Get premium membership and access questions with answers, video lessons as well as revision papers.

Eleza tofauti ya kimaana katika sentensi hizi i)Nisimamapo huchekwa ii)Ninaposimama huchekwa

      

Eleza tofauti ya kimaana katika sentensi hizi
i)Nisimamapo huchekwa
ii)Ninaposimama huchekwa

  

Answers


Kavungya
i) Wakati wowote
ii) Wakati maalumu
Kavungya answered the question on October 11, 2019 at 07:27


Next: Tambua kiima, shamirisho, chagizo na kiarifa katika sentensi ifuatayo Nyanya alimjengea mjukuu nyumba kwa matofali mwaka jana.
Previous: Eleza dhana ya kishazi tegemezi.

View More Kiswahili Questions and Answers | Return to Questions Index


Learn High School English on YouTube

Related Questions


  • Tambua kiima, shamirisho, chagizo na kiarifa katika sentensi ifuatayo Nyanya alimjengea mjukuu nyumba kwa matofali mwaka jana. (Solved)

    Tambua kiima, shamirisho, chagizo na kiarifa katika sentensi ifuatayo
    Nyanya alimjengea mjukuu nyumba kwa matofali mwaka jana.

    Date posted: October 11, 2019.  Answers (1)

  • Tunga sentensi ukitumia vihusishi vya: a) Kulinganisha b)Sababu c)Wakati (Solved)

    Tunga sentensi ukitumia vihusishi vya:
    a) Kulinganisha
    b)Sababu
    c)Wakati

    Date posted: October 11, 2019.  Answers (1)

  • Tofautisha sentensi zifuatazo. i) Ningekuwa na pesa ningenunua simu nzuri ii)Ningalikuwa na pesa ningalinunua simu nzuri (Solved)

    Tofautisha sentensi zifuatazo.
    i) Ningekuwa na pesa ningenunua simu nzuri
    ii)Ningalikuwa na pesa ningalinunua simu nzuri

    Date posted: October 11, 2019.  Answers (1)

  • Changanua sentensi ifuatayo kwa njia ya mistari Wanafunzi wenye bidii hufuzu mtihani (Solved)

    Changanua sentensi ifuatayo kwa njia ya mistari
    Wanafunzi wenye bidii hufuzu mtihani

    Date posted: October 11, 2019.  Answers (1)

  • Andika katika usemi wa taarifa “Mtapata mwaliko wenu kesho,” alisema Salim (Solved)

    Andika katika usemi wa taarifa
    “Mtapata mwaliko wenu kesho,” alisema Salim

    Date posted: October 11, 2019.  Answers (1)

  • Ainisha mofimu katika neno lifuatalo Sikumkaribisha (Solved)

    Ainisha mofimu katika neno lifuatalo
    Sikumkaribisha

    Date posted: October 11, 2019.  Answers (1)

  • Maneno haya yamo katika ngeli gani? Tayo Kipepeo (Solved)

    Maneno haya yamo katika ngeli gani?
    Tayo
    Kipepeo

    Date posted: October 11, 2019.  Answers (1)

  • Tofautisha sauti zifuatazo. /a/ /u/ (Solved)

    Tofautisha sauti zifuatazo.
    /a/
    /u/

    Date posted: October 11, 2019.  Answers (1)

  • Soma makala haya kisha ujibu maswali yafuatayo HAKI ZA BINADAMU Binadamu wana mazoea ya kufikiria kuwa jinsi wafanyavyo, waongeavyo na wafikiriavyo kuhusu vitu ndivyo inavyopasa...(Solved)

    Soma makala haya kisha ujibu maswali yafuatayo
    HAKI ZA BINADAMU
    Binadamu wana mazoea ya kufikiria kuwa jinsi wafanyavyo, waongeavyo na wafikiriavyo kuhusu vitu ndivyo inavyopasa kuwa. Kama binandamu tunaamini njia yetu ndiyo sahihi, yenye mantiki na inayopasa kufuatwa na kila mtu. Msingi huu huu unakwenda kinyume na kutambua kila binadamu ana haki ya kufikiri, kusema au kuongea na kutenda mradi asikiuke haki ya mwenzake iliyo sawa na yake. Nguzo mojawapo inayogongomelea hoja hii ni Haki za Binadamu.

    Azimio kutangaza Haki Bia za Binadamu liliafikiwa na Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa tarehe 10 Desemba 1948. Baraza kuu hilo liliyasisitizia mataifa wanachama umuhimu wa kuyasambaza, kuenezea, na kusisitiza kusambazwa kwa azimio hilo katika shule na taasisi za kielimu. Msingi wa uhuru, haki na amani ulimwenguni ni kutambua binadamu wote wana haki sawa. Ingawa kimsingi jamii na mataifa yote ya ulimwengu yanapaswa kuthamini, kusambaza na kuhimiza umuhimu wa Haki za Binadamu zipo jamii ambazo hukiuka haki hizo. Matokeo ya ukiukaji huu yana athari hasi sana kama ilivyotokea nchini Rwanda na Bosnia. Herzegovina kulikotokea mauaji ya halaiki.

    Azimio la Haki za Binadamu linajumuisha vipengele kadha ambavyo ni mihimili mikuu ya Azimio lenyewe. Kipengele msingi kabisa kinasisitiza kuwa kila kiumbe anazaliwa huru na ana haki na hadhi sawa na kiumbe mwingine. Ukweli wa kauli hii ulikokotezwa na kauli ya mwanafalsafa maarufu Jean Jacques Rosseau aliyesema kuwa kila kiumbe huzaliwa huru lakini huwa katika pingu ulimwengu mzima. Kauli hii ilitambua ukiukaji huu wa kipengele hiki. Kipengele cha pili kinasisitiza kuwa binadamu wote wana haki za kufurahia uhuru wao pasi na kutengwa au kubezwa kwa misingi yoyote ile si rangi, kabila, jinsia, lugha, dini, asilia, utajiri au chochote kile.

    Vipengele vingine vinatukumbusha kuwa kila mtu ana haki ya kuishi na kupata ulinzi. Hamna mtu anayepaswa kuishi maisha ya utumwa au unyonge wa kutumikishwa kwa namna yoyote ile. Suala hili linasisitizwa na kipengele cha sita kinachokataza kudhalilishwa kwa watu au kutunzwa kwa namna yoyote ambayo inamfedhehesha kama kiumbe. Azimio la Haki za Binadamu linasisitiza kuwa binadamu yoyote nyule ana haki ya kupata ulinzi wa kisheria. Binadamu huyo hapaswi kubaguliwa na ana haki ya kupata fidia ya kisheria taraa haki zake za kimsingi zikikiukwa.

    Hata hivyo sio watu wote ulimwenguni ambao wanazifurahia haki hizi za kimsingi. Zipo lukuki za jamii ulimwenguni ambako haki za kimsingi zinakiukwa. Katika nchi ambazo zinaongozwa na watawala wa kiimla, si ajabu kuona haki za binadamu zikikiukwa. Viongozi wa aina hiyo huwa wamegeuzwa ng’ombe wa shemere na tamaa, ubinafsi na ukatili usiojua thamani ya utu. Viongozi wa aina hii wanasahau kuwa kila binadamu ana haki ya kuishi maisha huru, asipotumikishwa wala kulanguliwa kama bidhaa.

    Nchi za kiimla aghalabu huongozwa na itikadi kuwa kiongozi ndiye pekee ambaye ana uwezo wa kufikiri, kuamua na kutenda. Watu wengine wanapaswa kumfuata kisilka kama yule mbwa wa Pavlov ambaye alitokwa na mate kila kengele ilipopigwa. Viongozi wa ama hii hawachelei kuwatenza nguvu raia zao: Kuwadhalilisha kwa namna nyingi. Viongozi wa aina hiyo huiona sheria ya nchi kama iliyowekwa kwa watu wengine bali sio wao. Msimamo huu unakwenda kinyume na kipengele cha saba cha Haki Bia za Binadamu kisemacho kuwa watu wote ni sawa mbele ya sheria.

    Baadhi ya haki zinazokiukwa katika jamii za kimabavu ni haki ya watu kuungana, kuwaza, kushiriki katika maamuzi ya serikali, kuwa mwanachama wa jumuia waitakayo, kumiliki mali, kutembea, kuishi anakotaka kutohukumiwa bila ya kuwako na utaratibu wa kisheria. Ni muhimu hata hivyo kujua ni muhimu kwa raia wenyewe kujielimisha na kuzijua haki zao. Serikali inapaswa kuwa mlinzi wa sheria zenyewe. Lakini muhimu kujua pia kuwa mlinzi naye hulindwa pia.

    Maswali
    a)Kwa maneno kati ya 90 – 100 fafanua Haki Bia za Binadamu zilizoafikiwa na Baraza kuu la umoja wa Mataifa.
    Nakala Chafu
    Nakala Safi
    b) Kwa nini viongozi wa kiimla hukiuka haki za binadamu. (Maneno 50 – 60).
    Nakala Chafu

    Date posted: October 11, 2019.  Answers (1)

  • Soma kifungu kifuatacho kisha ujibu maswali Tokea muundo mpya wa serikali ya ugatuzi uanze kutekelezwa miaka miwili iliyopita, kumeendelea kushuhudiwa matatizo mengi hali iliyopelekea kushuhudiwa kwa...(Solved)

    Soma kifungu kifuatacho kisha ujibu maswali
    Tokea muundo mpya wa serikali ya ugatuzi uanze kutekelezwa miaka miwili iliyopita, kumeendelea kushuhudiwa matatizo mengi hali iliyopelekea kushuhudiwa kwa msururu wa migomo na maandamano ya raia. Fujo za karibuni kabisa ni zile zinazoshuhudiwa katika miji mikubwa za wachuuzi na wafanyibiashara wakipinga hatua za serikali za kaunti kuwatoza ushuru takribani kwa kila huduma na bidhaa ikiwemo wanyama, kuku na ndege. La kuhuzunisha zaidi katika baadhi ya majimbo imeripotiwa kuwa raia wamelazimishwa kulipa ushuru kwa kutaka tu kuona maiti za jamaa zao kwenye vyumba vya kuhifadhi maiti.

    Wanasiasa wameonekana kuwa na wakati mgumu kutetea mfumo huu mpya wa ugatuzi huku baadhi wakisema kwamba matatizo yanayoshuhudiwa kwa sasa yametokana na ugeni wa mfumo huo. Wengine wameinyoshea kidole serikali ya kitaifa kwamba ndiyo inayosambaratisha muundo huu. Wengine wanahoji kuwa bado ni mapema na kwamba kunatajika muda mrefu ili kufaulu.

    Ni wazi kwamba kumekosekana nidhamu bora ya kusimamia maisha ya raia nchini Kenya. Matatizo yanayokumba raia kwa sasa ni dalili kuwa mfumo wa serikali ya ugatuzi umeongezea chumvi kwenye kidonda badala ya kutibu. Swali ni je, hadi lini nidhamu ya kusimamia raia itakuwa ni suala la majaribio na makosa?

    Hatua ya kuwarundikizia raia ushuru mkubwa ni kitendo cha unyonyaji na cha dhuluma kinachofaa kupingwa. La kufahamishiwa hapa ni kwamba ushuru ndio njia kubwa ya kuzalisha mapato ya serikali zinazojifunga na mfumo wa kimagharibi wa kiuchumi wa kibepari ikiwemo Kenya. Asilimia 90 ya mapato ya serikali za kibepari huegemea ushuru. Kwa hivyo hatua ya serikali za kaunti katika kuwanyonya raia kwa kuwalipisha ushuru si ajabu bali ni thibitisho kuwa jamii ya Kenya inaongozwa na nidhamu ya kiuchumi ya ubepari mfumo wa unyonyaji na ukandamizaji. Ukweli unabakia kuwa ndani ya serikali za kibepari raia ndio hubebeshwa mzigo wa ushuru unaoishia matumboni mwa viongozi!

    Miito ya mabadiliko ya katiba na ya miundo mipya ya kiutawala si lolote ila ni moja tu ya hatua za mfumo wa kibepari kujipa muda wa kuishi na kuziba aibu zake za kushindwa kusimamia maisha ya watu. Kufeli huku kwa mfumo huu kunashuhudiwa hadi kwenye nchi kubwa za kibepari kama Marekani na Uingereza hivyo nazo zimekumbwa tele na maandamano na fujo za raia wakilalamikia hali ngumu ya maisha.

    Maswali
    a)Yape makala haya anwani mwafaka.
    b)Eleza mtazamo wa wanasiasa kuhusu utepetevu wa mfumo huu.
    c)“Ugatuzi nchini Kenya ni mfumo wa kibepari” Thibitisha kauli hii kwa kurejelea makala.
    d)Migomo ni zao la matatizo yaliyogatuliwa kutoka kuu. Toa sababu nyingine zinazosababisha migomo katika serikali za ugatuzi
    e)Thibitisha jinsi mfumo wa ugatuzi umeongeza chumvi kwenye kidonda badala ya kutibu
    f)Eleza maana ya maneno yafuatayo
    i) Ugatuzi
    ii) Kibepari

    Date posted: October 11, 2019.  Answers (1)

  • (vigelegele vya harusi vililia alilili ; x3) Kuumeni : (waliimba) Tumeupata mpilipili na maua yake chikicha x2 Kukeni : (wimbo wao kwa sauti tofauti) Tausi waendaa x2 Tausi...(Solved)

    Soma kifungu kifuatacho kisha ujibu maswali yafuatayo :

    (vigelegele vya harusi vililia alilili ; x3)
    Kuumeni : (waliimba) Tumeupata mpilipili na maua yake chikicha x2

    Kukeni : (wimbo wao kwa sauti tofauti) Tausi waendaa x2
    Tausi waenda wamuacha mama kwenye banda.

    Kuumeni : (wakijibu wimbo) Mwacheni aendee x2
    Mwacheni aende akaone mambo ya nyumba.

    Kukeni : Mama ataota nini x2.
    Ataota nini, hana mtu wa kumletea kuni.

    Kuumeni : Ataota moto wa magunzi, wa magunzi wa magunzi. Twamchukua, kisura wetu,
    kisura wetu, kisura wetu.
    Tausi ni wetu sasa, ni kito chema, ni kito chema ni kito chema.

    (i) Wimbo huu ni wa aina gani, na unastahili katika hafla gani ?
    (ii) Bainisha wahusika Kuumeni na Kukeni
    (iii) Fafanua ujumbe uliojikita katika utungo huu
    (iv) Wimbo huu una umuhimu gani hafla ulioimbiwa?
    (v) Tambua mtindo uliotumika katika utungo huu

    Date posted: October 11, 2019.  Answers (1)

  • Onyesha tofauti kati ya vikundi hivi: (i) Hekaya Hurafa (ii) Visakale Visasili (iii) Ngano za mtanziko Ngano za mazimwi(Solved)

    Onyesha tofauti kati ya vikundi hivi:
    (i) Hekaya
    Hurafa

    (ii) Visakale
    Visasili

    (iii) Ngano za mtanziko
    Ngano za mazimwi

    Date posted: October 11, 2019.  Answers (1)

  • Elezea mbinu nne za kutongolea hadithi(Solved)

    Elezea mbinu nne za kutongolea hadithi

    Date posted: October 11, 2019.  Answers (1)

  • Ni nini maana ya Tendi?(Solved)

    Ni nini maana ya Tendi?

    Date posted: October 11, 2019.  Answers (1)

  • MUITALIA ANAZWE Saa kumi alfajiri Sote tuliamshwa Safari tuliianza Wengi wanauliza Mwitalia alikuja lini? Na...(Solved)

    Soma wimbo/shairi lifuatalo kisha ujibu maswali yanayofuata

    MUITALIA ANAZWE
    Saa kumi alfajiri
    Sote tuliamshwa
    Safari tuliianza
    Lazima tuimalize
    Maji ukiyavulia nguo
    Lazima uyaoge

    Wazee kwa vijana waliimba
    Muitalia lazima anazwe
    Mashamba yao walilia
    Uui! Jikaze wavulana
    Hawataki rangi hii

    Wengi wanauliza
    Mwitalia alikuja lini? Na ataondoka lini?
    Mnaze huyu mlowezi
    Hatuchoki
    Hatuchoki
    Lazima yeye anazwe

    Vifaranga na mbuzi
    Mbavu zao zahesabika
    Meee! Sauti zilihinikiza kote
    Haya yote hakika, ni madhila ya Muitalia
    Nguvu kweli tunayo
    Simama mbele tunayo
    Simama mbele uone !
    Muitalia ondoka !
    Au nikuondoe kwa nguvu

    (a) Taja madhila yaliyosababishwa na Muitalia katika makala haya.
    (b) Thibitisha kuwa utungo huu ni wimbo.
    (c) Eleza maana inayojitokeza katika mistari ifuatayo:-
    (i) Mbavu zao zahesabika.
    (ii) Haya yote hakika, ni madhila ya Muitalia.
    (d) Huu ni wimbo wa aina gani? Eleza ukitoa ushahidi
    (e) Eleza kwa sentensi mbili au tatu shughuli muhimu za kiuchumi za watu wanaimba wimbo huu
    (f) Taja mbinu za lugha zilizotumiwa katika wimbo huu. Toa ushahidi
    (g) Taja mafunzo mawili yanayotokana na wimbo huu

    Date posted: October 11, 2019.  Answers (1)

  • Jadili kwa kina matatizo ambayo huenda yakakabili fasihi simulizi katika jamii ya kesho kisha utoe mapendekezo ya jinsi ya kukabiliana na hali hii(Solved)

    Jadili kwa kina matatizo ambayo huenda yakakabili fasihi simulizi katika jamii ya kesho kisha utoe mapendekezo ya jinsi ya kukabiliana na hali hii

    Date posted: October 11, 2019.  Answers (1)

  • Bainisha tamathali za usemi zilizotumika katika methali zifuatazo:- (i) Ujana ni moshi ukienda haurudi (ii) Usipoziba ufaa utajenga ukuta(Solved)

    Bainisha tamathali za usemi zilizotumika katika methali zifuatazo:-
    (i) Ujana ni moshi ukienda haurudi
    (ii) Usipoziba ufaa utajenga ukuta

    Date posted: October 11, 2019.  Answers (1)

  • Wawe na kimai ni nini katika fasihi simulizi? Eleza faida zake(Solved)

    Wawe na kimai ni nini katika fasihi simulizi? Eleza faida zake

    Date posted: October 9, 2019.  Answers (1)

  • Hapo zamani za kale, Mungu alituma wajumbe wawili waende duniani. Wajumbe hawa ni Kinyonga na Mjusi. Kwanza...(Solved)

    Hapo zamani za kale, Mungu alituma wajumbe wawili waende duniani. Wajumbe hawa ni Kinyonga na Mjusi. Kwanza alimtuma Kinyonga na kumwagiza akaseme “wanadamu hamtakufa.” Kinyonga alienda kwa mwendo wa kuduwaa, akasimama hapa na pale akila matunda ya miti. Kwa sababu ya hali hii alichelewa sana kufikisha ujumbe kwa binadamu.
    Baada ya muda kupita, Mungu alimtuma Mjusi na ujumbe akaseme, “Mwanadamu sharti kufa.” Mjusi aliunyanyua mkia akafyatuka pu! Mbio akawahi duniani kabla ya kinyonga kuwasili. Kwa haraka alitangaza agizo kuu, “Wanadamu sharti kufa!” Akarejelea haraka kwa Mungu. Baada ya muda kinyonga naye akafika duniana na kutangaza, “Wanadamu hamtakufa!” Wanadamu wakapinga mara na kusema, “La! Tumeshapata ujumbe wa Mjusi, wanadamu sharti kufa! Hatuwezi kupokea tena neno lako! Basi kulingana na neno la mjusi, wanadamu hufa.

    (a) (i) Hadithi hii huitwaje?
    (ii) Toa sababu zako
    (b) Eleza sifa tatu zinazohusishwa na ngano za fasihi simulizi katika hadithi hii
    (c) Kinyonga ni mhusika wa aina gani?
    (d) Hadithi hii ina umuhimu gani?
    (e) Taja njia zozote nne za kukusanya kazi za fasihi simulizi
    (f) Tambulisha vipera hivi:-
    (i) Kula hepi
    (ii) Sema yako ni ya kuazima
    (iii) Baba wa Taifa

    Date posted: October 9, 2019.  Answers (1)

  • Lala mtoto lala x2 Mama atakuja lala Alienda sokoni lala Aje na ndizi lala Ndizi ya mtoto lala Na maziwa ya mtoto lala Andazi lako akirudi Pia nyama ya kifupa Kifupa, kwangu, wewe...(Solved)

    Lala mtoto lala x2
    Mama atakuja lala
    Alienda sokoni lala
    Aje na ndizi lala
    Ndizi ya mtoto lala
    Na maziwa ya mtoto lala
    Andazi lako akirudi
    Pia nyama ya kifupa
    Kifupa, kwangu, wewe kinofu
    Kipenzi mwana lala x2

    Titi laja x2

    Basi kipenzi lala
    Baba atakuja lala
    Aje na mkate lala
    Mkate wa mtoto lala
    Tanona ja ndovu lala


    (a) Huku ukithibitisha jibu lako eleza huu ni wimbo wa aina gani?
    (b) Eleza sifa za wimbo wa aina hii
    (c) Onyesha umuhimu wa wimbo huu
    (d) Eleza amali kuhusu jamii zinazojitokeza katika wimbo huu
    (e) Tambua mbinu zozote mbili za utunzi zilizotumika katika wimbo huu
    (f) Taja vitendo viwili vinavyoambatana na uimbaji wa aina hii ya wimbo
    (g) Wimbo huu una wahusika wangapi? Wataje

    Date posted: October 9, 2019.  Answers (1)