Get premium membership and access questions with answers, video lessons as well as revision papers.

"Ingawa walifahamu sababu ya kuitwa pale mpango uliokuwepo ulikuwa usiku wa giza."

      

Damu Nyeusi na Hadithi nyingine : Ken Walibora na Said A. Mohamed
"Ingawa walifahamu sababu ya kuitwa pale mpango uliokuwepo ulikuwa usiku wa giza."
(a) Fafanua muktadha wa maneno haya.
(b) Eleza tamathali iliyotumika katika dondoo hili.
(c) Onyesha vile wahusika mbalimbali hadithini waiivyoathiriwa na sababu ya kuitwa pale.

  

Answers


sharon
a) -Haya ni maelezo ya mwandishi
- Anawarejelea Sela na wasichana wengine wawili waliokuwa wameitwa na Bi Margaret
-Walikuwa katika chumba cha mapokezi
-Walikuwa wameitwa na Bi Margaret walipokuwa gwarideni na kuwataka wafike ofisini mwake 4x1 = 4
b) Istiara - mpango ulikuwa usiku wa giza
c)- Sela alifukuzwa shuleni na Bi Margaret kuwataka wazazi wake kumtafutia shule mbadala
Sela alikosa utulivu masomoni alipogunduliwa kuwa alikuwa na ujauzito
- Sela na wenzake waliaibika si haba majina yao yaliposomwa gwarideni
- Sela na mamake walifukuzwa nyumbani na mzee Butali na kukaa na jamaa zao kwa
- majuma matatu.
- Sela alilazimika kukaa nyumbani kwa miezi mitatu akikitunza kitoto kisha kurejea shuleni
- Masazu alikosa makini masomoni na hakuendeleza elimu yake baada ya kidato cha nne na kuambulia tu kazi ya vibarua.
- Sela aliandamwa na majuto kwa kuwa hakuwa na uhakika kuhusu mkondo arnbao maisha yake yangechukua
- Kutokana na umaskini uliowakumba Kadogo alivalishwa matambara alipozaliwa
- Sela, Masazu na Kadogo wanaangamia wakati Sela na Masazu walipokwenda kumchukua Kadogo kwa kuwa hawangemudu utaratibu ufaao.
- Mzee Butali alichanganyikiwa na kujawa na hasira kwa kuwa pesa alizomlipia Sela shuleni hazikuzaa matunda.
sharon kalunda answered the question on September 25, 2019 at 07:40


Next: Highlight four factors that may be considered by an insurance firm before determining Premiums to be charged for life assurance policy.
Previous: A pure Red flowered plant was crossed with a pure white flowered plant. All the F1 generation plants had pink flowers (a) Give an explanation for...

View More Kiswahili Questions and Answers | Return to Questions Index


Learn High School English on YouTube

Related Questions