Get premium membership and access questions with answers, video lessons as well as revision papers.

Questions and answers: Kiswahili

Q&A Categories


Do you have Q&A pairs? Post them here

2287 Questions  View: All | Solved | Unsolved



Search Results...
  • UFUPISHO Ujambazi wa kimataifa ni tatizo lilolowasumbua walimwengu kwa muda mrefu sana. Serikali nyingi zimetumia mapesi mengi kwa miaka mingi sana zikijitahidi kupambana na janga hii. Hata hivyo,...(Solved)

    UFUPISHO Ujambazi wa kimataifa ni tatizo lilolowasumbua walimwengu kwa muda mrefu sana. Serikali nyingi zimetumia mapesi mengi kwa miaka mingi sana zikijitahidi kupambana na janga hii. Hata hivyo, fanaka haijapatikana wala haielekei kamwe kuwa itapatikana leo au karne nyingi baadaye. Yumkini tatizo kubwa lililopo ni kuhusu jelezi la dhana ya “ujambazi” tena “wa kimataifa”. Hili ni tatizo mojawapo na yapo mengi sana. Tatizo la pili ni kiburi. Kuna wale watu binafsi na hasa viongozi wan chi kubwakubwa na serikali zao zilizojiaminisha kuwa ujambazi ni balaa kweli, tena belua, lakini huo ni wa huko, wala hauwezi kuwagusa licha ya kuwashtua wao. Kulingana na maoni watakaburi hao, ujambazi ni wa watu “washenzi” wasiostaarabika, wapatikanao katika nchi zisizoendelea bado. Ujambazi pekee wanaouona unafaa kukabiliwa ni dhidi ya mbubujiko wa madawa ya kulevya uliosababishwa na vinyangarika kutoka nchi hizo maaluni za “ ulimwengu wa tatu”. Kulingana na wastaarabu wan chi zilizoendelea, vinyangarika hivi ndivyo hasa adui mkubwa wa ustaarabu ulimwenguni na ni sharti vifagiliwe mbali bila huruma. Baada ya kusagwasagwa, ulimwengu mstaarabu utazidi kutononoka na ahadi ya mbingu hapa ardhini itakamilika. Imani ya watu ya kuwa ujambazi wa kimataifa. Hata iwapo upo, hauwezi kuwashtua wala kuwatingisha wao ilikuwa kamili na timamu. Ilikuwa kamili na timamu hadi hapo mwezi Septemba tarehe 11 mwaka wa 2001, ndege tatu za abiria zilipoelekezwa katika majumba mawili ya fahari, yenye urefu wa zaidi ya ghorofa mia moja na kuyatwangilia mbali. Mshtuko na kimako! Kimako kwa kuwa, kabla ya siku hiyo, wanarekani kudhai kwamba ingewezekana taifa lolote au mtu yeyote kuthubutu kuishambulia nchi yao, taifa wasifa lililojihami barabara dhidi ya aina yeyote ile ya uchokozi kutoka pembe lolote la dunia. Hakuna ulimwengu mzima, aliyeamini kuwa marekani ingeeza kushambuliwa. Kwa ajili hiyo, mshtuko uliitingisha ardhi yote na huzuni ilitanda kote, kama kwamba sayari nzima imeshambuliwa, wala sio marekani pekee. Mintarafu hiyo, marekani ilipolipiza kisasi kwa kuwaunguza waliokuwemo na wasiokuwemo kwa mabomu hatari huko Afghanistan, idadi kubwa ya watu duniani ilishangilia na kusherehekea. Kwa nahati mbaya, tafsiri ya shambulizi la minara- pacha ya Newyork na lile la Pentagon, uti wa uwezo wa kivita wa Marekani, ilizorota. Kuna wengi waliodhani huo ni mwanzo wa vita vya Waislamu dhidi ya Wakristo na kwa muda, Waislamu wote wakashukiwa kimakosa kuwa ni majambazi wa kimataifa. (a) Bila bubadilisha maana, fupisha aya tatu za kwanza ( maneno 65 – 75) Matayarisho Nakala safi (alama 10, 2 za utiririko) (b) Ukizingira aya, tatu za mwisho, fafanua fikira za watu wa mambo yote yaliyotokea Baada ya Septemba tarehe 11, 2001 (maneno 65 – 75) (alama 10, 2 za utiririko) Matayarisho Nakala safi

    Date posted: June 28, 2019.  

  • Soma makala yafuatayo kisha ujibu maswali Nairobi , mji mkuu wa Kenya, ni jiji la maajabu na mastaajabu chungu nzima. Nadhari ya mtu anayewahi kuingia jiji hili...(Solved)

    Soma makala yafuatayo kisha ujibu maswali Nairobi , mji mkuu wa Kenya, ni jiji la maajabu na mastaajabu chungu nzima. Nadhari ya mtu anayewahi kuingia jiji hili kwa mara ya kwanza huvutiwa na huo msheheneko wa majumba ya fahari, marefu ajabu, kiasi cha minazi mitano- sita iliyounganishwa kuelekea juu mbinguni. Jumba linalowavutia watu wengi ni lile la makongamano ya kimataifa liitwalo kwa kiingereza Kenyatta International Conference Centre. Jumba hili, hadi miaka michache ilipopita, ndilo lililokuwa refu zaidi mjini. Jumba lenyewe lina ghorofa ishirini na tisa hivi, Usipohesabu hilo pambo kama kofia kileleni mwake, linalojulikana kama mwavuli. Hata hivyo, miaka michache iliyopita jingo hili lilipitwa kwa urefu na mnara wa Nyakati ( Times Tower) Mnara huo hasa ni jumba linaloafiki lakabu yake ya kikwaruza mawingu. Jumba hili lina ghorofa zisizopungua thelathini na mbili. Mbali na majumba haya mawili, kuna majumba mengine zaidi ya ishirini katikati ya jiji ambayo, japo mengine ni mafupi kiasi, maumbo ya kustaajabisha kweli kweli. Hebu zingatia mwenyewe jumba liitwalo “mdomo wa kengele” au bell - bottom” ambalo ni vioo vitupu, toka chini hadi juu. Fauka ya haya, umbo lake ni la kipekee ulimwenguni kote. Jumba hili lina kama miguu, kisha kiuno mithili ya kinu hivi japo si mviringo. Linapaa juu, mbali sana, likichukua umbo pana kuliko lilivyo chini. Umbo la fua pana kama kengele. Halafu rudia barabara. Hizi hazina hesabu katikati ya jiji ni pona, tena safi sana. Magari yanayotumia barabara hizi ni kochokocho, ya kila aina na yanashindania nafasi. Ajabu kubwa ya Nairobi hata hivyo ni idadi ya watu. Hakuna hasa anayejua idadi kamili ya watu wa Nairobi, lakini sio kupiga chuku ninaposema kwamba, hasa nyakati za kuelekea kazini asubuhi, kwenda kula chakula cha mchana, kuelekea nyumbani baada ya kazi na kuvuka barabara wakati wa msongamano, watu hukanyagana. Mtu anayesema kwamba watu wa Nairobi ni wengi kama chungu, au kama mchanga wa ufuo wa bahari, hatii chumvi Watu wa Nairobi, kwa tabia na mavazi, si kama watu wa kwingineko nchini Kenya. Watu hawa kuvalia nadhifu sana. Wanawake ni warembo ajabu na hutengeneza nywele zao mithili ya hurulaini peponi. Wengi huvaa suruali ndefu! Kucha zao na midomo yao hupata rangi maridadi sana. Huzungumza Kiswahili na kiingereza takriban wakati wote. Wanawake wengi ajabu huendesha magari yao wenyewe, jambo ambalo litakushangaza mara tu uingiapo jijini, hasa kama ulilelewa ukidhani maskani mwafaka ya wanawake ni jikoni peke yake, yaani kuzingatia ile falsafa kuwa “ kuoa ni kupata jiko”. Wanaume nao huvaa suti safi, maridadi na shingoni wamefunga tai stahiki yao. Wanaume hao huendesha magari ya kuyaegesha karibu na afisi zao. Huingia afisini mwao kwa maringo na madaha, huku funguo za magari yao zikining’inia vidoleni. Hawa nao husema Kiswahili na kiingereza kupitia puani, utadhani ni waingereza hasa. Kwa upande mwingine, watoto ni nadhifu kweli hasa watoto wa shule. Hawa huvalia sare zilizofuliwa na kunyoshwa vizuri kwa pasi. Wake kwa waume, shingoni huvalia tai. Watoto wa shule Nairobi huongea Kiswahili, kiingereza na Sheng, ambayo ni “lahja” yao waliyoibuni. “Lugha” hii ni mchanganyiko wa Kiswahili. Kiingereza na msamiati mchache wa lugha nyingine za wakenya zisemwazo jijini Nairobi na vitongoji vyake. Kwa jumla, watu wote wa Nairobi hutembea kasi sana. Hawana hata wakati wa kutembea pole pole na kuangazaanga huku na huko. Iwapo wewe ni mgeni jijini, ukizubaa utapigwa kumbo na waendelee na hamsini zao kama vile hapakutokea jambo. Hili linapojiri, usidhani limefanywa maksudi. La, hasha ni vile tu kwamba Wanairobi hawana muda wa kupoteza. (a) Kwa nini majumba ya jiji la Nairobi yana majina au lakabu za kiingereza? (b) (i) Baadhi ya maajabu ya Nairobi ni barabara safi, msongamano wa magari na majumba marefu. Ongezea maajabu mengine manne (ii) Watu wa Nairobi wanajipenda kweli kweli. Fafanua (c) (i) Je, unadhani watu wa Nairobi kweli hukanyagana? Eleza ni kwa nini msimulizi ametoa maelezo hayo (ii) Unafikiri ni kwa nini hasa wanawake wa Nairobi wanaonekana nadhifu? (d) Kwa nini neno “lahja” limewekwa alama za mtajo? (e) Eleza maana ya maneno na tamathali za usemi zifuatazo: (i) Nadhari (ii) Linaloafiki (iii) Kikwaruza mawingu (iv) Waendelee na hamsini zao

    Date posted: June 28, 2019.  

  • Unda vitenzi kutokana na majina haya: (i) Mtukufu (ii) Mchumba(Solved)

    Unda vitenzi kutokana na majina haya: (i) Mtukufu (ii) Mchumba

    Date posted: June 27, 2019.  

  • Tunga sentensi mbili tofauti ukitumia vitenzi hivi vya silabi moja (i) Pa (ii) La(Solved)

    Tunga sentensi mbili tofauti ukitumia vitenzi hivi vya silabi moja (i) Pa (ii) La

    Date posted: June 27, 2019.  

  • Andika sentensi zifuatazo upya kwa kufuata maagizo (i) Alicheza kwa bidii akawafurahisha wengi waliohudhuria tamasha hizo Anza kwa: Kucheza (ii) Karamu hiyo ilifanya sana, kila mtu alikula chakula...(Solved)

    Andika sentensi zifuatazo upya kwa kufuata maagizo (i) Alicheza kwa bidii akawafurahisha wengi waliohudhuria tamasha hizo Anza kwa: Kucheza (ii) Karamu hiyo ilifanya sana, kila mtu alikula chakula akatosheka Anza kwa: chakula

    Date posted: June 27, 2019.  

  • (i) Taja vihusishi vitatu vinavyorejelea mahali, wakati na kiwango (ii) Tunga sentensi kuonyesha matumizi ya kila kihusishi(Solved)

    (i) Taja vihusishi vitatu vinavyorejelea mahali, wakati na kiwango (ii) Tunga sentensi kuonyesha matumizi ya kila kihusishi

    Date posted: June 27, 2019.  

  • Andika kifungu hiki kutoka usemi wa taarifa hadi usemi halisi Watoto waliambiwa na mama yao watakaporudi nyumbani waoge. Wale, halafu waanse kusoma moja kwa moja badala ya...(Solved)

    Andika kifungu hiki kutoka usemi wa taarifa hadi usemi halisi Watoto waliambiwa na mama yao watakaporudi nyumbani waoge. Wale, halafu waanse kusoma moja kwa moja badala ya kuharibu wakati wao kwa kutazama vipindi vya runinga. Aliwakumbusha kuwa wanaofanya maonyesho kwenye runinga tayari wamefuzu shuleni na wameajiriwa kazi

    Date posted: June 27, 2019.  

  • Tambulisha kielezi, kivumishi na mnyambuliko wa kitenzi katika sentensi ifuatayo: Msichana mrembo alikuja upesi akimkimbilia dadake(Solved)

    Tambulisha kielezi, kivumishi na mnyambuliko wa kitenzi katika sentensi ifuatayo: Msichana mrembo alikuja upesi akimkimbilia dadake

    Date posted: June 27, 2019.  

  • Tunga sentensi kuonyesha matumizi sahihi ya viunganishi hivi (i) Ingawaje (ii) Ilhali(Solved)

    Tunga sentensi kuonyesha matumizi sahihi ya viunganishi hivi (i) Ingawaje (ii) Ilhali

    Date posted: June 27, 2019.  

  • Tunga sentensi mbilimbili kuonyesha matumizi mawili tofauti ya I. Ka II. Ndivyo(Solved)

    Tunga sentensi mbilimbili kuonyesha matumizi mawili tofauti ya I. Ka II. Ndivyo

    Date posted: June 27, 2019.  

  • Tofautisha maana ya sentensi zifuatazo (i) Kazi yote ni muhimu (ii) Kazi yoyote ni muhimu(Solved)

    Tofautisha maana ya sentensi zifuatazo (i) Kazi yote ni muhimu (ii) Kazi yoyote ni muhimu

    Date posted: June 27, 2019.  

  • Eleza namna mbili za matumizi ya alama ifuatayo ya uakifishi (;) (Solved)

    Eleza namna mbili za matumizi ya alama ifuatayo ya uakifishi (;)

    Date posted: June 27, 2019.  

  • Andika udogo na ukubwa wa jina ngoma.(Solved)

    Andika udogo na ukubwa wa jina ngoma.

    Date posted: June 27, 2019.  

  • MUHTASARI Maendeleo ya taifa hutegemea jinsi wananchi wanavyolitolea katika kulibingirisha gurudumu la uchumi wao. Kila mwanajamii anahitajika kujibidisha katika kazi au taaluma yake. Mzalendo yeyote yule hupata motisha...(Solved)

    MUHTASARI Maendeleo ya taifa hutegemea jinsi wananchi wanavyolitolea katika kulibingirisha gurudumu la uchumi wao. Kila mwanajamii anahitajika kujibidisha katika kazi au taaluma yake. Mzalendo yeyote yule hupata motisha ya kufanya kazi iwapo anaweza kupata ile kazi aliyokuwa akitamani. Kumakinika katika taaluma Fulani si jambo jepesi na huchukua muda kutengeneza. Kwa mfano, ili mhazili apate staha ya uhazili sharti apitie ngazi mbali mbali. Mwanzo kabisa lazima kumpa fursa ya kujiunga na vyuo mbali mbali vya uhazili. Anapojiunga na vyuo hivyo ndipo safari inapoandaliwa. Kukamilisha safari hii inahitaji muda wa miaka minemitano. Anapohitimu kuwa tayari ameimudu shughuli hiyo. Hata hivyo, anatakiwa afanye mazoezi kila mara ili asisahau yanayohitajika katika taaluma hiyo. Wengi waliokwishapata ujuzi huo wa wale wenzao ambao katika masomo wana utaakamu kama wao. Ijapokuwa wote ni wahazili, viwango vyao ni tofauti na mishahara pia hutofautiana. Tofauti hapa ni daraja zao za vyeo. Baada ya kuhitimu na kupata vyeti vya uhazili ni rahisi kupata au kutopata kazi zenye ujira wa kuvutia. Anayefanikiwa ana sayari ya kujikakamua hasa kwa upande wa uzingatifu wa kazi kikamilifu na kutunza hadhi ya ofisi yake. Kuna mashirika makubwa yanayojiweza kiuchumi, ambayo rasimali yake ni imara. Mashirika madogo huwa yana rasilmali yenye kuyumbayumba. Mashirika haya yana wahazili na wanafunzi ambao hupata mishahara duni. Wanafunzi wote hao hufanya kazi kwa kutokuwa na uhakika wa kulipwa mwisho wa mwezi. Watu kama hao hawawezi kutilia maanani kazi zao. Mashirika mengine hayana utaratibu maalum, wa kulipa mishahara kwa vile hutegemea utu wa mkurugenzi. Badhi ya wakuu hao huwa wabanizi na huwapunja wafanyi kazi wao. Hili ni swala nyeti ambalo linahitaji litatuliwe kwa kuwa na chama cha kupigania haki za wafanyikazi. Wakati wanapotafuta kazi, Wahazili wengi huwa ni wahitaji na hukubali chochote wanachopewa. Wale waliobahatika kupata nafasi ya ajira katika kampuni kubwa za kimaataifa, mishahara huwa ni ya kutia moyo. Katika dunia hii wahazili wana vibarua vigumu, kwa sababu lazima wapate tajriba na uzoefu wa taaluma inayoendelea na shirika Fulani. Mhazili anapotumia msamiati usionda sambamba na shughuli za kiofisi hawasiti kufoka. Wavumilivu miongoni mwao hula mbivu. Hawa hawafi moyo bali hujitahidi zaidi ili wasikumbwe na kimbunga cha kufokewa. Kuna wengine ambao humwaga unga. (a) Bila kupoteza iliyokusudiwa na mwandishi wa taarifa, fupisha aya ya kwanza na ya pili ( maneno 60 – 70) Alama 2 kwa mtiririko) (b) Kwa kuzingatia aya mbili za mwisho, eleza mambo muhimu yanayoshughulika na mwandishi ( maneno 60 – 70) alama 2 kwa mtiririko)

    Date posted: June 27, 2019.  

  • Soma makala yafuatayo kisha ujibu maswali Wahenga walisema “mtoto umleavyo ndivyo akuavyo.” Hii ina maana ya kuwa ukiogopa kutumia ufito kumchapa mtoto wako, ukamdekeza atadeka na hatimaye...(Solved)

    Soma makala yafuatayo kisha ujibu maswali Wahenga walisema “mtoto umleavyo ndivyo akuavyo.” Hii ina maana ya kuwa ukiogopa kutumia ufito kumchapa mtoto wako, ukamdekeza atadeka na hatimaye ataharibika. Methali hii ina picha yake ambyo ni, “Ukicha mwana kulia, utalia wewe.” Hizi ni methali zilizojaa busara kubwa. Mathalini wewe ni mzazi au mtu yeyote mzima aliyetunikiwa madaraka juu ya watoto. Lakini kila wanapokiuka uadilifu au mmoja wao anapokosea wewe unambembeleza tu, basi huwa unaizorotesha tabia yake. Mwisho, mtoto huyo anaweza kuishia kuwa mtundu. Hata hivyo, ni sharti tujue ya kwamba tuko katika njia panda hapa. Kwa upande mmoja, zamani ilichukuliwa kwamba watoto na hata wanawake watu wazima hawana akili. Kwa ajili hiyo, iwapo mwanaume mtu mzima ana jambo la kuwaeleza, njia pekee ya kuliingiza katika “ akili” yao “ hafifu” ni kuwatwanga ili kulikongomeza jambo hili. Ukweli ni kwamba akili ya mtoto si hafifu hata. Unaweza kusema ni kama mmea, ambao usiporutubishwa kimakusudi, ukapaliliwa vyema na kustawishwa stahiki yake, basi hudhoofu” na mwishowe kufifia. Kwa upande mwingine, mtazamo wa kisasa ni tofauti kabisa, imethibitishwa ya kwamba wanawake ni sawa kabisa katika maumbile yao wakilinganishwa na wanaume. Kwa jinsi hiyo, kweli wapo wanawake amabo hawana mwelekeo timamu kuhusu maisha. Lakini ni kweli pia kuwa wapo wanaume watu wazima mamilioni ambao hawana akili. Kadhalika, si kweli kuwa watoto wote, kwa sababu ya umri wao tu, basi hawana akili. Ama kwa kusema kweli binadamu yeyote kuwaliwa na akili zake timamu isipokuwa wale ambao kwa bahati mbaya maumbile yamewapa akili pungufu. Hili litokeapo basi tunalikubali tu. Hatuwezi kumlaumu mtu kama huyo au muumba wake. Kwa hakika huu ndio msingi wa methali. “Akili ni nywele, kila mtu ana zake.” Vinginevyo, mtazamo wa kizamani ni taasubi kogwe tu za kiume zilizopitwa na wakati. Aidha, kwa sababu watu wote huzaliwa na akili timamu, tena hawawi watu wazimu kabla ya kuwa watoto kwanza, mtu mzima yeyote ana hali gani ya kuwadhulumu watoto na kujipambaniza na lawama za uongo dhidi ya vijana hao kwa madai kuwa hawana akili? Na je, ikiwa hawana akili, basi ndipo waonewe? Wanyanyaswe? Hili si jambo la busara. Kurudi mtoto kwa visa vya maonevu ni kumrudisha nyuma kiumbe huyo. Kurudi kufaako ni kwa kupeleka mbele, sio kwa kurudisha nyuma. Kurudi kuelekezako mbele ni kwa uongozi mwafaka, uongozi ambao lengo lake ni kummulikia mtoto kurunzi ilimradi kumwongoza mtoto. Mtoto ana haki ya kuhudumiwa kwa njia yoyote ifaayo ili akue na akili yake ikomae kikamilifu. Inafaa asomeshwe, apewe malezi bora ili naye aje alee wengine kistahiki. (a) “Mapenzi yasiyo kipimo yanaweza kuwa hatari kwa mtoto.” Eleza kikamilifu huku ukirejelea habari uliyosoma (b) Fafanua njia panda inayorejelewa na mtunzi (c) Mtoto analinganishwa na mmea katika taarifa hi, kwamba “usiporutubishwa kimakusudi, ukapaliliwa vyema na kustawishwa stahiki yake basi hudhofu.” Tahtmini kulinganishwa huku, huku ukirejelea taarifa (d) “Akili ni nywele, kila mtu ana zake.” Eleza maana ya ndani ya methali hii kulingana na taarifa (e) Onyesha kwamba unaelewa maana ya: “Kurudi mtoto kwa visa vya maonevu ni kumrudisha nyuma kiumbe huyo” (f) Eleza maana ya: (i) Kulikongomeza (ii) Kujipambaniza

    Date posted: June 27, 2019.  

  • Andika methali moja inayotokana na maelezo yafuatayo: Asiye na uwezo ataendelea kuwa bila uwezo hata akifanya bidii namna gani.(Solved)

    Andika methali moja inayotokana na maelezo yafuatayo: Asiye na uwezo ataendelea kuwa bila uwezo hata akifanya bidii namna gani.

    Date posted: June 27, 2019.  

  • Mdudu mwenye mkia uliopinda nchani ambao una sumu ni?(Solved)

    Mdudu mwenye mkia uliopinda nchani ambao una sumu ni?

    Date posted: June 27, 2019.  

  • Mdudu anayetengeneza utandu huitwa?(Solved)

    Mdudu anayetengeneza utandu huitwa?

    Date posted: June 27, 2019.  

  • Tumia tanakali za sauti zifaazo kukamilisha sentensi hizi; i) Sauti ya waimbaji haikusikika tena, ilikuwa imedidima…wageni walipofika katika jukwaa. ii) Simba ni mnyama hodari sana, akimkamata swara humrarua(Solved)

    Tumia tanakali za sauti zifaazo kukamilisha sentensi hizi; i) Sauti ya waimbaji haikusikika tena, ilikuwa imedidima…wageni walipofika katika jukwaa. ii) Simba ni mnyama hodari sana, akimkamata swara humrarua

    Date posted: June 27, 2019.  

  • Kamilisha tashbihi zifuatazo i) Baidika kama ii) Mzima kama(Solved)

    Kamilisha tashbihi zifuatazo i) Baidika kama ii) Mzima kama

    Date posted: June 27, 2019.  

  • Eleza tofauti baina ya sentensi hizi; i) Ningekuwa na pesa ningenunua shamba. ii) Ningelikuwa na pesa ningalinunua shamba(Solved)

    Eleza tofauti baina ya sentensi hizi; i) Ningekuwa na pesa ningenunua shamba. ii) Ningelikuwa na pesa ningalinunua shamba

    Date posted: June 27, 2019.  

  • Eleza maana nne-tofauti za sentensi hii; Alinunuliwa samaki na mtoto wake(Solved)

    Eleza maana nne-tofauti za sentensi hii; Alinunuliwa samaki na mtoto wake

    Date posted: June 27, 2019.  

  • Andika kinyume; Mjomba alichomeka upanga kwenye ala(Solved)

    Andika kinyume; Mjomba alichomeka upanga kwenye ala

    Date posted: June 27, 2019.  

  • Kanusha Ungemwuliza vizuri angekujibu bila wasiwasi(Solved)

    Kanusha Ungemwuliza vizuri angekujibu bila wasiwasi

    Date posted: June 27, 2019.  

  • Andika vitensi vinavyotokana na majina haya; i) Mfuasi ii) Kifaa iii) Mharibifu(Solved)

    Andika vitensi vinavyotokana na majina haya; i) Mfuasi ii) Kifaa iii) Mharibifu

    Date posted: June 27, 2019.  

  • Piga mstari vivumishi katika sentensi hizi i) Sina nguo yoyote niwezayo kuvaa ii) Mtoto mwenyewe ataileta kalamu(Solved)

    Piga mstari vivumishi katika sentensi hizi i) Sina nguo yoyote niwezayo kuvaa ii) Mtoto mwenyewe ataileta kalamu

    Date posted: June 27, 2019.  

  • Andika kwa msemo halisi sentensi. Tajiri alishangaa kuwa niliweza kuubeba mzigo huo peke yangu.(Solved)

    Andika kwa msemo halisi sentensi. Tajiri alishangaa kuwa niliweza kuubeba mzigo huo peke yangu.

    Date posted: June 27, 2019.  

  • Ziandike upya sentensi zifuatazo kwa kufuata maagizo uliyopewa. i) Nimemleta paka ili aue panya wote wanaotusumbua hapa kwetu nyumbani. (Anza: Panya…) ii) Mbwa ambaye aliripotiwa kuwa ameibwa amepatikana...(Solved)

    Ziandike upya sentensi zifuatazo kwa kufuata maagizo uliyopewa. i) Nimemleta paka ili aue panya wote wanaotusumbua hapa kwetu nyumbani. (Anza: Panya…) ii) Mbwa ambaye aliripotiwa kuwa ameibwa amepatikana katika bwawa la maji (Anza: katika bwawa…..)

    Date posted: June 27, 2019.  

  • Unganisha sentensi zifuatazo kwa kutumia viunganishi vifaavyo. i) Chakula hiki hakina mchuzi. Hakina chumve ii) Romeo aliamka. Alitazama saa yake Akala kiamsha kinywa mbio mbio(Solved)

    Unganisha sentensi zifuatazo kwa kutumia viunganishi vifaavyo. i) Chakula hiki hakina mchuzi. Hakina chumve ii) Romeo aliamka. Alitazama saa yake Akala kiamsha kinywa mbio mbio

    Date posted: June 27, 2019.  

  • Geuza sentensi zifuatazo ziwe katika hali ya umoja i) Huku kuimba kwenu kuzuri kutawapendez wageni ii) Hii miche ni mizuri sana, itatufaa(Solved)

    Geuza sentensi zifuatazo ziwe katika hali ya umoja i) Huku kuimba kwenu kuzuri kutawapendez wageni ii) Hii miche ni mizuri sana, itatufaa

    Date posted: June 27, 2019.