Trusted since 2008
Study resources on Kenyaplex

Get ready-made curriculum aligned revision materials

Exam papers, notes, holiday assignments and topical questions – all aligned to the Kenyan curriculum.

1. Nitampa nani, sauti yangu ya dhati Kwa kipimo gani, ingawa kiwakatiti Amefanya nini, la kutetea umati Kipimo ni kipi? 2. Yupi wa maani, asosita katikati Alo na maoni, yasojua...

1. Nitampa nani, sauti yangu ya dhati
Kwa kipimo gani, ingawa kiwakatiti
Amefanya nini, la kutetea umati
Kipimo ni kipi?

2. Yupi wa maani, asosita katikati
Alo na maoni, yasojua gatigati
Atazame chini, kwa kile ule wakati
Kipimo ni kipi?

3. Alo mzalendo, atambuaye shuruti
Asiye mafundo, asojua mangiriti
Anoshika pendo, hata katika mauti
Kipimo ni kipi?

4. Kipimo ni kipi, changu mimi kudhibiti
Utu uko wapi, ni wapi unapoketi
Nje kwa mkwapi, au ndani kwa buheti
Kipimo ni kipi?

a) Eleza umbo la shairi hili
b) Taja na ueleze jinsi mwandishi alivyotumia uhuru wa ushairi
c) Eleza ujumbe unaowasilishwa na mshairi
d) Andika ubeti wa tatu katika lugha ya nathari
e) Taja bahari tatu zinazojitokeza katika shairi na utoe sababu
f) Eleza msamiati ufuatao kama ulivyotumika katika shairi hili
i) Katiti
ii) Gatigati
iii) Mangiriti

Answers


Maurice
a) - Beti nne
- Mishororo mine katika kila ubet (tarbia)
- Mshororo wa nne mfupi (msuko)
- Mizani 6:8 mshororo wa 1-3 kikai
6 mshororo wa mwisho

b) Inkisari – Anoshika
- Alo
- Asosita
Lafudhi – Katiti
- mangiriti


c) - Anataka asikike (mawazo yake yasikika)
- Anatafuta atakayoeleza ujumbe wake
- anashindwa atatumia kipimo kipi
- Mtu huyo lazima awe mzalendo aliye jasiri
- Lazima awe anayetambua utu

d) Lugha ya nadharia
Aliye mzalendo na alambuaye haya mtu asiye mwoga, aliyejawa na upendo hata wakati wa
hatari, Ni kipimo kipi cha kumtambua mtu kama huyu

e) tarbia – Mishororo mine kila ubeti
Kikai – Mizani isiyozidi 15
Msuko – Kibwagizo kifupi

f) i) katili – Kidogo
Gati gati – Ubaguzi
Mangiriti - mambo ya upipi
maurice.mutuku answered the question on October 9, 2019 at 06:36

Answer Attachments

Exams With Marking Schemes

Related Questions