Get premium membership and access questions with answers, video lessons as well as revision papers.

Kwa kutoa mifano fafanua vipengele vitano vya kiisimu vinavyothibitisha kwamba kiswahili ni lugha ya kibantu

      

Kwa kutoa mifano fafanua vipengele vitano vya kiisimu vinavyothibitisha kwamba kiswahili ni lugha ya kibantu

  

Answers


Faith
Kiswahili ni moja Kati ya lahaja za kibantu.imethibitishwa kuwa kiswahili Ina maneno asilimia kubwa ya maneno ya kibantu.Tunaweza kuthibitisha hii kwa kuangalia ushahidi wa kiisimu unaotokana na utafiti wa sayansi ya lugha.
• Msamiati wa kiswahili.Guthrie(1967) alionyesha uhusiano uliopo katibya kiswahili na lugha zingine za kibantu.Alionyesha uhusiano wa mashina mengi ambayo yamezagaa katika lugha zingine za kibantu Alichunguza asili ya neno 'Bantu' au watu.Shina hili linapatikana katika lugha nyingi za kibantu na hii inaonyesha kuwa kiswahili ni mojawapo ya lahaja za kiswahili.
• Mnyambuliko wa vitenzi.Lugha za kibantu Kama ilivyo lugha ya kiswahili hudhihirisha mnyambuliko wa vitenzi. Kwa mfano;
Kutenda-lima
Kutendana-limana
Kutendeka-limika
Kutendatenda-limalima
Kulingana na myambuliko huo wa pamoja Basi kiswahili ni kibantu.
• Mfumo wa silabi wazi.Lugha za kibantu Kama ilivyo kiswahili hudhihirisha mfumo wa silabi wazi.Yaani Kila silabi ya neno lenye asili ya kibantu huishia kwa vokali.Hii pia inafanyika kwa lugha za kibantu.Maneno mengi ya kibantu huwa na muundo wa konsonanti vokali konsonanti vokali.Kwa mfano 'lima',kisu,meza na kadhalika.pia Kuna yasiyofuata muundo huu Kama vile cheka,mbuzi n.k
• Lugha za kibantu Kama ilivyo kiswahili huunganisha mofimu ili kuunda sentensi ya neno moja.Mfano 'alicheza' inaweza kuainishwa hivi.
A-kiambishi cha nafsi
Li-kiambishi Cha wakati uliopita
Chez-mzizi wa kitenzi
a-kiishio
• Katika lugha za kibantu na kiswahili Kuna uwezekano was kuunda nomino kutokana na vitenzi,vitenzi kutokana na nomino, vitenzi kwa vivumishi.kwa mfano
Kitenzi–nomino
Cheza-mchezo
Imba wimbo
Kivumishi–kitenzi
Bora-boresha
Safi-safisha

Titany answered the question on December 6, 2021 at 08:14


Next: Eleza upungufu wa nadharia inayodai kwamba Kiswahili ni lugha ya mseto
Previous: Ushahidi was kihistoria ni muhimu katika kujadili swala la chimbuko la kiswahili.Jadili kauli hii kwa kurejelea Ushahidi huo

View More Historical Development of Kiswahili Questions and Answers | Return to Questions Index


Learn High School English on YouTube

Related Questions