Get premium membership and access questions with answers, video lessons as well as revision papers.

Q&A Categories


Do you have Q&A pairs? Post them here

61904 Questions  View: All | Solved | Unsolved



Search Results...
  • Bainisha ngeli ya nomino iliyopigiwa mistari. Jeshi la Kenya lilihamisha kifaru hadi mbuga ya Masai mara.(Solved)

    Bainisha ngeli ya nomino iliyopigiwa mistari. Jeshi la Kenya lilihamisha kifaru hadi mbuga ya Masai mara.

    Date posted: November 25, 2022.  

  • Tambua aina za maneno zilizopigiwa mistari. Mwanafunzi mrefu alienda Nairobi(Solved)

    Tambua aina za maneno zilizopigiwa mistari. Mwanafunzi mrefu alienda Nairobi

    Date posted: November 25, 2022.  

  • Tunga sentensi moja na uonyeshe nomino dhahania.(Solved)

    Tunga sentensi moja na uonyeshe nomino dhahania.

    Date posted: November 25, 2022.  

  • Tambua sauti yenye sifa zifuatazo. konsonanti, kipasuo, ghuna, sauti ya mdomo.(Solved)

    Tambua sauti yenye sifa zifuatazo. konsonanti, kipasuo, ghuna, sauti ya mdomo.

    Date posted: November 25, 2022.  

  • Taja ala sogezi mbili za kutamkia.(Solved)

    Taja ala sogezi mbili za kutamkia.

    Date posted: November 25, 2022.  

  • Soma ufahamu ufuatao kisha ujibu maswali FUNGUA SESAME Jina la Nimrod lilipotea mara tualipoanza kufanya kazi jijini Nairobi.(Solved)

    Soma ufahamu ufuatao kisha ujibu maswali FUNGUA SESAME Jina la Nimrod lilipotea mara tualipoanza kufanya kazi jijini Nairobi. Marafiki na jamaa zake waliamini kuwa alikuwa ameajiriwa huko mjini ingawa hakuna aliyeijua kazi yenyewe vizuri. Hata hivyo waliamini kuwa lazima alikuwa na kibonge cha kazi kwa sababu alivalia kinadhifu na kuishi maisha ya starehe. Tena yeye mwenyewe alikazania kusema kuwa amejiriwa kazi ya maana. Marafiki zake walimfahamu kama “Bwana Sesame”. Mtu wa kwanza aliyempa jina hilo alisema alipendezwa na ujuzi na maarifa yake. “huyu hakosi ufumbuzi wa tatizo lolote. Ni kama ule mlango wa kisa cha Ali Baba na Wezi arobaini. Ukisema ‘fungua Sesame’ unafungu katu,” alisema mtu huyo. Jamaa walioishi naye katika mtaa wa Urumo walishangazwa na utaratibu wake wa kazi. Mchana kutwa alishinda chumbani mwake. Mara nyingi utamkuta ametulia akitazama runinga yake ndogo. Wakati mwingine atakuwa akifanya kazi yake ndogo ndogo huku akipiga mluzi bubu, ambao haukusikika vizuri. Wakati mwingine atakuwa akiusikiliza muziki kwenye chombo chake cha muziki kilichotingisha jingo zima kutokana na sauti yake nene. Kwa kawaida alitoka chumbani jioni. Waliomjua walimchangamkia kutokana na uchangamfu wake. Alipenda sana mizaha. Waliopenda kupiga soga walivutiwa na maongezi yake hasa kuhusiana na magari. Aliyajua magari mengi. Mimi naweza kuijua aina ya gari kwa kuusikiliza mlio wake tu”, alisema kila wakati. “wacha kutuvungavunga Bwana wee, haiwezekani !” atasema mwingine. “nini? Unajua mimi ndiye Bwana Sesame mwenyewe!” atasema, halafu wote wataangua kicheko. Ilifika wakati kampuni kadha zilipoamua kuwapunguza wafanyakazi wake kutokana na hali mbaya ya kiuchumi. Lakini Bwana Sesame hakuwa mmoja wa hao. Hali yake ilibakia vile vile. Aliendelea kuvalia kinadhifu na kuishi maisha yake ya fawaishi. Wakati wenzake wanalalamikia hali ngumu ya maisha, Bwana Sesame hakuwa na lolote la kumsumbua. Aliendelea kukaa bila kazi wala bazi. Lakini watu walitambua kuwa alikua na mazoea yakutoka chumbani majira ya jioni. Hakuna aliyejua alirejea lini. Sikumoja Bwana Sesame alitoka jioni kama kawaida na kuelekea kwenye shughuli zake za kawaida. Siku hiyo jamaa mmoja wa mtaani alikumbana naye kwenye lango kuu. “Bwana Sesame,leo wapi yahe?alimwuliza. Bwana Sesame alimwangalia na kusema, “natoka nje kidogo yahe. Jiji hili lataka ustaarabu,’ alijibu. Yule jamaa alimwangalia na kumwabia, “nina shida kidogo, sijui kama utanifaa mwenzangu. Wajua tena hali zenyewe siku hizi,” alisema. Nini tena?’ aliuliza Bwana Sesame. “Nina gari langu ambalo halina redio. Natafuta moja ya bei nafuu.... Kitu kama sony hivi,” alisema. Bwana Sesame alimwangalia na kusema, “hiyo kazi nyepesi kwangu yahe, papai kwa kijiko!” alisema Bwana Sesame akicheka. Jamaa Yule alishukuru na wakaagana. Bwana Sesame alishika njia kuelekea sehemu zake za kawaida majira kama haya.Naye Yule jamaaa kapinda kama anaangalia mtaani, lakini baada ya muda akageuka na kuamua kumfuata Bwana Sesame. Bwana Sesame alishika tariki mpaka sehemu ya mazoea. Yule jamaa alimfuata kwambali na mwendo wa paka. Alimwona Bwana Sesame akiingia mahali palipokuwa na banda kuukuu. Muda si muda alitoka na jamaa wengine wakiwa wamevalia maguo ya ajabu. Yule jamaa aliwafuata hadi mahali palipokuwa na ujia mwembamba ulioachana na barabara kuu. Alijificha mahali, na kutokana nahali ya sehemu ile akawa haonekani. Muda si muda palitokeza gari dogolililokuwa likiendeshwa na mwanamke mmoja. Bwana Sesame na wenzake walitokeza na kutupa gogo lililomzuia Yule mwanamke. Ghafla bin vuu walimvamia; wakaifungua milango ya gari mbio na kujivurumisha ndani. Gari lilitimuliwa kama risasi kuelekea upande wa pili. Wakati huo Yule jamaa ashaliangalia gari lenyewe na kuzihifadhi nambari zake. Alishika njia kurudi zake chumbani. Siku iliyofuata huyo jamaa hakuwa kazini. Alipokuwa akifungua kinywa alisikia sauti ya kugongwa kwa mlango. Aliinuka na kwenda kuufungua. Bwana Sesame aliingia ndani. “vipi yahe? Hujenda kazini leo? Au umelala sana Bwana?’ alisema Bwana Sesame kwa uchangamfu wake. Muda si muda alimwonyesha redio ya gari aliyokuwa nayo. “umeipata mara moja hii kumbe?’ aliuliza Yule jamaa. “si nilikwambia yahe! Mimi ndiyeBwana Sesame mwenyewe. Hii kwangu si kazi. Ninafahamiana na jamaa wengi wanaoifanya kazi hii,” alisema Bwana Sesame. “naona kweli. Ehh Bwana we! Ndipo waswahili wakasema,ukitaka kuvua vua na wavuvi! Alisema Yule jamaa. “ni kweli kabisa!’” alijibu Bwana Sesame huku akicheka kwa furaha. Yule jamaa alisimama kuelekea chumbani. Bwana Sesame alitulia akisubiri kupokea ujira wake. Muda mfupi ulipita, kasha mlango wa nyumba ukagongwa. “yahe Bwana, kunagogwa huku!” Bwana Sesame akasema. Yule jamaa alitoka chumbani na kuelekea mlangoni. Mlango ulipofunguliwa waliingia askari polisi wawili. Bwana Sesame hakuwa na upenyu wakutokea. Alitiwa mikononi.Hakujua kumbe Yule jamaa alikuwa kachero. Hapakuwa na ujanja tena. Siku hiyo pwagu alipata pwaguzi. Fungua Sesame haikufaa tena. Maswali 1. Kwa nini Nimrod alibatizwa ‘Bwana Sesame’? 2. Kwa nini watu walioishi mtaani Urumo walishangazwa na utaratibu wa kazi wa Bwana Sesame? 3. Unafikiria ni kwanini Bwana Sesame alifahamu sana juu ya magari? 4. Je, unafikiri yule jamaa aliagiza aletewe radio alikuwa na haja sana na kifaa hicho kama alivyosema? 5. Bwana Sesame alikuwa kachero. Unakubali? Toa maelezo? 6. Yule jamaa alipoingia chumbani na kumwancha Bwana Sesame sebuleni unafikiria alikwenda kufanya nini 7. Je, hadithi hii ina mafunzo gani kwako? 8. Eleza maana ya misemo ifuaayo kasha itumie katika sentensi a) Piga mluzi b) Piga soga c) Shika tariki

    Date posted: November 25, 2022.  

  • Taja vipera vitano vya semi.(Solved)

    Taja vipera vitano vya semi.

    Date posted: November 25, 2022.  

  • Soma dondoo lifuatalo kisha ujibu maswali yanayofuata. Mwatani: Rusha hiyo ball haraka tumechelewa five minutes. Twende daro. Omoshi: Harakisha mode anacome.(Solved)

    Soma dondoo lifuatalo kisha ujibu maswali yanayofuata. Mwatani: Rusha hiyo ball haraka tumechelewa five minutes. Twende daro. Omoshi: Harakisha mode anacome. Bwana Kipiti: Nendeni darasani haraka! Kisha kiranja awape vitabu vyenu vya insha ili mwandike barua. Mwatani: Sawa mwalimu. Samahani kwa kuchelewa uwanjani. Omoshi: Je, tutaandika barua rasmi au barua ya kawaida? Bwana Kipiti: Mwandike barua rasmi. Je, mnakumbuka muundo wake? Omoshi na Mwatani: Ndio mwalimu. Ulitufundisha jana. Asante sana mwalimu. Bwana Kipiti: Kumbukeni idadi ya maneno. Idadi ya maneno ni muhimu katika uandishi wa insha. (i) Eleza sajili katika dondoo. (ii) Eleza sifa nane za sajili hii zinazopatikana katika dondoo.

    Date posted: November 25, 2022.  

  • Ainisha vielezi katika katika sentensi ifuatayo. Mwanafunzi mzuri ni yule afanyaye mazoezi vizuri kila siku shuleni.(Solved)

    Ainisha vielezi katika katika sentensi ifuatayo. Mwanafunzi mzuri ni yule afanyaye mazoezi vizuri kila siku shuleni.

    Date posted: November 25, 2022.  

  • Tumia o-rejeshi kati katika sentensi ifuatayo. Kuta ambazo zilijengwa zimebomoka.(Solved)

    Tumia o-rejeshi kati katika sentensi ifuatayo. Kuta ambazo zilijengwa zimebomoka.

    Date posted: November 25, 2022.  

  • Kamilisha methali ifuatayo. Asiye na nadhari...(Solved)

    Kamilisha methali ifuatayo. Asiye na nadhari...

    Date posted: November 25, 2022.  

  • Andika kwa wingi. Kuwepo kwa mshauri wake kulimfurahisha waziri.(Solved)

    Andika kwa wingi. Kuwepo kwa mshauri wake kulimfurahisha waziri.

    Date posted: November 25, 2022.  

  • Badilisha kitenzi kisaidizi kilicho kwenye sentensi ifuatayo kiwe kishirikishi. Mvule alikuwa akilala bwenini.(Solved)

    Badilisha kitenzi kisaidizi kilicho kwenye sentensi ifuatayo kiwe kishirikishi. Mvule alikuwa akilala bwenini.

    Date posted: November 25, 2022.  

  • Andika sentensi ifuatayo katika ukubwa. Uteo alionunuliwa umezeeka sana.(Solved)

    Andika sentensi ifuatayo katika ukubwa. Uteo alionunuliwa umezeeka sana.

    Date posted: November 25, 2022.  

  • Yakinisha: Usipolipa usiingie ndani.(Solved)

    Yakinisha: Usipolipa usiingie ndani.

    Date posted: November 25, 2022.  

  • Tunga sentensi moja moja kudhihirisha matumizi ya i. Posa ii. Poza(Solved)

    Tunga sentensi moja moja kudhihirisha matumizi ya i. Posa ii. Poza

    Date posted: November 25, 2022.  

  • Kanusha sentensi katika hali ya kuamrisha wingi. Kimbia haraka – Amka -(Solved)

    Kanusha sentensi katika hali ya kuamrisha wingi. Kimbia haraka – Amka -

    Date posted: November 25, 2022.  

  • Tunga sentensi yenye kivumishi cha jina.(Solved)

    Tunga sentensi yenye kivumishi cha jina.

    Date posted: November 25, 2022.  

  • Tambulisha na ufafanue viambishi vilivyotumika katika Anamfundisha.(Solved)

    Tambulisha na ufafanue viambishi vilivyotumika katika Anamfundisha.

    Date posted: November 25, 2022.  

  • Kanusha sentensi ifuatayo kwa umoja. Nywele zenu hukatika mnapoachana.(Solved)

    Kanusha sentensi ifuatayo kwa umoja. Nywele zenu hukatika mnapoachana.

    Date posted: November 25, 2022.  

  • Huku ukitoa mifano taja miundo ya silabi.(Solved)

    Huku ukitoa mifano taja miundo ya silabi.

    Date posted: November 25, 2022.  

  • Sauti /p/ ni kipasuo, sauti hizi ni gani? i. / f / ii. / l /(Solved)

    Sauti /p/ ni kipasuo, sauti hizi ni gani? i. / f / ii. / l /

    Date posted: November 25, 2022.  

  • Soma taarifa ifuatayo kasha ujibu maswali Ilikuwa Jumamosi. Nilifika nyumbani kwangu saa moja jioni. Tangu nistaafu miaka miwili awali sikupenda kuchelewa Taarifa ya Habari.(Solved)

    Soma taarifa ifuatayo kasha ujibu maswali Ilikuwa Jumamosi. Nilifika nyumbani kwangu saa moja jioni. Tangu nistaafu miaka miwili awali sikupenda kuchelewa Taarifa ya Habari. Mwezi mmoja ukawa umepita tangu nipewe pesa za kiinua mgongo. Mwezi mmoja mzima nilikuwa katika shughuli za kulipa deni hapa na kulipa karo huku. Kuwekeza kwenye mradi ule na kununua hili. Sasa shilingi laki mbili tu zilikuwa zimesalia katika benki. Watu wengi walinishawishi nijaribu kilimo cha mahindi. Bei ilikuwa imeanza kuimarika. Katika taarifa ya habari jioni hiyo, Waziri wa kilimo alitangazaa bei mpya , shilingi 1,500 kwa kila gunia. Nami nilikuwa naanza kuumakinikia mradi huu. Baada ya taarifa, nilioga nikala na nikaenda kulala. Kwa sababu ya uchovu, usingizi ulinichukuwa mara moja. Usingizini niliota. Katika ndoto niliutekeleza mradi wangu. Msimu huo wa kulima nilitenga hekari kumi za shamba langu. Wataalamu walinishauri kuwa wakati mzuri wa kulima ni wa kiangazi. Mwezi wa Januari ulipoanza tu nilitafuta trekta na kulima. Malipo yalikuwa shilingi 1,200 kila ekari. Katikati ya mwezi wa Mechi, nilitafuta trekta la kutifua shamba tena kwa gharama ya shilingi 15,000 ekari zote kumi. Kufuatia ushauri wa manyakanga wa kilimo, nililipa shilingi elfu kumi na tatu kupiga shamba lote haro. Mwishoni mwa mwezi huo, nilienda mjini kutafuta pembejeo. Kwanza, nililipa shilingi 20,500 kwa magunia 15 ya mbolea. Kisha nilinunua magunia manne ya mbegu ya mahindi yenye uzani wa kilo 25 kwa shilingi 3,300 kila gunia. Mwezi wa Aprili ulipotimia tu, niliamua kupanda ili nipate mazao bora, nilipanda kwa tandazi. Gharama ilikuwa shilingi 1,000 kila ekari. Mvua ilinyesha vizuri na baada ya siku saba, mahindi yalianza kuota. Ilifurahisha kuhesabu mistari ya kijani iliyonyooka. Hali hii iliwezekana tu baada ya kuajiri vijana wa kuwafukuza korongo na vidiri ili wasifukue mbegu mchangani. Baada ya mwezi mmoja, hatua ya kupalilia ilifika. Nilitafuta vibarua wa kupalilia. Malipo yalikuwa shilingi 700 kila ekari. Kumbe kupalilia kulichochea mtifuko wa mahindi. Punde yakawa yananifikia magotini. Hii ikawa ishara kuwa yanahitaji kumwagiwa mbolea ya kunawirisha iitwayo ‘amonia’. Gharama yake ikawa shilingi 1,300 kila gunia. Hivyo , nikalipa shilingi 19,500 kwa magunia kumi na matano. Mahindi yalibadilika kimiujiza. Ghafla tu yalirefuka na kunenepa mashina. Yalibadilika rangi yakapiga weusi. Shamba liligeuka likawa kama msitu wa rangi ya kijani iliyokolea. Wapita njia waliajabia mimea na juhudi zangu. Shamba langu sasa likawa kielelezo. Maafisa wa kilimo wakawa kila siku wanawaleta wakulima wengine kujifunza siri ya ufanisi wangu. Hapo nikaanza kuhesabu mavuno nitakayopata na kukadiri faida. Nilipuuza kabisa ushauri wa wahenga kuwa ‘Usikate majani, mnyama hajauawa.’ Bila taarifa wala tahadhari mvua ilitoweka. Hayakupita majuma mawili mahindi yakaanza kubadilika. Juma moja baadaye mahindi yalinyauka. Badala ya mahindi, shamba likageuka la vitunguu vilivyochomwa na jua. Makisio yangu ya faida yaliyeyuka jinsi ufanyavyo moshi. Lakini ‘Muumba ndiye Muumbua.’Siku moja mawingu yalitanda na mvua ikanyesha , muda si muda mahindi yalianza kunawiri. Kumbe tukio lililowavunja moyo lilikuwa laja. Siku moja mvua kubwa ilinyesha. Asubuhi nilipotoka nje nilipigwa na butwa. Barafu ilitapakaa pote. Shamba lilikuwa limetapakaa barafu nafuu. Nilipotazama upande wa shamba niliona dalili za majani mapya ya mahindi yakianza kuchomoza. Maumbile ni kitu cha ajabu kweli. Muda si mrefu mahindi yalirudia hali yake tena, kasha yakakomaa. Harakati za kutafuta watu wa kuyakata na kuyakusanya zilianza. Gharama ya shughuli hii ikawa shilingi 5,000 kuvuna kusafirisha kutoka shamba na kukoboa kwa mashine magunia 200 yakachukua shilingi 20,500. Kufikia hapo nilikuwa nimetumia takribani shilingi 192,700. Gharama nyingine zilikuwa za usafiri, gharama ya dharura na usimamizi, usumbufu wangu binafsi, gharama ya magunia na kadhalika. Mahindi yalipokuwa tayari kwenye magunia nilifunga safari kwenda mjini kutafuta soko. Niliposhuka tu niliona gazeti. Habari motomoto siku hiyo ilikuwa ‘MAHINDI GUNIA 900/=’ Niligutuka usingizini. MASWALI a) Ni changamoto zipi zinazokumba kilimo. b) Msimulizi alikuwa na kiasi gani cha pesa katika benki baada ya mradi kukamilika? c) Eleza maana ya methali zifuatazo kwa mujibu wa makala. i. Usikate majani, mnyama hajauawa. ii. Muumba ndiye Muumba. d) Eleza mambo mawili yaliyosababisha msimulizi asipate faida alivyotarajia. e) Kwa nini msimulizi alisema maumbile ni kitu cha ajabu? f) Eleza maana ya: i. Kiinua mgongo ii. Manyakanga wa kilimo.

    Date posted: November 25, 2022.  

  • Bainisha nomino katika utungo huu. Watoto wameenda kucheza.(Solved)

    Bainisha nomino katika utungo huu. Watoto wameenda kucheza.

    Date posted: November 25, 2022.  

  • Taja nomino zozote mbili katika ngeli A-WA na uonyeshe miundo yake. (Solved)

    Taja nomino zozote mbili katika ngeli A-WA na uonyeshe miundo yake.

    Date posted: November 25, 2022.  

  • Andika udogo wa: Anacheza ngoma.(Solved)

    Andika udogo wa: Anacheza ngoma.

    Date posted: November 25, 2022.  

  • Tumia kiunganishi kifaacho kuunganisha sentensi hizi. Mwizi alishikwa. Mwizi alipigwa sana.(Solved)

    Tumia kiunganishi kifaacho kuunganisha sentensi hizi. Mwizi alishikwa. Mwizi alipigwa sana.

    Date posted: November 25, 2022.  

  • Bainisha aina za vielezi katika sentensi hii. Mtoto alikimbia mara sita uwanjani kisha akatembea kitausi.(Solved)

    Bainisha aina za vielezi katika sentensi hii. Mtoto alikimbia mara sita uwanjani kisha akatembea kitausi.

    Date posted: November 25, 2022.  

  • Tunga sentensi yenye kitenzi kishirikishi kipungufu. (Solved)

    Tunga sentensi yenye kitenzi kishirikishi kipungufu.

    Date posted: November 25, 2022.  

  • Pigia mstari vivumishi kwenye sentensi hizi na ueleze ni vya aina gani. (i) Mtoto mwenyewe ataleta kalamu. (ii) Kitabu cha Musa hakipo(Solved)

    Pigia mstari vivumishi kwenye sentensi hizi na ueleze ni vya aina gani. (i) Mtoto mwenyewe ataleta kalamu. (ii) Kitabu cha Musa hakipo

    Date posted: November 25, 2022.