
(a) Ujumbe wa mshairi.
(i) Anazungumzia kuhusu watu wapendao kusuta wengine.
(ii) Anazungumzia pia, watu ambao hupenda kusema ya wengine.
(b) Muundo wa ubeti wa tatu.
(i) Mishororo minne.
(ii) Vina vya kati (yo) na mwisho (sha) isipokuwa mshororo wa kipokeo; kina cha kati (sha) na mwisho (ya)
(iii) Mizani ni 16 kila mshororo.
(iv) Kila mshororo umegawika katika pande mbili.
(c) Aina ya ushairi;
Tarbia / unne - kila ubeti una mishororo minne.
(d) Arudhi za utunzi;
(i) Kila ubeti una mishororo minne.
(ii) Kila mshororo umegawanyika katika vipande viwili; ukwapi na utao.
(iii) Mizani 16 kila mshororo ; 8 kila kipande.
(iv) Kibwagizo cha aina ya kiishio / kimalizio.
(e) Toni ya mshairi;
(i) Malalamishi.
(ii) Ya onyo.
(iii) Kushtumu / kusuta.
(f) Lugha nathari;
(i) Mshairi anazungumzia yampatayo anapowazia mambo ya nyumbani. Huelezwa hali za kiafya za watu wake ambazo huonekana kuwa taabani. Hataki kuelezewa porojo kwani hayamhusu yeyote.
(g) Uhuru wa mshairi;
(i) Tabdila - ndiya badala ya njia
- ondokeya badala ya ondokea.
- sikiya badala ya sikia
- hunijiya badala ya hunijia
(ii) Mazida - Maiisha badala ya maisha
- Haistahamilikii badala ya haistahimiliki
- Siitaki badala ya sitaki
(iii) Inkisari - n‘ondokeya badala ya uniondokee.
- kunambiya badala ya kuniambia.
- Kaziyo badala ya kazi yako
(iv) lahoja - ndiya badala ya njia
- nde badala ya nje
- hino badla ya hiyo
- ziwate badala ya ziwache
(h) Msamiati.
(i) ndiya - njia
(ii) kisahani - fujo
(iii) nde – nje
sharon kalunda answered the question on October 1, 2019 at 10:57
-
Ajaye kisimani mbele hunywa maji maenge,
(Solved)
Soma ushairi ufuatao kisha ujibu maswali.
1. Ajaye kisimani mbele hunywa maji maenge,
Asinywe yalo na vunju,
Yakampa kigegezi,
Yakamkibua roho akaona na kinyaa,
Awali ndio awali, awali mbovu hamna.
2. Kiwa utalimatia.
Utayaramba makombo,
Utadata vitu cheche,
Kisomo chenye dhamana kikakupa kisogo,
Inajuzu ujihimu
Mwanafuu darasani,
Urauka po mapema,
Katu hutayaramba makombo,
Hutakosa kisebeho.
3. Dereva hata utingo,
Natija ni asubuhi,
Wateja utawawahi,
Wasaa kuzingatia,
Uwafikishe kazini,
Kwa wasaa ufaao,
Wasije wakateteshwa,
Na bosi wao kazini,
Nao wakakuapiza.
4. Na ewe mwanazaraa,
Mpini uukamate,
Kabla jua kuwaka sana,
Majasho kutiririsha mwilini,
Yang‘oe yote magugu,
Kutoka kwa lako konde.
5. Mhadimu mwenye ajizi,
Yakujuza ujihimu,
Ununue na maziwa,
Majogoo uyawahi mapema,
Usije ukayadata,
Chai mkandaa ukaandaa,
Wateja wakuambae mithili ya ibilisi.
Maswali
(a) Eleza nasaha yoyote inayotolewa kwa wafanyakazi wowote watatu kwenye shairi.
(b) Taja sifa zozote za kimuundo zilizotumiwa na mtunzi.
(c) Eleza toni ya mshairi.
(d) Nafsi nenewa anahimizwa kufanya nini.
(e) Andika ubeti wa tatu kwa lugha tutumbi.
(f) Toa mifano miwili ya uhuru wa mshairi.
(g) Eleza maana ya misamiati ifuatayo kama ilivyotumiwa kwenye shairi.
(i) Maji maenge
(ii) Natija
(iii) Majogoo
Date posted:
October 1, 2019
.
Answers (1)
-
Kufariki kwa kitoto Uhuru ni jazanda inayoashiria hali halisi ya mambo riwayani "kidagaa kimemwozea". Jadili
(Solved)
Kufariki kwa kitoto Uhuru ni jazanda inayoashiria hali halisi ya mambo riwayani "kidagaa kimemwozea". Jadili.
Date posted:
October 1, 2019
.
Answers (1)
-
Onyesha jinsi ukatili unavyojitokeza kwa kurejelea hadithi zifuatazo.
(Solved)
Onyesha jinsi ukatili unavyojitokeza kwa kurejelea hadithi zifuatazo.
(i) Kanda la usufi
(ii) Shaka ya mambo
(iii) Mwana wa darubini
(iv) Ndoa ya Samani.
Date posted:
October 1, 2019
.
Answers (1)
-
Thibitisha jinsi anwani "Damu Nyeusi" inaafiki yaliyomo katika hadithi.
(Solved)
Thibitisha jinsi anwani "Damu Nyeusi" inaafiki yaliyomo katika hadithi.
Date posted:
October 1, 2019
.
Answers (1)
-
Jadili matatizo KUMI ya kijamii ukirejelea hadithi "Mwana wa Darubini"
(Solved)
Jadili matatizo KUMI ya kijamii ukirejelea hadithi "Mwana wa Darubini"
Date posted:
October 1, 2019
.
Answers (1)
-
Riwaya ya kidagaa kimemwozea inaonyesha jitihada za vijana kujenga jamii mpya. Thibitisha kwa kutoa mifano
(Solved)
Riwaya ya kidagaa kimemwozea inaonyesha jitihada za vijana kujenga jamii mpya. Thibitisha kwa kutoa mifano
Date posted:
October 1, 2019
.
Answers (1)
-
Kwa kurejelea tamthilia ya Mstahiki Meya, fafanua vichocheo vya migogoro katika jamii ya Cheneo.
(Solved)
Kwa kurejelea tamthilia ya Mstahiki Meya, fafanua vichocheo vya migogoro katika jamii ya Cheneo.
Date posted:
October 1, 2019
.
Answers (1)
-
Matambiko ni nini? Eleza dhima zake mbili.
(Solved)
Matambiko ni nini? Eleza dhima zake mbili.
Date posted:
October 1, 2019
.
Answers (1)
-
Eleza maana ya maapizo.
(Solved)
Eleza maana ya maapizo.
Date posted:
October 1, 2019
.
Answers (1)
-
Eleza maana ya ngoma katika fasihi simulizi kisha utoe dhima zake nne.
(Solved)
Eleza maana ya ngoma katika fasihi simulizi kisha utoe dhima zake nne.
Date posted:
October 1, 2019
.
Answers (1)
-
Mtu mmoja alimpa mke wake nambari yake ya simu.
(Solved)
Soma utungo ufuatao kisha ujibu maswali.
Mtu mmoja alimpa mke wake nambari yake ya simu. Kila mara bibi akipigia mumewe simu, ilipokelewa na sauti nyororo "mteja wa nambari uliopiga hapatikani kwa sasa."Alifunga safari kumtembelea mume wake mjini na kukabiliana na huyu kisura.
MASWALI
a) Bainisha kipera cha utungo huu.
b) Onyesha sifa tano za kipera hiki.
c) Eleza manufaa tano ya kipera hiki.
Date posted:
October 1, 2019
.
Answers (1)
-
a) Kanda la usufi ni anwani mwafaka.
Fafanua kwa kutolea mifano.
(b) Lini angepata nafasi ya kupenya kwenye chungio…"
Fafanua jinsi msemewa angepata nafasi na changamoto zake.
(Solved)
Kanda la Usufi - (R. Nyaga)
(a) Kanda la usufi ni anwani mwafaka.
Fafanua kwa kutolea mifano.
(b) Lini angepata nafasi ya kupenya kwenye chungio…"
Fafanua jinsi msemewa angepata nafasi na changamoto zake.
Date posted:
October 1, 2019
.
Answers (1)
-
Assumpta Matei: Chozi la Heri
Alijiona kama mfa maji ambaye anakabiliwa na mtutumo wa mawimbi ya misiba, mmoja baada ya mwingine.
(a) Bainisha muktadha wa dondoo hili....
(Solved)
Assumpta Matei: Chozi la Heri
Alijiona kama mfa maji ambaye anakabiliwa na mtutumo wa mawimbi ya misiba, mmoja baada ya mwingine.
(a) Bainisha muktadha wa dondoo hili.
(b) Eleza sifa tatu za anayerejelewa katika dondoo hili.
(c) Eleza tamathali ya usemi iliyotumika katika dondoo hili.
(d) Fafanua masaibu yaliyomkumba mrejelewa.
(e) Huku ukitolea mifano riwayani, jadili matatizo yanayowakumba wanajamii katika ndoa.
Date posted:
September 24, 2019
.
Answers (1)
-
Alifa chokocho na Dumu Kayanda: Tumbo Lisiloshiba
'Doa ndio kawaida inayobainisha maisha ya mwanadamu.'Onyesha ukweli wa kauli hii kwa mujibu wa hadithi za: Shogake Dada ana...
(Solved)
Alifa chokocho na Dumu Kayanda: Tumbo Lisiloshiba
'Doa ndio kawaida inayobainisha maisha ya mwanadamu.'Onyesha ukweli wa kauli hii kwa mujibu wa hadithi za: Shogake Dada ana Ndevu, Mame Bakari, Shibe Inatumaliza na Mtihani wa Maisha.
Date posted:
September 24, 2019
.
Answers (1)
-
Taja baadhi ya maudhui yanayojitokeza katika hadithi ya tumbo lisiloshiba?
(Solved)
Taja baadhi ya maudhui yanayojitokeza katika hadithi ya tumbo lisiloshiba?
Date posted:
September 18, 2019
.
Answers (1)
-
Taja mifano ya taswira katika hadithi ya tumbo lisiloshiba?
(Solved)
Taja mifano ya taswira katika hadithi ya tumbo lisiloshiba?
Date posted:
September 18, 2019
.
Answers (1)
-
Taja vipera vya mazungumzo
(Solved)
Taja vipera vya mazungumzo
Date posted:
August 24, 2019
.
Answers (1)
-
RIWAYA
S.A MOHAMED: UTENGANO
“ Katu asingajitia kibuibui na kutanga na njia. Lo, kachoshwa na shimiri za baruti
anazoshindiliwa moyoni mwake.”
a) eleza muktadha wa dondoo hili.
b) taja na...
(Solved)
RIWAYA
S.A MOHAMED: UTENGANO
“ Katu asingajitia kibuibui na kutanga na njia. Lo, kachoshwa na shimiri za baruti
anazoshindiliwa moyoni mwake.”
a) eleza muktadha wa dondoo hili.
b) taja na ufafunue tamathali ya usemi iliyotumika katika dondoo hili
c) Eleza umuhimu wa kisa kinachorejelewa na dondoo.
d) kwa kurejelea matukio mengine katika riwaya ya Utengano, fafanua maudhui
mawili yayoashiriwa na dondoo hili.
Date posted:
June 29, 2019
.
Answers (1)
-
Bainisha maudhui yanayojitokeza katika riwaya ya chozi la heri
(Solved)
Bainisha maudhui yanayojitokeza katika riwaya ya chozi la heri
Date posted:
June 14, 2019
.
Answers (1)
-
Damu Nyeusi
Jadili maudhui ya elimu kwa mujibu wa "Kanda la Usufi", "Shaka ya Mambo"
na "Tazama na Mauti"
(Solved)
Damu Nyeusi
Jadili maudhui ya elimu kwa mujibu wa "Kanda la Usufi", "Shaka ya Mambo"
na "Tazama na Mauti"
Date posted:
May 7, 2019
.
Answers (1)