Mchuzi unalambwa na paka.
sharon kalunda answered the question on October 2, 2019 at 07:38
-
Inaaminika kuwa majeruhi wengi katika mikasa ya ajali huaga au huathirika vibaya zaidi kutokana na hali mbaya ya uokoaji.
(Solved)
Utoaji wa Huduma ya Kwanza.
Inaaminika kuwa majeruhi wengi katika mikasa ya ajali huaga au huathirika vibaya zaidi kutokana na hali mbaya ya uokoaji. Watu wengi ambao hujitolea kuokoa majeruhi baada ya ajali kama za barabarani, maporomoko ya ardhi au nyumba huwa hawang‘amui hata chembe jinsi ya kukabiliana na uokoaji. Hatima ya juhudi zao ambazo hulenga kutenda mema ni kuathirika zaidi kwa majeruhi.
Hali ya ukoaji inaweza kurekebishwa kwa kutoa elimu ya huduma ya kwanza kwa umma. Elimu hii yahitajika na kila Mkenya kwani mikasa ya ajali za barabarani na nyinginezo inaendelea kutokea kila siku.Ajali zinapotokea, si ajabu kuona makundi ya waokoaji yakibeba majeruhi hobelahobela bila kuzingatia madhara yanayoweza kuwaongezea kutokana na ubebaji wao. Kutojua namna ya kumbeba majeruhi kunaweza kumhatarisha na hata kusababisha kifo.
Kuna mambo mbalimbali ambayo makundi ya waokoaji yanatakiwa kuzingatia wakati yanatoa huduma ya kuokoa. Kwanza, ni muhimu kuchunguza kama kuna hatari yoyote inayoweza ikatokea na kuwatia majeruhi na waokoaji hatarini zaidi. Makundi ya waokoaji yameweza kuhatarisha majeruhi kwa kuliingilia eneo la ajali mbumbumbu kama mzungu wa reli.
Hatua ya pili ni kutafuta idadi ya majeruhi. Pana uwezekano wa majeruhi kutupwa mbali na eneo la ajali. Vivyo hivyo, kuna majeruhi ambao huweweseka baada ya ajali na kuanza kutembea wasijue wanakoelekea. Wengi wao huanguka karibu na eneo la ajali au wakaenda mbali.
Hatua ya tatu ni kuchunguza kama majeruhi amezimia, moyo unapiga na jinsi anavyopumua. Ili kuhakikisha kuwa majeruhi anapumua, mwokoaji atazame kama kifua kinapanda na kushuka. Halikadhalika, mwokoaji anaweza kusikiliza au kuguza kifua na kuona kama kuna ishara za kupumua. Iwapo majeruhi anapumua, mwokoaji amweke katika hali ambayo itaimarisha kupumua kwake. Anaweza akamlaza chali au kumgeuza kwa pamoja na kichwa chake ili kufungua mkondo wa hewa. Pia, mwokoaji ahakikishe hamna chochote kinywani kinachoweza kumsakama. Ikiwa hapumui, mwokoaji anaweza kujaribu kumfanya apumue kwa kupuliza hewa mdomoni mwake. Fauka ya hayo, upulizaji wa hewa utahakikisha kuwa damu inazunguka mwilini vizuri.
Maswali :
(a) Fupisha aya mbili za kwanza kwa maneno 55 – 65.
(b) Eleza kwa kutumia maneno 90-100, hatua zinazotakiwa kufuatwa wakati wa uokoaji.
Date posted:
October 2, 2019
.
Answers (1)
-
Zitavuma,
Zitakoma,
Nitakwima,
Mti-mle.
(Solved)
Soma shairi lifuatalo kisha ujibu maswali.
Zitavuma,
Zitakoma,
Nitakwima,
Mti-mle.
Na muda nikisimama,
Nitatongoa nudhuma,
Kwa tenzi zilizo njema,
Nilisifu mti – mle.
Tazipanga tathlitha, tungo zilizo na hekima,
Za huba na thiatha, za kuburudi mitima,
Mashairi mabuthutha, musome mnaosoma.
Mti nishainukia,namea kuwa mzima,
Mizizi yadidimia, ardhini imeuma,
Nanena kitarbia, tungo zilizo adhama
Japo ni tungo za zama, mti-mle hutumia.
Zingavuma zitapusa, pepo kali zitakoma,
Dharuba kinitikisa, mti-mle huinama,
Huyumba nikaziasa, matawi yakakingama,
Gharika ikishapisa, hurudi nikawa wima,
Na tungo za takhimisa, mti-mle huzipima.
Maswali
(1) Shairi hili ni la kimapokea. Toa sababu mbili kuunga kauli hii.
(2) Taja bahari kuu ya ushairi ambayo imetumiwa na mshairi. Fafanua.
(3) Fafanua dhamira ya mshairi.
(4) Kwa kutoa mifano bainisha tamathali mbili za usemi zilizotumika katika shairi hili.
(5) Eleza jinsi mshairi ametumia idhini ya ushairi katika utungo huu.
(6) Andika ubeti wa nne kwa lugha natharia.
(7) Mshairi anamaanisha nini anaposema "zingavuma zitapusa, pepo kali zitakoma,"
(8) Eleza toni ya shairi hili.
(9) Eleza maana ya msamiati ufuatao.
i) Nitatongoa
ii) Zitapusa.
Date posted:
October 1, 2019
.
Answers (1)
-
Eleza matatizo yanayomkabili mtu anapoitumia lugha yoyote isipokuwa ile ya kwanza.
(Solved)
Eleza matatizo yanayomkabili mtu anapoitumia lugha yoyote isipokuwa ile ya kwanza.
Date posted:
September 28, 2019
.
Answers (1)
-
Fafanua mambo matano yanaosababisha kutokea kwa lahaja.
(Solved)
Fafanua mambo matano yanaosababisha kutokea kwa lahaja.
Date posted:
September 28, 2019
.
Answers (1)
-
Andika kwa wingi.
Mimi ndimi shangazi yake.
(Solved)
Andika kwa wingi.
Mimi ndimi shangazi yake.
Date posted:
September 28, 2019
.
Answers (1)
-
Andika katika hali ya udogo:
Mvulana yule alibeba kiti kikubwa
(Solved)
Andika katika hali ya udogo:
Mvulana yule alibeba kiti kikubwa
Date posted:
September 28, 2019
.
Answers (1)
-
Taja sauti zinazotamkiwa kwenye ufizi.
(Solved)
Taja sauti zinazotamkiwa kwenye ufizi.
Date posted:
September 28, 2019
.
Answers (1)
-
Onyesha vishazi tegemezi na vishazi huru katika sentensi ifuatayo.
Nilimwona Agwambo nilipofika Mombasa
(Solved)
Onyesha vishazi tegemezi na vishazi huru katika sentensi ifuatayo.
Nilimwona Agwambo nilipofika Mombasa
Date posted:
September 28, 2019
.
Answers (1)
-
Tunga sentensi ukitumia viunganishi hivi vya kinyume Ingawaje, ila
(Solved)
Tunga sentensi ukitumia viunganishi hivi vya kinyume Ingawaje, ila
Date posted:
September 28, 2019
.
Answers (1)
-
Tunga sentensi moja ili kudhihirisha matumizi ya viwakifishi hivi:
i)Semi koloni
ii)Mshazari
(Solved)
Tunga sentensi moja ili kudhihirisha matumizi ya viwakifishi hivi:
i)Semi koloni
ii)Mshazari
Date posted:
September 28, 2019
.
Answers (1)
-
Kanusha katika wingi.
Alikuarifu kuhusu yule hajala.
(Solved)
Kanusha katika wingi.
Alikuarifu kuhusu yule hajala.
Date posted:
September 28, 2019
.
Answers (1)
-
Unganisha sentensi hizi kwa kutumia kirejeshi cha kati.
(i) Kalamu imeibwa
(ii) Kalamu ni yangu
(Solved)
Unganisha sentensi hizi kwa kutumia kirejeshi cha kati.
(i) Kalamu imeibwa
(ii) Kalamu ni yangu
Date posted:
September 28, 2019
.
Answers (1)
-
Unda nomino mbili kutokana na kitenzi arifu.
(Solved)
Unda nomino mbili kutokana na kitenzi arifu.
Date posted:
September 28, 2019
.
Answers (1)
-
Ainisha viambishi katika neno lifuatalo: aliyelima
(Solved)
Ainisha viambishi katika neno lifuatalo: aliyelima
Date posted:
September 28, 2019
.
Answers (1)
-
Tunga sentensi yenye kiingizi na kihusishi cha mahali.
(Solved)
Tunga sentensi yenye kiingizi na kihusishi cha mahali.
Date posted:
September 26, 2019
.
Answers (1)
-
Nyambua vitenzi vifuatavyo katika kauli zilizo kwenye mabano.
i) twaa (kutendeka)
ii) Kosa (Kutendesha)
iii) Cha (Kutendwa)
(Solved)
Nyambua vitenzi vifuatavyo katika kauli zilizo kwenye mabano.
i) twaa (kutendeka)
ii) Kosa (Kutendesha)
iii) Cha (Kutendwa)
Date posted:
September 26, 2019
.
Answers (1)
-
Maneno haya yamo katika ngeli gani?
i) Fagio
ii) Nyigu
(Solved)
Maneno haya yamo katika ngeli gani?
i) Fagio
ii) Nyigu
Date posted:
September 26, 2019
.
Answers (1)
-
Ngeli ni nini?
(Solved)
Ngeli ni nini?
Date posted:
September 26, 2019
.
Answers (1)
-
Ulimwengu unapaswa kuzuka na mbinu za Kulitadarukia tatizo la umaskini ambalo una kwamiza juhudi za maendeleo.
(Solved)
Soma nakala yafuatayo kishaujibu maswali
Ulimwengu unapaswa kuzuka na mbinu za Kulitadarukia tatizo la umaskini ambalo una kwamiza juhudi za maendeleo. Umaskini unaoukabili mataifa yanayoendelea. Unayatosa kwenye dhiki kubwa huku mataifa ya kimagharibi yakipiga hatua kubwa kimaendeleo. Ufa uliopo baina ya mataifa yanayoendelea na yaloyaliyoendelea kama vile Marekani, nchi za Ulaya na Ujapani unapanuka kila uchao.
Vyanzo vya umaskini huu ni anuwai ; mathalan, ufisadi, uongozi mbaya, turathi za kikoloni, uchumi kuegemea mvua isiyotabirika,idadi ya watu inayoupiku uwezo wa uchumi wa taifa linalo husika na ukosefu wa nyenzo na amali za kuwakwamua raia kutoka lindi la umaskini. Ukosefu na adimu za ajira huchangia pia katika tatizo hili.
Jamii ya xxxxxxx mpaswa kuelewa kuwa umaskini unaoathiri nchi fulani unaathari pana sana.Uvunigu unaotokana na umaskini unaweza kuwa msingi ambako matendo ya kihalifu ili kujinasua kutoka dhiki ile. Hii inaweza kuwa mbegu ya kuatika maovu kama ugaidi na uhalifu wa kila aina.
Mataifa ya magharibi yanapaswa kuyaburai madeni mataifa yanayoendelea kama njia mojawapo ya kupambana na umaskini. Asilimia kubwa ya pato la kitaifa katika mataifa mengi hutumika kuyalipa madeni hayo. Katika hali hii inakuwamuhali kwa mataifa hayo kujikwamua kutokana na pingu za umaskini. Njia nyingine ni kustahabu kutoa ruzuku za kimaendeleo badala ya mikopo kwa nchi zinazoendelea.
Kwa upande wake, mataifa yanayoendelea yanapaswa kuibuka na mikakati bora yakupambana na umaskini. Ni muhimu pawepo na sera zinazotambua ukweli kuwa asilimia kubwa ya raia wa mataifa hayo ni maskini. Pana dharura ya kuzalisha nafasi za ajira, kupanua viwanda hususan vinavyohusiana na zaraa ambayo ni tegemeo kuu la mataifa mengi, kuendeleza elimu na kuimarisha miundo msingi. Ipo haja pia ya mataifa haya kuhakikisha kuwa mfumo wa soko huru unaotawala ulimwengu sasa hauishii kuwa chanzo cha kufa kwa viwanda asilia na kuendeleza umasikini zaidi. Kwa ufupi, maamuzi yote ya sera za kiuchumi lazima ya zingatie uhalisi wa maisha ya raia wa mataifa hayo.
a) Kwa nini umaskini umetamalaki katika mataifa yanayoendelea?
b) Madeni yana athari gani kwa mataifa yanayoendelea?
c) Ni mapendekezo yapi ambayo mwandishi anatoa kwa mataifa machanga kuhusu utatuzi wa tatizo la umaskini?
d) Mfumo wa soko huru una mathara gani kwa mataifa machanga?
e) Ukirejea kifungu, eleza maana ya:
i) Kulitadarukia
ii) Kuatika
iii) Kuyaburai madeni
Date posted:
September 25, 2019
.
Answers (1)
-
Tunga sentensi kudhihirisha maana ya msemo ufuatao. enda benibeni.
(Solved)
Tunga sentensi kudhihirisha maana ya msemo ufuatao. enda benibeni.
Date posted:
September 25, 2019
.
Answers (1)