-
Tunga sentensi ukitumia neno katika ngeli ya YA-YA.
Date posted:
October 29, 2019
-
Changanua sentensi ifuatayo kwa njia ya matawi .
Mtoto alipoumia alitibiwa haraka sana.
Date posted:
October 29, 2019
-
Taja mfano mmoja kwa kila aina ya sauti zifuatazo;
Kipasuo-kwamizo –
Irabu ya nyuma wastani -
Date posted:
October 29, 2019
-
Soma makala yafuatayo kisha ujibu maswali
Nilianza kusikia habari za ugonjwa wa ukimwi mnamo mwaka wa 1984. Wakati huo nilikuwa nimemaliza masomo yangu ya kidato cha sita na kujiunga ia chuo cha walimu kilichoko wilayani Nyeri kiitwacho Kagumo. Nilihofu sana maradhi hayo hasa nilipowaona walioambukizwa wakikondeana mthili ya ng’onda. Baada ya waathiriwa kufariki, jamaa zao hawakuruhusiwa kuwazika. Wizara ya afya ilitoa amri kali kuwa wale wore waliofariki kutokana na maradhi ya ukimwi wazikwe na kikundi maalum cha madaktari ma wauguzi wa hospitali za wilayani. Kulikuwa na kasisi mmoja tuliyehusiana kiukoo aliyefariki kutokana na maradhi ya ukimwi. Sisi hatukuruhusiwa hata kumsongea karibu marehemu alipoletwa nyumbani.
Madaktari na wauguzi walivalia majoho meupe ungedhani ni malaika. Mikononi walivaa glovu nyeupe ambazo zilitutisha machoni.
Mara nyingi nimeshangazwa na athari za ugonjwa huu. Inasemekana kuwa kuna njia kadha za usambazaji wa ugonjwa wa ukimwi. Njia moja ni kuhusika katika kitendo cha mapenzi na mtu ambaye ameambukizwa virusi vya ugonjwa huo. Njia nyingine nimeelezwa kuwa ni kwa kutumia kwa pamoja vifaa vyenye makali na mtu aliyeambukizwa virusi vya ukimwi. Inasemekana kuwa kugusa damu ya mtu aliyeambukizwa ugonjwa huo pia kunaweza kukutia mashakani.
Mama mja mzito aliyeambukizwa ugonjwa huu anaweza kumwambukiza mtoto aliye tumboni anapojifungua na hati baadaye anapomnyonyesha mtoto wake mchanga. Kisha kuna kupokea damu kutoka kwa mtu ambaye tayari ameambukizwa virusi hivyo. Yote hayo yanachangia pakubwa katika kututumbukiza kwenye janga hili la ukimwi.
Lakini nimewahi kusikia watu wakisema kuwa ukimwi si maradhi. Yaani ni
upungufu tu wa kinga ya kukabiliana na magoniwa katika mwili wa binadamu. Maadamu ukiweza kuimarisha kinga ya magonjwa katika mwili wako basi unaweza kuishi kwa miaka ma mikaka. Anachohitajika mtu ni apate chakula na lishe bora, afanye mazoezi ya kutosha, na kujiepusha na mahusiano ya kimapenzi na watu wenine ambao huenda wakamwambukiza aina tofauti tofauti za virusi vya ukimwi. Hayo yakifanyika mwathiriwa huwa na matumaini ya kuishi kwa muda mrefu kwani hatazidiwa na maradhi hayo na mwishowe kwenda jongomeo. Kuna haja kubwa ya kujilinda na kuepukana kabisa na janga hili lililotuzingira. Wengi tayari wameshapoteza roho zao. Wengine walioambukizwa wanaugua mahospitalini ma na majumbani mwao kisirisiri. Mungu atujalie heri na shari, kwani utafiti wote ambao umefanywa kuhusu tiba ya uwele huu haujafua dafu hata kidogo. Hata hivyo Mola hamtupi mja wake.
Maswali
a) Ipe habari hii anwani ifaayo.
b) Kwa nini mwandishi ana hofu sana ya maradhi ya ukimwi?
c)Hapo awali watu waliwachukulia vipi walioambukizwa maradhi ya Ukimwi?
d)Eleza njia mbalimbali zinazomfanya mtu kuambukizwa maradhi ya ukimwi .
e)Je, tunawezaje kuepukana na janga hili la ukimwi?
f)Eleza maana ya vifungu hivi vya maneno kama vilivyotumika katika taarifa.
i)Wauguzi
ii)Makali
iii)Virusi
iv)Uwele
v)Janga
Date posted:
October 29, 2019
-
Eleza maana ya istilahi zifuatazo za isimu jamii.
i)Lugha ya taifa
(ii)Lugha ya ishara
(iii)Lugha mwiko
(iv)Sajili za lugha
(v)Uchanganyaji msimbo.
Date posted:
October 21, 2019
-
ISIMU JAMII
Ali: Wee kuja hapa. Wewe ni nani? Sema haraka!
Ebo: Mimi … ni … afande ni Ebo
Ali: Unatoka wapi sa ii? Hapa hakuna sheria?
Ebo: Samahani mkubwa. Mimi niku…
Ali: Mkubwa wa nani? Wakubwa wako ofisini.
Ebo: Pole mzee.
Ali: Mzee gani? Hii mtu lazima niiwekwa store. Yaani self-contained.
Toa viatu.
Ebo: Tafadhali Bwana Askari, nilichelewa …
Ali: Mimi sitaki hadithi! Hizo pelekea nyanya yako, eh. Fanya haraka!
Ebo: Naomba mkubwa …
Ali: Hapa si kanisani. Unaomba! Hata …
Fafanua sifa tano za sajili hii.
Date posted:
October 21, 2019
-
Eleza maana ya nomino.
Date posted:
October 21, 2019
-
Eleza maana tatu zinazopatikana katika sentensi hii.
Alikuwa amenijuza kuwa angefika kwao.
Date posted:
October 21, 2019
-
Eleza matumizi ya kwa katika sentensi hii.
Kwa nini umeishi kwao kwa miaka mingi?
Date posted:
October 21, 2019
-
Tumia kivumishi kionyeshi cha karibu pamoja na nomino katika ngeli ya I-ZI kisha utunge sentensi katika ukubwa - wingi.
Date posted:
October 21, 2019
-
Eleza dhana ya shamirisho.
Date posted:
October 21, 2019
-
Nyambua kitenzi ja katika kauli ya kutendewa kisha utunge sentensi.
Date posted:
October 21, 2019
-
Weka kirejeshi ‘O’ tamati kwenye kitenzi chunga kisha ukitungie sentensi.
Date posted:
October 21, 2019
-
Tunga sentensi moja kubainisha matumizi ya ‘na’ kama.
(i)Kihusishi cha ‘na’ ya mtenda.
(ii)Kiunganishi
Date posted:
October 21, 2019
-
Tumia mzizi –w- katika sentensi kama:
(i)Kitenzi kisaidizi.
(ii)Kitenzi Kishirikishi.
Date posted:
October 21, 2019
-
Onyesha vishazi katika sentensi ifuatayo kisha uelezee ni vya aina gani.
Ajapo tutamlaki kwa shangwe.
Date posted:
October 18, 2019
-
Neno lifuatalo liko katika ngeli gani?
Matukio
Date posted:
October 18, 2019
-
Viambishi vilivyopigiwa mstari vinawakilisha dhana zipi za kisarufi?
i)Udhaifu
ii)Walani?
Date posted:
October 18, 2019
-
Eleza ni kwa nini neno umma ni la asili ya kigeni.
Date posted:
October 18, 2019
-
Taja maneno yenye miundo ifuatayo ya silabi.
(i)KKKI
(ii)Irabu pekee (II)
Date posted:
October 18, 2019
-
Taja mambo yoyote manne yanayofanywa na serikali yetu kuimarisha lugha ya Kiswahili
Date posted:
October 17, 2019
-
Kanusha katika ukubwa
Mwizi huyu aliiba kisu na ng’ombe wa mwanamke yule.
Date posted:
October 17, 2019
-
Eleza tofauti iliyopo kati ya sentensi hizi
Tulipofika hotelini tulipewa soda na chupa
Tulipofika hotelini tulipewa soda kwa chupa
Date posted:
October 17, 2019
-
Eleza maana ya sentensi hii
Ningalikuwa na pesa ningalinunua gari na ningalistarehe.
Date posted:
October 17, 2019
-
Andika neno lenye maana sawa na
Hawala
Katani
Date posted:
October 17, 2019
-
Onyesha matumizi ya kiimbo katika sentensi hii
Ondoka hapa!
Date posted:
October 17, 2019
-
Eleza sifa mbili za vishazi tegemezi.
Date posted:
October 16, 2019
-
Bainisha aina za vitenzi katika sentensi ifuatayo.
Walimu ni watu wasiopendwa wanaposema ukweli kuhusu wanafunzi
Date posted:
October 16, 2019
-
Onyesha virai katika sentensi zifuatazo na ueleze ni vya aina gani.
i) Anachukia kusoma riwaya yenye masuala ya kisiasa.
ii) Watoto wa kike hudunishwa katika jamii nyingi
Date posted:
October 16, 2019
-
Yakinisha katika nafsi ya tatu wingi
Sijasafiri kwenda marekani
Date posted:
October 16, 2019