[1] [i] Asiyesikia na mkuu huvunjika guu
[ii] umekuwa pweza kujipalia makaa?
Sahihisha kichwa kingine chochote kinachoafiki kifungu hiki
[2] Kuitwa mama kabla ya kumkopoa mwana wake mwenyewe
[3] -Alijiona kuwa yeye ndiye mcukuzi bora
- Aliwaona wenzake kama maua yaliyonyauka na lake ndilo kwanza linaonana na jua
[4] -kwa kutosikiliza wakuu na kumkimbilia mtu ambaye hata hakuwa anamuelewa vizuri
- pesa na raha alizokimbilia akawa anazisikia kama hadithi ndotoni
[5]- mumewe hakutulia mambo ya nje , alikuwa kiguu na njia
-Alikuwa na wanawake wengi nje ya ndoa
[6] –kukonda
-homa hapa na pale
-vipelevipele mwilini
[7] –walikuwa walimfunza umuhimu wa kuwa na maadili
[8] [i] isiyo na makali
[ii] kuona aibu, soni, fedheha, haya
[iii] -akiwa bado mdogo
-Bado hajakomaa
[iv] kuondoka mahali kwa haraka
[v] vijinenoneno
Kavungya answered the question on November 21, 2022 at 11:20
-
Tambua kielezi katika sentensi ifuatayo. Kijana mkorofi ameadhibiwa vibaya
(Solved)
Tambua kielezi katika sentensi ifuatayo.
Kijana mkorofi ameadhibiwa vibaya
Date posted:
August 17, 2020
.
Answers (1)
-
Tambua kivumishi katika sentensi ifuatayo. Mwanafunzi mdogo amezungumza taratibu.
(Solved)
Tambua kivumishi katika sentensi ifuatayo.
Mwanafunzi mdogo amezungumza taratibu.
Date posted:
August 17, 2020
.
Answers (1)
-
Vita vina athari nyingi katika maisha ya binadamu, dhibitisha ukweli wa kauli hii ukiangazia riwaya ya chozi la heri.
(Solved)
Athari za vita katika riwaya ya Chozi la heri.
Date posted:
June 15, 2020
.
Answers (1)
-
"Maisha yangu yalijaa shubiri tangu utotoni." Rejelea Chozi la heri.
(Solved)
a) Eleza muktadha wa dondoo hili.
b) Bainisha tamathali ya usemi iliyotumika katika dondoo hili.
Date posted:
June 15, 2020
.
Answers (1)
-
Nini maana ya kishazi?toa mifano ya vishazi
(Solved)
Nini maana ya kishazi?toa mifano ya vishazi.
Date posted:
May 10, 2020
.
Answers (1)
-
Toa sababu nne zinazosababisha watu kufanya makosa katika matumizi ya lugha.
(Solved)
Toa sababu nne zinazosababisha watu kufanya makosa katika matumizi ya lugha.
Date posted:
November 20, 2019
.
Answers (1)
-
Fafanua mambo manne yaliyochochea usanifishaji wa Kiswahili wakati wa ukoloni nchini.
(Solved)
Fafanua mambo manne yaliyochochea usanifishaji wa Kiswahili wakati wa ukoloni nchini.
Date posted:
November 20, 2019
.
Answers (1)
-
Ni hisia zipi zinazodhihirika katika matumizi haya ya vihisishi.
(i) Maskini! Alinyimwa msaada na serikali
(ii) Wallahi! Nikikutana naye atajuta kwa nini kazaliwa.
(Solved)
Ni hisia zipi zinazodhihirika katika matumizi haya ya vihisishi.
(i) Maskini! Alinyimwa msaada na serikali
(ii) Wallahi! Nikikutana naye atajuta kwa nini kazaliwa.
Date posted:
November 20, 2019
.
Answers (1)
-
Ondoa ‘o’ rejeshi bila kubadilisha maana.
Kuimba kulikosifika siku nyingi sasa kunatia shaka
(Solved)
Ondoa ‘o’ rejeshi bila kubadilisha maana.
Kuimba kulikosifika siku nyingi sasa kunatia shaka
Date posted:
November 20, 2019
.
Answers (1)
-
Fafanua aina ya hali katika sentensi hii.
Mtoto acheza mpira
(Solved)
Fafanua aina ya hali katika sentensi hii.
Mtoto acheza mpira
Date posted:
November 20, 2019
.
Answers (1)
-
Tunga sentensi mbili tofauti ukitumia neno ‘haya’ kama:
(i) Nomino
(ii) Kivumishi
(Solved)
Tunga sentensi mbili tofauti ukitumia neno ‘haya’ kama:
(i) Nomino
(ii) Kivumishi
Date posted:
November 20, 2019
.
Answers (1)
-
Sentensi zifuatazo ni za aina gani?
(i) Japo alijitahidi hakufaulu.
(ii) Alijitahidi japo hakufaulu.
(Solved)
Sentensi zifuatazo ni za aina gani?
(i) Japo alijitahidi hakufaulu.
(ii) Alijitahidi japo hakufaulu.
Date posted:
November 20, 2019
.
Answers (1)
-
Nyambua kitenzi kifuatacho katika kauli ya kutendama.
‘Shika’
(Solved)
Nyambua kitenzi kifuatacho katika kauli ya kutendama.
‘Shika’
Date posted:
November 20, 2019
.
Answers (1)
-
Huku ukitoa mfano mmoja mmoja fafanua miundo miwili ya ngeli ya U-I.
(Solved)
Huku ukitoa mfano mmoja mmoja fafanua miundo miwili ya ngeli ya U-I.
Date posted:
November 20, 2019
.
Answers (1)
-
Unda kivumishi kutokana na kitenzi ‘sadiki’.
(Solved)
Unda kivumishi kutokana na kitenzi ‘sadiki’.
Date posted:
November 20, 2019
.
Answers (1)
-
Tunga sentensi ya neno moja yenye viungo vifuatavyo.
(i) Kiambishi cha nafsi ya kwanza umoja
(ii) Njeo
(iii) Yambwa tendwa
(iv) Mzizi
(v) Kauli ya kufanyiza
(vi) Kiishio
(Solved)
Tunga sentensi ya neno moja yenye viungo vifuatavyo.
(i) Kiambishi cha nafsi ya kwanza umoja
(ii) Njeo
(iii) Yambwa tendwa
(iv) Mzizi
(v) Kauli ya kufanyiza
(vi) Kiishio
Date posted:
November 20, 2019
.
Answers (1)
-
Taja kiwakilishi ngeli cha nomino ‘UMASKINI’
(Solved)
Taja kiwakilishi ngeli cha nomino ‘UMASKINI’
Date posted:
November 20, 2019
.
Answers (1)
-
Eleza tofauti kati ya kiimbo na shadda.
(Solved)
Eleza tofauti kati ya kiimbo na shadda.
Date posted:
November 20, 2019
.
Answers (1)
-
Taja sifa mbili za mizizi wa kitenzi.
(Solved)
Taja sifa mbili za mizizi wa kitenzi.
Date posted:
November 20, 2019
.
Answers (1)
-
Takwimu za tafiti za umaskini kila mara huonyesha kuwa bara la Afrika ndilo bara maskini kabisa kote duniani. Takriban wakaazi kiasi cha asilimia...
(Solved)
Takwimu za tafiti za umaskini kila mara huonyesha kuwa bara la Afrika ndilo bara maskini kabisa kote duniani. Takriban wakaazi kiasi cha asilimia themanini hawawezi kumudu kutumia dola moja kwa siku. Toka kaskazini hadi kusini. mashariki hadi magharibi mwa bara, makaazi ya vibanda yametamalaki. Wakaazi wengi hulala njaa kutokana na ukosefu wa chakula. Watu wa mitaani waliovaa mararuraru wamejaa katika miji ya bara hili. Swali ni: Je, kwa nini umaskini umeliganda bara la Afrika hivi mithili ya kupe? Kwa nini bara huselelea katika lindi la uchochole?
Ili kuelewa sababu za umaskini kuganda barani Afrika, yampasa mtu ima fa ima kurejelea historia ya bara hili. Kwa kipindi cha karne nyingi, Afrika ilidhibitiwa na walowezi pamoja na mabeberu. Wanawake ambao wangelistwawisha bara hili kiuchumi walitwaliwa kimabavu na kupelekwa, huku wamefungwa minyororo, kustawisha uchumi wa mabara mengine. Afrika ikaporwa nguvu ambayo ni rasilmali kuu katika ustawishaji wa uchumi. La kusikitisha ni kuwa Afrika haikufidiwa kutokana na wizi huu. Badala yake iliongezewa mizigo mingine.
Baada ya kipindi cha biashara ya utumwa kumalizika, Afrika ilijipata katika janga jingine. Wakoloni wakaliingilia bara kwa pupa. Wakaligawanya katika koloni mbalimbali miongoni mwao. Wakaingiwa na wendawazimu kuiba malighafi ya bara hili. Wakaiba mashamba, madini, miti na chochote cha maana walichokipata. Badala ya malighafi haya kutumika kunawirisha bara la Afrika, yalitwaliwa kustawisha chumi za walikotoka wakoloni. Afrika ikaachwa kuzidi kudidimia katika lindi la umaskini.
Wakoloni walipotoka barani Afrika na kuzipa dola nyingi za Afrika ‘uhuru’, waliacha mkururo wa madhila. Madhila haya hayangeikubalia Afrika kujikomboa kutoka katika biwi la uchochole. Tatizo la kwanza na kubwa zaidi ni wakoloni kugawanya na kukatakata Afrika katika mataifa mengi. Mgawanyo huu ukawa haukufuata utaratibu wowote. Kwa sababu hii, watu wa nasaba moja wakawekwa katika nchi tofauti. Mathalani , watu wa nasaba ya Kisomali waligawanywa na kuwekwa chini ya nchi huru ya Somali, wengine chini ya dola la Uhabeshi, huku wengine wakiwa nchini Kenya na Jibuti. Watu kama hawa hawakutaka mpango huu. Waliokuwa Kenya na Uhabeshi wakachukua silaha na kupigana ili warejeshwe chini ya himaya moja ya taifa huru la Somali. Watu kama hawa wakatumia muda mwingi kupigana; muda ambao ungetumika kuinua Afrika kiuchumi. Mapigano haya ya wenyewe kwa wenyewe yamekithiri kote katika bara la Afrika.
Halikadhalika, mkoloni hakufanya juhudi zozote za kuanzisha viwanda ambavyo vingenyanyua uchumi wa Afrika na kuwatoa Waafrika katika biwi la ufukara. Palipokuwa na ari yoyote ya kuanzisha kiwanda, kilipoanzishwa hakikusaidia Afrika kiuchumi. Vilikuwa viwanda vya kupunguza zigo la bidhaa na kuzifanya kuwa nyepesi ili zisafirishwe kwa ajili ya viwanda vya nchi walizotoka wakoloni.
Kwa kipindi cha muda ambao mkoloni amekuwa na maingiliano na wakaazi wa Afrika, amehakikisha kuwa mwafrika amekuwa mtegemezi wake. Malighafi ya Afrika yalipelekwa kutayarishiwa viwanda vya wakoloni. Kisha mwafrika alirudishiwa zikiwa bidhaa kamili za kutumiwa. Mwafrika akaonyeshwa kuwa chochote kilichotoka kwa wakoloni ni bora zaidi ya chake alichozalisha. Hii ikawa ni mbinu moja ya wakoloni kuwafukarisha Waafrika. Hata sasa, kilichotoka Ulaya, hata kama ni cha hali ya chini, huonekana bora zaidi kuliko alichozalisha Mwafrika
Kwa upande mwingine, inadhihirika kuwa wakoloni hawajawahi kuondoka na kuwaachia Waafrika jukumu kamili la kuendesha uhuru wao kisiasa, kijamii na kiuchumi. Waliondoka kupita mlango mmoja na kurudi kwa wa pili. Mlango wa pili ukawa ni ukoloni kuchukua sura nyingine, sura ya ukoloni mamboleo. Kupitia ukoloni huu, wakoloni hudhibiti uchumi na maendeleo ya Afrika kupitia asasi mbili walizozianzisha, yaani Benki Kuu ya Dunia na Shirika la Fedha Duniani. Ili kupata mikopo ya maendeleo, asasi hizi hutoa masharti ambayo hukwamiza badala ya kuchangia kuleta maendeleo barani Afrika.
Sasa hivi pana haja ya wana wa Afrika kufanya vikao vya dhurura ili kujadiliana kuhusu suluhisho la tatizo hili sugu la umaskini barani. Lazima wawahimize Waafrika wote kujikomboa kiakili na kung’amua kuwa maendeleo ya bara lazima yaongozwe na yadhibitiwe na Waafrika wenyewe. Wawahimize kuacha hulka za kukimbilia mataifa yaliyowafanya watumwa na kuwakalia kikoloni kwa misaada ya maendeleo. Misaada hii si ya dhati bali ni ya chati na hailengi kuondoa umaskini barani bali kuuendeleza.
Pana haja pia Waafrika kuwa na miungano ya kiuchumi. Miungano hii husaidia katika uteteaji wa soko pamoja na bei za bidhaa zao ikilinganishwa na taifa moja kuyaendeleza mambo haya. Halikadhalika, Waafrika wanapaswa kutambua kile wanachotaka na kupanga mikakati ya kufikia mahitaji ya kimsingi kwa wananchi wake. Kwa mfano, uimarishaji wa mbinu msingi ambazo zitachangia kuimarisha uchumi wa mataifa wahitaji kuwa mstari wa mbele badala ya ununuzi wa magari na ndege za hadhi za kuwabebea viongozi.
(a) Ipe taarifa uliyoisoma anwani mwafaka.
(b) Kutamalaki kwa umaskini barani Afrika kunadhihirishwa na nini.
(c) Onyesha jinsi ambavyo wakoloni wameendeleza umaskini barani Afrika.
(d) Thibitisha kwa kutoa hoja tatu, dhana ya kuwa “Waafrika wenyewe ndio wamechangia kuwepo kwa umaskini wa bara la Afrika.”
(e) Umaskini barani Afrika unaweza kukabiliwa vipi kwa mujibu wa makala haya?
(f) Eleza msamiati ufuatao kama ulivyotumika katika taarifa:
(i) kuselelea……………
(ii) mabeberu…………
Date posted:
November 20, 2019
.
Answers (1)