Get premium membership and access questions with answers, video lessons as well as revision papers.

Mwandishi wa hadithi, Nipe Nafasi ameshughulikia vipi suala la ’ utamaduni na mabadiliko’

      

Mwandishi wa hadithi, Nipe Nafasi ameshughulikia vipi suala la ’ utamaduni na mabadiliko’

  

Answers


Francis
1. Utamaduni
Japo Kazili anajua kwamba mumewe ana mke mwingine huko migodini anakofanya kazi, hatarajiwi kulalamika kwani utamaduni unamruhusu mume kuwa na wake wengi. Ndiye pia anatakiwa kufanya kazi na kukidhi familia yake.
Msimulizi anasema kuwa kama mama hangekuwa makini, angekumbushwa kuwa hakutolewa Swaziland aje kuwaua watoto bali kuwatengeneza. Mwanamke anachukuliwa kuwa kifaa cha uzazi. Anatarajiwa kuvyaa watoto wengi iwezekanavyo na kuwatunza. Anatarajiwa pia kuomba ruhusa kutoka kwa mumewe kabla ya kufanya lolote.
Matweba na wanaume wenzake wanamsikiza Kazili. Tunaambiwa wanasikiza kwa kimya kama kile kinachokuwa katika mahakama yao ya kitamaduni. Wanaume pia wana sehemu ambayo wanatumia kutoa maamuzi kuhusiana na masuala ya kifamilia kama hayo inayoitwa kraal. Hapo wanawake hawaruhusiwi. Maamuzi wanayotoa wanaume yanachukuliwa kuwa sheria.
Tunaambiwa kuwa Matweba na wenzake wanajitahidi kulinda tamaduni za jamii. Matweba anadai kuwa wanaume ambao hawajapata kazi kwenye migodi wana jukumu la kuhakikisha kwamba familia haisambaratiki. Wanafaa kuhakikisha kuwa wanawake wanawaheshimu waume zao.
Msimulizi anaeleza kisa cha mwanamke aliyesema mumewe ni mzembe. Hayo yalionekana kuwa matusi makubwa. Ilisemekana kuwa amerudi kwa wazazi wake au kuwa ngalile, mwanamke aliyerudi kwa wazazi wake. Wanagundua baadaye kuwa aliuawa na mumewe na akamzika kondeni mwao. Hata mama Kazili anapobisha kauli ya wanaume, wanawake wazee wanahisi kwamba anafaa kuomba msamaha.
Msimulizi na ndugu zake wanaandaliwa chakula kitamu cha papasane(aina ya mboga za mwituni) na nyama ya kondoo. Anasema kuwa jina lake la kupanga, Richman, linatokana na bwana mmoja wa jamaa ya Belo aliyefuga kondoo wengi. Isitoshe, anasema kuwa anawasikia ng’ombe wakikoroma kwenye kraal. Ni baadhi ya shughuli za kiuchumi zinazoendeshwa.

2. Mabadiliko
Mama Kazili anaondoka Habelo bila ruhusa kutoka kwa mumewe kama anavyotakiwa. Yuko tayari kupigania hali yake na ya wanawe. Hayuko tayari kutawaliwa na mwanamume kama jamii inavyotaka. Anawajuza haya wazi wazi Matweba na wanaume wenzake.
Wanapomaliza kupanda Milima ya Mailoti na Mkhathini kufariki, mama anaangua kilio. Wanapofika nyumbani kwa Matweba, hata hivyo, anajua hali inayomkabili. Sasa yuko makini na uso wake umejaa ujasiri. Anapozungumza baadaye kupinga maamuzi ya kraal, amerejea sautu ile ile ya milimani.
Kazili anapobisha kauli za wanaume, wanashtuka sana kwani hawajazoea hali hii. Wamezoea wasemalo ni sheria. Mwamko wake unaleta msisimko miongoni mwa wanawake wa makamo wanaohisi kwamba hatimaye amesema ukweli unaostahili kusemwa. Wanahisi kwamba ni wakati wao kusimama kidete kupinga mzigo mzito wa kiuchumi uanowalemea.
Msimulizi anakumbuka usemi wa mama kuwa ataboresha maisha yake na ya wanawe, jambo ambalo anashangaa kama linawezekana. Hii ni kwa sababu hili linawaziwa kuwa jukumu la wanaume. Hata hivyo, anaamini mwishoni mwa mwaka, mamake anapopata kazi ya kufunza shule ya msingi, kwani hawakosi chakula.
francis1897 answered the question on January 30, 2023 at 11:21


Next: Taasubi ya Kiume na migogoro ni baadhi ya masuala makuu katika hadithi, Nipe Nafasi. Jadili.
Previous: Huku ukitolea mifano, eleza matumizi ya mbinu zifuatazo katika hadithi, Nilitamani; (i) Kinaya (ii) Taharuki (iii) Taswira

View More Kiswahili Fasihi Questions and Answers | Return to Questions Index


Learn High School English on YouTube

Related Questions