Get premium membership and access questions with answers, video lessons as well as revision papers.

Andika methali inayotumiwa kutuhimiza kuthamini vitu viliyo karibu kwani ndivyo vitufaavyo wakatiwa janga.

      

Andika methali inayotumiwa kutuhimiza kuthamini vitu viliyo karibu kwani ndivyo vitufaavyo wakati wa janga.

  

Answers


sharon
Fimbo ya mbali haiui nyoka.
Kamba ya mbali haifungi kuni
Hamadi kibindoni silaha mkononi.
sharon kalunda answered the question on September 21, 2019 at 10:37


Next: Determine the term independent of x in the expansion of
Previous: Make n the subject of the formula

View More Kiswahili Questions and Answers | Return to Questions Index


Learn High School English on YouTube

Related Questions


  • Bainisha aina za vishazi vilivyotumika katika sentensi hii; Kule alikoenda alilakiwa vizuri.(Solved)

    Bainisha aina za vishazi vilivyotumika katika sentensi hii;
    Kule alikoenda alilakiwa vizuri.

    Date posted: September 21, 2019.  Answers (1)

  • Unda kitenzi kutokana na nomino; abiria(Solved)

    Unda kitenzi kutokana na nomino;
    abiria

    Date posted: September 21, 2019.  Answers (1)

  • Kanusha katika wakati ujao hali timilifu. Bwana arusi alivaa suti ya kupendeza.(Solved)

    Kanusha katika wakati ujao hali timilifu.
    Bwana arusi alivaa suti ya kupendeza.

    Date posted: September 21, 2019.  Answers (1)

  • Andika kitenzi kifuatacho katika hali ya kuamrisha kwa wingi. (-la).(Solved)

    Andika kitenzi kifuatacho katika hali ya kuamrisha kwa wingi.
    (-la).

    Date posted: September 21, 2019.  Answers (1)

  • Andika kulingana na maagizo. Sherehe ilikuwa na walakini kwa kukosa mpambe. (Tumia neno lingine badala ya walakini)(Solved)

    Andika kulingana na maagizo.
    Sherehe ilikuwa na walakini kwa kukosa mpambe.
    (Tumia neno lingine badala ya walakini)

    Date posted: September 21, 2019.  Answers (1)

  • Andika katika umoja. Ile ya kujengea haijaletwa.(Solved)

    Andika katika umoja.
    Ile ya kujengea haijaletwa.

    Date posted: September 21, 2019.  Answers (1)

  • Bainisha aina za nomino zilizotumika katika sentensi ifuatayo. Wema alimpa mtoto yule maji ya baraka.(Solved)

    Bainisha aina za nomino zilizotumika katika sentensi ifuatayo.
    Wema alimpa mtoto yule maji ya baraka.

    Date posted: September 21, 2019.  Answers (1)

  • Ainisha uamilifu wa viambishi katika neno lifuatalo. Alimlilia.(Solved)

    Ainisha uamilifu wa viambishi katika neno lifuatalo.
    Alimlilia.

    Date posted: September 21, 2019.  Answers (1)

  • Eleza maana ya buda.(Solved)

    Eleza maana ya buda.

    Date posted: September 21, 2019.  Answers (1)

  • Tofautisha kwa kueleza maneno ya istilahi zifuatazo. (i) Silabi funge (ii) Silabi mwambatano(Solved)

    Tofautisha kwa kueleza maneno ya istilahi zifuatazo.
    (i) Silabi funge
    (ii) Silabi mwambatano

    Date posted: September 21, 2019.  Answers (1)

  • Bainisha silabi katika neno lifuatalo. Nyweshwa.(Solved)

    Bainisha silabi katika neno lifuatalo.
    Nyweshwa.

    Date posted: September 21, 2019.  Answers (1)

  • Andika sifa mbilimbili bainifu za sauti. /gh/ /a/(Solved)

    Andika sifa mbilimbili bainifu za sauti.
    /gh/
    /a/

    Date posted: September 21, 2019.  Answers (1)

  • Je, mtazamo hasi ni nini? Huwa na athari gani kwa binadamu? Mtazamo hasi ni kukata tamaa, kutamauka kuhusu hali, mtu au jambo fulani.(Solved)

    Soma makala haya kisha ujibu maswali yanayofuata.
    Je, mtazamo hasi ni nini? Huwa na athari gani kwa binadamu? Mtazamo hasi ni kukata tamaa, kutamauka kuhusu hali, mtu au jambo fulani. Ni hisia ya kutotaka kushiriki wala kuhusishwa na jambo au hali fulani. Mtazamo huu ndio huwafanya wanafunzi wengi kuchukia au hata kudunisha baadhi ya masomo na walimu wanaoyafundisha. Licha ya wengi kuwa na mtazamo huu, kwa kweli huwa hawatambui. Asilimia kubwa ya wanaotambua hutatizika kujikwamua kutoka katika hali hii.
    Inakadiriwa kwamba mtu wa wastani huwa na takribani mawazo elfu sitini ya kibinafsi kwa kila saa 24. Asilimia 95 ya fikra hizi huwa sawa na siku iliyotangulia, na asilimia 80 ya fikra hizi zilizorudiwa huwa hasi. Isitoshe, fikra hizi nyingi hutokea bila mtu mwenyewe kutambua na huwa ni mazoea. Hii ina maana kwamba watu wengi hawana ufahamu wa athari za fikra hizi maishani mwao.
    Mitazamo hasi ina vyanzo na pia suluhu. Mwanzo kabisa ni imani potovu. Hiki ndicho chanzo cha mitazamo hasi. Kushikilia imani potovu kuhusu maisha pamoja na matukio fulani maishani hujenga mtazamo hasi. Unayaona maisha kwa macho ya imani zako na iwapo imani hizo ni potovu, basi hutayathamini maisha yako ili kukabiliana na hali hii, sharti kwanza ubadili imani yako. Uamini kwamba mabadiliko yanaweza kutokea na uchukue hatua ya kuanzisha mabadiliko hayo maishani mwako. Unahitaji kuepuka fikra hasi zinazoambatana na maisha yako ya awali na kulithamini kila tukio maishani kama tukio huru; Lisilo na uhusiano na yaliyowahi kukutamausha.
    Kujikwamua kutoka katika imani duni unahitaji kuibuka na idadi kubwa ya imani chanya kuliko zilizo hasi kuhusu hali mahsusi. Baada ya hilo, zikabili imani zako potovu moja baada ya nyingine huku ukijiuliza endapo imani hizo ni kweli na endapo zina mashiko. Tumia dakika tano hivi kila siku kushadidiafikra chanya inayokinzana na ile inayokudidimiza. Ukifanya hivi kwa takriban siku thelathini imani yako itaanza kuchukua mkondo unaofaa. Familia yako na rafiki unaoandamana nao huathiri pakubwa hisia zako. Wakiwa na mtazamo hasi huweza kukushawishi ukaanza kuhisi wanavyohisi na kuyaona mambo kwa mtazamo wao. Kukabiliana na hali wapaswa kudhibiti hisia zako.
    Tawala namna unavyohisi na kukabiliana na hali mbalimbali bila kuathiriwa na wandani hawa. Epuka wandani wa aina hii kadri inavyowezekana, ikiwezekana, jitenge nao ili ujifunze kuwa na uhuru wa kufanya maamuzi yako binafsi bila kuathiriwa nao. Unapaswa kupunguza ushirika hata na jamaa zako wanaokuingiza katika hali ya kutamauka. Punguza muda wa kukaa nao hasa wanapogeukia mkondo huu wa kukutatiza tamaa.
    Mazingira hasi ni kizingiti kingine. Pengine huoni ukuruba baina ya maisha yako na mazingira unamokulia au unamokaa. Ukweli ni kwamba, huenda umedumu katika mazingira hayo na kuyazoea hata ukafikiri huwezi kuyabadilisha. Kadri unavyohisi huna uwezo wa kuyabadilisha ndivyo unajizamisha zaidi mtazamo hasi. Ili kukabiliana na hali hii, unahitaji kuelewa kwamba fikra zako au za watangulizi wako ndizo silikuingiza katika mazingira haya. Kwa hivyo, unapaswa kubadili mkondo wa fikra zako na kuanza kujaribu mazoezi ambayo umekuwa ukiyaona kama usiyoyaweza. Hatua kwa hatua utagundua panapo jitihada na uelekezi unaofaa kwamba mazoezi hayo yamekuwa mepesi na hivyo kukubakikishia kuyabadilisha mazingira yako.
    unapojikuta ukilalamika jinsi ulivyokerwa na hali fulani, hii ndiyo sababu hasa ya kuwa na mtazamo hasi kuhusu hali hizo. Inaweza kukuwia vigumu kulikubali hili lakini kadiri utakavyolikubali mapema ndivyo utayaboresha maisha yako mapema. Kulalamika tu kutakudumisha katika hali zisizokuridhisha. Kwa hivyo, ili uyabadilishe maisha yako sharti ukome kulalamika tu kutakudumisha katika hali zisizokuridhisha. Kwa hivyo, ili uyabadilishe maisha yako sharti ukome kulalamika na kuanza kujikwamua toka kwenye hali hizo. Katika kufanikisha jambo lolote jema sharti viwepo vizingiti njiani. Mtendaji wa jambo lolote jema liwalo ana jukumu la kuibuka na mikakati mwafaka ya kuvikabili vizingiti hivi ili afanikishe ndoto yake. Hii ndiyo sababu unapaswa kuchukua hatua kutokea sasa ili kupanga na kutekeleza mikakati itakayoupindua mtazamo wako hasi uwe chanya. Kwa jinsi hii utayabadilisha maisha yako yawe ya kuridhisha zaidi na kuwa kielelezo kwa wengi waliotamaushwa na mitazamo hasi.
    Maswali.

    (a) Fupisha aya ya kwanza. (maneno 45-50)
    (b) Eleza namna ya kukabiliana na mitazamo hasi. (maneno 70 - 80)

    Date posted: September 21, 2019.  Answers (1)

  • Imefika wakati ambapo kila mmoja lazima ajiulize swali kuhusu tuelekeapo kama jamii, mustakabali wa kizazi cha sasa ni upi?(Solved)

    Soma kifungu kifuatacho kisha ujibu maswali yafuatayo.
    Imefika wakati ambapo kila mmoja lazima ajiulize swali kuhusu tuelekeapo kama jamii, mustakabali wa kizazi cha sasa ni upi?
    Nauliza swali kuhusiana na misururu ya visa ambayo kwa kweli imeibua hofu na wasiwasi kuhusu msingi wa kimaadili miongoni mwa vijana wetu. Kuna hatari ijapo; mbaya sana. Ni hali ambayo huenda ikatusahaulisha msingi wa tulikotoka na tuelekeapo.
    Kwanza, ni kisa cha Alhamisi usiku ambapo zaidi ya vijana 300 walinaswa katika nyumba moja katika mtaa wa Phenom, Nairobi katika kile kiliaminika kuwa ―hafla ya ukosefu wa maadili‖. Kisa hicho kilikujia siku chache baada ya serikali kupiga marufuku hafla moja ya burudani na ukosefu wa maadili maarufu ―Project X‖ ambapo vijana walikuwa wakitarajiwa kuhudhuria.
    Kulingana na taarifa za ‗kanuni‘ za tamasha hiyo, vijana walitakiwa kuvaa mavazi mafupi ambayo yanaonyesha sehemu zao za mwili kwa wazi. Taarifa zilisema kuwa washiriki pia wangeruhusiwa kucheza densi wakiwa uchi kama mojawapo ya kanuni za burudani. Isitoshe, kisa hicho kinakujia baada ya vingine vingi, ambapo vijana wamenaswa na maafisa wa polisi wakijiburudisha kwa vileo katika klabu nyakati za usiku. Vile vile wanafunzi wengi wamenaswa wakishiriki katika vitendo vya ukosefu wa maadili. Baadhi ya wanafunzi hao huwa chini ya miaka 18! Jijini Nairobi visa hivyo vimekuwa kama ―hali za kawaida‖.
    Yasikitisha kuwa nyakati za wikendi hutakosa kuona kila aina ya vioja na viroja, hasa katika maeneo ya mijini. Ni nyakati hizi ambapo mabinti huenda katika vituo vya burudani wakiwa wamevaa kila aina ya mavazi. La kushangaza ni kuwa, mabinti hao hushindana kuhusu mbinu za ―kuonyesha‖ uchi wao kwa njia mbalimbali. Kwa haya yote, kile kinadhihirika ni kuwa jamii yetu inaelekea kubaya tu katika safari ya kifo. Safari hii huenda ikatufikisha Jehanamu ambayo kuna uwezekano wa kutojikomboa. Kilicho wazi ni kwamba msingi wetu wa kimaadili umeterereka kiasi cha kutorekebika kabisa. Nchi imegeuka jaa la mwigo wa tamaduni zote za kimagharibi. Kwa mfano, tamasha ya Project X ni mwigo wa filamu maarufu ya wanafunzi wa shule za upili iliyorekodiwa nchini Amerika kwenye filamu hivyo, wanafunzi hao wanajihusisha katika kila aina ya uovu wa kimaadili, ufasiri wake mkuu ukiwa ni ‗burudani‘ kwa msingi wa tamaduni za kimagharibi.Kikweli, huu si msimamo wa tamaduni za Kiafrika. Huu si msingi wetu wa kimadili hata kidogo!.Huu ni mwigo wa kishetani ambao lengo lake ni kuizamisha jamii yetu katika lindi la mgogoro wa kitamaduni na kimaadili.
    Mawali.
    a. Maadili ya vijana yamezorota. Kwa mujibu wa taarifa hii thibitisha kauli hii.
    b. Ni nini asili ya projct X‘?
    c. Nyakati za wikendi hutakosa kuona kila aina ya vioja na viroja. Fafanua.
    d. Mwandishi ana maana gani anaposema visa hivyo vimekuwa kama hali za kawaida‘.
    e. Mwandishi ana msimamo upi kuhusu tamaduni za kimagharibi.
    f. Eleza maana ya msamiati ufuatao kama ulivyotumika kwenye kifungu.
    (i) Kupiga marufuku
    (ii) Mustakabali
    (iii) Umetetereka
    (iv) Filamu

    Date posted: September 21, 2019.  Answers (1)

  • Huku ukitoa mifano, bainisha mbinu mbili zinazotumiwa kuunda istilahi mpya katika jamii ya leo.(Solved)

    Huku ukitoa mifano, bainisha mbinu mbili zinazotumiwa kuunda istilahi mpya katika jamii ya leo.

    Date posted: September 21, 2019.  Answers (1)

  • Fafanua jinsi mambo hafuatayo huweza kusababisha kutoweka kwa lugha: i) Vita ii) Ndoa za mseto(Solved)

    Fafanua jinsi mambo hafuatayo huweza kusababisha kutoweka kwa lugha:
    i) Vita
    ii) Ndoa za mseto

    Date posted: September 21, 2019.  Answers (1)

  • Eleza sababu nne zinazowafanya vijana kupenda kutumia sheng' katika mawasiliano yao.(Solved)

    Eleza sababu nne zinazowafanya vijana kupenda kutumia sheng' katika mawasiliano yao.

    Date posted: September 21, 2019.  Answers (1)

  • Andika methali inayoafiki maelezo: Hakuna chema kisichokuwa na madhara.(Solved)

    Andika methali inayoafiki maelezo:
    Hakuna chema kisichokuwa na madhara.

    Date posted: September 21, 2019.  Answers (1)

  • Andika sentensi ifuatayo upya kwa kufuata maagizo. Mama anapika kutwa kwa sababu ya wageni (Tilia mkazo kwa kinyume)(Solved)

    Andika sentensi ifuatayo upya kwa kufuata maagizo.
    Mama anapika kutwa kwa sababu ya wageni (Tilia mkazo kwa kinyume)

    Date posted: September 21, 2019.  Answers (1)

  • Unganisha sentensi zifuatazo kwa kugeuza moja kuwa kishazi tegemezi i) Majisifu aliingia ukumbini ii) Sote tulisimama(Solved)

    Unganisha sentensi zifuatazo kwa kugeuza moja kuwa kishazi tegemezi
    i) Majisifu aliingia ukumbini
    ii) Sote tulisimama

    Date posted: September 21, 2019.  Answers (1)