kati lugha nathari.

View More Kiswahili Questions and Answers | Return to Questions Index


Learn High School English on YouTube

Related Questions