Trusted since 2008
Study resources on Kenyaplex

Get ready-made curriculum aligned revision materials

Exam papers, notes, holiday assignments and topical questions – all aligned to the Kenyan curriculum.

Tunga sentensi kuonyesha maana mbili za neno chuma

Tunga sentensi kuonyesha maana mbili za neno chuma

Answers


Kavungya
Watoto hao wanachuma machungwa
Nondo za madirisha hutengenezwa kwa chuma
Mimi ninafanya kazi ili kuchuma pesa
Kavungya answered the question on October 11, 2019 at 07:32

Answer Attachments

Exams With Marking Schemes

Related Questions

  • Eleza dhana ya kishazi tegemezi. (Solved)

    Eleza dhana ya kishazi tegemezi.

    Date posted: October 11, 2019 .    Answers (1)

  • Tambua kiima, shamirisho, chagizo na kiarifa katika sentensi ifuatayo Nyanya alimjengea mjukuu nyumba kwa matofali mwaka jana. (Solved)

    Tambua kiima, shamirisho, chagizo na kiarifa katika sentensi ifuatayo
    Nyanya alimjengea mjukuu nyumba kwa matofali mwaka jana.

    Date posted: October 11, 2019 .    Answers (1)

  • Tunga sentensi ukitumia vihusishi vya: a) Kulinganisha b)Sababu c)Wakati (Solved)

    Tunga sentensi ukitumia vihusishi vya:
    a) Kulinganisha
    b)Sababu
    c)Wakati

    Date posted: October 11, 2019 .    Answers (1)

  • Tofautisha sentensi zifuatazo. i) Ningekuwa na pesa ningenunua simu nzuri ii)Ningalikuwa na pesa ningalinunua simu nzuri (Solved)

    Tofautisha sentensi zifuatazo.
    i) Ningekuwa na pesa ningenunua simu nzuri
    ii)Ningalikuwa na pesa ningalinunua simu nzuri

    Date posted: October 11, 2019 .    Answers (1)

  • Changanua sentensi ifuatayo kwa njia ya mistari Wanafunzi wenye bidii hufuzu mtihani (Solved)

    Changanua sentensi ifuatayo kwa njia ya mistari
    Wanafunzi wenye bidii hufuzu mtihani

    Date posted: October 11, 2019 .    Answers (1)

  • Ainisha mofimu katika neno lifuatalo Sikumkaribisha (Solved)

    Ainisha mofimu katika neno lifuatalo
    Sikumkaribisha

    Date posted: October 11, 2019 .    Answers (1)

  • Maneno haya yamo katika ngeli gani? Tayo Kipepeo (Solved)

    Maneno haya yamo katika ngeli gani?
    Tayo
    Kipepeo

    Date posted: October 11, 2019 .    Answers (1)

  • Tofautisha sauti zifuatazo. /a/ /u/ (Solved)

    Tofautisha sauti zifuatazo.
    /a/
    /u/

    Date posted: October 11, 2019 .    Answers (1)

  • (vigelegele vya harusi vililia alilili ; x3) Kuumeni : (waliimba) Tumeupata mpilipili na maua yake chikicha x2 Kukeni : (wimbo wao kwa sauti tofauti) Tausi waendaa x2 Tausi... (Solved)

    Soma kifungu kifuatacho kisha ujibu maswali yafuatayo :

    (vigelegele vya harusi vililia alilili ; x3)
    Kuumeni : (waliimba) Tumeupata mpilipili na maua yake chikicha x2

    Kukeni : (wimbo wao kwa sauti tofauti) Tausi waendaa x2
    Tausi waenda wamuacha mama kwenye banda.

    Kuumeni : (wakijibu wimbo) Mwacheni aendee x2
    Mwacheni aende akaone mambo ya nyumba.

    Kukeni : Mama ataota nini x2.
    Ataota nini, hana mtu wa kumletea kuni.

    Kuumeni : Ataota moto wa magunzi, wa magunzi wa magunzi. Twamchukua, kisura wetu,
    kisura wetu, kisura wetu.
    Tausi ni wetu sasa, ni kito chema, ni kito chema ni kito chema.

    (i) Wimbo huu ni wa aina gani, na unastahili katika hafla gani ?
    (ii) Bainisha wahusika Kuumeni na Kukeni
    (iii) Fafanua ujumbe uliojikita katika utungo huu
    (iv) Wimbo huu una umuhimu gani hafla ulioimbiwa?
    (v) Tambua mtindo uliotumika katika utungo huu

    Date posted: October 11, 2019 .    Answers (1)

  • Onyesha tofauti kati ya vikundi hivi: (i) Hekaya Hurafa (ii) Visakale Visasili (iii) Ngano za mtanziko Ngano za mazimwi (Solved)

    Onyesha tofauti kati ya vikundi hivi:
    (i) Hekaya
    Hurafa

    (ii) Visakale
    Visasili

    (iii) Ngano za mtanziko
    Ngano za mazimwi

    Date posted: October 11, 2019 .    Answers (1)

  • Elezea mbinu nne za kutongolea hadithi (Solved)

    Elezea mbinu nne za kutongolea hadithi

    Date posted: October 11, 2019 .    Answers (1)

  • Ni nini maana ya Tendi? (Solved)

    Ni nini maana ya Tendi?

    Date posted: October 11, 2019 .    Answers (1)

  • MUITALIA ANAZWE Saa kumi alfajiri Sote tuliamshwa Safari tuliianza Wengi wanauliza Mwitalia alikuja lini? Na... (Solved)

    Soma wimbo/shairi lifuatalo kisha ujibu maswali yanayofuata

    MUITALIA ANAZWE
    Saa kumi alfajiri
    Sote tuliamshwa
    Safari tuliianza
    Lazima tuimalize
    Maji ukiyavulia nguo
    Lazima uyaoge

    Wazee kwa vijana waliimba
    Muitalia lazima anazwe
    Mashamba yao walilia
    Uui! Jikaze wavulana
    Hawataki rangi hii

    Wengi wanauliza
    Mwitalia alikuja lini? Na ataondoka lini?
    Mnaze huyu mlowezi
    Hatuchoki
    Hatuchoki
    Lazima yeye anazwe

    Vifaranga na mbuzi
    Mbavu zao zahesabika
    Meee! Sauti zilihinikiza kote
    Haya yote hakika, ni madhila ya Muitalia
    Nguvu kweli tunayo
    Simama mbele tunayo
    Simama mbele uone !
    Muitalia ondoka !
    Au nikuondoe kwa nguvu

    (a) Taja madhila yaliyosababishwa na Muitalia katika makala haya.
    (b) Thibitisha kuwa utungo huu ni wimbo.
    (c) Eleza maana inayojitokeza katika mistari ifuatayo:-
    (i) Mbavu zao zahesabika.
    (ii) Haya yote hakika, ni madhila ya Muitalia.
    (d) Huu ni wimbo wa aina gani? Eleza ukitoa ushahidi
    (e) Eleza kwa sentensi mbili au tatu shughuli muhimu za kiuchumi za watu wanaimba wimbo huu
    (f) Taja mbinu za lugha zilizotumiwa katika wimbo huu. Toa ushahidi
    (g) Taja mafunzo mawili yanayotokana na wimbo huu

    Date posted: October 11, 2019 .    Answers (1)

  • Jadili kwa kina matatizo ambayo huenda yakakabili fasihi simulizi katika jamii ya kesho kisha utoe mapendekezo ya jinsi ya kukabiliana na hali hii (Solved)

    Jadili kwa kina matatizo ambayo huenda yakakabili fasihi simulizi katika jamii ya kesho kisha utoe mapendekezo ya jinsi ya kukabiliana na hali hii

    Date posted: October 11, 2019 .    Answers (1)

  • Bainisha tamathali za usemi zilizotumika katika methali zifuatazo:- (i) Ujana ni moshi ukienda haurudi (ii) Usipoziba ufaa utajenga ukuta (Solved)

    Bainisha tamathali za usemi zilizotumika katika methali zifuatazo:-
    (i) Ujana ni moshi ukienda haurudi
    (ii) Usipoziba ufaa utajenga ukuta

    Date posted: October 11, 2019 .    Answers (1)

  • Wawe na kimai ni nini katika fasihi simulizi? Eleza faida zake (Solved)

    Wawe na kimai ni nini katika fasihi simulizi? Eleza faida zake

    Date posted: October 9, 2019 .    Answers (1)

  • Hapo zamani za kale, Mungu alituma wajumbe wawili waende duniani. Wajumbe hawa ni Kinyonga na Mjusi. Kwanza... (Solved)

    Hapo zamani za kale, Mungu alituma wajumbe wawili waende duniani. Wajumbe hawa ni Kinyonga na Mjusi. Kwanza alimtuma Kinyonga na kumwagiza akaseme “wanadamu hamtakufa.” Kinyonga alienda kwa mwendo wa kuduwaa, akasimama hapa na pale akila matunda ya miti. Kwa sababu ya hali hii alichelewa sana kufikisha ujumbe kwa binadamu.
    Baada ya muda kupita, Mungu alimtuma Mjusi na ujumbe akaseme, “Mwanadamu sharti kufa.” Mjusi aliunyanyua mkia akafyatuka pu! Mbio akawahi duniani kabla ya kinyonga kuwasili. Kwa haraka alitangaza agizo kuu, “Wanadamu sharti kufa!” Akarejelea haraka kwa Mungu. Baada ya muda kinyonga naye akafika duniana na kutangaza, “Wanadamu hamtakufa!” Wanadamu wakapinga mara na kusema, “La! Tumeshapata ujumbe wa Mjusi, wanadamu sharti kufa! Hatuwezi kupokea tena neno lako! Basi kulingana na neno la mjusi, wanadamu hufa.

    (a) (i) Hadithi hii huitwaje?
    (ii) Toa sababu zako
    (b) Eleza sifa tatu zinazohusishwa na ngano za fasihi simulizi katika hadithi hii
    (c) Kinyonga ni mhusika wa aina gani?
    (d) Hadithi hii ina umuhimu gani?
    (e) Taja njia zozote nne za kukusanya kazi za fasihi simulizi
    (f) Tambulisha vipera hivi:-
    (i) Kula hepi
    (ii) Sema yako ni ya kuazima
    (iii) Baba wa Taifa

    Date posted: October 9, 2019 .    Answers (1)

  • Lala mtoto lala x2 Mama atakuja lala Alienda sokoni lala Aje na ndizi lala Ndizi ya mtoto lala Na maziwa ya mtoto lala Andazi lako akirudi Pia nyama ya kifupa Kifupa, kwangu, wewe... (Solved)

    Lala mtoto lala x2
    Mama atakuja lala
    Alienda sokoni lala
    Aje na ndizi lala
    Ndizi ya mtoto lala
    Na maziwa ya mtoto lala
    Andazi lako akirudi
    Pia nyama ya kifupa
    Kifupa, kwangu, wewe kinofu
    Kipenzi mwana lala x2

    Titi laja x2

    Basi kipenzi lala
    Baba atakuja lala
    Aje na mkate lala
    Mkate wa mtoto lala
    Tanona ja ndovu lala


    (a) Huku ukithibitisha jibu lako eleza huu ni wimbo wa aina gani?
    (b) Eleza sifa za wimbo wa aina hii
    (c) Onyesha umuhimu wa wimbo huu
    (d) Eleza amali kuhusu jamii zinazojitokeza katika wimbo huu
    (e) Tambua mbinu zozote mbili za utunzi zilizotumika katika wimbo huu
    (f) Taja vitendo viwili vinavyoambatana na uimbaji wa aina hii ya wimbo
    (g) Wimbo huu una wahusika wangapi? Wataje

    Date posted: October 9, 2019 .    Answers (1)

  • 1. Ni sumu, sumu hatari Unahatarisha watoto Kwa ndoto zako zako leweshi Za kupanda ngazi Ndoto motomoto ambazo Zimejenga ukuta Baina ya watoto Na maneno laini Ya ulimi wa wazazi 2. Ni sumu, sumu... (Solved)

    1. Ni sumu, sumu hatari
    Unahatarisha watoto
    Kwa ndoto zako zako leweshi
    Za kupanda ngazi
    Ndoto motomoto ambazo
    Zimejenga ukuta
    Baina ya watoto
    Na maneno laini
    Ya ulimi wa wazazi

    2. Ni sumu, sumu hasiri
    Unahasiri watoto
    Kwa pupa yako hangaishi
    Ya kuwa tajiri mtajika
    Pupa pumbazi ambayo
    Imezaa jangwa bahili
    Badala ya chemichemi
    Ya mazungumzo na maadili
    Baina ya watoto na mzazi

    3. Ni sumu, sumu legezi
    Unalegeza watoto
    Kwa mazoea yako tenganishi
    Ya daima kunywa ‘moja baridi’
    Mazoea mabaya ambayo yanafunga katika klabu
    Hadi saa nane usiku
    Huku yakijenga kutofahamiana
    Baina ya watoto na mzazi

    4. Ni sumu, sumu jeruhi
    Unajeruhi watoto kwa pesa,
    Kwa mapenzi yako hatari
    Ya kuwaliwaza watoto kwa pesa
    Zinawafikisha kwenye sigara na ulevi
    Na kisha kwenye madawa ya giza baridi
    Barabara inayofikisha kwenye giza baridi la kaburi la asubuhi


    (a) Pendekeza kichwa kwa shairi hili
    (b) Fafanua maudhui ya shairi hili
    (c) Ni kwa njia gani kinachozungumziwa kinajenga ukuta?
    (d) Dondoa tamathali mbili za usemi zilizotumika katika shairi na uzitolee mfano
    (e) Eleza umbo la shairi hili
    (f) Uandike ubeti wa nne kwa lugha nathari
    (g) Eleza maana ya vifungu hivi vilivyotumika katika shairi ;
    (i) Giza baridi
    (ii) Yanakufunga katika klabu

    Date posted: October 9, 2019 .    Answers (1)

  • CHEMA HAKIDUMU Chema hakidumu, kingapendekeza, Saa ikitimu, kitakuteleza, Ukawa na hamu, kukingojeleza, Huwa ni vigumu, (Solved)

    CHEMA HAKIDUMU
    Chema hakidumu, kingapendekeza,
    Saa ikitimu, kitakuteleza,
    Ukawa na hamu, kukingojeleza,
    Huwa ni vigumu, kamwe hutaweza.

    Chema sikiimbi, kwamba nakitweza,
    Japo mara tumbi, kinshaniliza,
    Na japo siombi, kipate n’ongeza,
    Mtu haniambi, pa kujilimbikiza.

    Chema mara ngapi, kinaniondoka,
    Mwahanga yu wapi? Hakukaa mwaka,
    Kwa muda mfupi, aliwatilika,
    Ningefanya lipi, ela kumzika?

    Chema wangu babu, kibwana Bashee,
    Alojipa tabu, kwamba anilee, Na yakwe sababu, ni nitengenee,
    Ilahi wahhabu, mara amtwee.

    Chema wangu poni, kipenzi nyanyangu,
    Hadi siku hini, Yu moyoni mwangu,
    Yu moyoni ndani, hadi kufa kwangu,
    Ningamtamani, hatarudi kwangu.

    (a) Eleza dhamira ya mwandishi
    (b) Fafanua umbo la shairi hili
    (c) Andika ubeti wa kwanza kwa lugha ya nathari
    (d) Taja na kutoa mfano mmoja wa tamathali yoyote ya lugha inayojitokeza katika shairi
    (e) Taja mbinu nne za uhuru wa mshairi huku ukitolea kila mbinu mfano

    (f) Eleza maana ya maneno yafuatayo kulingana na vile yalivyotumika:-
    (i) Nitengenee
    (ii) Ningamtamani
    (iii) Ikitimu

    Date posted: October 9, 2019 .    Answers (1)