Watoto hao wanachuma machungwa
Nondo za madirisha hutengenezwa kwa chuma
Mimi ninafanya kazi ili kuchuma pesa
Kavungya answered the question on October 11, 2019 at 07:32
-
Eleza dhana ya kishazi tegemezi.
(Solved)
Eleza dhana ya kishazi tegemezi.
Date posted:
October 11, 2019
.
Answers (1)
-
Tambua kiima, shamirisho, chagizo na kiarifa katika sentensi ifuatayo
Nyanya alimjengea mjukuu nyumba kwa matofali mwaka jana.
(Solved)
Tambua kiima, shamirisho, chagizo na kiarifa katika sentensi ifuatayo
Nyanya alimjengea mjukuu nyumba kwa matofali mwaka jana.
Date posted:
October 11, 2019
.
Answers (1)
-
Tunga sentensi ukitumia vihusishi vya:
a) Kulinganisha
b)Sababu
c)Wakati
(Solved)
Tunga sentensi ukitumia vihusishi vya:
a) Kulinganisha
b)Sababu
c)Wakati
Date posted:
October 11, 2019
.
Answers (1)
-
Tofautisha sentensi zifuatazo.
i) Ningekuwa na pesa ningenunua simu nzuri
ii)Ningalikuwa na pesa ningalinunua simu nzuri
(Solved)
Tofautisha sentensi zifuatazo.
i) Ningekuwa na pesa ningenunua simu nzuri
ii)Ningalikuwa na pesa ningalinunua simu nzuri
Date posted:
October 11, 2019
.
Answers (1)
-
Changanua sentensi ifuatayo kwa njia ya mistari
Wanafunzi wenye bidii hufuzu mtihani
(Solved)
Changanua sentensi ifuatayo kwa njia ya mistari
Wanafunzi wenye bidii hufuzu mtihani
Date posted:
October 11, 2019
.
Answers (1)
-
Ainisha mofimu katika neno lifuatalo
Sikumkaribisha
(Solved)
Ainisha mofimu katika neno lifuatalo
Sikumkaribisha
Date posted:
October 11, 2019
.
Answers (1)
-
Maneno haya yamo katika ngeli gani?
Tayo
Kipepeo
(Solved)
Maneno haya yamo katika ngeli gani?
Tayo
Kipepeo
Date posted:
October 11, 2019
.
Answers (1)
-
Tofautisha sauti zifuatazo.
/a/
/u/
(Solved)
Tofautisha sauti zifuatazo.
/a/
/u/
Date posted:
October 11, 2019
.
Answers (1)
-
(vigelegele vya harusi vililia alilili ; x3)
Kuumeni : (waliimba) Tumeupata mpilipili na maua yake chikicha x2
Kukeni : (wimbo wao kwa sauti tofauti) Tausi waendaa x2
Tausi...
(Solved)
Soma kifungu kifuatacho kisha ujibu maswali yafuatayo :
(vigelegele vya harusi vililia alilili ; x3)
Kuumeni : (waliimba) Tumeupata mpilipili na maua yake chikicha x2
Kukeni : (wimbo wao kwa sauti tofauti) Tausi waendaa x2
Tausi waenda wamuacha mama kwenye banda.
Kuumeni : (wakijibu wimbo) Mwacheni aendee x2
Mwacheni aende akaone mambo ya nyumba.
Kukeni : Mama ataota nini x2.
Ataota nini, hana mtu wa kumletea kuni.
Kuumeni : Ataota moto wa magunzi, wa magunzi wa magunzi. Twamchukua, kisura wetu,
kisura wetu, kisura wetu.
Tausi ni wetu sasa, ni kito chema, ni kito chema ni kito chema.
(i) Wimbo huu ni wa aina gani, na unastahili katika hafla gani ?
(ii) Bainisha wahusika Kuumeni na Kukeni
(iii) Fafanua ujumbe uliojikita katika utungo huu
(iv) Wimbo huu una umuhimu gani hafla ulioimbiwa?
(v) Tambua mtindo uliotumika katika utungo huu
Date posted:
October 11, 2019
.
Answers (1)
-
Onyesha tofauti kati ya vikundi hivi:
(i) Hekaya
Hurafa
(ii) Visakale
Visasili
(iii) Ngano za mtanziko
Ngano za mazimwi
(Solved)
Onyesha tofauti kati ya vikundi hivi:
(i) Hekaya
Hurafa
(ii) Visakale
Visasili
(iii) Ngano za mtanziko
Ngano za mazimwi
Date posted:
October 11, 2019
.
Answers (1)
-
Elezea mbinu nne za kutongolea hadithi
(Solved)
Elezea mbinu nne za kutongolea hadithi
Date posted:
October 11, 2019
.
Answers (1)
-
Ni nini maana ya Tendi?
(Solved)
Ni nini maana ya Tendi?
Date posted:
October 11, 2019
.
Answers (1)
-
MUITALIA ANAZWE
Saa kumi alfajiri
Sote tuliamshwa
Safari tuliianza
Wengi wanauliza
Mwitalia alikuja lini? Na...
(Solved)
Soma wimbo/shairi lifuatalo kisha ujibu maswali yanayofuata
MUITALIA ANAZWE
Saa kumi alfajiri
Sote tuliamshwa
Safari tuliianza
Lazima tuimalize
Maji ukiyavulia nguo
Lazima uyaoge
Wazee kwa vijana waliimba
Muitalia lazima anazwe
Mashamba yao walilia
Uui! Jikaze wavulana
Hawataki rangi hii
Wengi wanauliza
Mwitalia alikuja lini? Na ataondoka lini?
Mnaze huyu mlowezi
Hatuchoki
Hatuchoki
Lazima yeye anazwe
Vifaranga na mbuzi
Mbavu zao zahesabika
Meee! Sauti zilihinikiza kote
Haya yote hakika, ni madhila ya Muitalia
Nguvu kweli tunayo
Simama mbele tunayo
Simama mbele uone !
Muitalia ondoka !
Au nikuondoe kwa nguvu
(a) Taja madhila yaliyosababishwa na Muitalia katika makala haya.
(b) Thibitisha kuwa utungo huu ni wimbo.
(c) Eleza maana inayojitokeza katika mistari ifuatayo:-
(i) Mbavu zao zahesabika.
(ii) Haya yote hakika, ni madhila ya Muitalia.
(d) Huu ni wimbo wa aina gani? Eleza ukitoa ushahidi
(e) Eleza kwa sentensi mbili au tatu shughuli muhimu za kiuchumi za watu wanaimba wimbo huu
(f) Taja mbinu za lugha zilizotumiwa katika wimbo huu. Toa ushahidi
(g) Taja mafunzo mawili yanayotokana na wimbo huu
Date posted:
October 11, 2019
.
Answers (1)
-
Jadili kwa kina matatizo ambayo huenda yakakabili fasihi simulizi katika jamii ya kesho kisha utoe mapendekezo ya jinsi ya kukabiliana na hali hii
(Solved)
Jadili kwa kina matatizo ambayo huenda yakakabili fasihi simulizi katika jamii ya kesho kisha utoe mapendekezo ya jinsi ya kukabiliana na hali hii
Date posted:
October 11, 2019
.
Answers (1)
-
Bainisha tamathali za usemi zilizotumika katika methali zifuatazo:-
(i) Ujana ni moshi ukienda haurudi
(ii) Usipoziba ufaa utajenga ukuta
(Solved)
Bainisha tamathali za usemi zilizotumika katika methali zifuatazo:-
(i) Ujana ni moshi ukienda haurudi
(ii) Usipoziba ufaa utajenga ukuta
Date posted:
October 11, 2019
.
Answers (1)
-
Wawe na kimai ni nini katika fasihi simulizi? Eleza faida zake
(Solved)
Wawe na kimai ni nini katika fasihi simulizi? Eleza faida zake
Date posted:
October 9, 2019
.
Answers (1)
-
Hapo zamani za kale, Mungu alituma wajumbe wawili waende duniani. Wajumbe hawa ni Kinyonga na Mjusi. Kwanza...
(Solved)
Hapo zamani za kale, Mungu alituma wajumbe wawili waende duniani. Wajumbe hawa ni Kinyonga na Mjusi. Kwanza alimtuma Kinyonga na kumwagiza akaseme “wanadamu hamtakufa.” Kinyonga alienda kwa mwendo wa kuduwaa, akasimama hapa na pale akila matunda ya miti. Kwa sababu ya hali hii alichelewa sana kufikisha ujumbe kwa binadamu.
Baada ya muda kupita, Mungu alimtuma Mjusi na ujumbe akaseme, “Mwanadamu sharti kufa.” Mjusi aliunyanyua mkia akafyatuka pu! Mbio akawahi duniani kabla ya kinyonga kuwasili. Kwa haraka alitangaza agizo kuu, “Wanadamu sharti kufa!” Akarejelea haraka kwa Mungu. Baada ya muda kinyonga naye akafika duniana na kutangaza, “Wanadamu hamtakufa!” Wanadamu wakapinga mara na kusema, “La! Tumeshapata ujumbe wa Mjusi, wanadamu sharti kufa! Hatuwezi kupokea tena neno lako! Basi kulingana na neno la mjusi, wanadamu hufa.
(a) (i) Hadithi hii huitwaje?
(ii) Toa sababu zako
(b) Eleza sifa tatu zinazohusishwa na ngano za fasihi simulizi katika hadithi hii
(c) Kinyonga ni mhusika wa aina gani?
(d) Hadithi hii ina umuhimu gani?
(e) Taja njia zozote nne za kukusanya kazi za fasihi simulizi
(f) Tambulisha vipera hivi:-
(i) Kula hepi
(ii) Sema yako ni ya kuazima
(iii) Baba wa Taifa
Date posted:
October 9, 2019
.
Answers (1)
-
Lala mtoto lala x2
Mama atakuja lala
Alienda sokoni lala
Aje na ndizi lala
Ndizi ya mtoto lala
Na maziwa ya mtoto lala
Andazi lako akirudi
Pia nyama ya kifupa
Kifupa, kwangu, wewe...
(Solved)
Lala mtoto lala x2
Mama atakuja lala
Alienda sokoni lala
Aje na ndizi lala
Ndizi ya mtoto lala
Na maziwa ya mtoto lala
Andazi lako akirudi
Pia nyama ya kifupa
Kifupa, kwangu, wewe kinofu
Kipenzi mwana lala x2
Titi laja x2
Basi kipenzi lala
Baba atakuja lala
Aje na mkate lala
Mkate wa mtoto lala
Tanona ja ndovu lala
(a) Huku ukithibitisha jibu lako eleza huu ni wimbo wa aina gani?
(b) Eleza sifa za wimbo wa aina hii
(c) Onyesha umuhimu wa wimbo huu
(d) Eleza amali kuhusu jamii zinazojitokeza katika wimbo huu
(e) Tambua mbinu zozote mbili za utunzi zilizotumika katika wimbo huu
(f) Taja vitendo viwili vinavyoambatana na uimbaji wa aina hii ya wimbo
(g) Wimbo huu una wahusika wangapi? Wataje
Date posted:
October 9, 2019
.
Answers (1)
-
1. Ni sumu, sumu hatari
Unahatarisha watoto
Kwa ndoto zako zako leweshi
Za kupanda ngazi
Ndoto motomoto ambazo
Zimejenga ukuta
Baina ya watoto
Na maneno laini
Ya ulimi wa wazazi
2. Ni sumu, sumu...
(Solved)
1. Ni sumu, sumu hatari
Unahatarisha watoto
Kwa ndoto zako zako leweshi
Za kupanda ngazi
Ndoto motomoto ambazo
Zimejenga ukuta
Baina ya watoto
Na maneno laini
Ya ulimi wa wazazi
2. Ni sumu, sumu hasiri
Unahasiri watoto
Kwa pupa yako hangaishi
Ya kuwa tajiri mtajika
Pupa pumbazi ambayo
Imezaa jangwa bahili
Badala ya chemichemi
Ya mazungumzo na maadili
Baina ya watoto na mzazi
3. Ni sumu, sumu legezi
Unalegeza watoto
Kwa mazoea yako tenganishi
Ya daima kunywa ‘moja baridi’
Mazoea mabaya ambayo yanafunga katika klabu
Hadi saa nane usiku
Huku yakijenga kutofahamiana
Baina ya watoto na mzazi
4. Ni sumu, sumu jeruhi
Unajeruhi watoto kwa pesa,
Kwa mapenzi yako hatari
Ya kuwaliwaza watoto kwa pesa
Zinawafikisha kwenye sigara na ulevi
Na kisha kwenye madawa ya giza baridi
Barabara inayofikisha kwenye giza baridi la kaburi la asubuhi
(a) Pendekeza kichwa kwa shairi hili
(b) Fafanua maudhui ya shairi hili
(c) Ni kwa njia gani kinachozungumziwa kinajenga ukuta?
(d) Dondoa tamathali mbili za usemi zilizotumika katika shairi na uzitolee mfano
(e) Eleza umbo la shairi hili
(f) Uandike ubeti wa nne kwa lugha nathari
(g) Eleza maana ya vifungu hivi vilivyotumika katika shairi ;
(i) Giza baridi
(ii) Yanakufunga katika klabu
Date posted:
October 9, 2019
.
Answers (1)
-
CHEMA HAKIDUMU
Chema hakidumu, kingapendekeza,
Saa ikitimu, kitakuteleza,
Ukawa na hamu, kukingojeleza,
Huwa ni vigumu,
(Solved)
CHEMA HAKIDUMU
Chema hakidumu, kingapendekeza,
Saa ikitimu, kitakuteleza,
Ukawa na hamu, kukingojeleza,
Huwa ni vigumu, kamwe hutaweza.
Chema sikiimbi, kwamba nakitweza,
Japo mara tumbi, kinshaniliza,
Na japo siombi, kipate n’ongeza,
Mtu haniambi, pa kujilimbikiza.
Chema mara ngapi, kinaniondoka,
Mwahanga yu wapi? Hakukaa mwaka,
Kwa muda mfupi, aliwatilika,
Ningefanya lipi, ela kumzika?
Chema wangu babu, kibwana Bashee,
Alojipa tabu, kwamba anilee, Na yakwe sababu, ni nitengenee,
Ilahi wahhabu, mara amtwee.
Chema wangu poni, kipenzi nyanyangu,
Hadi siku hini, Yu moyoni mwangu,
Yu moyoni ndani, hadi kufa kwangu,
Ningamtamani, hatarudi kwangu.
(a) Eleza dhamira ya mwandishi
(b) Fafanua umbo la shairi hili
(c) Andika ubeti wa kwanza kwa lugha ya nathari
(d) Taja na kutoa mfano mmoja wa tamathali yoyote ya lugha inayojitokeza katika shairi
(e) Taja mbinu nne za uhuru wa mshairi huku ukitolea kila mbinu mfano
(f) Eleza maana ya maneno yafuatayo kulingana na vile yalivyotumika:-
(i) Nitengenee
(ii) Ningamtamani
(iii) Ikitimu
Date posted:
October 9, 2019
.
Answers (1)