Get premium membership and access questions with answers, video lessons as well as revision papers.

Eleza matumizi ya kiambishi "ku" Kulia kwake kulisababisha msongamano wa watu alikoKuwa.

      

Eleza matumizi ya kiambishi "ku"
Kulia kwake Kulisababisha msongamano wa watu alikoKuwa.

  

Answers


sharon
- Kiambishi cha kitenzi
- Ngeli
- Mahali
sharon kalunda answered the question on September 24, 2019 at 13:05


Next: Solve for q in the equation Sin (3? + 1200) = v3/2 in the range 0= ? = 1800
Previous: Rationalize the denominator leaving your answer in the form a+bvc where a, b and c are constants

View More Kiswahili Questions and Answers | Return to Questions Index


Learn High School English on YouTube

Related Questions


  • Nomino zifuatazo zinapatikana katika ngeli zipi? i) Chumvi: ii) Nywele: iii) Mafuta:(Solved)

    Nomino zifuatazo zinapatikana katika ngeli zipi?
    i) Chumvi:
    ii) Nywele:
    iii) Mafuta:

    Date posted: September 24, 2019.  Answers (1)

  • Ukitolea mfano mwafaka, fafanua majukumu yoyote manne ya viambishi awali.(Solved)

    Ukitolea mfano mwafaka, fafanua majukumu yoyote manne ya viambishi awali.

    Date posted: September 24, 2019.  Answers (1)

  • Eleza maana ya mghuno katika lugha ya Kiswahili.(Solved)

    Eleza maana ya mghuno katika lugha ya Kiswahili.

    Date posted: September 24, 2019.  Answers (1)

  • Serikali kupitia Wizara ya Elimu imetoa mwongozo wa karo ambao unastahili kuzingatiwa katika shule za upili kufuatia haua ya shule mbalimbali kuongeza karo kwa viwango...(Solved)

    Serikali kupitia Wizara ya Elimu imetoa mwongozo wa karo ambao unastahili kuzingatiwa katika shule za upili kufuatia haua ya shule mbalimbali kuongeza karo kwa viwango mbalimbali. Hatua hiyo inadhamiriwa kumking mzazi dhidi ya kunyanyaswa kifedha walimu hasa ikizangiwa kuwa gharama ya maisha imepanda mara dufu.Hata hivyo, ingekuwa bora ikiwa serikali ingefanya maamzi kwa ushirikiano na walimu wakuu maana kwa hakika suala la karo linahusu matumizi ya fedha ambayo pia huja na gharama zake. Gharama hii inaokana na ununuzi wa vitabu vya Kada na vya mazoezi, karatasi za uchapishaji mitihani, kwa kuwa wanafunzi sharti wasome na waandike.Vilevile, gharama hii inatokana na ununuzi wa kemikali za kutumiwa katika maabara. Aidha kuna gharama ya kuendesha michezo na tamasha za muziki na drama. Wanafunzi wa shule za malazi hula na kulala na kwa sababu hiyo maamuzi ya kifedha lazima yafanywe.Jambo ambalo linastahili kuangaliwa kwa makini ni viwanga vya kupanda kwa gharama ya maisha. Lazima tujiulize gharama hiyo imepanda kwa kiasi gani na wapi? Kwa kweli haiwezekani kununua kilo moja ya mahindi kwa bei hiyo hiyo Kitale, Mombasa na Turkana. Vile vile ni muhimu kujiuliza ikiwa shule husika ni ya mashambani au ya mjini? Kwa hivyo sharti la kifedha ni muhimu katika kuamua karo ya shule na maeneo mbalimbali nchini.Pili, hebu tuangalie ikiwa shule inavyohusika ni ya kiwango cha kaunti ndogo, kaunti au cha kitaifa. Hili ni muhimu kwa kuwa hali ya masomo katika shule hizo hutofautiana. Tofauti kuu hutokana na miundomisingi na programu za masomo zinazoendeshwa.Kwa mfano, programu za kitahmini, kompyuta na zinazohusu ziara huhitaji fedha nyingi. Shule ambayo ina masomo kama vile muziki, sanaa na sayansikimu sharti zitoze karo ya juu kwa kuwa masomo hayo huandamana na gharama ya kununua vyombo na vyakula? Sasa mbona fedha za ziada? Wanaotetea kupunguzwa kwa karo wana punguza mchango wa motisha katika ufanifu wa masomo. Ndio, baadhi ya shule hutoza karo ya juu ili kuwamotisha walimu kwa vyakula na kwa zawadi ili kuwastahi wanapopata matokea mema. Hali hiyo huwafanya kujikakamua kazini na kutoa huduma ya hali ya juu.Fedha za ziada vile vile, hutumiwa kuwajiri walimu wa ziada ikizingatiwa kuwa serikali haijawaajiri walimu wa kutosha. Pia katika baadhi ya shule, wanafunzi huandaliwa vyakula spesheli tofauti na mseto wa maharagwe na mahindi almarufu "maram" uliozoeleka katika shule nyingi ikumbukwe kuwe lishe bora ni mojawapo ya haki za kimsingi kwa watoto ambayo sharti iheshimiwe.Kwa marefu na mafupi yake, serikali haipaswi kuweka viwango sawa vya karo kwa kila shule kwa maana hilo huenda likazua mgogoro wa kiutawala katika shule nyingi. Shinikizo za kupunguzwa kwa karo inayotozwa hasa katika shule za upili zinafaa kutetewa kimantiki wala si kihisia.Mambo huenda yangekuwa tofauti ikiwa serikali ingewajibika kwa upande wake kwa kuwaajiri walimu wa kutosha kuwaongeza walimu mshahara na kuwatambua kwa zawadi wanapofanya kazi nzuri na kuwapandisha vyeo. Hata hivyo, mgala muue na haki umpe; hatua kali zinapaswa kuchukuliwa dhidi ya walimu wanaowatoza wazazi karo ya juu kupindukia ili kuendeleza maslahi yao ya kibinafsi.Naamini kuwa hatua ya Waziri wa Elimu kukutana na washikadau katika sekta ya elimu kuhusu karo na uteuzi wa wanafunzi wa kujiunga na shule za upili ni ya busara na inafaa kuta mwelekeo mzuri kuhusu masuala tata yaliyopo kwa sasa.

    (a) Fafanua mambo muhimu yanayostahili kuzingatiwa katika kutathmini viwango vya karo katika shule nchini Kenya.(Maneno 65 – 70)
    (b) Fupisha aya tatu za mwisho.(maneno 40 – 45)

    Date posted: September 24, 2019.  Answers (1)

  • Waziri wa uchukuzi Bwana Msafiri ametoa mwito kwa kila mwananchi kusingatia sheria za barabarani ili kumaliza visa vya ajali vilivyokithiri.(Solved)

    Soma kifungu kifuatacho kisha ujibu maswali.
    Waziri wa uchukuzi Bwana Msafiri ametoa mwito kwa kila mwananchi kusingatia sheria za barabarani ili kumaliza visa vya ajali vilivyokithiri. Alisema kuwa ongezeko la ajali za barabarani linachangiwa pakubwa na watu binafsi.Akiongea katika hafla ya kuzindua mbinu za kuhakikisha usalama barabarani, Bwana Msafiri alisema yasikitisha kuona kuwa ajali za barabarani zimeongezeka katika siku za hivi majuzi. Alielezea kuwa wizara yake imekerwa na utekelezaji wa majukumu na mapuza miongoni mwa wanaohusika na sekta ya uchukuzi.Alisema wengi wa wenye magari wamepuza masharti mengi ambayo yaliwekwa na wizara, yaliyokusudiwa kugunguza ajali. Alisema magari mengi yamekuwa kachara na kwamba mengi yameng‘olewa vidhibiti mwendo. Basi magari yanaendeshwa kwa kasi ya umeme. Hili limeongeza ajali kwa kiasi kikubwa. Mengi hayana mishipi ya usalama na wasafiri hukabiliwa na hatari wanaposafiri. Aliongeza kuwa sura ya magari hayo ni dhihirisho kuwa wenye magari wamepotoka kabisa, ―magari mengi yamerembeshwa hata kwa picha chafu, jambo linalodhihirisha utovo wa mbeko na kutofuata sheria. Mengine yanacheza muziki kwa sauti ya juu hivi kwamba hata dereva na utingo hawawezi kusikia grudumu liking‘oka. Baadhi yao yanaonyesha picha chafu chafu za video na kuufanya usafiri kuwa vyumba vya sinema chafu!‖ Alisema kutovaa sare kwa madereva na makondakta na kuwapakia abiria kupita kiasi ni kilele cha upuui wa sheria zilizowekwa.
    Wasafiri pia wanapuuza masharti yaliyowekwa kwa lengo la kuwafaa, ―alisema waziri. Alisikitika kuwa wasafiri wengi hawafungi mishipi ya usalama hata inapopatikana, aidha wanakubali kuingia magari yaliyojaa tayari, hali inayoongenzea uwezekano wa gari kupata ajali kwa kulemewa na uzito. Aliwakumbusha kuwa gali likipata ajali wakiwa wamepakiwa hivi, hawezi kugharamiwa na bima ya gari kwa vile bima yenyewe hukatiwa idadi mahususi ya wasafiri. Aliwalaumu watembeaji barabarani kwa kutozingatia sheria za kawaida. Alisema kwa mfano katika gurufu kuna mahali ambako kuna vivuko ila hawavitumii na wengine huishia kugongwa na magari.Mwisho aliwalaumu maafisa wa trafiki wanaotekeleza majukumu yao. Akitisha kuwachukulia hatua kali, alisema kuwa yaskitisha kusikia kuwa wanachukua kadhongo na kuyaachilia magari yaliyo na kasoro badala ya kuyashtaki kulingana na sheria. Aliwaongezea lawama wasafiri kwa kunyamaza wanapoyaona haya yakitendeka machoni. Alisababisha kicheko aliposema kuwa baadhi ya wasafiri huwahimiza makondakta watoe chai haraka ili waendelee na usafiri ya bila kujali hatari wanazojiingiza kwazo.
    Akionya kuwa angechukua hatua ya kuregesha utulivu, alihitimisha kwa kusema kuwa wizara yake limetoa ilani kwa watumiaji wote wa barabarani. Alitoa makataa ya siku kumi na nne ambapo yoyote asiyefuata kaida zote za barabarani atachukuliwa hatua kisheria.

    a) Fafanua sababu za mwito wa waziri wa uchukuzi Bwana Msafiri?
    b) Eleza jinsi wenye magaari wamechangia katika kukithiri kwa visa vya ajali barabarani?
    c) Fafanua mchango wa wasafiri katika kudorora kwa hali ya usalama barabarani.
    d) Eleza majukumu ya maafisa wa trafiki katika kudumisha usafiri kulingana na ufahamu.
    e) Toa visawe vya maneno yafuatayo.
    (i) Kondakta:
    (ii) Toa ilani:
    (iii) Toa makataa:

    Date posted: September 24, 2019.  Answers (1)

  • Ainisha mofimu katika neno: Walichimba(Solved)

    Ainisha mofimu katika neno:
    Walichimba

    Date posted: September 24, 2019.  Answers (1)

  • Huku ukitumia mifano, tofautisha sentensi ambatano na sentensi changamano.(Solved)

    Huku ukitumia mifano, tofautisha sentensi ambatano na sentensi changamano.

    Date posted: September 24, 2019.  Answers (1)

  • Geuza sentensi hii hadi usemi wa taarifa: "sitakuja shuleni kesho", mwalimu mkuu akasema,nitaenda kuhudhuria mkutano Mombasa.(Solved)

    Geuza sentensi hii hadi usemi wa taarifa:
    "sitakuja shuleni kesho", mwalimu mkuu akasema,nitaenda kuhudhuria mkutano Mombasa.

    Date posted: September 24, 2019.  Answers (1)

  • Tunga sentensi moja kutofautisha "thibiti" na "dhibiti".(Solved)

    Tunga sentensi moja kutofautisha "thibiti" na "dhibiti".

    Date posted: September 24, 2019.  Answers (1)

  • Andika katika ukubwa. Mke wa mzee huyu hupenda watoto sana.(Solved)

    Andika katika ukubwa.
    Mke wa mzee huyu hupenda watoto sana.

    Date posted: September 24, 2019.  Answers (1)

  • Changanua kwa kutumia mchoro wa matawi. Mvuvi hodari alifurahi alipofanikiwa kuvua jodari.(Solved)

    Changanua kwa kutumia mchoro wa matawi.
    Mvuvi hodari alifurahi alipofanikiwa kuvua jodari.

    Date posted: September 24, 2019.  Answers (1)

  • Kanusha Mwanafunzi ambaye amefika ametuzwa.(Solved)

    Kanusha
    Mwanafunzi ambaye amefika ametuzwa.

    Date posted: September 24, 2019.  Answers (1)

  • Andika ngeli za nomino zifuatazo. (i) Uwele (ii) Vita(Solved)

    Andika ngeli za nomino zifuatazo.
    (i) Uwele
    (ii) Vita

    Date posted: September 24, 2019.  Answers (1)

  • Weka vitenzi hivi katika hali ya kuamrisha wingi. (i) -nywa (ii) Tubu(Solved)

    Weka vitenzi hivi katika hali ya kuamrisha wingi.
    (i) -nywa
    (ii) Tubu

    Date posted: September 24, 2019.  Answers (1)

  • Eleza matumizi ya "na" katika sentensi ifuatayo. Simba aliuawa na wawindaji haramu nasi tukawaripoti.(Solved)

    Eleza matumizi ya "na" katika sentensi ifuatayo.
    Simba aliuawa na wawindaji haramu nasi tukawaripoti.

    Date posted: September 24, 2019.  Answers (1)

  • Tumia kiwakilishi cha nafsi huru (nafsi ya pili wingi) katika sentensi.(Solved)

    Tumia kiwakilishi cha nafsi huru (nafsi ya pili wingi) katika sentensi.

    Date posted: September 24, 2019.  Answers (1)

  • Andika sentensi hii upya bila kubadilisha maana ukitumia "O" rejeshi. Mwanafunzi alitumwa nyumbani juzi na hajapata karo hadi leo.(Solved)

    Andika sentensi hii upya bila kubadilisha maana ukitumia "O" rejeshi.
    Mwanafunzi alitumwa nyumbani juzi na hajapata karo hadi leo.

    Date posted: September 24, 2019.  Answers (1)

  • Onyesha aina ya virai katika sentensi ifuatayo.Mwanafunzi mzuri husoma ndani ya darasa.(Solved)

    Onyesha aina ya virai katika sentensi ifuatayo.Mwanafunzi mzuri husoma ndani ya darasa.

    Date posted: September 24, 2019.  Answers (1)

  • Taja sauti zozote mbili zinazotamkiwa kwenye kaakaa gumu.(Solved)

    Taja sauti zozote mbili zinazotamkiwa kwenye kaakaa gumu.

    Date posted: September 24, 2019.  Answers (1)

  • Bwana Spika, ninaomba kufahamishwa kwa nini Waziri wa Biashara ameshindwa kuchukua hatua kukomesha uuzaji wa vileo hatari kwa watoto wa shule. (a) Fafanua sifa zozote tano...(Solved)

    Bwana Spika, ninaomba kufahamishwa kwa nini Waziri wa Biashara ameshindwa kuchukua hatua kukomesha uuzaji wa vileo hatari kwa watoto wa shule.

    (a) Fafanua sifa zozote tano za sajili inayorejelewa na maneno haya

    b)Eleza mambo yaliyochangia msambao wa Lugha ya Kiswahili kabla ya kuondoka kwa wakoloni barani

    Date posted: September 24, 2019.  Answers (1)