Get premium membership and access questions with answers, video lessons as well as revision papers.

Sahihisha sentensi hii. Wasichana mabinti mapacha waliozeshwa mume mmoja.

      

Sahihisha sentensi hii.
Wasichana mabinti mapacha waliozeshwa mume mmoja.

  

Answers


sharon
Wasichana pacha waliozwa mume mmoja.
sharon kalunda answered the question on September 21, 2019 at 07:46


Next: A new laptop depreciates at 8% per annum in the first year and 12% per year in the second year. If its value...
Previous: Mrs. Langat, a primary school head teacher, earns a basic salary of sh.38,300, house allowance of sh 12000 and medical allowance of sh 3600 every...

View More Kiswahili Questions and Answers | Return to Questions Index


Learn High School English on YouTube

Related Questions


  • Tumia mzizi- enye katika sentensi kama kihusishi.(Solved)

    Tumia mzizi- enye katika sentensi kama kihusishi.

    Date posted: September 21, 2019.  Answers (1)

  • Ainisha maneno katika sentensi ifuatayo:- Shehena ya dawa ilikuwa bandarini(Solved)

    Ainisha maneno katika sentensi ifuatayo:-
    Shehena ya dawa ilikuwa bandarini

    Date posted: September 21, 2019.  Answers (1)

  • Onyesha muundo wa silabi katika neno wachanjwao(Solved)

    Onyesha muundo wa silabi katika neno wachanjwao

    Date posted: September 21, 2019.  Answers (1)

  • Andika neno lenye mfumo ufuatao wa vitamkwa. Nazali ya ufizi + kipasuo cha kaakaa gumu + irabu ya juu nyuma + kizuiwa ghuna cha kaakaa...(Solved)

    Andika neno lenye mfumo ufuatao wa vitamkwa. Nazali ya ufizi + kipasuo cha kaakaa gumu + irabu ya juu nyuma + kizuiwa ghuna cha kaakaa laini + irabu ya chini wastani.

    Date posted: September 21, 2019.  Answers (1)

  • Tangu miaka ya uhuru, serikali za Afrika zimekuwa zikikariri kwa dhati na hata kula viapo vya kulinda na kutetea haki za raia wao kama zilivyoainishwa...(Solved)

    Soma taarifa ifuatayo kisha ujibu maswali.
    Tangu miaka ya uhuru, serikali za Afrika zimekuwa zikikariri kwa dhati na hata kula viapo vya kulinda na kutetea haki za raia wao kama zilivyoainishwa kwenye katiba. Kadiri miaka inavyozidi na ulevi wa mamlaka kuchukua nafasi katika nafsi za viongozi hao, kiapo chao huishia kuapuliwa katika muda wa kupepesa macho. Ikasalia hali ya maskini pita chini miye mwenye nazo nipite juu. Katika hali kama hii, wanaoishia kuumia aghalabu ni watoto.
    Kwa miaka mingi, mtoto wa Afrika amekuwa akiteseka na kusalitika katika dunia hii ya mwenye nguvu mpishe, hasa akiwa anatoka katika familia maskini na jamii isiyothamini utu. Si ajabu kupata mtoto wa Afrika akiishi katika mabanda yaliyo kando ya machimbo katika migodi akitumikishwa katika machimbo hayo. Katika hali kama hizi, siku nenda rudi, utawapata watoto wamevalia matambara, miguu imeparara na midomo kuwakauka huku vichwani wakiwa wamebeba karai za madini kutoka
    machimboni. Na mchakato wote wa kutafuta madini hayo unawashirikisha watoto, isipokuwa kupokea pesa, ambao hufanywa na mabwanyenye wanaoishia kuwapa (au hata kuwanyima) watoto wale malipo duni au badala yake wakawalipa wazazi wa watoto hao.
    Hali huwa sawa na hiyo katika maeneo ambayo shughuli za uvuvi hutekelezwa. Watoto wengihuingizwa katika ‗biashara‘ ya samaki kwa kisingizio cha kuwapa namna ya kujitegemea katika siku za usoni. Ajabu ni kwamba, mwisho wao huwa papo hapo uvuvini.
    Kinachosikitisha sana ni udhalimu ambao umekuwa ukitekelezwa na kundi la watu ambao wanafaa- kwa msingi wa kazi zao- kuwalinda watoto hao na kuwaelekeza katika masuala ya maisha. Je, ni kwa nini mtu mwenye akili zake timamu, ambaye tayari alikwishamaliza masomo na hata kupata kazi, amtunge mimba mwanafunzi na kumzimia ndoto yake maishani? Kwa nini mtoto kama huyo abebeshwe mzigo wa uzazi badala ya kumsaidia na kumtua (au kuwatua wazazi wake) mzigo wa elimu kwa kumpa vifaa vya elimu au kumlipia karo? Pigo kuu huwa pale mtoto kama huyo ni yatima na ndiye anayetegemewa na mhisani wake kuja kuwaauni ndugu zake, kama anao. Jamani, ubinadamu umeenda wapi?
    Sikitiko jingine ni pale watoto wanatekwa nyara na kutumikishwa vitani kupigana na mibabe wa kivita. Hii, bila shaka, ni dhuluma ya hali ya juu kwa watoto na ukiukaji mkubwa wa haki zao. Hebu niambie, mtoto mwenye uzani wa chini ya kilo arubaini kuvalishwa sare nzito za kijeshi na kubebeshwa bunduki au hata makombora ambayo yamewazidi uzani. Unyama ulioje huu?
    Pamoja na hayo, licha ya serikali za Afrika kuahidi mara kwa mara kwa vinywa vipana kuwa watalinda haki za kimsingi za kila mtoto katika himaya zao ambayo ni kuhakikisha wanapata lishe bora, wanaishi katika mazingira safi, wanapata elimu bora ya msingi na kupata tiba mwafaka - mamilioni ya watoto barani Afrika bado hawaendi shule kwa sababu ya changamoto mbalimbali. Aidha, wengine lukuki huaga kila mwaka kutokana na utapiamlo na ukosefu wa chakula. Dhana kuwa maradhi sugu yameangamizwa ni ya kupotosha kwani kila mwaka, maelfu ya watoto huaga kutokana na maradhi ya kuambukiza au yale yanayoweza kuzuiliwa au kutibiwa, kama malaria. Mamilioni ya wengine wangali
    wanaishi katika mitaa ya mabanda na hata kukosa huduma za kimsingi kama maji safi ya matumizi.
    Kwa kuwa changamoto hukabiliwa na changamoto, hakuna siku ambapo viongozi wataweza kumaliza utepetevu huu kimiujiza. Muhimu ni kwa kila kiongozi kuitazama jamii yake kwa jicho la ndani na kuweka mikakati ya namna bora ya kuikomboa kutoka katika rima la umaskini, magonjwa na ujinga.
    Hili litawezekana tu kwa kuwaona watu wote kuwa na umuhimu katika kuibadilisha jamii wala si kubagua kundi au jamii fulani na kuipendelea nyingine.
    a) Fafanua changamoto zinazomkabili mtoto wa Afrika kwa maneno 80.
    b) Bainisha mielekeo ambayo viongozi wa Afrika hukazania kuzingatia (maneno 65)

    Date posted: September 21, 2019.  Answers (1)

  • KUKITHIRI kwa visa vya utoaji wa hongo kwa wapiga kura walioshiriki chaguzi ndogo zilizofanyika Jumatatu katika eneobunge la Malindi na Kaunti ya Kericho ni ithibati...(Solved)

    Soma taarifa ifuatayo kisha ujibu maswali.
    KUKITHIRI kwa visa vya utoaji wa hongo kwa wapiga kura walioshiriki chaguzi ndogo zilizofanyika Jumatatu katika eneobunge la Malindi na Kaunti ya Kericho ni ithibati tosha kuwa ufisadi ume-kita mizizi nchini.
    Kadhalika, visa hivyo vilidhihirisha kuwa demokrasia imedidimia na taasisi za kupambana na visa vya ufisadi zimefifia.
    Mwezi uliopita, Wakenya kupitia mitandao ya kijamii walishtumu Rais wa Uganda Yoweri Museveni kutokana na kile walichotaja kuwa matumizi ya ‗mabavu‘ kuhifadhi kiti chake baada ya kuwatishia wapinzani wake.
    Watumiaji wa mitandao ya kijamii pia walimkosoa Rais Uhuru Kenyatta kwa kumpongeza mwenzake wa Uganda huku wakisema aliunga mkono ukandamizaji wa demokrasia.
    Lakini, visa vya uhongaji wa wapiga kura vilivyoshuhudiwa katika maeneo ya Malindi na Kericho vikitekelezwa na viongozi wa kisiasa hata wengine wakiwa wa muungano tawala wa Jubilee, ni dhihirisho tosha kuwa Wakenya hawakuwa na sababu ya kushutumu Rais Museveni.
    Utumiaji wa mabavu au kununua wapiga kura ili kushinda uchaguzi ni hujuma kwa demokrasia. Baadhi ya wanasiasa pia wameripotiwa kuwa wanatumia fedha zao kusafirisha watu kutoka eneo moja hadi jingine ili wajiandikishe kuwa wapiga kura na wawachague katika uchaguzi ujao. Huu pia ni ukiukaji wa misingi ya demokrasia.
    Ununuaji wa wapiga kura unamaanisha mabwanyenye ambao wamehusishwa na sakata mbalimbali za ufisadi ndio wataendelea kushikilia nyadhifa mbalimbali za uongozi kwa kuwa wao ndio wana mabunda ya fedha za kuhonga wapiga kura.
    Viongozi wanaochaguliwa baada ya kuwahonga wapiga kura hawatafanya maendeleo yoyote na badala yake, watakuwa wakihusika na wizi wa rasilimali za umma ili kupata fedha za kuwahonga watu katika uchaguzi unaofuatia. Mabwanyenye hawa wanafanya kila wawezalo kuhakikisha wapiga kura wanaendelea kuzama katika lindi la umaskini ili waweze kununuliwa kwa urahisi. Sawa na Esau tuliyeelezwa katika Biblia kwamba aliuza urithi wake wa kuzaliwa kwa Yakobo kwa kubadilishana na chakula, maskini pia wako tayari kuuza haki yao ya kuchagua kiongozi bora kwa shilingi mia moja.
    Viongozi wanaotoa hongo kwa wapiga kura kwa lengo la kushinda uchaguzi ni ishara kwamba hawana maono wala sera za mandeleo. Badala yake wanang‘ang‘ania mamlaka ili kujilimbikizia utajiri wala si kusaidia mpiga kura kujiinua kimaisha.
    Maswali
    a) Kwa kurejelea kifungu, visa vya kutoa rushwa kwa wapiga kura vinadhihirisha nini?
    b) Bainisha jinsi nne ambazo viongozi wa kisiasa wanatumia kuendeleza ukiukaji wa misingi ya demokrasia
    c) Fafanua athari za uozo unaorejelewa katika taarifa kwa
    (i) Viongozi
    (ii) Raia
    d) Thibitisha kuwa nyani haoni ngokoye katika muktadha wa makala haya.
    e) Eleza maana ya msamiati ufuatao kama ulivyotumika katika taarifa.
    (i) Mitandao ya kijamii
    (ii) Mabwanyenye

    Date posted: September 21, 2019.  Answers (1)

  • Eleza jinsi uwililugha unaweza kuleta athari katika lugha na mawasiliano miongoni mwa wanajamii.(Solved)

    Eleza jinsi uwililugha unaweza kuleta athari katika lugha na mawasiliano miongoni mwa wanajamii.

    Date posted: September 19, 2019.  Answers (1)

  • Eleza juhudi zozote tano zinazotumiwa kukiendeleza Kiswahili sanifu nchini Kenya.(Solved)

    Eleza juhudi zozote tano zinazotumiwa kukiendeleza Kiswahili sanifu nchini Kenya.

    Date posted: September 19, 2019.  Answers (1)

  • Tambua kishazi huru na kishazi tegemezi. Tumeanzisha shirika ili tunyanyue hali yetu.(Solved)

    Tambua kishazi huru na kishazi tegemezi.
    Tumeanzisha shirika ili tunyanyue hali yetu.

    Date posted: September 19, 2019.  Answers (1)

  • Kanusha sentensi hii Ugonjwa huu ungalidhibitiwa mapema kifo kingaliepukwa(Solved)

    Kanusha sentensi hii
    Ugonjwa huu ungalidhibitiwa mapema kifo kingaliepukwa

    Date posted: September 19, 2019.  Answers (1)

  • Badilisha katika kauli ya kutendua. Tundika picha hiyo ukutani na uyabandike maandishi kitabuni.(Solved)

    Badilisha katika kauli ya kutendua.
    Tundika picha hiyo ukutani na uyabandike maandishi kitabuni.

    Date posted: September 19, 2019.  Answers (1)

  • Tambua shamirisho kipozi, kitondo na shamirisho ala katika sentensi ifuatayo. Baba amemnunulia mtoto fulana nzuri iliyoshonwa kwa uzi mwekundu.(Solved)

    Tambua shamirisho kipozi, kitondo na shamirisho ala katika sentensi ifuatayo.
    Baba amemnunulia mtoto fulana nzuri iliyoshonwa kwa uzi mwekundu.

    Date posted: September 19, 2019.  Answers (1)

  • Andika katika msemo wa taarifa; "Tusipofanya kazi yetu kwa bidii na kujitegemea,tutabaki kuwa watumwa katika nchi yetu" Rais alisema.(Solved)

    Andika katika msemo wa taarifa;
    "Tusipofanya kazi yetu kwa bidii na kujitegemea,tutabaki kuwa watumwa katika nchi yetu" Rais alisema.

    Date posted: September 19, 2019.  Answers (1)

  • Kwa kutungia sentensi, tofautisha vitate hivi. i) Ghali ii) Gari(Solved)

    Kwa kutungia sentensi, tofautisha vitate hivi.
    i) Ghali
    ii) Gari

    Date posted: September 19, 2019.  Answers (1)

  • Tumia =O‘ rejeshi. i) Msichana ambaye huja ni mwanasheria ii) Maovu ambayo aliyatenda hayasahauliki(Solved)

    Tumia ‗O‘ rejeshi.
    i) Msichana ambaye huja ni mwanasheria
    ii) Maovu ambayo aliyatenda hayasahauliki

    Date posted: September 19, 2019.  Answers (1)

  • Tambua aina ya vitenzi kwa kutaja majina yake. Babu angali anasoma gazeti(Solved)

    Tambua aina ya vitenzi kwa kutaja majina yake.
    Babu angali anasoma gazeti.

    Date posted: September 19, 2019.  Answers (1)

  • Andika katika hali ya udogo Mbwa mwenye ukali alimfukuza mtoto(Solved)

    Andika katika hali ya udogo
    Mbwa mwenye ukali alimfukuza mtoto

    Date posted: September 19, 2019.  Answers (1)

  • Tambua na ueleze aina za vielezi katika sentinsi hizi. i) Mama alimwamrisha mtoto wake kijeshi ii) Askari hutembea makundi makundi(Solved)

    Tambua na ueleze aina za vielezi katika sentinsi hizi.
    i) Mama alimwamrisha mtoto wake kijeshi
    ii) Askari hutembea makundi makundi

    Date posted: September 19, 2019.  Answers (1)

  • Tunga sentensi kwa kutumia nomino katika ngeli ya pa- ku- mu.(Solved)

    Tunga sentensi kwa kutumia nomino katika ngeli ya pa- ku- mu.

    Date posted: September 19, 2019.  Answers (1)

  • Changanua sentensi ifuatayo kwa njia ya jedwali. Msichana mtukutu alifukuzwa shule leo asubuhi(Solved)

    Changanua sentensi ifuatayo kwa njia ya jedwali.
    Msichana mtukutu alifukuzwa shule leo asubuhi

    Date posted: September 19, 2019.  Answers (1)