Trusted since 2008
Study resources on Kenyaplex

Get ready-made curriculum aligned revision materials

Exam papers, notes, holiday assignments and topical questions – all aligned to the Kenyan curriculum.

Eleza kanuni ya kutia shadda katika lugha ya Kiswahili.

Eleza kanuni ya kutia shadda katika lugha ya Kiswahili.

Answers


Kavungya
Hutiwa kwa silabi ya pili kutoka mwisho.
Kavungya answered the question on October 31, 2019 at 06:24

Answer Attachments

Exams With Marking Schemes

Related Questions

  • Toa mfano wa maneno mawili ambayo yana sauti mwambatano mbili. (Solved)

    Toa mfano wa maneno mawili ambayo yana sauti mwambatano mbili.

    Date posted: October 31, 2019 .    Answers (1)

  • Taja sifa mbili za irabu /e/ na /i/ ambazo zinafanana. (Solved)

    Taja sifa mbili za irabu /e/ na /i/ ambazo zinafanana.

    Date posted: October 31, 2019 .    Answers (1)

  • Historia na fasihi zina uhusiano wa karibu sana hasa fasihi ya kihistoria. Hata hivyo fasihi siohistoria na historia si fasihi kwa... (Solved)

    UHUSIANO WA FASIHI NA HISTORIA

    Historia na fasihi zina uhusiano wa karibu sana hasa fasihi ya kihistoria. Hata hivyo fasihi sio
    historia na historia si fasihi kwa sababu hizi ni taaluma mbili ambazo zina uhusiano tu. Hata hivyo, fasihi
    na historia zina mambo ambayo yanafana na yale ambayo hayafanani.
    Kati ya mambo ambayo yanafanana ni kwamba fasihi na historia wakati mwingine huweza kuwa
    na wahusika ambao wanafanana kitabia, kimaumbile na hata wakati mwingine matendo ya kukumbukwa
    waliyofanywa. Mfano ni katika shairi la “Hongera Rais Moi” katika diwani ya ' Malenga wa ziwa kuu'
    ambapo mhusika ni rais Moi na mhusika kama yule pia aliishi katika kipindi Fulani katika nchi ya Kenya.
    Jambo jingine ambalo linapatikana katika fasihi na pia kinaoana na historia ni mandhari. Wakati
    mwingine, mandhari ambayo ni ya kihistoria yanakaribiana sana na ya kifasihi na hata wakati mwingine
    kufanana. Mandhari ya shamba la bwana Delamon katika 'kilio cha haki' yanaweza kuwa shamba lolote na
    mabwanyenye kama hata ni ya Bwana Dalamere.
    Wakati mwingine matukio katika fasihi huwa karibu sawa na yale ambayo yanapatikana katika
    historia ya kawaida. Mfano katika shairi la ' wasifu wa baba Kenyatta', mhusika mkuu yasemekana
    alipigania uhuru wa nchi ambayo aliiongoza. Matukio kama kufungwa jela ambayo mhusika huyu
    anapitia katika kujaribu kukomboa nchi ni sawa na yale ambayo mhusika wa kihistoria ambaye ni rais wa
    kwanza wa nchi ya Kenya.
    Pia, wakati mwingi historia na fasihi huwa na maudhui na dhamira sawa. Tamthilia kama 'Mstahiki
    Meya' ambayo nia yake ni kuonyesha jinsi waafrika ambao walichuukua uongozi baada ya ukoloni
    walivyowanyanyasa waafrika wenzao yaweza kuwa sawa na historia ambapo waafrika ambao
    walichukua uongozi waliwanyanyasa waafrika wenzao.
    Uhusiano mwingine wa karibu ni kwamba wakati mwingine fasihi huchota kutoka kwa historia na
    inapofanya hivyo fasihi hiyo inakuwa ya kufanana sana na historia yenyewe.Mfano ni kitabu cha
    mzalendo kimathi ambapo matukio mengi katika kitabu hicho kinadhihirisha kwamba kimechota kutoka
    kwa historia. Pia baada ya kipindi Fulani, fasihi husika inakuwa historia.
    Uhusiano mwingine ni kwamba zote huandikwa kwa lugha na zinapoandikwa fasihi hufufua majina
    ya wale ambao majina yao hayakuweza kuingia katika vitabu vya historia.
    Mwisho, historia na fasihi hufanya jukumu la kumjuza mwanadamu kuhusu mazingira yake hasa
    yale ya zamani na kumuwezesha kuweza aidha kuyarekebisha au kuyakubali. Mfano ni katika tamthilia ya
    kidagaa, Mtemi Nasaba Bora anawapokonya waafrika wezake mashamba kwa kutumia nguvu. Fasihi hii
    pia inaoana na jinsi ambavyo historia inafunza ambavyo viongozi wa kwanza walivyojipatia vipande
    vikubwa vikubwa vya ardhi.Fasihi na historia pia zinakaribiana sana kutokana kwamba mwanahistoria na
    mwanafasihi ni wanajamii wote. Wale ambao huchunguza matukio ya kihistoria na wale ambao huandika
    fasihi pia ni wanajamii.
    Mojawapo wa tofauti ya historia na fasihi ni tofauti ya kiwakati. Historia imefungika kiwakati hivi
    kwamba upeo wake ni sasa. Mwanahistoria akitaka kujuza kuhusu nchi Fulani anaeleza ilikoanza hadi
    ilikofika lakini mwanafasihi anaweza kueleza mahali nchi fulani ilikoanza, iliko sasa na itakavyokuwa
    baada ya miaka mingi baada ya sasa. Mwanafasihi anaweza kuandika kuhusu nchi ya kesho peke yake na
    fasihi iwe imekamilika. Mfano mwema ni George Orwell ambaye alikiandika kitabu mwaka wa 1978 na
    akakiita 1984. Pia Riwaya ya 'Walenisi' ni riwaya ambayo inazungumza kuhusu dunia ambayo ni ya kesho
    jambo ambalo historia haiwezi.
    Tofauti nyingine ni kwamba historia hutegemea ithibati ili iweze kufahamisha. Kama
    inazungumzia kuhusu tukio Fulani, lazima iwe na dhibitisho sahihi na hamna nafasi ya ubunifu. Kwa
    upande mwingine, fasihi ina nafasi ya ubunifu na sio lazima mwanafasihi adhibitishe yale ambayo
    ameandikia yalifanyika. Hata kama Mstahiki Meya ni jina ambalo ni la kihalisia katika masikio ya
    Wakenya, mwandishi wa tamthilia ya Mstahiki hana jukumu la kutoa idhibati za kuonyesha kwamba aliishi
    na pia cheneo ni mojawapo wa miji ya nchi fulani.
    Tofauti nyingine ni kwamba kila mwanafasihi huwa na itikadi yake lakini mwanahistoria huweka
    mambo jinsi yalivyo na kumwachia msomaji awe wa kuamua. Mwandishi kama wa tamthilia ya 'Mstahiki
    Meya' ana itikadi kwamba viongozi dhalimu wanastahili kuondolewa mamlakani kwa nguvu lakini
    mwanahistoria hawezi kuwa na msimamo kama huo.
    Tofauti nyingine ni kwamba fasihi hujikita sana kwa wahusika na maisha yao lakini jambo kuu na
    ambalo historia huzingatia sana ni matukio na wakati ambao matukio hayo yalitokea. Hili hufanya takriban
    fasihi zote kuwa na mhusika mkuu lakini kipindi fulani cha historia chaweza kosa hata mhusika mmoja
    mkuu.
    Jambo jingine ni kwamba historia na fasihi hutofautiana kiwakati, mahali na mandhari ambamo
    matukio fulani yanatokea. Tamthilia kama ya ‘Mstahiki Meya’ ina uwezakano kwamba inazungumza
    kuhusu Kenya na viongozi wa baada ya uhuru lakini mahali ambapo matukio ya tamthilia yanafanyikia ni
    cheneo ala sio wa mji kama Nakuru au Nairobi.
    Tofauti nyingine ni kwamba hamna nafasi ya ubunifu katika historia lakini fasihi huwa ni zao la
    ubunifu. Mambo ambayo wanahistoria huwa wamekosa katika historia yanaweza yakawa wazi kupitia
    ubunifu wa mwandishi. Fasihi pia inaweza ikaumba wahusika au hata dunia ambayo haiwezi ikapatikana
    katika ulimwengu wa kawaida.

    Maswali.
    a. Fupisha aya tatu za kwanza kwa maneno 20-30.
    Nakala safi
    b. Fupisha aya tano za mwisho kwa maneno kati ya 60-70
    Matayarisho

    Date posted: October 31, 2019 .    Answers (1)

  • Fafanua sababu tatu zilizochochea usanifishaji wa lugha ya Kiswahili kabla ya uhuru . (Solved)

    Fafanua sababu tatu zilizochochea usanifishaji wa lugha ya Kiswahili kabla ya uhuru .

    Date posted: October 29, 2019 .    Answers (1)

  • Eleza mambo manne yaliyochangia kuenea kwa lugha ya Kiswahili kabla ya uhuru wa mataifa ya Afrika mashariki . (Solved)

    Eleza mambo manne yaliyochangia kuenea kwa lugha ya Kiswahili kabla ya uhuru wa mataifa ya Afrika mashariki .

    Date posted: October 29, 2019 .    Answers (1)

  • Tambua hali na nyakati katika sentensi ifuatayo Atakuwa ameondoka utakapofika. (Solved)

    Tambua hali na nyakati katika sentensi ifuatayo
    Atakuwa ameondoka utakapofika.

    Date posted: October 29, 2019 .    Answers (1)

  • Toa visawe viwili vya ‘uchochole’ (Solved)

    Toa visawe viwili vya ‘uchochole’

    Date posted: October 29, 2019 .    Answers (1)

  • Kanusha sentensi ifuatayo: Aimbapo vizuri mtuze (Solved)

    Kanusha sentensi ifuatayo:
    Aimbapo vizuri mtuze

    Date posted: October 29, 2019 .    Answers (1)

  • Andika sentensi ifuatayo katika hali ya ukubwa Paka huyu aliguguna mfupa wa mtoto huyu. (Solved)

    Andika sentensi ifuatayo katika hali ya ukubwa
    Paka huyu aliguguna mfupa wa mtoto huyu.

    Date posted: October 29, 2019 .    Answers (1)

  • Tambua kiima na kiarifa katika sentensi hii (Solved)

    Tambua kiima na kiarifa katika sentensi hii

    Taa yake inatoa moshi mwingi

    Date posted: October 29, 2019 .    Answers (1)

  • Tunga sentensi ukitumia neno katika ngeli ya YA-YA. (Solved)

    Tunga sentensi ukitumia neno katika ngeli ya YA-YA.

    Date posted: October 29, 2019 .    Answers (1)

  • Changanua sentensi ifuatayo kwa njia ya matawi . Mtoto alipoumia alitibiwa haraka sana. (Solved)

    Changanua sentensi ifuatayo kwa njia ya matawi .
    Mtoto alipoumia alitibiwa haraka sana.

    Date posted: October 29, 2019 .    Answers (1)

  • Taja mfano mmoja kwa kila aina ya sauti zifuatazo; Kipasuo-kwamizo – Irabu ya nyuma wastani - (Solved)

    Taja mfano mmoja kwa kila aina ya sauti zifuatazo;
    Kipasuo-kwamizo –
    Irabu ya nyuma wastani -

    Date posted: October 29, 2019 .    Answers (1)

  • Nilianza kusikia habari za ugonjwa wa ukimwi mnamo mwaka wa 1984. Wakati huo nilikuwa nimemaliza masomo yangu ya kidato... (Solved)

    Soma makala yafuatayo kisha ujibu maswali

    Nilianza kusikia habari za ugonjwa wa ukimwi mnamo mwaka wa 1984. Wakati huo nilikuwa nimemaliza masomo yangu ya kidato cha sita na kujiunga ia chuo cha walimu kilichoko wilayani Nyeri kiitwacho Kagumo. Nilihofu sana maradhi hayo hasa nilipowaona walioambukizwa wakikondeana mthili ya ng’onda. Baada ya waathiriwa kufariki, jamaa zao hawakuruhusiwa kuwazika. Wizara ya afya ilitoa amri kali kuwa wale wore waliofariki kutokana na maradhi ya ukimwi wazikwe na kikundi maalum cha madaktari ma wauguzi wa hospitali za wilayani. Kulikuwa na kasisi mmoja tuliyehusiana kiukoo aliyefariki kutokana na maradhi ya ukimwi. Sisi hatukuruhusiwa hata kumsongea karibu marehemu alipoletwa nyumbani.
    Madaktari na wauguzi walivalia majoho meupe ungedhani ni malaika. Mikononi walivaa glovu nyeupe ambazo zilitutisha machoni.
    Mara nyingi nimeshangazwa na athari za ugonjwa huu. Inasemekana kuwa kuna njia kadha za usambazaji wa ugonjwa wa ukimwi. Njia moja ni kuhusika katika kitendo cha mapenzi na mtu ambaye ameambukizwa virusi vya ugonjwa huo. Njia nyingine nimeelezwa kuwa ni kwa kutumia kwa pamoja vifaa vyenye makali na mtu aliyeambukizwa virusi vya ukimwi. Inasemekana kuwa kugusa damu ya mtu aliyeambukizwa ugonjwa huo pia kunaweza kukutia mashakani.
    Mama mja mzito aliyeambukizwa ugonjwa huu anaweza kumwambukiza mtoto aliye tumboni anapojifungua na hati baadaye anapomnyonyesha mtoto wake mchanga. Kisha kuna kupokea damu kutoka kwa mtu ambaye tayari ameambukizwa virusi hivyo. Yote hayo yanachangia pakubwa katika kututumbukiza kwenye janga hili la ukimwi.
    Lakini nimewahi kusikia watu wakisema kuwa ukimwi si maradhi. Yaani ni
    upungufu tu wa kinga ya kukabiliana na magoniwa katika mwili wa binadamu. Maadamu ukiweza kuimarisha kinga ya magonjwa katika mwili wako basi unaweza kuishi kwa miaka ma mikaka. Anachohitajika mtu ni apate chakula na lishe bora, afanye mazoezi ya kutosha, na kujiepusha na mahusiano ya kimapenzi na watu wenine ambao huenda wakamwambukiza aina tofauti tofauti za virusi vya ukimwi. Hayo yakifanyika mwathiriwa huwa na matumaini ya kuishi kwa muda mrefu kwani hatazidiwa na maradhi hayo na mwishowe kwenda jongomeo. Kuna haja kubwa ya kujilinda na kuepukana kabisa na janga hili lililotuzingira. Wengi tayari wameshapoteza roho zao. Wengine walioambukizwa wanaugua mahospitalini ma na majumbani mwao kisirisiri. Mungu atujalie heri na shari, kwani utafiti wote ambao umefanywa kuhusu tiba ya uwele huu haujafua dafu hata kidogo. Hata hivyo Mola hamtupi mja wake.

    Maswali
    a) Ipe habari hii anwani ifaayo.
    b) Kwa nini mwandishi ana hofu sana ya maradhi ya ukimwi?
    c)Hapo awali watu waliwachukulia vipi walioambukizwa maradhi ya Ukimwi?
    d)Eleza njia mbalimbali zinazomfanya mtu kuambukizwa maradhi ya ukimwi .
    e)Je, tunawezaje kuepukana na janga hili la ukimwi?
    f)Eleza maana ya vifungu hivi vya maneno kama vilivyotumika katika taarifa.
    i)Wauguzi
    ii)Makali
    iii)Virusi
    iv)Uwele
    v)Janga

    Date posted: October 29, 2019 .    Answers (1)

  • Eleza maana ya istilahi zifuatazo za isimu jamii. i)Lugha ya taifa (ii)Lugha ya ishara (iii)Lugha mwiko (iv)Sajili za lugha (v)Uchanganyaji msimbo. (Solved)

    Eleza maana ya istilahi zifuatazo za isimu jamii.
    i)Lugha ya taifa
    (ii)Lugha ya ishara
    (iii)Lugha mwiko
    (iv)Sajili za lugha
    (v)Uchanganyaji msimbo.

    Date posted: October 21, 2019 .    Answers (1)

  • ISIMU JAMII Ali: Wee kuja hapa. Wewe ni nani? Sema haraka! Ebo: Mimi … ni … afande ni Ebo Ali: Unatoka wapi sa ii? Hapa hakuna sheria? Ebo:... (Solved)

    ISIMU JAMII
    Ali: Wee kuja hapa. Wewe ni nani? Sema haraka!
    Ebo: Mimi … ni … afande ni Ebo
    Ali: Unatoka wapi sa ii? Hapa hakuna sheria?
    Ebo: Samahani mkubwa. Mimi niku…
    Ali: Mkubwa wa nani? Wakubwa wako ofisini.
    Ebo: Pole mzee.
    Ali: Mzee gani? Hii mtu lazima niiwekwa store. Yaani self-contained.
    Toa viatu.
    Ebo: Tafadhali Bwana Askari, nilichelewa …
    Ali: Mimi sitaki hadithi! Hizo pelekea nyanya yako, eh. Fanya haraka!
    Ebo: Naomba mkubwa …
    Ali: Hapa si kanisani. Unaomba! Hata …

    Fafanua sifa tano za sajili hii.

    Date posted: October 21, 2019 .    Answers (1)

  • Eleza maana ya nomino. (Solved)

    Eleza maana ya nomino.

    Date posted: October 21, 2019 .    Answers (1)

  • Eleza maana tatu zinazopatikana katika sentensi hii. Alikuwa amenijuza kuwa angefika kwao. (Solved)

    Eleza maana tatu zinazopatikana katika sentensi hii.
    Alikuwa amenijuza kuwa angefika kwao.

    Date posted: October 21, 2019 .    Answers (1)

  • Eleza matumizi ya kwa katika sentensi hii. Kwa nini umeishi kwao kwa miaka mingi? (Solved)

    Eleza matumizi ya kwa katika sentensi hii.
    Kwa nini umeishi kwao kwa miaka mingi?

    Date posted: October 21, 2019 .    Answers (1)

  • Tumia kivumishi kionyeshi cha karibu pamoja na nomino katika ngeli ya I-ZI kisha utunge sentensi katika ukubwa - wingi. (Solved)

    Tumia kivumishi kionyeshi cha karibu pamoja na nomino katika ngeli ya I-ZI kisha utunge sentensi katika ukubwa - wingi.

    Date posted: October 21, 2019 .    Answers (1)