buda - mwanaume aliyezeeka sana/ndovu mzee asiyekuwa na pembe/mtu asiye na meno
sharon kalunda answered the question on September 21, 2019 at 09:54
-
Tofautisha kwa kueleza maneno ya istilahi zifuatazo.
(i) Silabi funge
(ii) Silabi mwambatano
(Solved)
Tofautisha kwa kueleza maneno ya istilahi zifuatazo.
(i) Silabi funge
(ii) Silabi mwambatano
Date posted:
September 21, 2019
.
Answers (1)
-
Bainisha silabi katika neno lifuatalo.
Nyweshwa.
(Solved)
Bainisha silabi katika neno lifuatalo.
Nyweshwa.
Date posted:
September 21, 2019
.
Answers (1)
-
Andika sifa mbilimbili bainifu za sauti.
/gh/
/a/
(Solved)
Andika sifa mbilimbili bainifu za sauti.
/gh/
/a/
Date posted:
September 21, 2019
.
Answers (1)
-
Je, mtazamo hasi ni nini? Huwa na athari gani kwa binadamu? Mtazamo hasi ni kukata tamaa, kutamauka kuhusu hali, mtu au jambo fulani.
(Solved)
Soma makala haya kisha ujibu maswali yanayofuata.
Je, mtazamo hasi ni nini? Huwa na athari gani kwa binadamu? Mtazamo hasi ni kukata tamaa, kutamauka kuhusu hali, mtu au jambo fulani. Ni hisia ya kutotaka kushiriki wala kuhusishwa na jambo au hali fulani. Mtazamo huu ndio huwafanya wanafunzi wengi kuchukia au hata kudunisha baadhi ya masomo na walimu wanaoyafundisha. Licha ya wengi kuwa na mtazamo huu, kwa kweli huwa hawatambui. Asilimia kubwa ya wanaotambua hutatizika kujikwamua kutoka katika hali hii.
Inakadiriwa kwamba mtu wa wastani huwa na takribani mawazo elfu sitini ya kibinafsi kwa kila saa 24. Asilimia 95 ya fikra hizi huwa sawa na siku iliyotangulia, na asilimia 80 ya fikra hizi zilizorudiwa huwa hasi. Isitoshe, fikra hizi nyingi hutokea bila mtu mwenyewe kutambua na huwa ni mazoea. Hii ina maana kwamba watu wengi hawana ufahamu wa athari za fikra hizi maishani mwao.
Mitazamo hasi ina vyanzo na pia suluhu. Mwanzo kabisa ni imani potovu. Hiki ndicho chanzo cha mitazamo hasi. Kushikilia imani potovu kuhusu maisha pamoja na matukio fulani maishani hujenga mtazamo hasi. Unayaona maisha kwa macho ya imani zako na iwapo imani hizo ni potovu, basi hutayathamini maisha yako ili kukabiliana na hali hii, sharti kwanza ubadili imani yako. Uamini kwamba mabadiliko yanaweza kutokea na uchukue hatua ya kuanzisha mabadiliko hayo maishani mwako. Unahitaji kuepuka fikra hasi zinazoambatana na maisha yako ya awali na kulithamini kila tukio maishani kama tukio huru; Lisilo na uhusiano na yaliyowahi kukutamausha.
Kujikwamua kutoka katika imani duni unahitaji kuibuka na idadi kubwa ya imani chanya kuliko zilizo hasi kuhusu hali mahsusi. Baada ya hilo, zikabili imani zako potovu moja baada ya nyingine huku ukijiuliza endapo imani hizo ni kweli na endapo zina mashiko. Tumia dakika tano hivi kila siku kushadidiafikra chanya inayokinzana na ile inayokudidimiza. Ukifanya hivi kwa takriban siku thelathini imani yako itaanza kuchukua mkondo unaofaa. Familia yako na rafiki unaoandamana nao huathiri pakubwa hisia zako. Wakiwa na mtazamo hasi huweza kukushawishi ukaanza kuhisi wanavyohisi na kuyaona mambo kwa mtazamo wao. Kukabiliana na hali wapaswa kudhibiti hisia zako.
Tawala namna unavyohisi na kukabiliana na hali mbalimbali bila kuathiriwa na wandani hawa. Epuka wandani wa aina hii kadri inavyowezekana, ikiwezekana, jitenge nao ili ujifunze kuwa na uhuru wa kufanya maamuzi yako binafsi bila kuathiriwa nao. Unapaswa kupunguza ushirika hata na jamaa zako wanaokuingiza katika hali ya kutamauka. Punguza muda wa kukaa nao hasa wanapogeukia mkondo huu wa kukutatiza tamaa.
Mazingira hasi ni kizingiti kingine. Pengine huoni ukuruba baina ya maisha yako na mazingira unamokulia au unamokaa. Ukweli ni kwamba, huenda umedumu katika mazingira hayo na kuyazoea hata ukafikiri huwezi kuyabadilisha. Kadri unavyohisi huna uwezo wa kuyabadilisha ndivyo unajizamisha zaidi mtazamo hasi. Ili kukabiliana na hali hii, unahitaji kuelewa kwamba fikra zako au za watangulizi wako ndizo silikuingiza katika mazingira haya. Kwa hivyo, unapaswa kubadili mkondo wa fikra zako na kuanza kujaribu mazoezi ambayo umekuwa ukiyaona kama usiyoyaweza. Hatua kwa hatua utagundua panapo jitihada na uelekezi unaofaa kwamba mazoezi hayo yamekuwa mepesi na hivyo kukubakikishia kuyabadilisha mazingira yako.
unapojikuta ukilalamika jinsi ulivyokerwa na hali fulani, hii ndiyo sababu hasa ya kuwa na mtazamo hasi kuhusu hali hizo. Inaweza kukuwia vigumu kulikubali hili lakini kadiri utakavyolikubali mapema ndivyo utayaboresha maisha yako mapema. Kulalamika tu kutakudumisha katika hali zisizokuridhisha. Kwa hivyo, ili uyabadilishe maisha yako sharti ukome kulalamika tu kutakudumisha katika hali zisizokuridhisha. Kwa hivyo, ili uyabadilishe maisha yako sharti ukome kulalamika na kuanza kujikwamua toka kwenye hali hizo. Katika kufanikisha jambo lolote jema sharti viwepo vizingiti njiani. Mtendaji wa jambo lolote jema liwalo ana jukumu la kuibuka na mikakati mwafaka ya kuvikabili vizingiti hivi ili afanikishe ndoto yake. Hii ndiyo sababu unapaswa kuchukua hatua kutokea sasa ili kupanga na kutekeleza mikakati itakayoupindua mtazamo wako hasi uwe chanya. Kwa jinsi hii utayabadilisha maisha yako yawe ya kuridhisha zaidi na kuwa kielelezo kwa wengi waliotamaushwa na mitazamo hasi.
Maswali.
(a) Fupisha aya ya kwanza. (maneno 45-50)
(b) Eleza namna ya kukabiliana na mitazamo hasi. (maneno 70 - 80)
Date posted:
September 21, 2019
.
Answers (1)
-
Huku ukitoa mifano, bainisha mbinu mbili zinazotumiwa kuunda istilahi mpya katika jamii ya leo.
(Solved)
Huku ukitoa mifano, bainisha mbinu mbili zinazotumiwa kuunda istilahi mpya katika jamii ya leo.
Date posted:
September 21, 2019
.
Answers (1)
-
Fafanua jinsi mambo hafuatayo huweza kusababisha kutoweka kwa lugha:
i) Vita
ii) Ndoa za mseto
(Solved)
Fafanua jinsi mambo hafuatayo huweza kusababisha kutoweka kwa lugha:
i) Vita
ii) Ndoa za mseto
Date posted:
September 21, 2019
.
Answers (1)
-
Eleza sababu nne zinazowafanya vijana kupenda kutumia sheng' katika mawasiliano yao.
(Solved)
Eleza sababu nne zinazowafanya vijana kupenda kutumia sheng' katika mawasiliano yao.
Date posted:
September 21, 2019
.
Answers (1)
-
Andika methali inayoafiki maelezo:
Hakuna chema kisichokuwa na madhara.
(Solved)
Andika methali inayoafiki maelezo:
Hakuna chema kisichokuwa na madhara.
Date posted:
September 21, 2019
.
Answers (1)
-
Andika sentensi ifuatayo upya kwa kufuata maagizo.
Mama anapika kutwa kwa sababu ya wageni (Tilia mkazo kwa kinyume)
(Solved)
Andika sentensi ifuatayo upya kwa kufuata maagizo.
Mama anapika kutwa kwa sababu ya wageni (Tilia mkazo kwa kinyume)
Date posted:
September 21, 2019
.
Answers (1)
-
Kanusha sentensi ifuatayo katika hali ya mazoea.
Amekuja hapa.
(Solved)
Kanusha sentensi ifuatayo katika hali ya mazoea.
Amekuja hapa.
Date posted:
September 21, 2019
.
Answers (1)
-
Nomino zifuatazo zimo katika ngeli gani?
(i)Siwa
(ii)Kipunye
(Solved)
Nomino zifuatazo zimo katika ngeli gani?
(i)Siwa
(ii)Kipunye
Date posted:
September 21, 2019
.
Answers (1)
-
Changanua vipashio vya kisarufi katika kiarifa cha sentensi ifuatayo.
Hawa ndio waliopigana.
(Solved)
Changanua vipashio vya kisarufi katika kiarifa cha sentensi ifuatayo.
Hawa ndio waliopigana.
Date posted:
September 21, 2019
.
Answers (1)
-
Tunga sentensi mbili tofauti kudhihirisha kuwa neno "bunda" ni kitawe.
(Solved)
Tunga sentensi mbili tofauti kudhihirisha kuwa neno "bunda" ni kitawe.
Date posted:
September 21, 2019
.
Answers (1)
-
Andika visawe viwili vya nahau:
Fanya inda.
(Solved)
Andika visawe viwili vya nahau:
Fanya inda.
Date posted:
September 21, 2019
.
Answers (1)
-
Changanua sentensi ifuatayo kwa kielelezo cha jedwali:
Ule mkongojo ulioletewa babu utauzwa na fundi maarufu.
(Solved)
Changanua sentensi ifuatayo kwa kielelezo cha jedwali:
Ule mkongojo ulioletewa babu utauzwa na fundi maarufu.
Date posted:
September 21, 2019
.
Answers (1)
-
Ainisha virai katika sentensi ifuatayo.
Amenijibu kwa hasira.
(Solved)
Ainisha virai katika sentensi ifuatayo.
Amenijibu kwa hasira.
Date posted:
September 21, 2019
.
Answers (1)
-
Tumia mzizi- enye katika sentensi kama kihusishi.
(Solved)
Tumia mzizi- enye katika sentensi kama kihusishi.
Date posted:
September 21, 2019
.
Answers (1)
-
Ainisha maneno katika sentensi ifuatayo:-
Shehena ya dawa ilikuwa bandarini
(Solved)
Ainisha maneno katika sentensi ifuatayo:-
Shehena ya dawa ilikuwa bandarini
Date posted:
September 21, 2019
.
Answers (1)
-
Onyesha muundo wa silabi katika neno wachanjwao
(Solved)
Onyesha muundo wa silabi katika neno wachanjwao
Date posted:
September 21, 2019
.
Answers (1)
-
Andika neno lenye mfumo ufuatao wa vitamkwa. Nazali ya ufizi + kipasuo cha kaakaa gumu + irabu ya juu nyuma + kizuiwa ghuna cha kaakaa...
(Solved)
Andika neno lenye mfumo ufuatao wa vitamkwa. Nazali ya ufizi + kipasuo cha kaakaa gumu + irabu ya juu nyuma + kizuiwa ghuna cha kaakaa laini + irabu ya chini wastani.
Date posted:
September 21, 2019
.
Answers (1)