Ukipitia kwao utabarikiwa.
sharon kalunda answered the question on October 4, 2019 at 08:29
-
Andika maana mbili za neno "mlango".
(Solved)
Andika maana mbili za neno "mlango".
Date posted:
October 4, 2019
.
Answers (1)
-
Jibu kulingana na maagizo.
(i) Ufisadi (unda kitenzi)
(ii) - pya (unda nomino)
(Solved)
Jibu kulingana na maagizo.
(i) Ufisadi (unda kitenzi)
(ii) - pya (unda nomino)
Date posted:
October 4, 2019
.
Answers (1)
-
Kanusha sentensi hii katika hali ya "a"
Kibofu hupaa angani.
(Solved)
Kanusha sentensi hii katika hali ya "a"
Kibofu hupaa angani.
Date posted:
October 4, 2019
.
Answers (1)
-
CHIMBUKO LA USHAIRI
Ushairi ni fani kongwe kama mwanadamu mwenyewe alivyo mkongwe duniani. Na mashairi yamekuwepo kitambo sana hata kabla ya lugha...
(Solved)
CHIMBUKO LA USHAIRI
Ushairi ni fani kongwe kama mwanadamu mwenyewe alivyo mkongwe duniani. Na mashairi yamekuwepo kitambo sana hata kabla ya lugha ya Kiswahili bado haijanawiri na kushamiri kama ilivyo hivi leo. Ndipo tunasikia kuna mashiri ya kipemba, mashairi ya kimvita, mashairi ya kivumba, mashairi ya kipate, mashairi ya kiyunani, ya kirumi na kadhalika,. Almradi kila jamii na kila kabila lilikuwa na mashairi yake.
Katika utafiti na kongomano zao, wataalam wa arudhi za Kiswahili asili wamechambua na kufafanua kwamba mashairi ya Kiswahili asili yake ni nyimbo za jadi zilizokuwa zikiimbwa na manju, wangoi au waimbaji stadi wa tangu na tangu walipojumuika katika matukio na hafla mbalimbali kama za jando, arusi, matanga, ngoma na shangwe zao za maishani.
Nyimbo hizi zilitumiwa na watangulizi wetu, kidhamira hazikuhitalafiana hata kidogo na mashairi ya Kiswahili tunayohimiza wakati huu. Farka iko katika lugha na umbo kwani kila jamii ilitumia lugha yake na lahaja ya mazingira yake. Na kwa upande wa umbo, tungo hizo za awali kabisa hazikuwa na sanaa kwa maana ya ushauri tunauona leo. Bali tungo hizo zilijengeka katika nguzo mbili kuu. Kwanza ni uzito wa mawazo maadilifu ambayo yalitaamaniwa sana. Na pili ni mizani ya sauti ya manju kulingana na lahani, pumzi zake pamoja na madoido katika uimbaji ambao ulikuwa burudani naathari katika noyo za wasikilizaji wake.
Kwa kifupi ni kwamba, nyimbo hizo ziliuhifaid umma kwa njia mbili, mawaidha kwa mapana na taathira au jadhba kutokana na sauti tamu ya manju.
Kama utakubalika, basi huo ndio ushairi wa awali kabisa ullioambatana na nyimbo zetu za kienyeji. Kila kabila katika nchi zetu lilikuwa na ushauri wake au nyimbo zake zenye undani uliolenga sababu maalum na tukio maalum katika jamii.
Nyimbo kama hizo kwa jina la sasa tunaweza kuita mashairi ndizo zile zilizoitwa ‘mwali’ na wakamba; gichandi kwa ‘wakikuyu’; ‘gigia gi sigele’ kwa waluo na ‘wagashe’ kwa wasukuma zilikuwa na undani wa kipekee tena uliodidimia ambao si bure kutolewa hadharani.
Aina za mashairi ya watu wa mwambao ni kama lelemama, misemele, gungu, nyiso, kongozi n.k.
(Walla Bin Walla – Malenga wa Ziwa Kuu , E.A.E.P)
1. Ni nini haswa chimbuko la ushairi?
2. Kulingana na kifungu hiki, ni nini umuhimu wa ushairi ?
3. Ni maswala gani yaliyowapendeza wasikilizaji wa tungo hizo za zama ?
4. Tofauti kati ya nyimbo za zama na ushairi wa leo upo kwenye vipengele gani viwili ?
5. Kifungu : ‘haijanawiri na kushamiri’ ina maana gani katika lugha nyepesi ?
6. Eleza maana ya :
(a) Kongamano …
(b) Jadhiba
(c) Farka
(d) Awali..
Date posted:
October 4, 2019
.
Answers (1)
-
Andika katika msemo halisi. Mwalimu alishangaa ni kwa nini Juma hakuwa amebeba mkoba wake siku hiyo.
(Solved)
Andika katika msemo halisi.
Mwalimu alishangaa ni kwa nini Juma hakuwa amebeba mkoba wake siku hiyo.
Date posted:
October 4, 2019
.
Answers (1)
-
Andika sentensi ifuatayo kwa udogo wingi.
Mtu yule haachi kuandamana na mbwa wake aliyedhoofika kiafya.
(Solved)
Andika sentensi ifuatayo kwa udogo wingi.
Mtu yule haachi kuandamana na mbwa wake aliyedhoofika kiafya.
Date posted:
October 4, 2019
.
Answers (1)
-
Tunga sentensi moja yenye kishazi huru na kishazi kitegemezi ukitumia "O" rejeshi tamati.
(Solved)
Tunga sentensi moja yenye kishazi huru na kishazi kitegemezi ukitumia "O" rejeshi tamati.
Date posted:
October 4, 2019
.
Answers (1)
-
Changanua sentensi hii kwa kutumia jedwali.
Mama alilima kwa bidii ingawa hakupata faida.
(Solved)
Changanua sentensi hii kwa kutumia jedwali.
Mama alilima kwa bidii ingawa hakupata faida.
Date posted:
October 4, 2019
.
Answers (1)
-
Tunga sentensi ukitumia kitenzi cha katika hali ya kutendwa.
(Solved)
Tunga sentensi ukitumia kitenzi cha katika hali ya kutendwa.
Date posted:
October 4, 2019
.
Answers (1)
-
Bainisha shamirisho na chagizo katika sentensi ifuatayo. Kimathi alimwandikia babake barua kwa kalamu jana jioni.
(Solved)
Bainisha shamirisho na chagizo katika sentensi ifuatayo.
Kimathi alimwandikia babake barua kwa kalamu jana jioni.
Date posted:
October 4, 2019
.
Answers (1)
-
Asifuye mvua imemnyea. Huu ni msemo wenye hakika isiopingika, na kutilia shaka ni sawa na kudai jua linaweza kubadilika na kuchomozea upande...
(Solved)
Soma taarifa hii kisha ujibu maswali
Asifuye mvua imemnyea. Huu ni msemo wenye hakika isiopingika, na kutilia shaka ni sawa na kudai jua linaweza kubadilika na kuchomozea upande wa magharibi badala ya mashariki. Huu ndio ukweli uliodhihirika juzi katika vyombo vyetu vya magazeti.
Lisemwalo lipo, na kama halipo li njiani. Waama, pafukapo moshi pana moto. Mwanafunzi mmoja wa kike kwa jina P.N. katika chuo kikuu kimojawapo nchini alishangaza umma wa Kenya na ulimwengu kwa jumla alipodai kuwaambukiza wanafunzi wenzake wa kiume mia moja na ishirini na wanne virusi vya Ukimwi.
Kisa na maana? Aliambukizwa Ukimwi na mwanafunzi mwenzake aliyekuwa akifanya majaribio ya ualimu katika shule yao ya upili. Baada ya kushawishika sana alijuana naye kimwili, na matokeo yakawa kifo ambacho sasa alikuwa anawagawia wenzake.
Kisa kama hiki kinachangia kueleza kina kirefu cha kutamauka na upweke ambao maisha ya waja wengi yameingia kiasi cha kuwaacha wanyama ijapo wanaenda kwa miguu miwili bado. Katika mojawapo ya mafunzo ya kidini ambayo Padre alinifunza mimi na wanafunzi wenzangu, tuliambiwa kisasi ni chake Mola, sisi waja wetu ni kushukuru tu. Mbona basi mwanafunzi kama huyu kutaka kulipiza?
Ima fa ima, na waswahili husema, “mlaumu nunda na kuku pia”. Huyu mwanafunzi hawezi kuachiwa atende alivyotenda. Aliyekula naye raha alikuwa mtu aliyefahamika vizuri sana kwake. Isitoshe, huenda wakati huo alikosana na mama na baba kulala nje. Huenda alikosana na ndugu zake kwa kuepa nyumbani usiku wa manane kwenda kumwona huyu kalameni. Huenda alikosana na mwalimu wake kwa sababu kiburi kilianza kuingia. Kwa vyovyote vile, alikula raha na hastahili kuwaadhibu watu wasio na hatia kufidia makosa yake. Je, kama yeye na huyo jamaa wasingekuwa na Ukimwi, raha kiasi gani wangezila hadi leo?
Jamii na watu wote kwa jumla hawana budi basi kulaani vitendo vya P.N. vya kuambukiza wanafunzi wenzake virusi huku akijua. Hili ni kosa ambalo linastahili adhabu ya kifo. Dawa ya moto ni moto ni adhabu inastahili kuchukuliwa haraka ili P.N. ambaye tayari amekiri hatia, atiwe nguvuni na adhabu itolewe.
Barua ya P.N. inafafanua jambo jingine sugu. Kwamba kiwango cha maadili katika vyuo vyetu kimezorota kiasi cha kufanyiana unyama usiosemeka. Vijana wengi siku hizi wanashiriki tendo la ndoa bila haya. Huu upotofu wa maadili katika jamii wapaswa kushutumiwa na wote. P.N. hana sababu yoyote ya kibinadamu, kidini au kitu chochote kile kudai haki kwa uovu huo wake.
1.Taja kichwa kwa makala haya
2. Katika aya mbili za kwanza, mwandishi anamlaumu mwanafunzi kwa kosa gani? Eleza chanzo cha tabia za P.N
4. Mwandishi wa taarifa hii anataka P.N achukuliwe hatua gani? Kwa nini?
5. Barua ya P.N. bila shaka imeonyesha uvumbuzi mpya. Utaje
6. Eleza maana ya vifungu hivi kama vilivyotumiwa katika taarifa:
(a) Kina kirefu cha kutamauka
(b) Ima fa ima
(c) Kufidia makosa yake
Date posted:
October 4, 2019
.
Answers (1)
-
Tunga sentensi kwa kutumia.
(i) Kivumishi cha "ki" ya mfanano.
(ii) Kielezi cha kiasi cha jumla.
(Solved)
Tunga sentensi kwa kutumia.
(i) Kivumishi cha "ki" ya mfanano.
(ii) Kielezi cha kiasi cha jumla.
Date posted:
October 4, 2019
.
Answers (1)
-
Uundaji wa istilahi – hasa za lugha ya Kiswahili ni shughuli nyeti na nzito hivi
kwamba, haipaswi kupapiwa na mtu yeyote. Hii...
(Solved)
Soma kifungu kifuatacho kisha ujibu maswali:-
Uundaji wa istilahi – hasa za lugha ya Kiswahili ni shughuli nyeti na nzito hivi
kwamba, haipaswi kupapiwa na mtu yeyote. Hii ni shughuli inayohitaji umakinifu zaidi kwa wanaoshiriki katika mchakato wa uundaji istilahi za kutufaa katika mawasiliano na kukuza Kiswahili kwa jumla. Ufanisi wa watu binafsi, vyombo vya habari kama vile Shirika la Habari la Kenya (KBC), Taifa Leo na mashirika mengineyo katika ukuzaji wa lugha hutegemea mno sera na utayarishaji wa serikali katika kugharamia shughuli hii. Aidha, shughuli za kukuza lugha hukwama kwa sababu ya ukosefu wa fedha pamoja na sera maalum ya serikali kuhusu lugha.
Hata hivyo, katika kuyakwepa matatizo haya, pamekuwepo na hatua za kimataifa za kujaribu kusawazisha shughuli ya uundaji wa maneno. Hatua hii ilichochea kubuniwa kwa shirikisho la kimataifa la vyama vya usanifishaji istilahi mnamo 1936. Lengo la kitengo hiki lilikuwa ni kufafanua msingi madhubuti ya uundaji wa istilahi duniani. Kwa hakika, shirikisho hilo limesaidia mno katika kuweka misingi ya shughuli za ukuzaji wa istilahi. Misingi hiyo ni ya jumla na haihusu taaluma yoyote mahususi. Katika makala hii, tunapiga darubini baadhi ya misingi hiyo pamoja na mapendekezo yake.
Mosi, uundaji istilahi unafaa uanzie kwenye dhana na wala sio neno. Hii ina maana kwamba, kwanza pawepo na dhana au hali ambayo inahitaji itafutiwe neno au istilahi ya kuielezea. Inasikitisha sana kwamba pana wataalamu ambao wanaukaidi au kuukiuka msingi huu. Wanataaluma hawa hufanya mambo kinyume kwa kujibunia maneno yao na kuyahifadhi kwenye mikoba yao – halafu wakasubiri dhana izuke ndiposa waipachike istilahi yao. Pili, dhana zinabuniwa au kutolea istilahi au maneo ni muhimu zielezwe kwa ukamilifu na uwazi. Istilahi zinazoundwa zinafaa ziwe fupi iwezekanavyo na ziwe na uwezo wa kuelezea dhana kwa njia inayoeleweka bila utata. Tatu, maneno yanayoundwa sharti yawe na uhusiano wa aina fulani na dhana zinazowakilishwa na maneno hayo.
Uhusiano huo unaweza kuwa ama ni wa kimaumbile au wa kiutendaji. kwa mfano, Mzee Sheikh Nanhany wa Mombasa alipobuni istilahi ‘uka’ kwa maana ya ‘ray’. Neno hili latokana na kupambauka au (kupambazuka kwa lafudhi ya kiamu. Neno ‘image’ ni jazanda kwa Kiswahili. ‘Mirage’ kwa Kiswahili ni ‘mangati’ (kutoka kwa mang’aanti) – yaani kung’aa kwa nchi. Mtaalamu mwingine aliyewazia uendajikazi wa kifaa na kubuni istilahi inayokubalika mpaka sasa ni Prof. Rocha Chimerah ambaye alibuni istilahi ‘tarakilishi’. Pengine Prof. Chimerah alifikiria kazi ni kifaa husika na kuunda neno la Kiswahili linaloakisi kazi hiyo. Tunajua kwamba kompyuta hufanya kazi inayohusu tarakimu kwa haraka kama umeme. Labda Chimerah ameegemea sifa hii kuibuka na istilahi hii.
Maneno mengine ambayo yamebuniwa kufuatana na msingi huu ni ya Mzee Nabhany-mathalan ‘barua pepe’ (e-mail), na wavuti (website). Tukiegemea maumbile, neno ‘kifaru’ lina maana ya vita ilihali tuna zana ya vita iliyopewa jina hilo kwa sababu ya labda kuwa na maumbile sawa na kifarumnyama. Nne, istilahi zinaweza kukopwa kutoka lugha nyingine. Yamkini hakuna lugha hata moja ulimwenguni-zikiwemo lugha duniani kama vile kiingereza zinazoweza kujitosheleza. Takriban asilimia 80 ya maneno katika kiingereza ni ya kukopwa. Kwa hivyo, lugha ya Kiswahili inapokopa, hali hiyo haipaswi kuchukuliwa kuwa ni lugha dhaifu.
Hata hivyo, istilahi zinazokopwa zi-nafaa zichukuliwe zilivyo katika umbo lao asili. Umbo hili linaweza kufanyiwa marekebisho machache tu, kulingana na sarufi na matumizi ya lugha kopaji. Mifano ya istilahi kama hizi ni ‘televisheni’ (television), kopmpyuta (computer), kioski (kutokana na jina ‘kiosk’ la Kijerumani) na redio (radio), Tano, pale istilahi haiwezi kukopwa, lugha husika ijaribu kubuni msamiati ufaao, kufanya hivyo ni kuhakikisha kwamba, lugha inastawi. Lakini tahadhari inapaswa kuchukuliwa hivi kwamba, Kiswahili kisikope maneno kiasi cha kupoteza upekee wake. Mwisho, uundaji wa istilahi uzingatie mofolojia ya kawaida ya lugha. Istilahi zinazoundwa kwa kuzingatia mofolojia huwa rahisi kuiua maneno yenye uhusiano wa istilahi asili kwa njia ya mnyambuliko.
(i) Taja mambo ambayo huchangia ukuaji na ufanisi wa jumla wa lugha ya Kiswahili
(ii) “Lugha ya Kiswahili ni dhaifu na isiyotosheleza” Je, mwandishi wa makala haya
ana msimamo upi kuhusu kauli hii?
(iii) Tahadhari zipi zinazofaa kuchukuliwa kabla ya kukopa istilahi kutoka lugha zingine?
(iv) Yape makala haya anwani mwafaka
(v) Eleza maana ya maneno yafuatayo:
(a) Dhana-
(b) Takribani –
(c) Istilahi – .
(d) Mofolojia –...
Date posted:
October 4, 2019
.
Answers (1)
-
Ufisadi ni uhalifu unaohusu kuzitumia njia za ulaghai kujipatia pesa, mali au vitu hasa vya umma.
Nchini Kenya ufisadi hujitokeza...
(Solved)
Soma taarifa ifuatayo kisha ujibu maswali.
Ufisadi ni uhalifu unaohusu kuzitumia njia za ulaghai kujipatia pesa, mali au vitu hasa vya umma.
Nchini Kenya ufisadi hujitokeza kwa njia mbalimbali na kila mojawapo ina athari zake. Kwa mfano kuna maafisa wa serikali wajipatiao pesa kwa kuuza stakabadhi za serikali kama vile pasi, vyeti vya kuzaliwa, vyeti vya kumiliki mashamba, vitambulisho n.k. kwa raia, kuna hatari kubwa kwa sababu watu wasio raia wa Kenya wameweza kusajiliwa kama wakenya na kuendeleza uhalifu kama ugaidi, wizi na ulanguzi wa dawa za kulevya.
Wengine hujipatia vibali vya kufanya kazi na kuajiriwa kazi ambazo zingefanywa na wakenya. Hii imechangia ongezeko la uhaba wa kazi nchini.
Watumizi wengine wa umma huuza mali ya serikali kama vile magari nyumba na ardhi na kufutika pesa za mauzo mifukoni mwao. Wengine wao hujinyakulia na kufanya vitu hivyo kuwa mali yao. Ufisadi wa aina hii umegharibu serikali kiasi kikubwa cha fedha. Serikali imelazimika kununulia maafisa wake magari baada ya muda mfupi, kulipia wafanyi kazi wake kodi za nyumba na kukosa viwanja vya upanuzi na ujenzi wa shule hospitali, vituo vya polisi na taasisi zingine maalumu.
Baadhi ya wataalamu kama madaktari huiba dawa kutoka hospitali za umma kupeleka vituo vyao vyaafya. Pia hutumia wakati wao mwingi katika kazi zao za kibinafsi na kuwaacha wagonjwa katika hospitali za umaa wakihangaika. Sio madaktari tu, kuna masoroveya, whandisi, mawakili, walimu na mahesibu ambao hukwepa majukumu yao serikalini na kufanya kazi za kibinafsi.. Wengine wasio wataalam huendesha biashara za aina tofauti, na huku wanaendelea kupokea mishahara.
Wanafunzi wanaotaka kujiunga na vyuo na shule bora za umma na hawakuhitimu wakati mwinginehulazimika kusalimu amri na kutoa hongo hili wapate nafasi za kusoma. Kiasi cha pesa kinachohitajika huwa kikubwa hivi kwamba ni wachache humudu hizo rushwa. Wale wasiojimudu kifedha hubaki wakilia ngoa. Kuna wazazi ambao hutumia vyeo vyao na ‘undugu’ kupata nafasi zilizotajwa, jambo ambalo huwanyima wanafunzi werevu kutoka jamii maskini nafasi ya kupata elimu. Matokeo huwa ni kuelimisha watu wasiostahili na ambao mwishowe hawaziwezi kazi wanazosomea wakihitimu na kuanza hudumia jamii.
Ufisadi umekita mizizi na kushamiri katika sekta za umma za kibinafsi kwa upande wa kuajiri wafanyikazi. Ni vigumu kupata kazi ikiwa hujui mtu mkubwa katika shirika linalohusika au uzunguke mbuyu. Matokeo ni kuajiri wafanyikazi wasiohitimu na wasiohitimu na wasiowajibika kazini.
Vyeo na madaraka katika baadhi ya mashirika hutolewa kwa njia ya mapendeleo na ufisadi. Kwa hivyo, wafanyikazi wenye biddi hufa moyo kwa sababu hawasaidiwi ipasavyo. Badala yake wale wasioleta bidii hupandishwa vyeo na kuwaacha palepale.
Hata hivyo, mbio za sakafuni huishaia ukingoni. Serikali imetangaza vita dhidi ya ufisadi. Tayari tume kadhaa zimeteuliwa kuchunguza visa vya ufisadi uliotekelezwa hapo mbeleni. Mojawapo ya tume hizo ni Tume ya Kuchunguzavisa vya ufisadi uliotekelezwa hapo mbeleni. Mojawapo ya tume hizo ni Tume ya kuchunguza Kashfa ya “Goldenberg” ambapo pesa za umma (mabilioni ya shilingi) ziliporwa na mashirika na watu binafsi kwa njia siziso halali. Watakaopatikana na hatia ya kushiriki ufisadi huo watahitajika kurudisha pesa hizo.
Serikali pia imeunda kamati ya kupikea malalamiko kutoka kwa wananchi waliohasiriwa na mawakili walaghai ambao hupokea ridhaa kwa niaba ya wateja wao na kukosa wakalipa, au wakilipwa kuwatetea mahakamani wanakwepa jukumu hilo ilhali wamekwishalipwa. Ni matumaini yetu kuwa ulaghai huu utaangamizwa kabisa kwani hakuna refu lisilokuwa na ncha.
1. Eleza aina nne za ufisadi zilizotajwa katika kifungu ulichosoma
2. Kulingana na kifungu ulichosoma, ufisadi umeathiri nchi yetu kwa njia gani?
3. Serikali inafanya jitihada gani ili kukomesha ufisadi?
4. Kwa maoni yako, unafikiri ufisadi husababishwa na nini?
5. Toa msamiati mwingine wenye maana sawa na rushwa
6. Eleza mana ya msamiati ufuatao kama ulivyotumiwa kifunguni;
(a) Majukumu
(b) Kashfa
(c) Shamiri
(d) wakilia ngoa
(e) Waliohasiriwa
(f) Kita mizizi
Date posted:
October 4, 2019
.
Answers (1)
-
HADITHI FUPI
DAMU NYEUSI NA HADITHI ZINGINEZO
(KEN WALIBORA NA SAID A. MOHAMED)
Mwana wa Darubini (Kristina Mwende Mbai)
“Ulijuaje alikuwa anaangalia kwetu?
a.Eleza muktadha wa dondoo hili.
b.Hadithi...
(Solved)
HADITHI FUPI
DAMU NYEUSI NA HADITHI ZINGINEZO
(KEN WALIBORA NA SAID A. MOHAMED)
Mwana wa Darubini (Kristina Mwende Mbai)
“Ulijuaje alikuwa anaangalia kwetu?
a.Eleza muktadha wa dondoo hili.
b.Hadithi hii inaonyesha matatizo ya kijamii. Fafanua.
c.Eleza yaliyotokea baada ya mazungumzo haya.
Date posted:
October 4, 2019
.
Answers (1)
-
Kimya changu kimezidi, navunja yangu subira,
(Solved)
Soma shairi ifuatayo kisha ujibu maswali yatakayofuata.
Kimya changu kimezidi, navunja yangu subira,
Marejeya ya miradi, kuhitimisha dhamira,
Kukejeli sina budi, niwafunze utu bora,
Nani aali zaidi, Wakenya au vinara?
Serikali bila hadi, ndo kiini cha madhara,
Yanopiga kama radi, isokuwa na ishara,
Yamini kuwa gaidi, wakitupora mishahara,
Nani aali zaidi, Wakenya au vinara?
Wamejifanya hasidi, wasopatana kifikira,
Wana yao maksuudi, kijisombea ujira,
Wakilenga kufaidi, tumbo zao za kichura,
Nani aali zaidi, Wakenya au vinara?
Nchi yetu kufisidi, ni jambo linonikera,
Tangia siku za jadi, ufukara ndo king‘ora,
Kutujazeni ahadi, nyie mkitia for a,
Nani aali zaidi, Wakenya au vinara?
Maskini watozwa kodi, wapwani na walo bara,
Kwa uvumba na uudi, mwawalipa kwa hasara,
Hamudhamini miradi, mejihisi masongora,
Nani aali zaidi, Wakenya au vinara?
Mesema kazi ni chudi, basi sirikali gura,
Nafsi zenu mzirudi, mkubali kuchakura,
Makondeni mkirudi, muondoe ufukara,
Nani aali zaidi, Wakenya au vinara?
Ujanjenu umezidi, demokrasia bakora,
Debeni takaporudi, michirizi kwenye sura,
Kuwachuja a! muradi, kwa za mkizi hasira
Nani aali zaidi, Wakenya au vinara?
Maswali
a) Toa anwani mwafaka kwa shairi hili.
b) Ainisha shairi hili kwa jinsi tatu huku ukitoa sababu.
c) Onyesha Mbinu mbili za lugha katika shairi hili.
d) Bainisha matumizi matatu ya uhuru wa mshairi katika shairi hii.
e) Andika ubeti wa nne katika mtindo tutumbi.
f) Fafanua maudhui matatu yanayojitokeza katika shairi hili.
g) Taja mpango mmoja unaotajwa kama njia ya kutatua matatizo ya nchi.
h) Eleza muhudo wa shairi hili.
Date posted:
October 4, 2019
.
Answers (1)
-
Tunga sentensi moja kubainisha tofauti kati ya:
i) Samani
ii) Zamani
(Solved)
Tunga sentensi moja kubainisha tofauti kati ya:
i) Samani
ii) Zamani
Date posted:
October 4, 2019
.
Answers (1)
-
Habari kuwa watoto chini ya miaka mitatu ‘huwindwa’ kitandani na kuraushwa na wazazi wao waende shuleni mwendo wa saa kumi na moja asubuhi...
(Solved)
Soma taarifa ifuatayo kisha ujibu maswali.
Habari kuwa watoto chini ya miaka mitatu ‘huwindwa’ kitandani na kuraushwa na wazazi wao waende shuleni mwendo wa saa kumi na moja asubuhi ni za kusikitisha.
Kwa mujibu wa ripoti za wataalamu wa elimu ya watoto wachanga (ECD), watoto hao hutakikana kuwa darasani kabla ya saa kumi na mbili asubuhi.
Wanapowasili wao huanza kufukuza ratiba ya masomo ambayo huwapatia muda mfupi mno wa kula, kucheza, kupumzika na hata kuchunguza afya na usalama wao.
Badala ya kuondoka mapema kuelekea nyumbani, wengi wao hufika saa za usiku pamoja na wazazi wao wakitoka kazini. Wanapowasili nyumbani wanapaswa kuoga na kupata chakula cha jioni kwa pupa ili wafanye mazoezi waliyopewa na walimu wao.
Mazoezi hayo huwa ya masomo yote matano huku kila somo likiwa na zaidi ya maswali thelathini. Badala ya kupumzika mwishoni mwa juma, watoto hao huhitjika kuhudhuria shule siku nzima ya Jumamosi. Jumapili wanatakiwa Kanisani na hali hii hujirudia mpaka muhula umalizike. Ikiwa ulidhani watapewa nafasi ya kupumzika wakati wa likizo , umekosea kwa sababu watoto hao huhitajika kuhudhuria shule. Hili limekuwa likiendelea hata baada ya Wizara ya Elimu kupiga marufuku kusomesha wakati wa likizo.
Wazazi-hasa wale wanaofanya kazi mijini- wamekuwa wakiunga mkono mtindo huu kwa sababu unawaondolea mzigo wa malezi na gharama ya kuwaajiri walezi.
Wataalamu wanasema matokeo ya hali hii ni watoto wakembe wenye afya na maadili mabaya kutokana na kuchanganyishwa akili na walimu wanaowataka wajue kila kitu wakiwa na umri mdogo.
Kuwashinikiza watoto wakembe wahudhurie shule na zaidi ya hayo wajue kila kitu kuna madhara mengi. Kwanza kabisa, kuraushwa kwa watoto macheo waende shule kunawanyima fursa ya kulala na kupumzika. Utafiti unaonyesha kuwa watoto wanahitaji kulala na kupumzika kwa zaidi ya saa 12 kwa siku. Hii ina maana kuwa mbali na muda mfupi wanaolala na kupumzika mchana kutwa, watoto wanapaswa kutumia usiku mzima kwa usingizi.
Hii huwasaidia kukua wakiwa na afya nzuri hasa kiakili. Matokeo ya kuwarausha watoto hao waende shule saa hizo huwafanya wakose furaha mbali na kuwafanya wachanganyikiwe kiakili.
Pili, kuwalazimisha watoto wakae darasani kuanzia saa kumi na mbili asubuhi hadi saa kumi na mbili jioni huwa kunawanyima fursa ya kucheza na kutangamana. Wataalamu wa afya ya watoto wanapendekeza kuwa watoto wachanga wanapaswa kucheza ili viungo vya miili yao kama moyo, akili, mapafu na kadhalika vifanye kazi vizuri.
Kinyume na watu wazima ambao hufanya kazi nzito nzito na kuwawezesha kufanya mazoezi, watoto huwa hawafanyi kazi hizo. Wazazi na walimu wanapaswa kufahamu kuwa kazi ya watoto ni mchezo na wana kila haki ya kupewa furaha ya kucheza wakiwa shuleni na hata nyumbani.
Tatu, wazazi wengi ambao hufurahia kuwaachia walimu jukumu la kuwalea watoto wao huku wao wakiwa kazini huwa wanasahau kuwa sio kila mwalimu ana maadili yanayopaswa kuigwa na mwanawe. Ingawa tunawatarajia walimu wawe mifano bora ambayo inaweza kuigwa na kila mtu, ukweli ni kwamba baadhi ya walimu hawajui maana wala hawana maadili. Hatari ni kwamba watoto wakembe husoma kwa kuiga wakubwa wao na ikiwa walimu wanaoshinda nao shule wamepotoka kimaadili, kuna uwezekano mkubwa wa watoto hao kupotoka pia. Hii ndiyo sababu wazazi wengi wamekuwa wakilalamika kuwa wanawao tabia mbaya ambazo hawaelewi zilipotoka.
Kila mzazi anayejali maisha ya mwanawe anapaswa kutekeleza jukumu lake la kumlea na kumwelekeza jinsi anavyotaka akue. Ni kinaya kuwa wanawatarajia wanawao wawe na tabia na maadili kama yao ilhali hawachukui muda wa kukaa nao na kuwaelekeza.
Nne, kuwawinda, kuwaamsha, kuwaosha na kuwalazimisha watoto waende shule kila siku hata ingawa hawataki huwa kunawafanya wawe wategemezi wasioweza kujipangia na kutekeleza mambo kivyao.
(a) Ipe taarifa anwani mwafaka
(b) Mwandishi anatoa maoni gani kuhusu ratiba ya masomo?
(c) Eleza athari za mfumo wa elimu unaoangaziwa hapa
(d) Ni ushauri upi unaotolewa kwa wazazi ?
(e)Taja mbinu zozote mbili za lugha alizotumia mwandishi
(f) Eleza maana ya maneno haya kama yalivyotumiwa katika taarifa.
(i) ‘huwindwa’ kitandani
(ii) Maadili
(iii) Kuwashinikiza…
(iv) Wakembe…
Date posted:
October 4, 2019
.
Answers (1)
-
Weka dagaa kwa ngeli yake.
(Solved)
Weka dagaa kwa ngeli yake.
Date posted:
October 4, 2019
.
Answers (1)
-
Unda nomino kutokana na kitenzi nena.
(Solved)
Unda nomino kutokana na kitenzi nena.
Date posted:
October 4, 2019
.
Answers (1)