Get premium membership and access questions with answers, video lessons as well as revision papers.

Tathmini mchango wa kamati ya Kiswahili ya Afrika Mashariki(K.K.A.M) katika kusanifisha lugha ya Kiswahil

      

Tathmini mchango wa kamati ya Kiswahili ya Afrika Mashariki(K.K.A.M) katika kusanifisha lugha ya Kiswahil

  

Answers


Faith
• Kamati ya Kiswahili ya Afrika Mashariki ilisaidia kwa kusanifisha maandishi na kuhakikisha mtindo mmoja unazingatiwa katika kuendeleza maneno za kiswahili.
• Kamati ilichapisha vitabu vilivyohitajika na pia vya ziada ambayo iliwasaidia pia katika kazi ya usanifishaji.
• Kamati iliwasaidia na kuwahimiza waandishi wa vitabu vya kiswahili ambao pia walikuja kusaidia katika kazi ya usanifishaji wa kiswahili.
• Kamati ilikuwa ikiwapasha waandishi habari zozote zile kuhusu njia tofauti au mitindo ya kusomesha katika kila nchi .Hii iliwasaidia kwa kuwa usanifishaji ilihusisha nchi zote ili kuepuka kutoeleweka.
• Kamati ilisaidia kwa kuchapisha kamusi mbili.moja ya kiswahili kwa kiswahili na nyingine kiswahili kwa kingereza.Hii ilisaidia wanafunzi na walimu jinsi ya kuendeleza maneno mbalimbali.
• Kamati ilikuwa ikiyajibu maswali yote ya umma na kuchapisha katika jarida la ILC Bulletin.
• Kamati ilisaidia katika usimamizi wa utafiti wa lahaja za kiswahili na mayokeo ya utafiti kuchapishwa kwa studies in Swahili dialects.
• Kamati pia ilikuwa ikiandaa mashindano ya kuandika insha na vitabu ili kuwatia ari waandishi wa kiswahili na Hii ilisaidia sana katika shughuli za usanifishaji wa kiswahili.

Titany answered the question on December 6, 2021 at 09:53


Next: Eleza ni kwa nini lugha ya Kiswahili ilisanifishwa wakati wa ukoloni
Previous: Kiswahili kinahitaji kusanifisha upya.Jadili kauli hii

View More Historical Development of Kiswahili Questions and Answers | Return to Questions Index


Learn High School English on YouTube

Related Questions