Get premium membership and access questions with answers, video lessons as well as revision papers.

Andika sifa bainifu za /d/ na /f/.

      

Andika sifa bainifu za /d/ na /f/.

  

Answers


Kavungya
/d/ - kipasuo cha ufizi; sauti ghuna
/f/ - kikwamizo cha mdomo na meno; sighuna
Kavungya answered the question on October 12, 2019 at 09:47


Next: Ponografia ni tendo, maandishi, picha au mchoro unaoonyesha au kueleza uchi wa mtu au vitendo vya ngono kwa ajili...
Previous: Andika kinyume cha sentensi hii. Mama alianika nguo zilizofuliwa na Kitwana.

View More Kiswahili Questions and Answers | Return to Questions Index


Learn High School English on YouTube

Related Questions


  • Ponografia ni tendo, maandishi, picha au mchoro unaoonyesha au kueleza uchi wa mtu au vitendo vya ngono kwa ajili...(Solved)

    Soma taarifa ifuatayo kisha ujibu maswali

    Ponografia ni tendo, maandishi, picha au mchoro unaoonyesha au kueleza uchi wa mtu au vitendo vya ngono kwa ajili ya kuchochea ashiki ya kuifanya. Mambo haya machafu huwasilishwa ana kwa ana kupitia sinema, video, magazeti, vitabu, muziki, televisheni. DVD, n.k.

    Ponorafia imekuwepo tangu jadi, hasa katika nchi za magharibi. Lakini sasa limekuwa tatizo sugu. Hii ni kwa sababu imeenea ulimwenguni kote mithili ya moto katika mbuga wakati wa kiangazi. Uenezi umechangiwa na mambo kadha wa kadha. Mchango mkubwa zaidi umetokana na kuimarika kwa vyombo vya teknolojia ya habari na mawasiliano. Matumizi ya tarakilishi, mdahilishi na viungambali vya picha yamesambaza ponografia ilivyoanza. Hata hivyo, hubuniwa au kutengenezwa na makundi mbali mbali ya watu. Miongoni mwa hawa ni watu wasiojali maadili. Pili, kuna wale wenye matatizo ya kisaikolojia na kijamii. Wao hutengeneza na kueneza uchafu huu kwa lengo la ama kuvuruga maadili katika jamii au kuchukiza wanajamii waadilifu. Kundi lingine ni lile la wanaoichukulia ponografia kama nyenzo ya kutosheleza ashiki zao. Hivi sasa, kundi kubwa ni lile la wanotumia matusi haya kama njia ya kuchuma. Kwa mfano, wanamziki ambao hutumia ponografia kuvutia wateja na hivyo kuzidisha mauzo yao.

    Kushamiri kwa wimbi na uonyeshaji ponografia kuna athari kubwa kwa jamii na hasa watoto. Ingawa watu wengine hudai picha hizi haziwaathiri, upo ushahidi kuonyesha kuwa wanaotazama picha za ngono hupata matatizo. Lazima ieleweke kuwa kinachoonekana na jicho au kusikika kwa sikio huathiri fikira au hisia. Picha za matusi zinachangia kwa kiasi kikubwa kuharibu akili. Badala ya kuzingatia mambo muhimu kama masomo watu huanza kutafakari mambo machafu.

    Vijana wengi ni kama bendera. Hivyo basi huanza kuiga wanayoyaona na kusikia. Hili ni tatizo linalowafanya kuacha mkondo wa maadili. Kutokana na uchafu huu, watu wengi hushawishiwa kuingilia shughuli za ngono mapema kabla hawajakomaa kimwili, kiakili na kihisia. Matokeo yake ni mengi. Haya ni pamoja na ukahaba, utendaji mbaya shuleni, mahudhurio mabaya darasani na mimba zisizotarajiwa. Vijana wengi huacha shule kabisa. Wengine nao huambukizwa magonjwa ya zinaa ambayo huwaletea mauti.

    Inasemekana kuwa akili za binadamu hunata zaidi mambo yanayowasilishwa kwa picha. Si ajabu vijana huyadumisha matusi haya katika kumbukumbu zao na kuyasanya sehemu ya maisha yao. Wengi huanza kuandama tabia mbovu kama ushoga, ubasha na usagaji. Kuna wale ambao huanza kujichua. Kujichua ni hali ya mwanamke au mwanaume kumaliza haja za kimaumbile bila kufanya mapenzi na mtu mwingine. Ponografia imechangia pakubwa kuenea kwa haya.

    Jambo hili limegeuza mielekeo ya vijana. Wanaiga mitindo mibaya ya mavazi yanayoanika uchi wao. Hali kadhalika, huiga lugha, ishara na miondoko inayohusiana na ngono. Yote haya yanapingana na desturi za Mwafrika. Si ajabu visa vya ubakaji vinaongezeka kila kukuchapo.

    Utazamaji wa picha chafu aghalabu huandamana na maovu mengine kama unywaji pombe, matumizi ya dawa za kulevya, uvutaji sigara na utumiaji wa dawa za kuchochea uchu wa ngono. Mambo haya huwapa vijana kutazama tabia za unyama.

    Jambo hatari ni kuwa kuendelea kutazama picha hizi huzifanya nishai na hisia za watu kuwa butu, yaani huondoa makali. Hata katika utu uzima, mtu atapoteza mhemko wa kawaida na kugeuzwa kuwa mtegemezi wa ponografia. Tatizo hili linaenea kwa vishindo mijini na vijijini. Ipo haja ya dharura kuikinga jamii kutokana na maenezi haya yasio na kizuizi.

    Jambo la kwanza ni kuongeza ufahamu wa umma wote kuhusu uovu wa picha hizi. Kwa namna hii itawezekana kupunguza mahitaji na uuzaji wa ponografia. Tatizo hili linaenea kwa vishindo mijini na vijijini. Ipo haja ya dharura kuikinga jamii kutokana na maenezi haya yasiyo na kizuizi.

    Tatizo la kuenea kwu ponografia limeendelea kuwepo kwa sababu ya udhaifu wa sheria. Kilichoko basi ni kuweka sheria za kuzuia utengenezaji wa upujufu huu. Kuambatana na haya, hatua kali zichukuliwe kwa wanaovunja sheria hizi. Hali kadhalika, ushirikiano wa karibu baina ya wadau uimarishwe katika ulimwengu mzima. Serikali na wanaohusika wakabiliwe ipasavyo. Jamii ingependa kuona michakato ya kuharamisha utengenezaji, usambazaji na utangazaji wa ponografia ikiwekwa.

    Wazazi nao wasijipweteke tu bali nao wasaidie. Ni muhimu washikilie kwa sharti juhudi zao za kuwaelekeza na kuwashauri watoto kuzingatia uongofu na kukwepa picha hizi najisi. Watoto lazima waeleweshwe kuwa haifai kutazama picha au michoro michafu. Itikadi na imani za kidini na utamaduni wa Kiafrika unakataza vikali mtu kuona uchi wa mtu mwingine. Matokeo ya kuasi makatazo haya yana madhara makubwa kwa watu na jamii.

    Maswali
    a)Fupisha ujumbe wa aya ya pili na ya tatu kwa maneno 20 – 25
    Matayarisho
    Nakala safi
    b)Kwa kutumia maneno 55 – 60, eleza mambo muhimu yanayojitokeza katika aya ya nne hadi ya tisa
    kuhusu athari za ponografia .
    Matayarisho
    Nakala safi

    Date posted: October 12, 2019.  Answers (1)

  • Kwa kipindi cha miezi kadha iliyopita tumeshuhudia vyombo vya dola vikitia makali yake kwenye upekuzi na hata kupiga...(Solved)

    Soma taarifa ifuatayo kisha ujibu maswali yanayofuata.

    Kwa kipindi cha miezi kadha iliyopita tumeshuhudia vyombo vya dola vikitia makali yake kwenye upekuzi na hata kupiga doria usiku na mchana katika jitihada za kulinda nchi.
    Mpango huu ni kweli umeonekana kufanya kazi hivi kwamba hata magaidi wenyewe wameshindwa kupenya katika miji na sasa kuhiari kijinga kushambulia magari ya abiria, kitendo ambacho ni cha kuonyesha uwoga. Kwa hatua hiyo, navipa vyombo vya dola kongole. Jambo ambalo lafaa kujulikana ni kwamba mikakati ya kulinda nchi haifai kuwa ni ya wakati mmoja tu, mbali inafaa kuwa ni zoezi la kila siku.
    Magaidi nao huwa macho huku yakijua bayana kwamba wakati wa kulala kwa walinzi unapokuwepo, basi wanapata nafasi ya kututupia ‘viazi’ ukipenda grunedi.
    Kama ilivyo kawaida katika mataifa mengi barani Afrika, ni bayana kwamba bado kungali na mianya mingi ambayo magaidi wa kimataifa huendelea kutumia. Dosari bado zipo. Kwa mfano, mipaka mingi ya nchi hizi huwa kama lango kuu la ugaidi wa kimataifa, kwani kuenea kwa saratani ya ufisadi halimo tu maofisini mbali pia kwenye mipaka yetu.
    Kama kupata kitambulisho, pasipoti na stakabadhi zingine za kusafiri nchini Kenya ashakum si matusi ziligeuzwa ‘maandazi’ ya Kariakoo basi niambie ni nani hawezi kuingia na kutoka nchini bila usumbufu wowote ule bora tu anayehitaji ana hela mkononi? Kwa kuikubali hongo kuwa ufunguo wa kila kitu, Wakenya wenzangu hapo naona ni kama tumejiweka kwenye kikaango kilicho juu ya moto mkali. Hapa hakuna aliye na bahati, tajiri kwa masikini wamo kwenye mtego huu hatari.
    Kwa mtindo ambao tunafuata wa kutoa ajira katika idara mbalimbali za ulinzi, inabidi serikali iwe na uangalifu sana hasa kwenye suala nzima la kuhakikisha stakabadhi wanazohitaji si ghushi.
    Pasina kufanya hivyo hapo tena tunaweza kuwapata maadui wanaopenya na kujifanya walinzi wetu kumbe ni majasusi wa magaidi. Kila Mkenya anafaa kujihisi kulindwa. Miji, vijiji na hata vitongoji vinafaa kuwa na usalama wa kutosha, kwani kila Mkenya ni mlipa ushuru na hatufai kuona labda tabaka la juu likipendelewa huku mitaa ya mabanda ikiachiwa mbwa koko kama walinzi wao.
    Suala lingine muhimu ni kuangaziwa upya usalama kwenye magari ya usafiri.
    Juzi tulishuhudia mabasi mawili yakilipuliwa kwenye barabara ya Thika huku tukijua fika kwamba, mpango wa walinda nchi ungalipo.
    La kusikitisha ni kuona kwamba, madereva na utingo wao walikamatwa na kufunguliwa mashtaka kwa kutozuia shambulizo hilo. Je, hii ni sheria gani? Dereva ataendesha gari au atachukua jukumu la walinda usalama?
    Waswahili walinena kwamba ukubwa ni jaa na kwa hivyo Rais wa taifa ndiye anayefaa kubeba mzigo mzima wa usalama wetu bila kubananga wasaa. Wengine ambao wanafaa kuwajibika ni wakuu wote wa idara mbalimbali za usalama.
    Usalama wako na wangu ni muhimu, elewa bayana kwamba bila usalama watalii hawawezi kuja kututembelea. Bila ya usalama maendeleo ya taifa kamwe hayawezi kupatikana, ndiposa kila jitihada sharti zifanywe ili wote waweze kuendelea kuyafurahia matunda ya uhuru wetu.
    Ada ya mja kunena muungwana ni vitendo, hatufai tu kuimba wimbo wa ‘linda nchi’ ilhali mabasi barabarani hayana usalama. Hebu na tuuone ulinzi endelevu na hapo tutawakomoa magaidi kwa yakini.

    Maswali
    1.Ipe taarifa hii anwani mwafaka.
    2.Kwa nini magaidi wanashambulia magari ya abiria?
    3.Kulingana na taarifa pamoja na maoni yako, eleza njia tatu ambazo zinatumiwa na magaidi ili kufanikisha utekelezaji wa unyama wao.
    4.Ni njia gani ambazo magaidi hutumia kuingia katika nchi wanapoazimia kutekeleza uhalifu?
    5.Kwa nini suala la usalama kwenye magari ya usafiri muhimu?
    6.Ni njia zipi zinazoweza kutumiwa kupunguza mashambulizi ya kigaidi kulingana na mwandishi?
    7.Eleza athari za utovu wa usalama.
    8.Eleza neno au mafungu ya maneno kama yalivyotumiwa katika kifungu.
    a)Vyombo vya dola
    b)Jaa

    Date posted: October 12, 2019.  Answers (1)

  • Eleza njia tatu za kupunguza tofauti za kilahaja (Solved)

    Eleza njia tatu za kupunguza tofauti za kilahaja

    Date posted: October 11, 2019.  Answers (1)

  • Tunga sentensi kuonyesha maana mbili za neno chuma (Solved)

    Tunga sentensi kuonyesha maana mbili za neno chuma

    Date posted: October 11, 2019.  Answers (1)

  • Eleza dhana ya kishazi tegemezi.(Solved)

    Eleza dhana ya kishazi tegemezi.

    Date posted: October 11, 2019.  Answers (1)

  • Eleza tofauti ya kimaana katika sentensi hizi i)Nisimamapo huchekwa ii)Ninaposimama huchekwa (Solved)

    Eleza tofauti ya kimaana katika sentensi hizi
    i)Nisimamapo huchekwa
    ii)Ninaposimama huchekwa

    Date posted: October 11, 2019.  Answers (1)

  • Tambua kiima, shamirisho, chagizo na kiarifa katika sentensi ifuatayo Nyanya alimjengea mjukuu nyumba kwa matofali mwaka jana. (Solved)

    Tambua kiima, shamirisho, chagizo na kiarifa katika sentensi ifuatayo
    Nyanya alimjengea mjukuu nyumba kwa matofali mwaka jana.

    Date posted: October 11, 2019.  Answers (1)

  • Tunga sentensi ukitumia vihusishi vya: a) Kulinganisha b)Sababu c)Wakati (Solved)

    Tunga sentensi ukitumia vihusishi vya:
    a) Kulinganisha
    b)Sababu
    c)Wakati

    Date posted: October 11, 2019.  Answers (1)

  • Tofautisha sentensi zifuatazo. i) Ningekuwa na pesa ningenunua simu nzuri ii)Ningalikuwa na pesa ningalinunua simu nzuri (Solved)

    Tofautisha sentensi zifuatazo.
    i) Ningekuwa na pesa ningenunua simu nzuri
    ii)Ningalikuwa na pesa ningalinunua simu nzuri

    Date posted: October 11, 2019.  Answers (1)

  • Changanua sentensi ifuatayo kwa njia ya mistari Wanafunzi wenye bidii hufuzu mtihani (Solved)

    Changanua sentensi ifuatayo kwa njia ya mistari
    Wanafunzi wenye bidii hufuzu mtihani

    Date posted: October 11, 2019.  Answers (1)

  • Andika katika usemi wa taarifa “Mtapata mwaliko wenu kesho,” alisema Salim (Solved)

    Andika katika usemi wa taarifa
    “Mtapata mwaliko wenu kesho,” alisema Salim

    Date posted: October 11, 2019.  Answers (1)

  • Ainisha mofimu katika neno lifuatalo Sikumkaribisha (Solved)

    Ainisha mofimu katika neno lifuatalo
    Sikumkaribisha

    Date posted: October 11, 2019.  Answers (1)

  • Maneno haya yamo katika ngeli gani? Tayo Kipepeo (Solved)

    Maneno haya yamo katika ngeli gani?
    Tayo
    Kipepeo

    Date posted: October 11, 2019.  Answers (1)

  • Tofautisha sauti zifuatazo. /a/ /u/ (Solved)

    Tofautisha sauti zifuatazo.
    /a/
    /u/

    Date posted: October 11, 2019.  Answers (1)

  • Soma makala haya kisha ujibu maswali yafuatayo HAKI ZA BINADAMU Binadamu wana mazoea ya kufikiria kuwa jinsi wafanyavyo, waongeavyo na wafikiriavyo kuhusu vitu ndivyo inavyopasa...(Solved)

    Soma makala haya kisha ujibu maswali yafuatayo
    HAKI ZA BINADAMU
    Binadamu wana mazoea ya kufikiria kuwa jinsi wafanyavyo, waongeavyo na wafikiriavyo kuhusu vitu ndivyo inavyopasa kuwa. Kama binandamu tunaamini njia yetu ndiyo sahihi, yenye mantiki na inayopasa kufuatwa na kila mtu. Msingi huu huu unakwenda kinyume na kutambua kila binadamu ana haki ya kufikiri, kusema au kuongea na kutenda mradi asikiuke haki ya mwenzake iliyo sawa na yake. Nguzo mojawapo inayogongomelea hoja hii ni Haki za Binadamu.

    Azimio kutangaza Haki Bia za Binadamu liliafikiwa na Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa tarehe 10 Desemba 1948. Baraza kuu hilo liliyasisitizia mataifa wanachama umuhimu wa kuyasambaza, kuenezea, na kusisitiza kusambazwa kwa azimio hilo katika shule na taasisi za kielimu. Msingi wa uhuru, haki na amani ulimwenguni ni kutambua binadamu wote wana haki sawa. Ingawa kimsingi jamii na mataifa yote ya ulimwengu yanapaswa kuthamini, kusambaza na kuhimiza umuhimu wa Haki za Binadamu zipo jamii ambazo hukiuka haki hizo. Matokeo ya ukiukaji huu yana athari hasi sana kama ilivyotokea nchini Rwanda na Bosnia. Herzegovina kulikotokea mauaji ya halaiki.

    Azimio la Haki za Binadamu linajumuisha vipengele kadha ambavyo ni mihimili mikuu ya Azimio lenyewe. Kipengele msingi kabisa kinasisitiza kuwa kila kiumbe anazaliwa huru na ana haki na hadhi sawa na kiumbe mwingine. Ukweli wa kauli hii ulikokotezwa na kauli ya mwanafalsafa maarufu Jean Jacques Rosseau aliyesema kuwa kila kiumbe huzaliwa huru lakini huwa katika pingu ulimwengu mzima. Kauli hii ilitambua ukiukaji huu wa kipengele hiki. Kipengele cha pili kinasisitiza kuwa binadamu wote wana haki za kufurahia uhuru wao pasi na kutengwa au kubezwa kwa misingi yoyote ile si rangi, kabila, jinsia, lugha, dini, asilia, utajiri au chochote kile.

    Vipengele vingine vinatukumbusha kuwa kila mtu ana haki ya kuishi na kupata ulinzi. Hamna mtu anayepaswa kuishi maisha ya utumwa au unyonge wa kutumikishwa kwa namna yoyote ile. Suala hili linasisitizwa na kipengele cha sita kinachokataza kudhalilishwa kwa watu au kutunzwa kwa namna yoyote ambayo inamfedhehesha kama kiumbe. Azimio la Haki za Binadamu linasisitiza kuwa binadamu yoyote nyule ana haki ya kupata ulinzi wa kisheria. Binadamu huyo hapaswi kubaguliwa na ana haki ya kupata fidia ya kisheria taraa haki zake za kimsingi zikikiukwa.

    Hata hivyo sio watu wote ulimwenguni ambao wanazifurahia haki hizi za kimsingi. Zipo lukuki za jamii ulimwenguni ambako haki za kimsingi zinakiukwa. Katika nchi ambazo zinaongozwa na watawala wa kiimla, si ajabu kuona haki za binadamu zikikiukwa. Viongozi wa aina hiyo huwa wamegeuzwa ng’ombe wa shemere na tamaa, ubinafsi na ukatili usiojua thamani ya utu. Viongozi wa aina hii wanasahau kuwa kila binadamu ana haki ya kuishi maisha huru, asipotumikishwa wala kulanguliwa kama bidhaa.

    Nchi za kiimla aghalabu huongozwa na itikadi kuwa kiongozi ndiye pekee ambaye ana uwezo wa kufikiri, kuamua na kutenda. Watu wengine wanapaswa kumfuata kisilka kama yule mbwa wa Pavlov ambaye alitokwa na mate kila kengele ilipopigwa. Viongozi wa ama hii hawachelei kuwatenza nguvu raia zao: Kuwadhalilisha kwa namna nyingi. Viongozi wa aina hiyo huiona sheria ya nchi kama iliyowekwa kwa watu wengine bali sio wao. Msimamo huu unakwenda kinyume na kipengele cha saba cha Haki Bia za Binadamu kisemacho kuwa watu wote ni sawa mbele ya sheria.

    Baadhi ya haki zinazokiukwa katika jamii za kimabavu ni haki ya watu kuungana, kuwaza, kushiriki katika maamuzi ya serikali, kuwa mwanachama wa jumuia waitakayo, kumiliki mali, kutembea, kuishi anakotaka kutohukumiwa bila ya kuwako na utaratibu wa kisheria. Ni muhimu hata hivyo kujua ni muhimu kwa raia wenyewe kujielimisha na kuzijua haki zao. Serikali inapaswa kuwa mlinzi wa sheria zenyewe. Lakini muhimu kujua pia kuwa mlinzi naye hulindwa pia.

    Maswali
    a)Kwa maneno kati ya 90 – 100 fafanua Haki Bia za Binadamu zilizoafikiwa na Baraza kuu la umoja wa Mataifa.
    Nakala Chafu
    Nakala Safi
    b) Kwa nini viongozi wa kiimla hukiuka haki za binadamu. (Maneno 50 – 60).
    Nakala Chafu

    Date posted: October 11, 2019.  Answers (1)

  • Soma kifungu kifuatacho kisha ujibu maswali Tokea muundo mpya wa serikali ya ugatuzi uanze kutekelezwa miaka miwili iliyopita, kumeendelea kushuhudiwa matatizo mengi hali iliyopelekea kushuhudiwa kwa...(Solved)

    Soma kifungu kifuatacho kisha ujibu maswali
    Tokea muundo mpya wa serikali ya ugatuzi uanze kutekelezwa miaka miwili iliyopita, kumeendelea kushuhudiwa matatizo mengi hali iliyopelekea kushuhudiwa kwa msururu wa migomo na maandamano ya raia. Fujo za karibuni kabisa ni zile zinazoshuhudiwa katika miji mikubwa za wachuuzi na wafanyibiashara wakipinga hatua za serikali za kaunti kuwatoza ushuru takribani kwa kila huduma na bidhaa ikiwemo wanyama, kuku na ndege. La kuhuzunisha zaidi katika baadhi ya majimbo imeripotiwa kuwa raia wamelazimishwa kulipa ushuru kwa kutaka tu kuona maiti za jamaa zao kwenye vyumba vya kuhifadhi maiti.

    Wanasiasa wameonekana kuwa na wakati mgumu kutetea mfumo huu mpya wa ugatuzi huku baadhi wakisema kwamba matatizo yanayoshuhudiwa kwa sasa yametokana na ugeni wa mfumo huo. Wengine wameinyoshea kidole serikali ya kitaifa kwamba ndiyo inayosambaratisha muundo huu. Wengine wanahoji kuwa bado ni mapema na kwamba kunatajika muda mrefu ili kufaulu.

    Ni wazi kwamba kumekosekana nidhamu bora ya kusimamia maisha ya raia nchini Kenya. Matatizo yanayokumba raia kwa sasa ni dalili kuwa mfumo wa serikali ya ugatuzi umeongezea chumvi kwenye kidonda badala ya kutibu. Swali ni je, hadi lini nidhamu ya kusimamia raia itakuwa ni suala la majaribio na makosa?

    Hatua ya kuwarundikizia raia ushuru mkubwa ni kitendo cha unyonyaji na cha dhuluma kinachofaa kupingwa. La kufahamishiwa hapa ni kwamba ushuru ndio njia kubwa ya kuzalisha mapato ya serikali zinazojifunga na mfumo wa kimagharibi wa kiuchumi wa kibepari ikiwemo Kenya. Asilimia 90 ya mapato ya serikali za kibepari huegemea ushuru. Kwa hivyo hatua ya serikali za kaunti katika kuwanyonya raia kwa kuwalipisha ushuru si ajabu bali ni thibitisho kuwa jamii ya Kenya inaongozwa na nidhamu ya kiuchumi ya ubepari mfumo wa unyonyaji na ukandamizaji. Ukweli unabakia kuwa ndani ya serikali za kibepari raia ndio hubebeshwa mzigo wa ushuru unaoishia matumboni mwa viongozi!

    Miito ya mabadiliko ya katiba na ya miundo mipya ya kiutawala si lolote ila ni moja tu ya hatua za mfumo wa kibepari kujipa muda wa kuishi na kuziba aibu zake za kushindwa kusimamia maisha ya watu. Kufeli huku kwa mfumo huu kunashuhudiwa hadi kwenye nchi kubwa za kibepari kama Marekani na Uingereza hivyo nazo zimekumbwa tele na maandamano na fujo za raia wakilalamikia hali ngumu ya maisha.

    Maswali
    a)Yape makala haya anwani mwafaka.
    b)Eleza mtazamo wa wanasiasa kuhusu utepetevu wa mfumo huu.
    c)“Ugatuzi nchini Kenya ni mfumo wa kibepari” Thibitisha kauli hii kwa kurejelea makala.
    d)Migomo ni zao la matatizo yaliyogatuliwa kutoka kuu. Toa sababu nyingine zinazosababisha migomo katika serikali za ugatuzi
    e)Thibitisha jinsi mfumo wa ugatuzi umeongeza chumvi kwenye kidonda badala ya kutibu
    f)Eleza maana ya maneno yafuatayo
    i) Ugatuzi
    ii) Kibepari

    Date posted: October 11, 2019.  Answers (1)

  • (vigelegele vya harusi vililia alilili ; x3) Kuumeni : (waliimba) Tumeupata mpilipili na maua yake chikicha x2 Kukeni : (wimbo wao kwa sauti tofauti) Tausi waendaa x2 Tausi...(Solved)

    Soma kifungu kifuatacho kisha ujibu maswali yafuatayo :

    (vigelegele vya harusi vililia alilili ; x3)
    Kuumeni : (waliimba) Tumeupata mpilipili na maua yake chikicha x2

    Kukeni : (wimbo wao kwa sauti tofauti) Tausi waendaa x2
    Tausi waenda wamuacha mama kwenye banda.

    Kuumeni : (wakijibu wimbo) Mwacheni aendee x2
    Mwacheni aende akaone mambo ya nyumba.

    Kukeni : Mama ataota nini x2.
    Ataota nini, hana mtu wa kumletea kuni.

    Kuumeni : Ataota moto wa magunzi, wa magunzi wa magunzi. Twamchukua, kisura wetu,
    kisura wetu, kisura wetu.
    Tausi ni wetu sasa, ni kito chema, ni kito chema ni kito chema.

    (i) Wimbo huu ni wa aina gani, na unastahili katika hafla gani ?
    (ii) Bainisha wahusika Kuumeni na Kukeni
    (iii) Fafanua ujumbe uliojikita katika utungo huu
    (iv) Wimbo huu una umuhimu gani hafla ulioimbiwa?
    (v) Tambua mtindo uliotumika katika utungo huu

    Date posted: October 11, 2019.  Answers (1)

  • Onyesha tofauti kati ya vikundi hivi: (i) Hekaya Hurafa (ii) Visakale Visasili (iii) Ngano za mtanziko Ngano za mazimwi(Solved)

    Onyesha tofauti kati ya vikundi hivi:
    (i) Hekaya
    Hurafa

    (ii) Visakale
    Visasili

    (iii) Ngano za mtanziko
    Ngano za mazimwi

    Date posted: October 11, 2019.  Answers (1)

  • Elezea mbinu nne za kutongolea hadithi(Solved)

    Elezea mbinu nne za kutongolea hadithi

    Date posted: October 11, 2019.  Answers (1)

  • Ni nini maana ya Tendi?(Solved)

    Ni nini maana ya Tendi?

    Date posted: October 11, 2019.  Answers (1)