a) 1. Ponografia imekuwepo tangu jadi.
2. Tatizo sugu duniani sasa
3. Imeenezwa na vyombo vya teknolojia ya habari na mawasiliano
4. Chanzo hakijulikani
5. Huundwa na makundi mbalimbali ya watu wa nia tofauti
b)1.Ponografia huharibu akili
2. Hufanya vijana kuingilia ngono mapema
3. Utendaji mbaya shuleni
4.Huchangia ukahaba
5.Mahudhurio mabaya darasani
6.Mimba zisizotarajiwa
7.Kuacha shule
8.Mauti
9.Kuandama ushoga, ubasha na usagaji
Magonjwa ya zinaa
10.Kuiga lugha, ishara na miondoko ya kingono
11.Ubakaji
12.Kushiriki ulevi, dawa za kulevya, pombe, sigara na kutumia dawa za kuchochea uchu wa ngono
13. Hufanya nishai na hisi kuwa butu
14. Hupoteza mhemko wa kawaida
15. Hufanya mtu kuwa mtegemezi wa ponografia
16. Kujichua
Kavungya answered the question on October 12, 2019 at 09:45
-
Kwa kipindi cha miezi kadha iliyopita tumeshuhudia vyombo vya dola vikitia makali yake kwenye upekuzi na hata kupiga...
(Solved)
Soma taarifa ifuatayo kisha ujibu maswali yanayofuata.
Kwa kipindi cha miezi kadha iliyopita tumeshuhudia vyombo vya dola vikitia makali yake kwenye upekuzi na hata kupiga doria usiku na mchana katika jitihada za kulinda nchi.
Mpango huu ni kweli umeonekana kufanya kazi hivi kwamba hata magaidi wenyewe wameshindwa kupenya katika miji na sasa kuhiari kijinga kushambulia magari ya abiria, kitendo ambacho ni cha kuonyesha uwoga. Kwa hatua hiyo, navipa vyombo vya dola kongole. Jambo ambalo lafaa kujulikana ni kwamba mikakati ya kulinda nchi haifai kuwa ni ya wakati mmoja tu, mbali inafaa kuwa ni zoezi la kila siku.
Magaidi nao huwa macho huku yakijua bayana kwamba wakati wa kulala kwa walinzi unapokuwepo, basi wanapata nafasi ya kututupia ‘viazi’ ukipenda grunedi.
Kama ilivyo kawaida katika mataifa mengi barani Afrika, ni bayana kwamba bado kungali na mianya mingi ambayo magaidi wa kimataifa huendelea kutumia. Dosari bado zipo. Kwa mfano, mipaka mingi ya nchi hizi huwa kama lango kuu la ugaidi wa kimataifa, kwani kuenea kwa saratani ya ufisadi halimo tu maofisini mbali pia kwenye mipaka yetu.
Kama kupata kitambulisho, pasipoti na stakabadhi zingine za kusafiri nchini Kenya ashakum si matusi ziligeuzwa ‘maandazi’ ya Kariakoo basi niambie ni nani hawezi kuingia na kutoka nchini bila usumbufu wowote ule bora tu anayehitaji ana hela mkononi? Kwa kuikubali hongo kuwa ufunguo wa kila kitu, Wakenya wenzangu hapo naona ni kama tumejiweka kwenye kikaango kilicho juu ya moto mkali. Hapa hakuna aliye na bahati, tajiri kwa masikini wamo kwenye mtego huu hatari.
Kwa mtindo ambao tunafuata wa kutoa ajira katika idara mbalimbali za ulinzi, inabidi serikali iwe na uangalifu sana hasa kwenye suala nzima la kuhakikisha stakabadhi wanazohitaji si ghushi.
Pasina kufanya hivyo hapo tena tunaweza kuwapata maadui wanaopenya na kujifanya walinzi wetu kumbe ni majasusi wa magaidi. Kila Mkenya anafaa kujihisi kulindwa. Miji, vijiji na hata vitongoji vinafaa kuwa na usalama wa kutosha, kwani kila Mkenya ni mlipa ushuru na hatufai kuona labda tabaka la juu likipendelewa huku mitaa ya mabanda ikiachiwa mbwa koko kama walinzi wao.
Suala lingine muhimu ni kuangaziwa upya usalama kwenye magari ya usafiri.
Juzi tulishuhudia mabasi mawili yakilipuliwa kwenye barabara ya Thika huku tukijua fika kwamba, mpango wa walinda nchi ungalipo.
La kusikitisha ni kuona kwamba, madereva na utingo wao walikamatwa na kufunguliwa mashtaka kwa kutozuia shambulizo hilo. Je, hii ni sheria gani? Dereva ataendesha gari au atachukua jukumu la walinda usalama?
Waswahili walinena kwamba ukubwa ni jaa na kwa hivyo Rais wa taifa ndiye anayefaa kubeba mzigo mzima wa usalama wetu bila kubananga wasaa. Wengine ambao wanafaa kuwajibika ni wakuu wote wa idara mbalimbali za usalama.
Usalama wako na wangu ni muhimu, elewa bayana kwamba bila usalama watalii hawawezi kuja kututembelea. Bila ya usalama maendeleo ya taifa kamwe hayawezi kupatikana, ndiposa kila jitihada sharti zifanywe ili wote waweze kuendelea kuyafurahia matunda ya uhuru wetu.
Ada ya mja kunena muungwana ni vitendo, hatufai tu kuimba wimbo wa ‘linda nchi’ ilhali mabasi barabarani hayana usalama. Hebu na tuuone ulinzi endelevu na hapo tutawakomoa magaidi kwa yakini.
Maswali
1.Ipe taarifa hii anwani mwafaka.
2.Kwa nini magaidi wanashambulia magari ya abiria?
3.Kulingana na taarifa pamoja na maoni yako, eleza njia tatu ambazo zinatumiwa na magaidi ili kufanikisha utekelezaji wa unyama wao.
4.Ni njia gani ambazo magaidi hutumia kuingia katika nchi wanapoazimia kutekeleza uhalifu?
5.Kwa nini suala la usalama kwenye magari ya usafiri muhimu?
6.Ni njia zipi zinazoweza kutumiwa kupunguza mashambulizi ya kigaidi kulingana na mwandishi?
7.Eleza athari za utovu wa usalama.
8.Eleza neno au mafungu ya maneno kama yalivyotumiwa katika kifungu.
a)Vyombo vya dola
b)Jaa
Date posted:
October 12, 2019
.
Answers (1)
-
Eleza njia tatu za kupunguza tofauti za kilahaja
(Solved)
Eleza njia tatu za kupunguza tofauti za kilahaja
Date posted:
October 11, 2019
.
Answers (1)
-
Tunga sentensi kuonyesha maana mbili za neno chuma
(Solved)
Tunga sentensi kuonyesha maana mbili za neno chuma
Date posted:
October 11, 2019
.
Answers (1)
-
Eleza dhana ya kishazi tegemezi.
(Solved)
Eleza dhana ya kishazi tegemezi.
Date posted:
October 11, 2019
.
Answers (1)
-
Tambua kiima, shamirisho, chagizo na kiarifa katika sentensi ifuatayo
Nyanya alimjengea mjukuu nyumba kwa matofali mwaka jana.
(Solved)
Tambua kiima, shamirisho, chagizo na kiarifa katika sentensi ifuatayo
Nyanya alimjengea mjukuu nyumba kwa matofali mwaka jana.
Date posted:
October 11, 2019
.
Answers (1)
-
Tunga sentensi ukitumia vihusishi vya:
a) Kulinganisha
b)Sababu
c)Wakati
(Solved)
Tunga sentensi ukitumia vihusishi vya:
a) Kulinganisha
b)Sababu
c)Wakati
Date posted:
October 11, 2019
.
Answers (1)
-
Tofautisha sentensi zifuatazo.
i) Ningekuwa na pesa ningenunua simu nzuri
ii)Ningalikuwa na pesa ningalinunua simu nzuri
(Solved)
Tofautisha sentensi zifuatazo.
i) Ningekuwa na pesa ningenunua simu nzuri
ii)Ningalikuwa na pesa ningalinunua simu nzuri
Date posted:
October 11, 2019
.
Answers (1)
-
Changanua sentensi ifuatayo kwa njia ya mistari
Wanafunzi wenye bidii hufuzu mtihani
(Solved)
Changanua sentensi ifuatayo kwa njia ya mistari
Wanafunzi wenye bidii hufuzu mtihani
Date posted:
October 11, 2019
.
Answers (1)
-
Ainisha mofimu katika neno lifuatalo
Sikumkaribisha
(Solved)
Ainisha mofimu katika neno lifuatalo
Sikumkaribisha
Date posted:
October 11, 2019
.
Answers (1)
-
Maneno haya yamo katika ngeli gani?
Tayo
Kipepeo
(Solved)
Maneno haya yamo katika ngeli gani?
Tayo
Kipepeo
Date posted:
October 11, 2019
.
Answers (1)
-
Tofautisha sauti zifuatazo.
/a/
/u/
(Solved)
Tofautisha sauti zifuatazo.
/a/
/u/
Date posted:
October 11, 2019
.
Answers (1)
-
(vigelegele vya harusi vililia alilili ; x3)
Kuumeni : (waliimba) Tumeupata mpilipili na maua yake chikicha x2
Kukeni : (wimbo wao kwa sauti tofauti) Tausi waendaa x2
Tausi...
(Solved)
Soma kifungu kifuatacho kisha ujibu maswali yafuatayo :
(vigelegele vya harusi vililia alilili ; x3)
Kuumeni : (waliimba) Tumeupata mpilipili na maua yake chikicha x2
Kukeni : (wimbo wao kwa sauti tofauti) Tausi waendaa x2
Tausi waenda wamuacha mama kwenye banda.
Kuumeni : (wakijibu wimbo) Mwacheni aendee x2
Mwacheni aende akaone mambo ya nyumba.
Kukeni : Mama ataota nini x2.
Ataota nini, hana mtu wa kumletea kuni.
Kuumeni : Ataota moto wa magunzi, wa magunzi wa magunzi. Twamchukua, kisura wetu,
kisura wetu, kisura wetu.
Tausi ni wetu sasa, ni kito chema, ni kito chema ni kito chema.
(i) Wimbo huu ni wa aina gani, na unastahili katika hafla gani ?
(ii) Bainisha wahusika Kuumeni na Kukeni
(iii) Fafanua ujumbe uliojikita katika utungo huu
(iv) Wimbo huu una umuhimu gani hafla ulioimbiwa?
(v) Tambua mtindo uliotumika katika utungo huu
Date posted:
October 11, 2019
.
Answers (1)
-
Onyesha tofauti kati ya vikundi hivi:
(i) Hekaya
Hurafa
(ii) Visakale
Visasili
(iii) Ngano za mtanziko
Ngano za mazimwi
(Solved)
Onyesha tofauti kati ya vikundi hivi:
(i) Hekaya
Hurafa
(ii) Visakale
Visasili
(iii) Ngano za mtanziko
Ngano za mazimwi
Date posted:
October 11, 2019
.
Answers (1)
-
Elezea mbinu nne za kutongolea hadithi
(Solved)
Elezea mbinu nne za kutongolea hadithi
Date posted:
October 11, 2019
.
Answers (1)
-
Ni nini maana ya Tendi?
(Solved)
Ni nini maana ya Tendi?
Date posted:
October 11, 2019
.
Answers (1)
-
MUITALIA ANAZWE
Saa kumi alfajiri
Sote tuliamshwa
Safari tuliianza
Wengi wanauliza
Mwitalia alikuja lini? Na...
(Solved)
Soma wimbo/shairi lifuatalo kisha ujibu maswali yanayofuata
MUITALIA ANAZWE
Saa kumi alfajiri
Sote tuliamshwa
Safari tuliianza
Lazima tuimalize
Maji ukiyavulia nguo
Lazima uyaoge
Wazee kwa vijana waliimba
Muitalia lazima anazwe
Mashamba yao walilia
Uui! Jikaze wavulana
Hawataki rangi hii
Wengi wanauliza
Mwitalia alikuja lini? Na ataondoka lini?
Mnaze huyu mlowezi
Hatuchoki
Hatuchoki
Lazima yeye anazwe
Vifaranga na mbuzi
Mbavu zao zahesabika
Meee! Sauti zilihinikiza kote
Haya yote hakika, ni madhila ya Muitalia
Nguvu kweli tunayo
Simama mbele tunayo
Simama mbele uone !
Muitalia ondoka !
Au nikuondoe kwa nguvu
(a) Taja madhila yaliyosababishwa na Muitalia katika makala haya.
(b) Thibitisha kuwa utungo huu ni wimbo.
(c) Eleza maana inayojitokeza katika mistari ifuatayo:-
(i) Mbavu zao zahesabika.
(ii) Haya yote hakika, ni madhila ya Muitalia.
(d) Huu ni wimbo wa aina gani? Eleza ukitoa ushahidi
(e) Eleza kwa sentensi mbili au tatu shughuli muhimu za kiuchumi za watu wanaimba wimbo huu
(f) Taja mbinu za lugha zilizotumiwa katika wimbo huu. Toa ushahidi
(g) Taja mafunzo mawili yanayotokana na wimbo huu
Date posted:
October 11, 2019
.
Answers (1)
-
Jadili kwa kina matatizo ambayo huenda yakakabili fasihi simulizi katika jamii ya kesho kisha utoe mapendekezo ya jinsi ya kukabiliana na hali hii
(Solved)
Jadili kwa kina matatizo ambayo huenda yakakabili fasihi simulizi katika jamii ya kesho kisha utoe mapendekezo ya jinsi ya kukabiliana na hali hii
Date posted:
October 11, 2019
.
Answers (1)
-
Bainisha tamathali za usemi zilizotumika katika methali zifuatazo:-
(i) Ujana ni moshi ukienda haurudi
(ii) Usipoziba ufaa utajenga ukuta
(Solved)
Bainisha tamathali za usemi zilizotumika katika methali zifuatazo:-
(i) Ujana ni moshi ukienda haurudi
(ii) Usipoziba ufaa utajenga ukuta
Date posted:
October 11, 2019
.
Answers (1)
-
Wawe na kimai ni nini katika fasihi simulizi? Eleza faida zake
(Solved)
Wawe na kimai ni nini katika fasihi simulizi? Eleza faida zake
Date posted:
October 9, 2019
.
Answers (1)
-
Hapo zamani za kale, Mungu alituma wajumbe wawili waende duniani. Wajumbe hawa ni Kinyonga na Mjusi. Kwanza...
(Solved)
Hapo zamani za kale, Mungu alituma wajumbe wawili waende duniani. Wajumbe hawa ni Kinyonga na Mjusi. Kwanza alimtuma Kinyonga na kumwagiza akaseme “wanadamu hamtakufa.” Kinyonga alienda kwa mwendo wa kuduwaa, akasimama hapa na pale akila matunda ya miti. Kwa sababu ya hali hii alichelewa sana kufikisha ujumbe kwa binadamu.
Baada ya muda kupita, Mungu alimtuma Mjusi na ujumbe akaseme, “Mwanadamu sharti kufa.” Mjusi aliunyanyua mkia akafyatuka pu! Mbio akawahi duniani kabla ya kinyonga kuwasili. Kwa haraka alitangaza agizo kuu, “Wanadamu sharti kufa!” Akarejelea haraka kwa Mungu. Baada ya muda kinyonga naye akafika duniana na kutangaza, “Wanadamu hamtakufa!” Wanadamu wakapinga mara na kusema, “La! Tumeshapata ujumbe wa Mjusi, wanadamu sharti kufa! Hatuwezi kupokea tena neno lako! Basi kulingana na neno la mjusi, wanadamu hufa.
(a) (i) Hadithi hii huitwaje?
(ii) Toa sababu zako
(b) Eleza sifa tatu zinazohusishwa na ngano za fasihi simulizi katika hadithi hii
(c) Kinyonga ni mhusika wa aina gani?
(d) Hadithi hii ina umuhimu gani?
(e) Taja njia zozote nne za kukusanya kazi za fasihi simulizi
(f) Tambulisha vipera hivi:-
(i) Kula hepi
(ii) Sema yako ni ya kuazima
(iii) Baba wa Taifa
Date posted:
October 9, 2019
.
Answers (1)