Get premium membership and access questions with answers, video lessons as well as revision papers.

Taja aina ya mashairi kulingana na idadi ya mishororo katika ubeti

      

Taja aina ya mashairi kulingana na idadi ya mishororo katika ubeti

  

Answers


Francis
1. Tathmina/umoja – ni shairi lenye mshororo mmoja katika kila ubeti. Mashairi ya aina hii hayapatikani kwa wingi.

2. Tathnia/uwili – ni shairi lenye mishororo miwili katika kila ubeti. Mashairi haya ingawaje yapo, lakini pia kwa uchache.

3. Tathlitha/utatu/wimbo – ni shairi lenye mishororo mitatu katika kila ubeti. Shairi la aina hii wakati mwingine pia huitwa wimbo.

4. Tarbia/unne – ni shairi lenye mishororo minne katika kila ubeti. Mashairi mengi ambayo yametungwa huwa ni ya aina hii.

5. Takhmisa/utano – ni shairi lenye mishororo mitano katika kila ubeti.

6. Tasdisa/usita – ni shairi lenye mishororo sita katika kila ubeti.

7. Tasbia/usaba – ni shairi lenye mishororo saba katika kila ubeti.

8. Naudi/unane – ni shairi lenye mishororo minane katika kila ubeti.

9. Telemania/utisa – ni shairi lenye mishororo tisa katika kila ubeti.

10. Ukumi – ni shairi lenye mishororo kumi katika kila ubeti. Pia shairi hili huitwa ushuri.

11. Soneti- ni shairi lenye mishororo kumi na minne katika kila ubeti.
francis1897 answered the question on February 1, 2023 at 06:23


Next: Uainisho wa bahari za mashairi hutegemea pakubwa vigezo mbalimbali. Taja vigezo hivyo.
Previous: Eleza aina za mashairi kulingana na idadi ya vipande katika mshororo

View More Ushairi Questions and Answers | Return to Questions Index


Learn High School English on YouTube

Related Questions