
i) Taja nafsi nenewa. Thibitisha.
Nafsi nenewa ni pesa/fulusi- waja wanazitumiwa kusuluhusha matatizo mbalimbali kama vile kununulia vifaa kulipa madeni.
(ii) Eleza toni ya nafsi neni.
- Toni ya nafsi neni ni ya kulalamika. Analalamika kuwa pesa zimemkimbia.
- Toni ya kusifia – ndiwe sabuni ya roho, ndiwe mvunja mlima.
(iii) Eleza arudhi zozote nne zilizozingatiwa katika utunzi wa shairi hili.
- Beti nne
- Mishororo mine katika kila mshororo
- Vina vinabadilika katika kila ubeti isipokuwa kibwagizo
- Mshororo wa mwisho ni kibwagizo- sabuni ya roho, ndiwe mvunja mlima.
(iv) Mshairi anawasilisha ujumbe gani katika mleo wa ubeti wa sita?
- Pesa zimeteka nyara roho za wapendanao na kuwafanya kuuana majumbani mwao.
(v) Ukitoa mfano eleza mbinu zozote tatu za lugha alizotumia mshairi.
- Balagha – ewe tunu ya mtima, kwa nini wanikimbia?
- Tashbihi – sinilipe ja bomu.
- Jazanda – jehanamu ni tatizo.
- Tashhisi – fulusi zinazoombwa kumwondoa mnenaji jehanamu, zina uchoyo.
- Takriri – ndiwe sabuni ya roho, ndiwe mvunja mlima.
(vi) Andika ubeti wa nne katika lugha nathari.
Mshairi anamsihi mvunja mlima (pesa) kuwasaidia maskini na mayatima ambao hali zao duni. Awabebe waliokwama na kuwainua walio chini. Ndiye sabuni ya roho na mvunja mlima (mtimiza yote).
(vii) Jadili jinsi mshairi anatumia ruhusa ya mshairi.
- inkisari – mfano; sinilipue – usinilipue
'mefufua – umefufua
- kuboronga sarufi - mfano wema wako wameonja badala ya wameonja wema wako.
Naondoka wangu moyo badala ya naondoka moyo wangu.
(viii) Kwa kurejelea mpangilio wa vina eleza bahari ambamo shairi hili linaweza kuainishwa.
- Bahari; ukaraguni – kila ubeti una vina tofauti na vya ubeti mwingine.
(ix) Fafanua maana ya : )
(i) ndiwe sabuni ya roho, ndiwe mvunja mlima
- ni wewe ambaye hufurahisha na kusuluhisha matatizo yote
(ii) Jehanamu
- tatizo
sharon kalunda answered the question on October 1, 2019 at 13:45
-
Jadili matumizi ya mbinu ya ishara katika tamthilia hii.
(Solved)
Mstahiki Meya
Jadili matumizi ya mbinu ya ishara katika tamthilia hii.
Date posted:
October 1, 2019
.
Answers (1)
-
Riwaya ya Kidagaa Kimemwozea imesheheni hali zinazotukia bila kutarajiwa. Fafanua.
(Solved)
Riwaya ya Kidagaa Kimemwozea imesheheni hali zinazotukia bila kutarajiwa. Fafanua.
Date posted:
October 1, 2019
.
Answers (1)
-
"………Alimaliza kwa kuandika, "yajayo yapokee"
(Solved)
Damu Nveusi na Hadithi nyingine
"………Alimaliza kwa kuandika, "yajayo yapokee"
(a) Eleza muktadha wa dondoo hili.
(b) Thibitisha ufaafu wa anwani ya hadithi hii.
Date posted:
October 1, 2019
.
Answers (1)
-
"Alikuwa na kiu lakini si ya maji, kadhalika alikuwa na njaa lakini si ya chakula Habebeki mwanamume habebeki……."
(Solved)
Kidagaa kimemwozea
"Alikuwa na kiu lakini si ya maji, kadhalika alikuwa na njaa lakini si ya chakula Habebeki mwanamume habebeki……."
(a) Weka dondoo hili katika muktadha wake .
(b) Eleza tamathali mbili zilizotumika katika dondoo hili.
(c) Eleza aina za kiu na njaa zilizomkumba mrejelewa wa kwanza.
(d) Mrejelewa wa pili alishindwa mtihani wa maisha. Jadili.
Date posted:
October 1, 2019
.
Answers (1)
-
"Duniani kuna watu na viatu"
(Solved)
Tamthilia nzima ya Mstahiki Meya.
"Duniani kuna watu na viatu"
(a) Fafanua muktadha wa dondoo hili.
(b) Thibitisha ukweli wa kauli hii ukirejelea tamthilia nzima ya Mstahiki Meya.
Date posted:
October 1, 2019
.
Answers (1)
-
Mwandishi wa tamthilia ya Mstahiki Meya ametumia wahusika kukuza kazi yake, Thibitisha kauii hili kwa kuwarejelea wahusika wafuatao.
(Solved)
Mwandishi wa tamthilia ya Mstahiki Meya ametumia wahusika kukuza kazi yake, Thibitisha kauii hili kwa kuwarejelea wahusika wafuatao.
(i) Diwani wa tatu
(ii) Bili
(iii) Mhubiri
(iv) Diwani I na II
Date posted:
October 1, 2019
.
Answers (1)
-
Kila nikaapo hushika tama.
(Solved)
Kila nikaapo hushika tama
Na kuwazia hali inayonizunguka.
Huyawazia madhila
Huziwazia shida
Huiwazia dhiki
Dhiki ya ulezi
Shida ya kudhalilishwa kazini.
Madhila ya kufanyiwa dharau
Kwa sababu ya jinsia ya kike.
Hukaa na kujidadisi
Hujidadisi kujua kwa nini
Jamii haikisikii kilio changu
Wenzangu hawanishiki mikono
Bali wananidharau kwa kuukosoa utamaduni
Hukaa na kujiuliza
I wapi raha yangu uiimwengu huu?
I wapi jamaa nzima ya wanawake?
MASWALI
(a) Shairi hili ni la aina. gani? Eleza
(b) Eleza dhamira ya mtunzi wa shairi hili.
(c) Kwa kutolea mifano eleza maana ya mistari mishata.
(d) Taja na ueleze tamathali mbili zilizotumika katika shairi hili.
(e) Tambulisha nafsi-neni katika shairi hili.
(f) Fafanua toni ya shairi hili.
(g) Fafanua maudhui mawili ya shairi hili.
(h) Onyesha namna nafasi neni anavyosalitiwa.
(i) Eleza maana ya maneno haya kama yalivyotumiwa katika shairi.
(i) Madhila
(ii) Kudhalilishwa.
Date posted:
October 1, 2019
.
Answers (1)
-
Wasiwasi n‘ondokeya, ondoka enenda zako,
(Solved)
Soma ushairi ufuatao kisha ujibu maswali.
1. Wasiwasi n‘ondokeya, ondoka enenda zako,
Ondoka andama ndiya, nondosheya uso wako,
Ondoka wanisikiya, ziwate jeuri zako,
Jishughulishe na yako, yangu wayatakiyani?
2. Wasiwasi siitaki, suhuba yako si nzuri,
Haistahamilikii, uovu umekithiri,
Inganyoshwa hainyoki, ikukutene kikiri,
Sikati yako shari, enda zako wasiwasi.
3. Huna kazi ufanyayo, ela kuwafitinisha,
Viumbe na zao nyoyo, vitina kuwagotanisha,
Hiino ndio kaziyo, yenye kukufurahisha,
Ni kazi isiyokuchosha, mno umeizoeya.
4. Mara waja na habari, mambo yalivyo nyumbani,
Ati mambo si mazuri, mambo yote tatashani,
Wanitaka nifikiri, usemayo ni yakini,
Nisononeke moyoni, upate kufurahika.
5. Au mara hunijiya, na kingine kisahani,
Kuhusu zao afiya, hao waliyo nyumbani,
Huwa husishi nambiya, hali zao taabani,
Zingawa wakati gani? Ni zako au ni zao?
6. Na mara kuja mambiya, nitakapotoka humu,
Na kwamba yaningojea, nde maisha magumu,
Uliloni kusudiya, ni kunitiya wazimu,
Kama ndiyo yako hamu, basi unshatahayari.
(a) Eleza ujumbe uliojitokeza katika shairi hili.
(b) Fafanua muundo wa ubeti wa tatu.
(c) Eleza aina ya shairi hili.
(d) Fafanua arudhi za utunzi alizozingatia mshairi.
(e) Eleza toni ya mshairi.
(f) Andika ubeti wa tano katika lugha ya kinathari.
(g) Eleza mifano mitatu ya uhuru wa mshairi.
(h) Eleza maana ya misamiati ifuatayokama ilivyotumika katika shairi.
(i) ndiya
(ii) kisahani
(iii) nde
Date posted:
October 1, 2019
.
Answers (1)
-
Ajaye kisimani mbele hunywa maji maenge,
(Solved)
Soma ushairi ufuatao kisha ujibu maswali.
1. Ajaye kisimani mbele hunywa maji maenge,
Asinywe yalo na vunju,
Yakampa kigegezi,
Yakamkibua roho akaona na kinyaa,
Awali ndio awali, awali mbovu hamna.
2. Kiwa utalimatia.
Utayaramba makombo,
Utadata vitu cheche,
Kisomo chenye dhamana kikakupa kisogo,
Inajuzu ujihimu
Mwanafuu darasani,
Urauka po mapema,
Katu hutayaramba makombo,
Hutakosa kisebeho.
3. Dereva hata utingo,
Natija ni asubuhi,
Wateja utawawahi,
Wasaa kuzingatia,
Uwafikishe kazini,
Kwa wasaa ufaao,
Wasije wakateteshwa,
Na bosi wao kazini,
Nao wakakuapiza.
4. Na ewe mwanazaraa,
Mpini uukamate,
Kabla jua kuwaka sana,
Majasho kutiririsha mwilini,
Yang‘oe yote magugu,
Kutoka kwa lako konde.
5. Mhadimu mwenye ajizi,
Yakujuza ujihimu,
Ununue na maziwa,
Majogoo uyawahi mapema,
Usije ukayadata,
Chai mkandaa ukaandaa,
Wateja wakuambae mithili ya ibilisi.
Maswali
(a) Eleza nasaha yoyote inayotolewa kwa wafanyakazi wowote watatu kwenye shairi.
(b) Taja sifa zozote za kimuundo zilizotumiwa na mtunzi.
(c) Eleza toni ya mshairi.
(d) Nafsi nenewa anahimizwa kufanya nini.
(e) Andika ubeti wa tatu kwa lugha tutumbi.
(f) Toa mifano miwili ya uhuru wa mshairi.
(g) Eleza maana ya misamiati ifuatayo kama ilivyotumiwa kwenye shairi.
(i) Maji maenge
(ii) Natija
(iii) Majogoo
Date posted:
October 1, 2019
.
Answers (1)
-
Kufariki kwa kitoto Uhuru ni jazanda inayoashiria hali halisi ya mambo riwayani "kidagaa kimemwozea". Jadili
(Solved)
Kufariki kwa kitoto Uhuru ni jazanda inayoashiria hali halisi ya mambo riwayani "kidagaa kimemwozea". Jadili.
Date posted:
October 1, 2019
.
Answers (1)
-
Onyesha jinsi ukatili unavyojitokeza kwa kurejelea hadithi zifuatazo.
(Solved)
Onyesha jinsi ukatili unavyojitokeza kwa kurejelea hadithi zifuatazo.
(i) Kanda la usufi
(ii) Shaka ya mambo
(iii) Mwana wa darubini
(iv) Ndoa ya Samani.
Date posted:
October 1, 2019
.
Answers (1)
-
Thibitisha jinsi anwani "Damu Nyeusi" inaafiki yaliyomo katika hadithi.
(Solved)
Thibitisha jinsi anwani "Damu Nyeusi" inaafiki yaliyomo katika hadithi.
Date posted:
October 1, 2019
.
Answers (1)
-
Jadili matatizo KUMI ya kijamii ukirejelea hadithi "Mwana wa Darubini"
(Solved)
Jadili matatizo KUMI ya kijamii ukirejelea hadithi "Mwana wa Darubini"
Date posted:
October 1, 2019
.
Answers (1)
-
Riwaya ya kidagaa kimemwozea inaonyesha jitihada za vijana kujenga jamii mpya. Thibitisha kwa kutoa mifano
(Solved)
Riwaya ya kidagaa kimemwozea inaonyesha jitihada za vijana kujenga jamii mpya. Thibitisha kwa kutoa mifano
Date posted:
October 1, 2019
.
Answers (1)
-
Kwa kurejelea tamthilia ya Mstahiki Meya, fafanua vichocheo vya migogoro katika jamii ya Cheneo.
(Solved)
Kwa kurejelea tamthilia ya Mstahiki Meya, fafanua vichocheo vya migogoro katika jamii ya Cheneo.
Date posted:
October 1, 2019
.
Answers (1)
-
Matambiko ni nini? Eleza dhima zake mbili.
(Solved)
Matambiko ni nini? Eleza dhima zake mbili.
Date posted:
October 1, 2019
.
Answers (1)
-
Eleza maana ya maapizo.
(Solved)
Eleza maana ya maapizo.
Date posted:
October 1, 2019
.
Answers (1)
-
Eleza maana ya ngoma katika fasihi simulizi kisha utoe dhima zake nne.
(Solved)
Eleza maana ya ngoma katika fasihi simulizi kisha utoe dhima zake nne.
Date posted:
October 1, 2019
.
Answers (1)
-
Mtu mmoja alimpa mke wake nambari yake ya simu.
(Solved)
Soma utungo ufuatao kisha ujibu maswali.
Mtu mmoja alimpa mke wake nambari yake ya simu. Kila mara bibi akipigia mumewe simu, ilipokelewa na sauti nyororo "mteja wa nambari uliopiga hapatikani kwa sasa."Alifunga safari kumtembelea mume wake mjini na kukabiliana na huyu kisura.
MASWALI
a) Bainisha kipera cha utungo huu.
b) Onyesha sifa tano za kipera hiki.
c) Eleza manufaa tano ya kipera hiki.
Date posted:
October 1, 2019
.
Answers (1)
-
a) Kanda la usufi ni anwani mwafaka.
Fafanua kwa kutolea mifano.
(b) Lini angepata nafasi ya kupenya kwenye chungio…"
Fafanua jinsi msemewa angepata nafasi na changamoto zake.
(Solved)
Kanda la Usufi - (R. Nyaga)
(a) Kanda la usufi ni anwani mwafaka.
Fafanua kwa kutolea mifano.
(b) Lini angepata nafasi ya kupenya kwenye chungio…"
Fafanua jinsi msemewa angepata nafasi na changamoto zake.
Date posted:
October 1, 2019
.
Answers (1)