
(a) Bainisha muktadha wa dondoo hili.
1. Ni maneno ya mwandishi/msimulizi.
2. Anamrejelea Lunga Kiriri Kangata
3. Ni baada ya kutolewa katika Msitu wa Mamba.
4. Moyo wa Lunga ulikuwa umekataa kuyakubali mazingira mapya katika Mlima wa Simba.
(b) Eleza sifa tatu za anayerejelewa.
1. Msomi – alikuwa anasomea kilimo ambapo baadaye aliajiriwa kama Afisa wa Kilimo nyanjani.
2. Mhifadhi mazingira/mwajibikaji – aliasisi Chama cha Watunza Mazingira wasio na Mipaka akiwa shuleni. Anawahutubia kuhusu uhifadhi wa mazingira.
3. Mwenye bidii – baada ya kustaafishwa anafanya kazi ya ukulima kwa bidii hadi anaitwa jina la msimbo ‘ mkulima namba wani’.
4. Mwenye msimamo thabiti – licha ya rai za wakubwa anapinga tendo la kuwapa raia mahindi yaliyoharibika.
5. Mtetezi wa haki – anahiari kupoteza riziki ili kuyaokoa maisha ya wanyonge wasio na hatia.
6. Mwenye tamaa- anapoona uzuri wa zao la mahindi katika shamba la babake, anapatwa na uchu unaolemaza uadilifu wake.
7. Mwenye mapenzi ya dhati – anajisabilia kwa hali na mali kumridhia na kumpendeza mkewe.
(c) Eleza tamathali ya usemi katika dondoo.
Tashbihi – alijiona kama mfa maji
d)Fafanua masaibu yaliyomkumba mrejelewa
1. Kuachishwa kazi kwa kupinga uagizaji wa mahindi mabaya.
2. Kufukuzwa katika Msitu wa Mamba hivyo kupoteza mali yake yote.
3. Anakosa pesa za kuwapeleka wanawe hata katika shule za watu wa kima wastani kwa sababu alilipwa fidia isiyotosha.
4. Anawapoteza ndugu na marafiki zake.
5. Kuachwa na mkewe Naomi.
6. Kufurushwa kutoka kwa Kiriri wakati wa wa zahama baada ya kutawazwa
(e) Huku ukitoa mifano riwayani, jadili matatizo yanayowakumba wanajamii katika ndoa.
i. Wanaume kushtakiwa kwa kubaka wake zao. Tete anasema kuwa sheria hiyo inamnyima mwanaume haki ya kuhusiana kimapenzi na mkewe.
ii. Upweke katika ndoa unaosababisha majonzi na hata kifo - Kiriri anaaga dunia kutokana na kihoro cha kufilisika na ukiwa alioachiwa na mkewe, Annete.
iii. Umaskini unasambaratisha ndoa. Ndoa ya Lunga na Naomi inavunjika kutokana na hali ya umaskini.
iv. Kuna uzinifu katika ndoa - Bwana Tenge alizini na wanawake wengi mkewe Bi. Kimai alipoenda mashambani.
v. Wakwe kuingilia ndoa - Ndoa kati ya Subira na Kaizari inavunjika kwa kuwa Subira alihisi kuwa anaonewa hasa na mama mkwe; vivyo hivyo na ile ya Selume.
vi. Kutofautiana kimsimamo/ kisiasa - Selume analaumiwa kwa kumuunga mkono Mwekevu ambaye alikuwa mpinzani mkuu wa muwaania kiti waliyemuunga mkono wakweze. (uk. 30)
vii. Ukabila - Selume anaachwa na mkewe na kumwoa mke mwingine kutoka kabila lake.
viii. Kukosa kupata watoto katika ndoa - Neema anakosa kujaliwa kupata watoto
marto answered the question on September 24, 2019 at 07:59
-
Alifa chokocho na Dumu Kayanda: Tumbo Lisiloshiba
'Doa ndio kawaida inayobainisha maisha ya mwanadamu.'Onyesha ukweli wa kauli hii kwa mujibu wa hadithi za: Shogake Dada ana...
(Solved)
Alifa chokocho na Dumu Kayanda: Tumbo Lisiloshiba
'Doa ndio kawaida inayobainisha maisha ya mwanadamu.'Onyesha ukweli wa kauli hii kwa mujibu wa hadithi za: Shogake Dada ana Ndevu, Mame Bakari, Shibe Inatumaliza na Mtihani wa Maisha.
Date posted:
September 24, 2019
.
Answers (1)
-
Taja baadhi ya maudhui yanayojitokeza katika hadithi ya tumbo lisiloshiba?
(Solved)
Taja baadhi ya maudhui yanayojitokeza katika hadithi ya tumbo lisiloshiba?
Date posted:
September 18, 2019
.
Answers (1)
-
Taja mifano ya taswira katika hadithi ya tumbo lisiloshiba?
(Solved)
Taja mifano ya taswira katika hadithi ya tumbo lisiloshiba?
Date posted:
September 18, 2019
.
Answers (1)
-
Taja vipera vya mazungumzo
(Solved)
Taja vipera vya mazungumzo
Date posted:
August 24, 2019
.
Answers (1)
-
RIWAYA
S.A MOHAMED: UTENGANO
“ Katu asingajitia kibuibui na kutanga na njia. Lo, kachoshwa na shimiri za baruti
anazoshindiliwa moyoni mwake.”
a) eleza muktadha wa dondoo hili.
b) taja na...
(Solved)
RIWAYA
S.A MOHAMED: UTENGANO
“ Katu asingajitia kibuibui na kutanga na njia. Lo, kachoshwa na shimiri za baruti
anazoshindiliwa moyoni mwake.”
a) eleza muktadha wa dondoo hili.
b) taja na ufafunue tamathali ya usemi iliyotumika katika dondoo hili
c) Eleza umuhimu wa kisa kinachorejelewa na dondoo.
d) kwa kurejelea matukio mengine katika riwaya ya Utengano, fafanua maudhui
mawili yayoashiriwa na dondoo hili.
Date posted:
June 29, 2019
.
Answers (1)
-
Bainisha maudhui yanayojitokeza katika riwaya ya chozi la heri
(Solved)
Bainisha maudhui yanayojitokeza katika riwaya ya chozi la heri
Date posted:
June 14, 2019
.
Answers (1)
-
Damu Nyeusi
Jadili maudhui ya elimu kwa mujibu wa "Kanda la Usufi", "Shaka ya Mambo"
na "Tazama na Mauti"
(Solved)
Damu Nyeusi
Jadili maudhui ya elimu kwa mujibu wa "Kanda la Usufi", "Shaka ya Mambo"
na "Tazama na Mauti"
Date posted:
May 7, 2019
.
Answers (1)
-
Fafanua jinsi mwandishi wa ‘Tumbo Lisiloshiba’ alivyotumia kinaya kufanikisha maudhui yake
(Solved)
Fafanua jinsi mwandishi wa ‘Tumbo Lisiloshiba’ alivyotumia kinaya kufanikisha maudhui yake
Date posted:
May 6, 2019
.
Answers (1)
-
Fafanua changamoto zinazokabili asasi ya ndoa ukirejelea hadithi ya Masharti ya kisasa
(Solved)
Fafanua changamoto zinazokabili asasi ya ndoa ukirejelea hadithi ya Masharti ya kisasa
Date posted:
May 6, 2019
.
Answers (1)
-
Ulezi umewapa wazazi wengi changamoto nyingi. Ukirejelea hadithi ya shogake, dada ana ndevu dhihirisha ukweli wa kauli hii
(Solved)
Ulezi umewapa wazazi wengi changamoto nyingi. Ukirejelea hadithi ya shogake, dada ana ndevu dhihirisha ukweli wa kauli hii
Date posted:
May 6, 2019
.
Answers (1)
-
Dhihirisha ukweli wa methali “mzoea sahani vya vigae haviwezi” katika hadithi ya mapenzi ya kifaurongo
(Solved)
Dhihirisha ukweli wa methali “mzoea sahani vya vigae haviwezi” katika hadithi ya mapenzi ya kifaurongo
Date posted:
May 6, 2019
.
Answers (1)
-
Jadili matatizo yanayowakumba wakaazi wa Madongo poromoka katika tumbo lisiloshiba
(Solved)
Jadili matatizo yanayowakumba wakaazi wa Madongo poromoka katika tumbo lisiloshiba
Date posted:
May 6, 2019
.
Answers (1)
-
Jadili maudhui ya usaliti katika hadithi ,’Mapenzi ya kifaurongo’ na ‘Mame Bakari.
(Solved)
Jadili maudhui ya usaliti katika hadithi ,’Mapenzi ya kifaurongo’ na ‘Mame Bakari.
Date posted:
May 6, 2019
.
Answers (1)
-
Thibitisha kuwa ulitima ni kati ya maudhui ya hadithi ya mkubwa.
(Solved)
Thibitisha kuwa ulitima ni kati ya maudhui ya hadithi ya mkubwa.
Date posted:
May 6, 2019
.
Answers (1)
-
Mhini na mhiniwa njia yao moja. Jadili ukweli wa methali hii ukirejelea hadithi ya mkubwa
(Solved)
Mhini na mhiniwa njia yao moja. Jadili ukweli wa methali hii ukirejelea hadithi ya mkubwa
Date posted:
May 6, 2019
.
Answers (1)
-
Kwa kurejelea hadithi zozote tano katika ‘Tumbo lisiloshiba na Hadithi nyingine’, fafanua maudhui ya utabaka.
(Solved)
Kwa kurejelea hadithi zozote tano katika ‘Tumbo lisiloshiba na Hadithi nyingine’, fafanua maudhui ya utabaka.
Date posted:
May 6, 2019
.
Answers (1)
-
Fafanua sifa kumi za mzee Mago katika hadithi ya tumbo lisiloshiba.
(Solved)
Fafanua sifa kumi za mzee Mago katika hadithi ya tumbo lisiloshiba.
Date posted:
May 6, 2019
.
Answers (1)
-
Kwa kurejelea hadithi ya Tumbo Lisiloshiba na ya Mapenzi ya Kifaurongo, fafanua maudhui ya utabaka.
(Solved)
Kwa kurejelea hadithi ya Tumbo Lisiloshiba na ya Mapenzi ya Kifaurongo, fafanua maudhui ya utabaka.
Date posted:
May 6, 2019
.
Answers (1)
-
‘Shogake dada ana ndevu’ Safia
Eleza sifa za wahusika wafuatao.
i) Mwalimu Musi
ii) Jairo
iii) Sera
iv) Mke wa Jairo
(Solved)
‘Shogake dada ana ndevu’ Safia
Eleza sifa za wahusika wafuatao.
i) Mwalimu Musi
ii) Jairo
iii) Sera
iv) Mke wa Jairo
Date posted:
May 6, 2019
.
Answers (1)
-
Huku ukirejelea diwani ya Tumbo lisiloshiba fafanua matatizo yanayokumba vijana katika jamii
(Solved)
Huku ukirejelea diwani ya Tumbo lisiloshiba fafanua matatizo yanayokumba vijana katika jamii
Date posted:
May 6, 2019
.
Answers (1)