Trusted since 2008
Study resources on Kenyaplex

Get ready-made curriculum aligned revision materials

Exam papers, notes, holiday assignments and topical questions – all aligned to the Kenyan curriculum.

"………Alimaliza kwa kuandika, "yajayo yapokee"

Damu Nveusi na Hadithi nyingine
"………Alimaliza kwa kuandika, "yajayo yapokee"
(a) Eleza muktadha wa dondoo hili.
(b) Thibitisha ufaafu wa anwani ya hadithi hii.

Answers


sharon
a).Haya ni maneno ya mwandishi
- Akimrejelea Masazu
- Ni maneno aliyoandika katika barua ya kumjibu Sela
- Sela amegundua kuwa ana mimba ndipo anamjulisha Masazu. Maneno hayo yanaonyesha kuwa Masazu hakuchukulia suala la ujauzito kwa Sela kuwa zito 4x1 =4
b) i) Anwani ni kanda la usufi - maana yake ni kuwa shida za watu wengine ni shida zao na haziwahusu wengine
- Baada ya Masazu kumpachika Sela mimba na kutaarifiwa anamlaumu kwa kutojikinga na kumwambia yajapo yapokee, kwake ni jambo rahisi
- Mzee Butali alipoitwa shuleni na kujulishwa kuwa bintiye ni mjamzito, hachukuiii suala la ulezi kwa uzito
- analielekeza kwa mwalimu mkuu Bi Margaret
- Bi Margaret alipoita majina ya wanafunzi watatu gwarideni, wanafunzi waliangua kicheko
- Mzee Butali alimlaumu mkewe na bintiye kwa shida iliyoikabili familia yake
- Rozina hakujali na litakalowapata Masazu na Sela usiku wenye mvua nyingi na kiza tele
- Bi Margaret hakujali hatima ya wasichana watatu kwani alitaka waende shule za kutwa
- Sela alisitisha masomo ilhaii Masazu aliachwa akisoma ingawa wote walikuwa wahusika Masazu haguswi na jambo hili
- Mwajiri wa Masazu alimpa mshahara mdogo hakujali matatizo yake
- Wazazi wa Sela hawakujali uzito wa Masazu wa Sela. Walimtaka Masazu atimize matakwa ya utamaduni ndipo waungane na mtoto wao
sharon kalunda answered the question on October 1, 2019 at 12:18

Answer Attachments

Exams With Marking Schemes

Related Questions

  • "Alikuwa na kiu lakini si ya maji, kadhalika alikuwa na njaa lakini si ya chakula Habebeki mwanamume habebeki……." (Solved)

    Kidagaa kimemwozea
    "Alikuwa na kiu lakini si ya maji, kadhalika alikuwa na njaa lakini si ya chakula Habebeki mwanamume habebeki……."
    (a) Weka dondoo hili katika muktadha wake .
    (b) Eleza tamathali mbili zilizotumika katika dondoo hili.
    (c) Eleza aina za kiu na njaa zilizomkumba mrejelewa wa kwanza.
    (d) Mrejelewa wa pili alishindwa mtihani wa maisha. Jadili.

    Date posted: October 1, 2019 .    Answers (1)

  • "Duniani kuna watu na viatu" (Solved)

    Tamthilia nzima ya Mstahiki Meya.
    "Duniani kuna watu na viatu"
    (a) Fafanua muktadha wa dondoo hili.
    (b) Thibitisha ukweli wa kauli hii ukirejelea tamthilia nzima ya Mstahiki Meya.

    Date posted: October 1, 2019 .    Answers (1)

  • Mwandishi wa tamthilia ya Mstahiki Meya ametumia wahusika kukuza kazi yake, Thibitisha kauii hili kwa kuwarejelea wahusika wafuatao. (Solved)

    Mwandishi wa tamthilia ya Mstahiki Meya ametumia wahusika kukuza kazi yake, Thibitisha kauii hili kwa kuwarejelea wahusika wafuatao.
    (i) Diwani wa tatu
    (ii) Bili
    (iii) Mhubiri
    (iv) Diwani I na II

    Date posted: October 1, 2019 .    Answers (1)

  • Kila nikaapo hushika tama. (Solved)

    Kila nikaapo hushika tama
    Na kuwazia hali inayonizunguka.
    Huyawazia madhila
    Huziwazia shida
    Huiwazia dhiki

    Dhiki ya ulezi
    Shida ya kudhalilishwa kazini.
    Madhila ya kufanyiwa dharau
    Kwa sababu ya jinsia ya kike.

    Hukaa na kujidadisi
    Hujidadisi kujua kwa nini
    Jamii haikisikii kilio changu
    Wenzangu hawanishiki mikono
    Bali wananidharau kwa kuukosoa utamaduni

    Hukaa na kujiuliza
    I wapi raha yangu uiimwengu huu?
    I wapi jamaa nzima ya wanawake?

    MASWALI
    (a) Shairi hili ni la aina. gani? Eleza
    (b) Eleza dhamira ya mtunzi wa shairi hili.
    (c) Kwa kutolea mifano eleza maana ya mistari mishata.
    (d) Taja na ueleze tamathali mbili zilizotumika katika shairi hili.
    (e) Tambulisha nafsi-neni katika shairi hili.
    (f) Fafanua toni ya shairi hili.
    (g) Fafanua maudhui mawili ya shairi hili.
    (h) Onyesha namna nafasi neni anavyosalitiwa.
    (i) Eleza maana ya maneno haya kama yalivyotumiwa katika shairi.
    (i) Madhila
    (ii) Kudhalilishwa.

    Date posted: October 1, 2019 .    Answers (1)

  • Wasiwasi n‘ondokeya, ondoka enenda zako, (Solved)

    Soma ushairi ufuatao kisha ujibu maswali.
    1. Wasiwasi n‘ondokeya, ondoka enenda zako,
    Ondoka andama ndiya, nondosheya uso wako,
    Ondoka wanisikiya, ziwate jeuri zako,
    Jishughulishe na yako, yangu wayatakiyani?

    2. Wasiwasi siitaki, suhuba yako si nzuri,
    Haistahamilikii, uovu umekithiri,
    Inganyoshwa hainyoki, ikukutene kikiri,
    Sikati yako shari, enda zako wasiwasi.

    3. Huna kazi ufanyayo, ela kuwafitinisha,
    Viumbe na zao nyoyo, vitina kuwagotanisha,
    Hiino ndio kaziyo, yenye kukufurahisha,
    Ni kazi isiyokuchosha, mno umeizoeya.

    4. Mara waja na habari, mambo yalivyo nyumbani,
    Ati mambo si mazuri, mambo yote tatashani,
    Wanitaka nifikiri, usemayo ni yakini,
    Nisononeke moyoni, upate kufurahika.

    5. Au mara hunijiya, na kingine kisahani,
    Kuhusu zao afiya, hao waliyo nyumbani,
    Huwa husishi nambiya, hali zao taabani,
    Zingawa wakati gani? Ni zako au ni zao?

    6. Na mara kuja mambiya, nitakapotoka humu,
    Na kwamba yaningojea, nde maisha magumu,
    Uliloni kusudiya, ni kunitiya wazimu,
    Kama ndiyo yako hamu, basi unshatahayari.

    (a) Eleza ujumbe uliojitokeza katika shairi hili.
    (b) Fafanua muundo wa ubeti wa tatu.
    (c) Eleza aina ya shairi hili.
    (d) Fafanua arudhi za utunzi alizozingatia mshairi.
    (e) Eleza toni ya mshairi.
    (f) Andika ubeti wa tano katika lugha ya kinathari.
    (g) Eleza mifano mitatu ya uhuru wa mshairi.
    (h) Eleza maana ya misamiati ifuatayokama ilivyotumika katika shairi.
    (i) ndiya
    (ii) kisahani
    (iii) nde

    Date posted: October 1, 2019 .    Answers (1)

  • Ajaye kisimani mbele hunywa maji maenge, (Solved)

    Soma ushairi ufuatao kisha ujibu maswali.
    1. Ajaye kisimani mbele hunywa maji maenge,
    Asinywe yalo na vunju,
    Yakampa kigegezi,
    Yakamkibua roho akaona na kinyaa,
    Awali ndio awali, awali mbovu hamna.

    2. Kiwa utalimatia.
    Utayaramba makombo,
    Utadata vitu cheche,
    Kisomo chenye dhamana kikakupa kisogo,
    Inajuzu ujihimu
    Mwanafuu darasani,
    Urauka po mapema,
    Katu hutayaramba makombo,
    Hutakosa kisebeho.

    3. Dereva hata utingo,
    Natija ni asubuhi,
    Wateja utawawahi,
    Wasaa kuzingatia,
    Uwafikishe kazini,
    Kwa wasaa ufaao,
    Wasije wakateteshwa,
    Na bosi wao kazini,
    Nao wakakuapiza.

    4. Na ewe mwanazaraa,
    Mpini uukamate,
    Kabla jua kuwaka sana,
    Majasho kutiririsha mwilini,
    Yang‘oe yote magugu,
    Kutoka kwa lako konde.

    5. Mhadimu mwenye ajizi,
    Yakujuza ujihimu,
    Ununue na maziwa,
    Majogoo uyawahi mapema,
    Usije ukayadata,
    Chai mkandaa ukaandaa,
    Wateja wakuambae mithili ya ibilisi.

    Maswali
    (a) Eleza nasaha yoyote inayotolewa kwa wafanyakazi wowote watatu kwenye shairi.
    (b) Taja sifa zozote za kimuundo zilizotumiwa na mtunzi.
    (c) Eleza toni ya mshairi.
    (d) Nafsi nenewa anahimizwa kufanya nini.
    (e) Andika ubeti wa tatu kwa lugha tutumbi.
    (f) Toa mifano miwili ya uhuru wa mshairi.
    (g) Eleza maana ya misamiati ifuatayo kama ilivyotumiwa kwenye shairi.
    (i) Maji maenge
    (ii) Natija
    (iii) Majogoo

    Date posted: October 1, 2019 .    Answers (1)

  • Kufariki kwa kitoto Uhuru ni jazanda inayoashiria hali halisi ya mambo riwayani "kidagaa kimemwozea". Jadili (Solved)

    Kufariki kwa kitoto Uhuru ni jazanda inayoashiria hali halisi ya mambo riwayani "kidagaa kimemwozea". Jadili.

    Date posted: October 1, 2019 .    Answers (1)

  • Onyesha jinsi ukatili unavyojitokeza kwa kurejelea hadithi zifuatazo. (Solved)

    Onyesha jinsi ukatili unavyojitokeza kwa kurejelea hadithi zifuatazo.
    (i) Kanda la usufi
    (ii) Shaka ya mambo
    (iii) Mwana wa darubini
    (iv) Ndoa ya Samani.

    Date posted: October 1, 2019 .    Answers (1)

  • Thibitisha jinsi anwani "Damu Nyeusi" inaafiki yaliyomo katika hadithi. (Solved)

    Thibitisha jinsi anwani "Damu Nyeusi" inaafiki yaliyomo katika hadithi.

    Date posted: October 1, 2019 .    Answers (1)

  • Jadili matatizo KUMI ya kijamii ukirejelea hadithi "Mwana wa Darubini" (Solved)

    Jadili matatizo KUMI ya kijamii ukirejelea hadithi "Mwana wa Darubini"

    Date posted: October 1, 2019 .    Answers (1)

  • Riwaya ya kidagaa kimemwozea inaonyesha jitihada za vijana kujenga jamii mpya. Thibitisha kwa kutoa mifano (Solved)

    Riwaya ya kidagaa kimemwozea inaonyesha jitihada za vijana kujenga jamii mpya. Thibitisha kwa kutoa mifano

    Date posted: October 1, 2019 .    Answers (1)

  • Kwa kurejelea tamthilia ya Mstahiki Meya, fafanua vichocheo vya migogoro katika jamii ya Cheneo. (Solved)

    Kwa kurejelea tamthilia ya Mstahiki Meya, fafanua vichocheo vya migogoro katika jamii ya Cheneo.

    Date posted: October 1, 2019 .    Answers (1)

  • Matambiko ni nini? Eleza dhima zake mbili. (Solved)

    Matambiko ni nini? Eleza dhima zake mbili.

    Date posted: October 1, 2019 .    Answers (1)

  • Eleza maana ya maapizo. (Solved)

    Eleza maana ya maapizo.

    Date posted: October 1, 2019 .    Answers (1)

  • Eleza maana ya ngoma katika fasihi simulizi kisha utoe dhima zake nne. (Solved)

    Eleza maana ya ngoma katika fasihi simulizi kisha utoe dhima zake nne.

    Date posted: October 1, 2019 .    Answers (1)

  • Mtu mmoja alimpa mke wake nambari yake ya simu. (Solved)

    Soma utungo ufuatao kisha ujibu maswali.
    Mtu mmoja alimpa mke wake nambari yake ya simu. Kila mara bibi akipigia mumewe simu, ilipokelewa na sauti nyororo "mteja wa nambari uliopiga hapatikani kwa sasa."Alifunga safari kumtembelea mume wake mjini na kukabiliana na huyu kisura.

    MASWALI
    a) Bainisha kipera cha utungo huu.
    b) Onyesha sifa tano za kipera hiki.
    c) Eleza manufaa tano ya kipera hiki.

    Date posted: October 1, 2019 .    Answers (1)

  • a) Kanda la usufi ni anwani mwafaka. Fafanua kwa kutolea mifano. (b) Lini angepata nafasi ya kupenya kwenye chungio…" Fafanua jinsi msemewa angepata nafasi na changamoto zake. (Solved)

    Kanda la Usufi - (R. Nyaga)
    (a) Kanda la usufi ni anwani mwafaka.
    Fafanua kwa kutolea mifano.
    (b) Lini angepata nafasi ya kupenya kwenye chungio…"
    Fafanua jinsi msemewa angepata nafasi na changamoto zake.

    Date posted: October 1, 2019 .    Answers (1)

  • Assumpta Matei: Chozi la Heri Alijiona kama mfa maji ambaye anakabiliwa na mtutumo wa mawimbi ya misiba, mmoja baada ya mwingine. (a) Bainisha muktadha wa dondoo hili.... (Solved)

    Assumpta Matei: Chozi la Heri

    Alijiona kama mfa maji ambaye anakabiliwa na mtutumo wa mawimbi ya misiba, mmoja baada ya mwingine.

    (a) Bainisha muktadha wa dondoo hili.

    (b) Eleza sifa tatu za anayerejelewa katika dondoo hili.

    (c) Eleza tamathali ya usemi iliyotumika katika dondoo hili.

    (d) Fafanua masaibu yaliyomkumba mrejelewa.

    (e) Huku ukitolea mifano riwayani, jadili matatizo yanayowakumba wanajamii katika ndoa.

    Date posted: September 24, 2019 .    Answers (1)

  • Alifa chokocho na Dumu Kayanda: Tumbo Lisiloshiba 'Doa ndio kawaida inayobainisha maisha ya mwanadamu.'Onyesha ukweli wa kauli hii kwa mujibu wa hadithi za: Shogake Dada ana... (Solved)

    Alifa chokocho na Dumu Kayanda: Tumbo Lisiloshiba

    'Doa ndio kawaida inayobainisha maisha ya mwanadamu.'Onyesha ukweli wa kauli hii kwa mujibu wa hadithi za: Shogake Dada ana Ndevu, Mame Bakari, Shibe Inatumaliza na Mtihani wa Maisha.

    Date posted: September 24, 2019 .    Answers (1)

  • Taja baadhi ya maudhui yanayojitokeza katika hadithi ya tumbo lisiloshiba? (Solved)

    Taja baadhi ya maudhui yanayojitokeza katika hadithi ya tumbo lisiloshiba?

    Date posted: September 18, 2019 .    Answers (1)